Zitto: Njia pekee ya kumuenzi Sitta ni kuimarisha uhuru na heshma ya bunge

Casuist

JF-Expert Member
Jul 23, 2014
1,179
2,940


Siku ya Jana ilikuwa ni siku ya kumuaga aliyepata kuwa spika wa bunge la tisa, Samwel Sitta kwa mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma. Sitta aliagwa bungeni Dodoma sehemu aliyoitumikia muda mrefu kama mbunge na hatimae spika wa bunge almaarufu kama bunge la tisa lenye kasi na viwango na kuwa mtu wa kwanza kuagwa ndani ya ukumbi wa bunge kwa heshma kubwa aliyojijengea wakati akiongoza bunge hilo. Miongoni mwa waliopata nafasi ya kutoa salam za pole ni mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe.

Zitto katika salam zake fupi alisema Sitta anakumbukwa kama spika pamoja na vyeo vingi alivyoshika kwa sababu ya 'Legacy' yake aliyoiacha kwenye bunge ikiwemo kuandikwa sheria mpya ya bunge na uanzishwaji wa mfuko wa bunge.

Pia Zitto alimsema Sitta kama mtu aliewabana mawaziri wajibu kwa ufasaha na kutoa fursa kwa wabunge wote ikiwemo wa vyama vya upinzani. Kuomba radhi popote alipokosea na Zitto amesema unafaa kuwa mfano wa kuigwa kwa viongozi.

Zitto aliongeza kwa kusema njia pekee ya kumuenzi Samwel Sitta ni kuimarisha uhuru na heshma ya bunge. Zitto alimaliza kwa kusema Sitta Ameishi katika uzalendo, ndoto ya Tanzania imara na yenye heshima na vijana wengi aliowafunda.

Aidha Tundu Lissu katika salam zake alisema Sitta alama ya Sitta katika miaka yake mingi ya utumishi, ni miaka mitano ya uspika wake katika bunge, alitaka bunge lenye meno na kuisimamia na kuidhibiti serikali. Alihitaji bunge kama mhimili wa dola na sio msindikizaji wa mihimili mingine ya dola. Aliongeza hakuwa kibaraka wa mtu yeyote na alionyesha kuwa mtu mwenye msimamo huru.

Mwili wa Samwel Sitta unatarajia kuzikwa leo Urambo mkoani Tabora, ameacha mjane na watoto watano.
 
Katika viongozi bora 10 wa kisiasa nchini kwetu, Mh Sitta yumo katika nafasi za juu.
Hata familia yake imeijenga vizuri sana kuanzia watoto hadi mama yake mzazi,
PUMZIKA KWA AMANI MH SITTA.
 
Ni wachache Sana Kuwapata kama Mh Samweli Sitta.Mtu Amefariki na Ameumiza Watu wengi sana.
Ni Bora kutenda wema Kuliko kuishi Kama Shetani kwani siku ikifika Badala ya Watu Kukuaga kwa uchungu kutoka Rohoni watu wanasema Bora Hata Ameenda zake huyo.Mh Sitta Ni Mfano Wa kuigwa Sana Milele na Milele.
 
Njia pekee ya kumuenzi sitta ni kuimarisha uhuru na heshima ya bunge?, haya maoni ya zitto yalitakiwa kupata Kibali kutoka kwa tuli
 
Yaani ile katiba angeiachia ikapita, leo hii tungekuwa katika mwelekeo tofauti kisiasa, kiutendaji na hata kimaendeleo. Anyway apumzike kwa amani ila viongozi mliobaki jifunzeni: sote tu wapitaji tu hapa duniani na hakuna haja ya kubana matakwa ya wengi ili kunufaisha kikundi cha watu wachache. Utumikieni umma uliowachagua na kutii matakwa yake na siku yenu ya kuondoka ikifika mtakumbukwa kwa dhati na siyo ngonjera za kinafiki zilizoandikwa na walipa fadhira na walambishwa asali.
 
Alisaidia hata kututafutia nafasi wengine za kusoma, na tukaenda Zanzibar kwa ajili yake. Pengine isingekuwa Sitta kuunga mnyororo katika maisha yetu tusingekuwa wabunge au wanasiasa leo hii. Sitta aliweza kuziba pengo la baba kwa sisi tuliyekuwa na pengo hilo.Namuomba Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pake panapostahili.
 
Alisaidia hata kututafutia nafasi wengine za kusoma, na tukaenda Zanzibar kwa ajili yake. Pengine isingekuwa Sitta kuunga mnyororo katika maisha yetu tusingekuwa wabunge au wanasiasa leo hii. Sitta aliweza kuziba pengo la baba kwa sisi tuliyekuwa na pengo hilo.Namuomba Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pake panapostahili.
146293a28299d204bf390844bf255fce.jpg
 
RIP Sitta,
Mengi yatasemwa, lakini kubwa uliloacha kama fundisho kwa wanasiasa wetu ni kuacha kutanguliza tamaa binafsi kwa jina la uzalendo.... Chuki za kisiasa na kutafuta madaraka kwa nguvu yeyote hata kuharibu uhusiano na wengine na kupakazia wengine ubaya...
Hilo hukuwa nalo kabisa... Natamani uwe mwisho wa siasa uchwara ndani na nje ya bunge letu.... Kuna namna nyingi za kupata madaraka bila kuvuruga na kuharibu personalities za watu.

May your soul Rest in Eternal peace.
 
Bila ya Mzee Sitta kuwa Jasiri na Mzalendo Chadema wasingempigania Apewe Uspika wa Bunge la Katiba
 
Katika viongozi bora 10 wa kisiasa nchini kwetu, Mh Sitta yumo katika nafasi za juu.
Hata familia yake imeijenga vizuri sana kuanzia watoto hadi mama yake mzazi,
PUMZIKA KWA AMANI MH SITTA.
Wewe ni muongo na mnafiki kama huyo sita wakooooo,yuko kama huyu tuuu
 

Attachments

  • 1478937303483.jpg
    1478937303483.jpg
    12.6 KB · Views: 32
Alisaidia hata kututafutia nafasi wengine za kusoma, na tukaenda Zanzibar kwa ajili yake. Pengine isingekuwa Sitta kuunga mnyororo katika maisha yetu tusingekuwa wabunge au wanasiasa leo hii. Sitta aliweza kuziba pengo la baba kwa sisi tuliyekuwa na pengo hilo.Namuomba Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pake panapostahili.
Inabidi umfuate mkazikwe nayee alikuwa mnafiki tuuuualituharibia katibaa.
 
Aliyo yazungumza ZZK ni msg nzuri hasa kwa huyu Mama Naibu Spika.
Kwamba anapojaribu kuligeuza Bunge hivi sasa kuwa ni sehemu ya kupitisha kila jambo la serikali sio ivyo marehemu Sitta alivyokuwa akitenda.
Wakati wa Sitta mara kadhaa mawaziri waliamriwa kurudia kujibu maswali kwa yale majibu ambayo walikuwa wameyatoa kwa kiwango cha kutoridhisha, pamoja na mengine mengi yaliyoliweka bunge kwenye hadhi ya juu.
Lakini Mama Naibu Spika tofauti kabisa, amekuwa pale kulinda mawaziri, kukandamiza wapinzani, kupindisha kanuni nk nk.
Mama Naibu Spika ajaribu kujiuliza yeye ndie angekuwa amefariki kama Sitta ivi sasa.. Je angepata credibility ya kuingizwa bungeni namna ile ya jana na kuzungumziwa vizuri na wabunge wa pande zote?? Au wengine ndio wangepishana na jeneza lake kutoka nje..!!??
Atafakari.
 
Back
Top Bottom