Zitto: Nitafanya maamuzi kuhusu hatima yangu CHADEMA mwezi Machi, 2015

Status
Not open for further replies.
Akitangaza kujitoa CDM, angalia magazeti ya kufungia vitumbua yatakavyosema: Zitto aipasua CDM; ahama na zaidi ya nusu ya wafuasi wa CDM.
 
Chadema ndiyo wanaotakiwa kumuomba msamaha zitto kwanza wanajua kuwa bila zitto hakuna chadema kwahiyo lazima wampigie magoti zitto wapende wasipende.
Hivi wewe Dada akili yako iko sawa, kipi kilichosimama toka Zitto kapigwa chini? CCM mtaacha upumbavu huo lini maana kuna vitu mnaandika kama mmekatwa vichwa vile?
 
Zito huaminiki hata kidogo tena! Wewe ni mtu wa kupenda 'mlungula' sana!hata ya escrow fuu ni kuwa ulikosa mgao! Na yataanikwa mengi yakozaidi! Kumbuka issue ya CRDB na pesa ulizopeleka Ujermani kwa a/c a yule dada!
 
Zito ni muumini wa 'nyerereism' Zito yupi? thubutu! Huyu ni mtu wa kupiga 'madili' kwa sana hana lolote!Ukiona anapiga sana kelele ujue kakosa mgao!
 
Waswahili wanasema mti wenye matunda daima hupigwa mawe na zitto naamini ni mti wenye matunda kwa jinc anavopigwa mawe humu, kubali kataa zitto ni mwanasiasa mahiri na mpambanaji na athari zake zinaonekana wazi lazima tuwe wa kweli, hivi hapo chadema ni mwanasiasa gani unaweza kumlinganisha na zitto kwa kujenga hoja zenye akili na usimamizi wa mambo?watu mnakariri zitto msaliti mkiulizwa usaliti wake ni upi eti alitaka kumpindua mbowe kwenye nafasi yake ya uenyeketi sasa ndo usaliti huo jamani, kwa hyo ukawa wanavopanga mipango ya kuwang'oa ccm ili kuchukua nchi nao tuite ni usaliti?
 
Jimboni kwake ndio walimtoa kisiasa sasa anahamia twitter kupiga kampeni! ha ha ha haaaaassaaaaaaaaaaa! Wananchii wake kwa kheri maana watakaokuwa huko twitter! hawazidi 10
 
Kama kuna mwanasiasa anadhani anaweza kupata mafaniko kupitia siasa za mitandaoni anapoteza mda,ukweli ni kwamba wapiga kura wenye access ya mitandao ni chini ya 10%.wapiga kura halisi wako vijijini.
 
Zitto malizana na viongozi wako wa chama uingie mzigoni...la sivyo ndiyo basi tena!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu lakini kumbuka ACT ni sawa kikundi cha wahuni wachache wavuta bangi hivyo kimekufa hata kabla ya wakati wake, Zitto akienda ACT atazidi kujiharibia tu.

Mkuu,
Hicho kikundi yasemekana yeye ndiye muasisi wake lakini
 
Waswahili wanasema mti wenye matunda daima hupigwa mawe na zitto naamini ni mti wenye matunda kwa jinc anavopigwa mawe humu, kubali kataa zitto ni mwanasiasa mahiri na mpambanaji na athari zake zinaonekana wazi lazima tuwe wa kweli, hivi hapo chadema ni mwanasiasa gani unaweza kumlinganisha na zitto kwa kujenga hoja zenye akili na usimamizi wa mambo?watu mnakariri zitto msaliti mkiulizwa usaliti wake ni upi eti alitaka kumpindua mbowe kwenye nafasi yake ya uenyeketi sasa ndo usaliti huo jamani, kwa hyo ukawa wanavopanga mipango ya kuwang'oa ccm ili kuchukua nchi nao tuite ni usaliti?

Umairi wa zitto ni nini kupiga kelele kwenye ishu zisizokuwa na mwisho bro, Tanzania tunataka mabadiliko na sio kuimba nyimbo za ufisadi kila siku, ufisadi so what. Kila siku tunaenda bungeni na kashfa za ufisadi ndio umaarufu huo, \

Watanzania tunataka system ambayo iko well organized which can make mabadiliko, tunahitaji system ambayo italeta mabadiliko kama mtu awezi kuingi kwenye system akafilie mbali,

naongea kwa uchungu sana,Brother devcon hata kama mama yako yuko na shida utakuwa ni ujinga na upumbavu kwa mtoto kuwaita majirani na kuwaeleza udhaifu wa baba yako na mama yako ....and this is one of the reason ambayo siku zote huwa namuona huyu jamaa kwangu ni Hopeless .............kama kweli kulikukuwa na shida chadema ambazo yeye anayejihita msafi alichukua hatua gani za kuziadress kama sikuwatumia wale vijana kusambaza propaganda with backup from CCM na anfanya hivyo kwa lengo la kuwafurahisha CCM(wafadhili wake )

kaka Tanzania tunataka mabadiliko na sio Umaarufu wa @Dr slaa ama Zitto, umarufu wa Dr slaa is nothing to me, JK alikuwa maarufu tupepata nini watanzania zaidi ya misemo ya za kupewa changanya na za kwako, pesa za madafu etc

Watanzania tuungane pamoja tuweze kulitoa hili taifa kwenye mikono ya wachache na kuurudisha madarka kwa wanchi na sio kwa wachache wenye nguvu

Tafakari

  1. Labda tukumbushane toka huyo jamaa kasimamishwa wapi umesikia propaganda za udini, Je propaganda imechuja au waliofukuzwa ndio waliokuwa wameibeba na wameondoka nayo
  2. Tukumbushane toka hawa jamaa wameondoka lini umesikia propaganda ya ukabila, Je chadema hakuna wahaya, hakuna wapare, hakuna wasukuma, hakuna wanyeramba na wengine wengi, Je waliokuwa na kabila ni zitto kitilana na mwigamba JIbu ni NO
  3. Tukumbushane toka hawa jamaa wamefukuzwa lini umesikia propaganda ya ukanda, nani basi alikuwa mratibu wa uchafu huu ambao ulikuuwa unatugawa watanzania

tutafakari kwa utulivu kabis then uchukue maamuzi, maana hakuna mabadiliko pasipo kufanya maamuzi na maamuzi lazima yawe magum na yenye kuwaumiza hata baadhi ya watu

 
Kama kuna mwanasiasa anadhani anaweza kupata mafaniko kupitia siasa za mitandaoni anapoteza mda,ukweli ni kwamba wapiga kura wenye access ya mitandao ni chini ya 10%.wapiga kura halisi wako vijijini.

kati ya lema na zitto nani maarufu?
 
Kwa namna Zitto alivyosaliti mabadiliko ya nchi hii katika kipindi muhimu hata anihakikishie uwaziri kwa kura yangu moja,akiwa nje ya Chadema hataipata tena ya kwangu na familia yangu ntakuwa nimetimiza wajibu wangu hata kama wengine mtampigia.
 
kuwa na followers laki 2 its not a big deal. Amekiuka misingi ya maadili atafute suluhisho kwa kuomba radhi akishindwa atoke watu wengine wataendeleza alipoachia.
Akifanya kampen chafu twitter sisi tutafanya mitandao mingine najua atapumzika na siasa akimbie nchi akaishi ughaibuni
 
Tuliokuwa chadema kwa kufuata Agenda tulishaondoka maana kwa sasa hakuna tena Agenda ndani ya Chadema,mambo yanaenda kwa kufuata mtu mmja alie feli shule.
Think tank ya chadema kwa sasa iko passive,hivyo hakuna jipya zaidi ya kugawana kinachopatikana.

wazalendo kama Zitto waliojitolea kuusema ukweli wakatungiwa tuhuma na kupewa kitengo cha mitandao ya kijamii chini ya Ben saanane na Yeriko Nyerere ili wachafue haiba ya Mzalendo Zitto Kabwe.

Mpaka sasa vihoja vinavyotolewa ni mwendelezo wa kujitoa ufahamu .

Werevu tumehama na kujiunga na chama cha wazalendo.
 
mbowe na slaa tumbo joto wakisikia zito anataka kuongea. mimi chadema niliwadharau sana walipohamishia bifu mpaka kwenye msiba
 
Hii nchi ina wajinga wengi sana...

hivi nani alieturoga?

Yaani mnaambiwa Slaa na Mbowe walinajisi katiba na kufuta ukomo wa madaraka,lkn hamuhoji...


Slaa na Mbowe wanatumia vibaya fedha za chama na ktk hili Shonza alisema jinsi Slaa anavyojikopesha bila kurejesha na Slaa alikiri kukopa fedha mbele ya waandishi wa habari lkn mnajifanya vipofu...


Zitto aliwahi kusema kuwa vyama vya siasa havijakaguliwa ...Slaa akaja juu kuwa Zitto katumwa lkn tukashuhudia jinsi CAG alivyowaanika kwa kuambulia hati yenye mashaka lkn mmepofuka macho....

Mbowe alituhumiwa na Zitto kupewa Fedha na wana ccm kama vile Nimrod Mkono na Rostam Azizi ili kukisaidia chama lkn Mbowe kwa ubinafsi wake akakikopesha chama fedha hizo akadai na akalipwa lkn kimya sana mnajifanya hamliini hili..


Mbowe Alituhumiwa na Zitto Kucheza dili na Kinana kuhusu wizi wa fedha za umma za NSSF na Mbowe akatishia kumpeleka Zitto Mahakamani lkn mpaka hajaenda mahakamani ......mmewahi kumuuliza Mbowe kwanini mpaka sasa anaogopa kwenda Mahakamani?


Mbowe alitudanganya kuwa halitaki gari la mkuu wa kambi ya upinzani KUB na kutamba Bungeni kupitia TBC kuwa kutumia V8 ni Matumizi mabaya ya fedha za Umma lkn chakushangaza eti akalifuata kimya...kimya bila hata kuutarifu umaa halafu bado mnamuamini?


Mbowe na Slaa ndio waliinadi ilani ya Chadema nchi nzima kuwa ,chadema
kinapinga posho na hivyo msimamo wa chama ukawa kupinga posho lkn cha Ajabu ni kuwa Chadema nzima walisaliti makubaliano wakiongozwa na Mbowe isipokuwa Shujaa Zitto Kabwe ndio alitii agizi la chama kwa vitendo,......Aibu ya mbowa akamua kumtungia tuhuma ili kuharibu Usafi wake.

Nina mengi ya kusema kuhusu usaliti wa Mbowe na Slaa na Uadilifu wa Zitto Kabwe,lkn niishie hapa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom