MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,975
Ukweli husemwa:
Ni haki yake kikatiba na fikra ni za kwake bila kujali ametumia kigezo gani kujua kama anazo hizo sifa anazozitaja na kama ndizo pekee zinatosha kwa Mtanzania kuwa Raisi wa Tanzania.
Kama ilivyo CCM, pia katika CHADEMA, kulitaja swala la URAISI ni taboo au kwa lugha nyingine 'NO GO ZONE' achilia mbali kusimama na kusema unataka kuwa Raisi. Sababu kuu ni fikra za wapenzi na wanachama wa vyama hivi kuwa na imani na tumaini kuwa Raisi ajaye lazima atatoka tu katika chama chao. Fikra hizi zimezaa makundi na misuguano ndani ya vyama hivyo.
Zito anapata mashambulizi makali siyo tu kwa sababu anaonekana ni tishio na kizingiti katika makundi mengine ndani ya chama chake bali pia kwa vyama vingine vinavyoinyemelea hii ofisi kuu nchini
Itanishangaza kama Mzee Mapesa (John Cheyo) akisimama na kusema anataka kuwa raisi kama atapata mashambulizi makali kama haya anayoyapata Zito Kabwe kwa sababu jamii katika makundi hayo inamuona kama siyo kizingiti kikubwa kufikia lengo lao.
Tutasikia na kuona mengi na Zito Kabwe hatakuwa wa kwanza na wa mwisho kutamka kama anaitaka hii ofisi kuu nchini kabla ya michakato ya kumtafuta huyo mwanachama ndani ya vyama kuanza.
Yetu Macho na Masikio.
Ni haki yake kikatiba na fikra ni za kwake bila kujali ametumia kigezo gani kujua kama anazo hizo sifa anazozitaja na kama ndizo pekee zinatosha kwa Mtanzania kuwa Raisi wa Tanzania.
Kama ilivyo CCM, pia katika CHADEMA, kulitaja swala la URAISI ni taboo au kwa lugha nyingine 'NO GO ZONE' achilia mbali kusimama na kusema unataka kuwa Raisi. Sababu kuu ni fikra za wapenzi na wanachama wa vyama hivi kuwa na imani na tumaini kuwa Raisi ajaye lazima atatoka tu katika chama chao. Fikra hizi zimezaa makundi na misuguano ndani ya vyama hivyo.
Zito anapata mashambulizi makali siyo tu kwa sababu anaonekana ni tishio na kizingiti katika makundi mengine ndani ya chama chake bali pia kwa vyama vingine vinavyoinyemelea hii ofisi kuu nchini
Itanishangaza kama Mzee Mapesa (John Cheyo) akisimama na kusema anataka kuwa raisi kama atapata mashambulizi makali kama haya anayoyapata Zito Kabwe kwa sababu jamii katika makundi hayo inamuona kama siyo kizingiti kikubwa kufikia lengo lao.
Tutasikia na kuona mengi na Zito Kabwe hatakuwa wa kwanza na wa mwisho kutamka kama anaitaka hii ofisi kuu nchini kabla ya michakato ya kumtafuta huyo mwanachama ndani ya vyama kuanza.
Yetu Macho na Masikio.