Zitto na Muhongo Live on BBC; ni kuhusu mafuta na gesi

Zitto,
Utaandikaje sera kama hujui mikataba mliyo nayo ina kasoro gani? Katika tume ya Bomani kwa nini hamkupendekeza mikataba ibadilishwe? Kuna uoga gani Tanzania kubadilisha mikataba wakati hii imeshafanyika Australia na hata Congo baada ya Mobutu kupinduliwa? Unasema anachotaka kufanya profesa Muhongo kimewahi kufanywa huko nyuma lakini haujaona manufaa, na hii ni kwa sababu hamkutoa mapendekezo yeyote ya mabadiliko yafanyike kwenye mikataba. Muache profesa apitie mikataba yake huenda akaja na mapendekezo mapya wakati ninyi mlishindwa kubadilisha mikataba ya madini katika tume ya Bomani. Hata kama mikataba itawekwa wazi, then what? Lakini inaonekana unataka kumkatisha tamaa hata kabla ya zoezi lake kuanza. Give him time, and the benefit of the doubt.

Nadhani mnapata tabu sana kumuelewa Zitto juu ya mapitio ya mikataba. Anasema jambo hilo lishafanyika zaidi ya mara moja na hakuna kilichofanyika kwa hiyo agizo hilo ni marudio ya kilichowahi kufanyika hapo au kwingineko.

Kama kweli lishawahi kufanyika hakuna haja ya kurudia hilo isipokuwa kupitia records na hivyo lile lililokusudiwa kufanyika kutokana na findings hizo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mikataba hiyo inaacha kuwa labelled siri nzito.
 
Labda tu kwa kuongezea ni kwamba yule mtanzania aliyeteuliwa na barrick kuwa meneja pale tulawaka mine ndio alikuwa meneja wa mgodi maarufu wa almasi pale botswana na labda leo Profesa na akina Zitto wangemtafuta na kukaa nae kumuuliza kuhusu jinsi gani hiyo mikataba ilivyo.
 
labda anachotaka zitto kuwa mikataba iwekwe wazi ni kutaka kujua nani alituingiza kwenye mikataba mibovu na kwa kiasi gani!!!ni kama zitto ana shida ya kumjua mchawi ni nani?labda hili ni agizo la jk kupitia kwa zitto kutaka kuwaambia wananchi utawala uliopita ndio wamesababisha madudu yote haya...or may be my mind is playing tricks on me.
 
Kufanya mapitio ya mikataba kupitia TPDC ni kucheza makidamakida. TPDC ndio iliyoingia mikataba hiyo. Prof alikuwa anafanya siasa ili kuwapa matumaini kuwa kuna jambo linafanyika. Ndio maana jumapili alisema 'mikataba mibovu tutaivunja' na siku mbili baadaye akageuka na kusema 'hatutavunja mkataba wowote'. Sasa unafanya review ili ufanye nini? ukikuta mkataba mbovu unafanya nini? Kwanini usiweke mikataba yote wazi na watanzania wa kila namna na wachambuzi wa mambo wakaichambua na kutoa maoni na kusema mikataba kadhaa haitufai kisha serikali ianze majadiliano nao waboreshe mikataba hiyo.
Bado ninaamini sana kuwa uwazi wa mikataba ndio suluhisho la ufisadi kwenye rasilimali zetu

Contracts review and transparency in contracts are NOT on Opposing sides...you can review contracts and then make them public!
 
ZZK anaulizwa anasema kila nchi ina utaratibu wake, lakini anaelezea Fiscal Regime, na anatoa mfano wa Botwsana, kakatizwa anaulizwa mapato ni mazuri au la, anarudi kwa Botwsana kuwa ni 50%, lakini makubaliana yao hakuna corporate tax na mrahaba hakuna, na SA mrahaba ni 0%, anasema tatizo kwa TZ ni kuwa hatuna wataalam wa kiuchumi kwa hiyo tunachopata ni kidogo, kwani kuna misaada mingi sana ya kodi, lakini tatizo la wataalam wa Geolojia hakuna, na akatolea misamaha mingi sana inatolewa katika sector ya madini.

Ona aibu ya viongozi wangu....Mimi nimejaa tele mtaalamu wa natural Resource Economics under training ya miaka zaidi ya kumi nikijifunza the management, economics and bio-enginering ya natural resources eti hatuna wataalamu! Duuh hii nchi bab kubwa kama hawafanyi inventory kwenye human resources zao tuwafanyeje na wanawapa tender watu wasio na ujuzi wowote? Nawafahamu wachumi zaidi ya sita wa Resource Economics eti kiongozi anathubutu kusema hatuna wataalamu?
 
Hao viongozi hawatakiwi kwenda mbali kwenye issue ya energy nimetoa thread na kuwapa hints za nini kinatakiwa kufanya thread yenyewe hata wachangiaji hawakuwepo eti watu wanakuja na siasa za hakuna wataalamu; aibu zingine jamani mziepuke maana wenzenu wanawachekeni..Wamewapa funds na technical assistance katika ku-train watu wenu lakini bado mnaongopa hadharani....No right to speak without research...Nchi hii inawataalamu kibao wa Resource Economics ila hawapewi nafasi...Rafiki yangu yuko pale Mzumbe University frustrated akipgwa majungu na ma-prof wa makaratasi kila siku eti watu mnakuja na lawama za ajabu...Zanzibar yupo Colleague wangu naibu katibu mkuu kasoma hiyo resource Economics hata yeye hafahamiki kama ss tulio madongo kuinama hamtujui? university of Dar yupo Dr. Razak na Dr. Mkenda nao hawajui la kufanya?
 
Hao viongozi hawatakiwi kwenda mbali kwenye issue ya energy nimetoa thread na kuwapa hints za nini kinatakiwa kufanya thread yenyewe hata wachangiaji hawakuwepo eti watu wanakuja na tararira hakuna wataalamu; aibu zingine jamani mziepuke maana wenzenu wanawachekeni..Wamewapa funds na technical assistance katika ku-train watu wenu lakini bado mnaongopa hadharani....No right to speak without research...Nchi hii inawataalamu kibao wa Resource Economics ila hawapewi nafasi...Rafiki yangu yuko pale Mzumbe University frustrated akipgwa majungu na ma-prof wa makaratasi kila siku eti watu mnakuja na lawama za ajabu...Zanzibar yupo Colleague wangu naibu katibu mkuu kasoma hiyo resource Economics hata yeye hafahamiki kama ss tulio madongo kuinama hamtujui? university of Dar yupo Dr. Razak na Dr. Mkenda nao hawajui la kufanya?

Mkuu, shukrani sana kwa taarifa, nafikri wana JF watakuwa wamekupata. Ila naomba hii post ZZK aipate kwa haraka sana, ili tuendelee kujadili!
 
WATU MNAOKULA NA KUSAZA HUKO KWA KUTAZAMANA VILEMBA VYA KI-CCM KICHWANI KWA NINI MTUTUKANISHIE TAIFA ETI HATUNA WATAALAM TENA WA TAALUM ZA MIAKA NENDA RUDI KIHIVI

Ni kuidharaulisha taifa letu kwenye vyombo vya habari vya kimataifa, ni

1. kudhalilisha watumishi wetu hodari serikalini ambao kila siku mawazo yao kamwe hayazingatiwi,

2. ni kutukana Tanzania Public Service Commission kwamba inafanya kazi ki-itikadi zaidi kiasi kwamba wakibaini kwamba ndani ya kundi la Wana-CCM na maswahiba wao kumekosekana utaalam sasa ni sawa tu na kusema kwamba Tanzania nzima haakuna wataalam,

3. Miaka zaidi ya 45 ya uhuru taifa kulilia wataalam wa michepuo hii ya kawaida tu kama vile uchumi na sheria ni kule kutukana uhuru wetu (tunaposema hivyo BBC ina maana siku mtu anapojitambulisha kokote duniani aanze kuonekana mbumbumbu sio)

4. Hakika niliumia sana sana nikikumbuka matukio ya nyuma, pamoja na utaalamu wangu, jinsi gani ilivyo ndoto kupata kazi katika serikali hii.

... hivi kwa nini wengine hatukubahatika kuwa WATOTO WA WAKUBWA au hata na uswahiba tu wa kihistoria za kifamilia n chama ili kidogo utaalam wetu uweze kuonekana na kuachiwa huru kufanya kazi kwa miongozo ya kitaaluma tu bila kuletewa vimemo vya kisiasa mezani kila kukicha??????????????

Utaalam kitu gani, ni utaalam gani huo uliokoseka Tanzania huo; mnakula na kusaza kodi zetu kwa kurushiana kwa kutazamana vilemba kichwani halafu bado mnoa ujasiri wa kututemea mate usoni eti hakuna wataalam ndani ya nchi hii na kusababisha sehemu kubwa ya fedha wanazotoa wawekezaji kupeperushwa kwenda Uwisi ...???

Nauliza ni utaala waaina gani huo mnaouzungumzia hapa wakati vijana tumetapakaa kila kona ya taifa hili bila ajira lakini vyeti vikiendelea kukusanya ukungu sandukuni, ni utaalam wa kitu gani hicho? Kumbe mmbwa aliyeshiba anaweza akawachezea wenzie wenye njaa kihivi!!!!!!!!!!!

Haki ya Mungu ....!!!!!!!!!!!!!!!!!!!


Ona aibu ya viongozi wangu....Mimi nimejaa tele mtaalamu wa natural Resource Economics under training ya miaka zaidi ya kumi nikijifunza the management, economics and bio-enginering ya natural resources eti hatuna wataalamu! Duuh hii nchi bab kubwa kama hawafanyi inventory kwenye human resources zao tuwafanyeje na wanawapa tender watu wasio na ujuzi wowote? Nawafahamu wachumi zaidi ya sita wa Resource Economics eti kiongozi anathubutu kusema hatuna wataalamu?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Hakika kauli hii inayogusa MASAULA YA UTAALAM NA NAFASI ZA AJIRA SERIKALINI viongozi wetu chonde msiendelee kututonesha kiasi hiki. Nilipotulia mahala na kuanza kukumbuka eti nilisikia gitu gani vile BBC; nusura nirukwe akili nikikumbuka tatizo la AJIRA ZA UPENDELEO NCHINI. Utaalam upi huo ...?????????????
 
An outright politically leaning Employment discrimination and 'equal opportunity for the chosen few SACRED COWS' is the bane for our country's most miserably selling off her chances to leap forward emphatically in tapping in our her large mix of very competent professionls in various fields as numerous of our numbers are daily forcefully swept into the periferral hand-and-mouth type of jobs where only 10% of their knowledge is at work.

Indeed we, most of the youth professionals now wallowing in abject poverty amid dormant skills application, are more than BITTER on this score selective employment opportunities thence we expect nobody to ever attempt to scornfully use this our undoing and most sensitive national challenge so leisurely like that at a radio talk shop or so!!!
 
Labda swali: kuweka mikataba wazi na watu wakaiona na kuipitia inasaidia vipi kubadilisha mikataba hiyo? Maana inaonekana tayari kuna mikataba mingi tu ambayo iko wazi na inajulikana kwa kina lakini haijabadilishwa? Au itasaidia kulinda mikataba mipya? Maana hata hilo linaweza kuwa na shida kwani kuweka tu wazi hakuguarantee kuwa mikataba itabadilishwa.

Lakini ili kuweka mikataba wazi si inabidi itangulie sheria kwanza yenye kutaka hiilo lifanyike? kuna juhudi gani sasa hivi bungeni za kufanya mabadiliko - ama ya Katiba - au ya Sheria ili kulazimisha mikataba (once concluded) kuwekwa wazi kwa wananchi kupitia? Kitu ambacho kinaleta swali jingine: Kama mikataba itawekwa wazi baada ya kuwa signed inasaidia nini hasa zaidi ya kuwaumiza watu mioyo tu maana mingine mingi (kama wa Dowans/Tanesco) imewekwa wazi lakini bado hakuna chochote kilichosaidia kutuokoa na gharama za bilioni 90 na ushee zinazokuja.

Kuwekwa wazi kwa mikataba kutasaidia vipi kubadilisha mikataba hiyo? Labda hapa likiwekwa sawa watu wataappreciate kwanini unapigania transparency.


Nadhani Zitto ana maanisha transparency in the sense that after negotiations, before signing the contact, the contract should be made public, preferably through Bunge. Most developed countries have mechanisms that allow contracts on strategic national assets be ratified by parliament or congress. Kwa sababu mikataba inapitishwa na bunge. Mapungufu yote yana kuwa wazi. The public/ civil society/ individual experts/interest groups get an opportunity to scrutinize the deal and then decide whether national interests have been met. So yes transparency is critical, and it does make a huge difference.
 
Nimewasoma makamanda wetu mkituletea habari hizi moja kwa moja.. Inasikitisha tu pale napowasoma viongozi wangu wanapojikanyaga wenyewe. Muhongo kashindwa kujibu kwa nini mikataba yote iliypopita haifuati sheria zilizowekwa na kamati ya kina ZZK. Muhongo ameshindwa kuwaeleza wananchi kwa Ufasaha kwamba Mrahaba hutolewa kwa asilimia 3 au 4 lakini hii haijumuishi Ubia waloingia baina ya nchi na shirika la ndani ambao unaweza kuwa asilimia 40 hadi 50. Muhimu zaidi kuliko yote ni Share kiasi gani nchi hiyo imechukua ktk Partnership na sii Mrahaba wa asilimia 3 au 4.

Kwa mkuu wangu ZZK kuhusiana na Corporate tax amekosea maana Botswana wanalipa isiyopungua asilimia 22 pamoja na Royalties ya asilimia 10, 5 na 3 kutokana na madini unayochimba. Kifupi Madini yanachangia asilimia 50 ya makusanyo ya mapato ya nchi hiyo. Mnaweza kupitia Google na kuandika - Is Taxation of Meneral in Botswana a success story? Mtakuta Pdf nzima inayoweza sana kutusaidia sisi ktk mikataba yetu. Kuna Page imesema hivi:-

• Taxes applicable to mining are royalties, corporate tax (22%) and withholding tax on dividends (7.5%).
•​
Royalties paid on gross market value @
–​
10% for diamonds
–​
5% for precious metals (gold, platinum etc.)
–​
3% for all others minerals.

•
Mining companies taxed using variable income tax rate (for all minerals except diamonds) using formula:
Annual Tax Rate = 70-1500/x, where x = taxable income/gross income
– Minimum rate is the standard corporate rate of 22% of the profit
• Tax Regime for diamonds requires negotiations on issues covering technical, financial and commercial aspects of the project.
•​
Immediate 100% write-off of capital.
• Unlimited carry forward of losses.
 
Nadhani Zitto ana maanisha transparency in the sense that after negotiations, before signing the contact, the contract should be made public, preferably through Bunge....So yes transparency is critical, and it does make a huge difference.

Kwanini umefikiria anamaanisha hivyo? hakuna shaka hata kidogo transparency if critical lakini believe me Tanzania is not lacking in transparency. We know quite a lot to be frank. What don't we know about our government and its undertakings? Labda tunajua zaidi hadi vinavyotokea kwenye mahoteli wanapokutana wakiamini ni siri! Lakini imetusaidiaje zaidi ya kutufanya tujue zaidi tu? Ni lazima iwe ni zaidi ya kujua zaidi au kufanya watu wajue zaidi. Maana ripoti za CAG zina tarehe, namba, akaunti na kiasi cha fedha.... every year!
 
Mikataba hii ni dhaifu na kufaidisha wageni maana wakati TANESC0 inakosa gesi wao wanauzia viwanda

Nchi inaingia gizani maana bei ya TANESCO na viwanda ni tofauti, lakini gesi yetu wenyewe...
 
Mwanakijiji:

Labda swali: kuweka mikataba wazi na watu wakaiona na kuipitia inasaidia vipi kubadilisha mikataba hiyo? Maana inaonekana tayari kuna mikataba mingi tu ambayo iko wazi na inajulikana kwa kina lakini haijabadilishwa?
Au itasaidia kulinda mikataba mipya? Maana hata hilo linaweza kuwa na shida kwani kuweka tu wazi hakuguarantee kuwa mikataba itabadilishwa.

Lakini ili kuweka mikataba wazi si inabidi itangulie sheria kwanza yenye kutaka hiilo lifanyike? kuna juhudi gani sasa hivi bungeni za kufanya mabadiliko - ama ya Katiba - au ya Sheria ili kulazimisha mikataba (once concluded) kuwekwa wazi kwa wananchi kupitia? Kitu ambacho kinaleta swali jingine: Kama mikataba itawekwa wazi baada ya kuwa signed inasaidia nini hasa zaidi ya kuwaumiza watu mioyo tu maana mingine mingi (kama wa Dowans/Tanesco) imewekwa wazi lakini bado hakuna chochote kilichosaidia kutuokoa na gharama za bilioni 90 na ushee zinazokuja.

Kuwekwa wazi kwa mikataba kutasaidia vipi kubadilisha mikataba hiyo? Labda hapa likiwekwa sawa watu wataappreciate kwanini unapigania transparency.


Zitto:
Kufanya mapitio ya mikataba kupitia TPDC ni kucheza makidamakida. TPDC ndio iliyoingia mikataba hiyo. Prof alikuwa anafanya siasa ili kuwapa matumaini kuwa kuna jambo linafanyika. Ndio maana jumapili alisema 'mikataba mibovu tutaivunja' na siku mbili baadaye akageuka na kusema 'hatutavunja mkataba wowote'. Sasa unafanya review ili ufanye nini? ukikuta mkataba mbovu unafanya nini? Kwanini usiweke mikataba yote wazi na watanzania wa kila namna na wachambuzi wa mambo wakaichambua na kutoa maoni na kusema mikataba kadhaa haitufai kisha serikali ianze majadiliano nao waboreshe mikataba hiyo.

Bado ninaamini sana kuwa uwazi wa mikataba ndio suluhisho la ufisadi kwenye rasilimali zetu.

Nionavyo mimi, uwazi wa mikataba ni mojawapo ya njia za kutusogeza kwenye ufumbuzi wa tatizo. Hii itasaidia kutufanya wananchi tuwe na nguvu ya kushinikiza mabadiliko. Ingawa Mwanakijiji inaonekana kama huridhiki na suala la uwazi pekee, lakini mi naamini hii itatufanya watanzania wengi tupate taarifa kwa wakati, hivyo hata tukiamua kushinikiza, wengi tuwe tunakijua tunachokidai, tofauti na hizo mnazozipata nyie za kwenye mahoteli, kwani sio watanzania wote tuna uwezo wa kufukunyua na kujua hawa wezi wetu wamejichimbia kwenye hoteli gani kufanya hizo dili za mikataba mibovu ya kutuibia. Au, Mwanakijiji wewe ulikuwa unapendekeza njia ipi muafaka???
 
Back
Top Bottom