Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,191
- 4,103
Na Mwandishi Wetu, Kilwa
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema sasa ni wakati mwafaka kwa Benard Membe kujiunga na upinzani rasmi hapa nchini.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kilwa, Zitto alisema mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa mbunge na waziri wa wizara nyeti hapa nchini ana fursa ya kuunganisha Watanzania wenye kiu ya mabadiliko kupitia vyama mbadala vya siasa.
"Ndugu yangu Benard Membe kafukuzwa uanachama wa CCM. Ninajua bado anatetea haki yake ya uanachama huko. Ni hatua sahihi.
"Hata hivyo muda wa kuleta mabadiliko katika nchi umewadia, ninamsihi afanye maamuzi ya kuunganisha nguvu kupitia vyama mbadala ili kuwapa Watanzania Mabadiliko wanayoyataka," alisema.
Kiongozi huyo wa ACT ambaye yuko katika ziara ya kichama ya mikutano ya ndani Kusini mwa Tanzania, alisema anaelewa mwanasiasa huyo bado anapambana kubaki ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) lakini muda huu anahitajika zaidi kwenye upinzani.
Membe, mmoja wa wanasiasa mashuhuri nchini, alifukuzwa uanachama wake CCM miezi michache iliyopita na hali yake kwa sasa iko kwenye sintofahamu.
Akizungumza na redio moja ya kimataifa hivi karibuni, Membe alisema ingawa kwa sasa bado anaangalia hatma yake ndani ya CCM, upo uwezekano wa kuwania Urais kupitia vyama vingine mbadala.
Lakini, katika mkutano huo wa Kilwa; Kusini mwa Tanzania anakotokea Membe, Zitto alisema historia itamhukumu vibaya mwanasiasa huyo endapo hatafanya uamuzi wa kujiunga na upinzani sasa.
"Mimi najua Membe anaipenda Tanzania na ni Mwana demokrasia.
Adhihirishe mapenzi yake kwa nchi yetu kwa kuongeza nguvu wa vyama mbadala.
"Kama kuna kosa la uhaini basi itakuwa ni kwa Membe kutofanya maamuzi ya kuwatumikia Watanzania nje ya CCM. Ninamsihi kuwa afanye tafakari na kufanya maamuzi sahihi na wananchi," alisema Zitto huku akishangiliwa na umati uliohudhuria mkutano huo.
Membe amegeuka kuwa mmoja wa wakosoaji wa utawala wa Rais John Magufuli, akikosoa hadharani mambo anayodhani hayako sawa kiutawala.
Ukosoaji huo umemjengea umashuhuri mkubwa kiasi kwamba sasa anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa wanaotajwa kuweza kuwania Urais wa Tanzania kupitia upinzani ( vyama mbadala) mwezi Oktoba mwaka huu.
Zitto anaendelea na ziara yake ya mikoa ya Kusini.
Mwisho
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema sasa ni wakati mwafaka kwa Benard Membe kujiunga na upinzani rasmi hapa nchini.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kilwa, Zitto alisema mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa mbunge na waziri wa wizara nyeti hapa nchini ana fursa ya kuunganisha Watanzania wenye kiu ya mabadiliko kupitia vyama mbadala vya siasa.
"Ndugu yangu Benard Membe kafukuzwa uanachama wa CCM. Ninajua bado anatetea haki yake ya uanachama huko. Ni hatua sahihi.
"Hata hivyo muda wa kuleta mabadiliko katika nchi umewadia, ninamsihi afanye maamuzi ya kuunganisha nguvu kupitia vyama mbadala ili kuwapa Watanzania Mabadiliko wanayoyataka," alisema.
Kiongozi huyo wa ACT ambaye yuko katika ziara ya kichama ya mikutano ya ndani Kusini mwa Tanzania, alisema anaelewa mwanasiasa huyo bado anapambana kubaki ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) lakini muda huu anahitajika zaidi kwenye upinzani.
Membe, mmoja wa wanasiasa mashuhuri nchini, alifukuzwa uanachama wake CCM miezi michache iliyopita na hali yake kwa sasa iko kwenye sintofahamu.
Akizungumza na redio moja ya kimataifa hivi karibuni, Membe alisema ingawa kwa sasa bado anaangalia hatma yake ndani ya CCM, upo uwezekano wa kuwania Urais kupitia vyama vingine mbadala.
Lakini, katika mkutano huo wa Kilwa; Kusini mwa Tanzania anakotokea Membe, Zitto alisema historia itamhukumu vibaya mwanasiasa huyo endapo hatafanya uamuzi wa kujiunga na upinzani sasa.
"Mimi najua Membe anaipenda Tanzania na ni Mwana demokrasia.
Adhihirishe mapenzi yake kwa nchi yetu kwa kuongeza nguvu wa vyama mbadala.
"Kama kuna kosa la uhaini basi itakuwa ni kwa Membe kutofanya maamuzi ya kuwatumikia Watanzania nje ya CCM. Ninamsihi kuwa afanye tafakari na kufanya maamuzi sahihi na wananchi," alisema Zitto huku akishangiliwa na umati uliohudhuria mkutano huo.
Membe amegeuka kuwa mmoja wa wakosoaji wa utawala wa Rais John Magufuli, akikosoa hadharani mambo anayodhani hayako sawa kiutawala.
Ukosoaji huo umemjengea umashuhuri mkubwa kiasi kwamba sasa anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa wanaotajwa kuweza kuwania Urais wa Tanzania kupitia upinzani ( vyama mbadala) mwezi Oktoba mwaka huu.
Zitto anaendelea na ziara yake ya mikoa ya Kusini.
Mwisho