Zitto, Makamba na mwakilishi wa TANESCO ndani ya mdahalo wa Star Tv

SG8

JF-Expert Member
Dec 12, 2009
3,955
2,125
Wakuu hivi punde Star Tv wametangaza kuwa Jumapili ya tar 16.10.2011 kutakuwa na Mdahalo kuhusu Nishati na Tanzania tuitakayo. Mdahalo utaongozwa na Rosemary Mwakitwange kuanzia saa 3.00 mpaka saa 5.00 Usiku.

Washiriki ni Zitto Kabwe (Mb), William Mhando (CEO-Tanesco), January Makamba (M/kiti-Kamati ya Bunge nishati na Madini) na Eliakim Maswi (Jairo wa sasa i.e Kaimu Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini)

LIVE TEXTS:
  • Mwakilishi TANESCO: Sisi ni watumishi wa watanzania, sisi si waheshimiwa.
  • Zitto: Tumebwagwa kwenye kesi ICC na hata Mahakama Kuu ya Tanzania. TANESCO haistahili kubebeshwa deni la DOWANS.
  • Zitto: Hakuna tofauti ya DOWANS na Symbion, tofauti moja inatoka Marekani (Symbion) na nyingine haitoki Marekani. Terms ni zilezile.
  • Makamba: TANESCO wanajitahidi kupunguza upotevu wa umeme kutoka 21% mpaka 14% ifikapo mwaka 2014
  • Makamba: Haina haja ya kubadilisha gari, masuala haya tuyazungumze kwakuwa yanazungumzika.
  • Marcus (LHRC): Ili miaka 50 ijayo tupate umeme wa uhakika, basi kwa mujibu wa katiba serikali inaposhindwa tuchukue hatua za kuiwajibisha serikali hii, hatuwezi kuvumilia kuendelea hivi.
  • Dr. Kitila: Kuna tofauti gani kati ya Symbion na DOWANS?
  • Dr. Kitila: Kulalamika na kupiga kelele ni sehemu ya kazi ya mbunge kwa niaba ya wananchi.
  • Dr. Kitila: January, kama gari lililotubeba limeelemewa, unaonaje mkikabidhi gari jingine liendelee na safari?
  • Dr. Kitila: Kujumuisha maoni ya January na Zitto ni kuwa TUMESHINDWA.
  • Regia: Kama tumewafikishia wananchi 14% tu ya Tanzania kwa miaka 50, inakuwaje watudanganye kuwa miaka 3 ijayo tutawafikia 30% kwa ujumla?
  • Makamba: Maelezo ya Zitto ni sahihi. Kama waziri mwenye dhamana na Mwanasheria mkuu walishasema kuwa 'TULIPE' basi deni hili si la TANESCO bali serikali. Wanasheria wanaitumia kesi kama biashara.
  • Zitto: Tumebwagwa kwenye kesi ICC na hata Mahakama Kuu ya Tanzania. TANESCO haistahili kubebeshwa deni la DOWANS.
  • Zitto: Nitayaongea ninayoamini ni sahihi, mpende kuyasikia au msipende kuyasikia juu ya DOWANS.
  • Zitto: Turuhusu wazalishaji na wasambazaji binafsi kwenye sekta ya umeme
  • Zitto: Athari za mgao wa umeme kwa watu wa kima cha chini zinajidhihirisha wazi, ametoa mfano
  • Makamba: Ni afadhali kutokuwa waziri kuliko kuwa waziri ukawa unatoa kauli tata zisizotekelezeka
  • Makamba: Watu wanadai sisi tunaopigia kelele sana masuala haya tunatafuta uwaziri. Hapana, wanaokaa kimya labda ndo wanaoutaka uwaziri
  • Makamba: Hatuwezi kulazimisha mtu kujiuzulu, tutasema tunachoamini ni sahihi ili mtu ajihukumu mwenyewe.
  • Makamba: Kuna tatizo la ucheleweshwaji wa 'procurement' ndani ya TANESCO
  • Zitto: NSSF walienda kuangalia mwekezaji wa kushirikiana naye huko Marekani wakakuta hakuwa na ofisi, ikawa ni sawa na Richmond nyingine.
  • Zitto: Ukweli ni kuwa kilichoahidiwa bungeni juu ya kutatua tatizo la mgao hakijatekelezwa. Ni 37MW zilizozalishwa kati ya 207 zilizotakiwa. Wengine wote bado!
  • Mwakilishi TANESCO: Ni kweli TANESCO inapoteza 21% ya umeme uliozalishwa (wakati wa transmission) lakini tunatafuta ufumbuzi
  • Mwakilishi TANESCO: Katika hali ya kawaida mitambo ya haraka kubabiliana na hali tuliyo nayo ya mgao ni lazima iwe ya mafuta.
  • Mwakilishi TANESCO: Shirika lipo chini ya serikali, hivyo mwenye mali bado anaweza kuingilia maamuzi.
  • Zitto: Iwe marufuku wanasiasa kuingilia utendaji wa TANESCO
  • Zitto: Reform ya TANESCO ni jambo ambalo halina mjadala.
  • Makamba: Hatujawekeza vyema kwenye transmission system, tunapoteza umeme mwingi njiani kabla haujafika kwa watumiaji.
  • Makamba: Kwa miezi minne tu, TANESCO inaiomba serikali Bilioni 108 kuweza kuzalisha umeme (mzigo mkubwa)
  • Zitto: Utamaduni wa kulalamika tu hauwezi kutatua matatizo yetu, mimi (Zitto) na January ni mifano hai.
  • Zitto kaulizwa nani atatua tatizo la 'Poor Planning' na Mwakitwange. Kasema tuache kuainisha matatizo tu, tuanze kusuluhisha matatizo yenyewe.
  • Zitto: Tuna 'poor planning'. Hatutakiwi kuendelea kutegemea umeme wa mafuta wala wa maji.
  • Zitto: Tuna rasilimali za kutosha kuzalisha umeme, gharama ingepungua kama tungetumia gesi asilia na makaa ya mawe
  • Makamba: Kama mvua haitegemewi tena kwenye kilimo ni wazi haiwezi kutegemewa pia kwenye umeme!
  • Makamba: Hali si nzuri, uwekezaji umekuwa mdogo sekta hii na mipango haikuwa madhubuti
  • Makamba: Mwaka 1990 hatukuwa na mgodi hata mmoja, kwa sasa migodi ni 8 na inakula umeme sana.
  • Zitto: Hatujawekeza kwa miaka 10 wakati wa 'transition period' ya TANESCO kipindi cha ubinafsishaji.
  • Zitto: Kuna tatizo la kuingia kwenye mikataba inayotubana kiasi tunashindwa kujiondoa.
  • Zitto: Toka uhuru (miaka 50) tumewafikishia umeme watanzania asilimia 14 tu.
  • EWURA wamehudhuria, Zitto Kabwe na January Makamba wapo. Wizara haijapata mwakilishi na wala Mhando hajaja katuma mwakilishi (Engineer Maneno)
  • LHRC wamehudhuria pia, watapewa nafasi
 
Ni sifa zipi zimetumika kwa Zitto kuwa ktk huo mdahalo wakati yeye sio waziri kivuli wa nishati na madini?

Ukiangalia wajumbe wengine wote wana mahusiano ya moja kwa moja na mambo ya umeme. Hapo ni bora wafanye mabadiliko aende Mnyika ambaye hiyo ni wizara yake na Zitto asubirie siku ya wizara yake apambane na Mkullo
 
Mhmm kweli Tanzania inaongozwa na vipofu na viziwi, hivi kazi ya viongozi ni kufanya midahalo au kutenda kazi zionekane?

Kama si wapuuzi hawa watu basi ni wajinga nadhani mdahalo ungeweza kufanywa na academia na si watendaji! Umeme haupo na wao ndio viongozi mdahalo wanini badala ya kuleta umeme? Enyi Watanzania mtaendelea kuchaguwa hawa viongozi mbumbumbu hadi lini? Viongozi wa tume na uchunguzi na midahalo! Vipi nyie hamuoni aibu kulipwa kwa kodi za Watanzania kufanya kazi msiyoijuwa wala kuiweza?
 
Kweli hata mimi napendekeza waziri kivuli Mh John Mnyika akapambane na hao,maana ndo waziri kivuli wa wizara hiyo,any way kama kunamtu anajua vigezo vilivyotumika basi atuambie
 
Kweli hata mimi napendekeza waziri kivuli Mh John Mnyika akapambane na hao,maana ndo waziri kivuli wa wizara hiyo,any way kama kunamtu anajua vigezo vilivyotumika basi atuambie
kwani waziri wa nishati na madini atakuwepo??
by the way, Zitto alijikita kwenye madini na nishati long time.........mpaka mafisadi wakamnunulia hummer!!........sorry......sijasema mimi.
 
Zitto aje hapa jamvini aseme ni kwann aende yeye wakati waziri kivuli yupo? Hiki kitakuwa kimbele mbele na uroho wa madaraka. km kwenye midahalo tu anakuwa mroho hv je akipata huo urais si atakuwa anaenda hadi kwenye midahalo ya kata
 
Ni sifa zipi zimetumika kwa Zitto kuwa ktk huo mdahalo wakati yeye sio waziri kivuli wa nishati na madini?

Ukiangalia wajumbe wengine wote wana mahusiano ya moja kwa moja na mambo ya umeme. Hapo ni bora wafanye mabadiliko aende Mnyika ambaye hiyo ni wizara yake na Zitto asubirie siku ya wizara yake apambane na Mkullo

Zitto wa 2007 alikuwa bora kuliko Zitto wa 2010/11. Kuna kila dalili ya 'uswaiba' kati ya Zitto na January Makamba. Na kwa kiasi kikubwa huu uswaiba hauna manufaa kwa watanzania wa kawaida waliopigika kimaisha, ni wa 'ki-mtandao zaidi. Kwenye sherehe za Sudan ya Kusini Zitto alikuwa kwenye msafara na niliuliza kwa nini yeye na sio 'waziri kivuli'? Sasa kwenye mjadala wa nishati kwa nini yeye na sio waziri kivuli? Kamaliza kuchunguza UDA? Huu mng'aro wa Zitto CCM haujakaa vizuri hata kidogo!

Pili, Zitto ni waziri kivuli wa fedha, shilingi ya Tanzania inashuka thamani kila kukicha, uchumi unashuka bei za bidhaa zinapanda. Kwa nini Zitto asijishughulishe na mambo yanayomsuhu yeye moja kwa moja badala ya kuingiza pua kwenye ofisi za wengine? Zitto ana ujuzi gani wa ziada kwenye mambo ya umeme? kasomea umeme? Mnyika alialikwa kwenye huu mjadala akakataa?
 
Ni sifa zipi zimetumika kwa Zitto kuwa ktk huo mdahalo wakati yeye sio waziri kivuli wa nishati na madini?

Ukiangalia wajumbe wengine wote wana mahusiano ya moja kwa moja na mambo ya umeme. Hapo ni bora wafanye mabadiliko aende Mnyika ambaye hiyo ni wizara yake na Zitto asubirie siku ya wizara yake apambane na Mkullo

Mkuu kwa kweli umeuliza swali la msingi sana. Hapa ilikuwa John Mnyika awepo kwenye huo mdahalo. Labda ana udhuru ndio maana anaenda Zitto. Na kama hana udhuru na Zitto akapendekezwa na kukubali basi hapo kuna kashida manake ni kuingiliana katika madaraka.
 
Zitto wa 2007 alikuwa bora kuliko Zitto wa 2010/11. Kuna kila dalili ya 'uswaiba' kati ya Zitto na January Makamba. Na kwa kiasi kikubwa huu uswaiba hauna manufaa kwa watanzania wa kawaida waliopigika kimaisha, ni wa 'ki-mtandao zaidi. Kwenye sherehe za Sudan ya Kusini Zitto alikuwa kwenye msafara na niliuliza kwa nini yeye na sio 'waziri kivuli'? Sasa kwenye mjadala wa nishati kwa nini yeye na sio waziri kivuli? Kamaliza kuchunguza UDA? Huu mng'aro wa Zitto CCM haujakaa vizuri hata kidogo!

Pili, Zitto ni waziri kivuli wa fedha, shilingi ya Tanzania inashuka thamani kila kukicha, uchumi unashuka bei za bidhaa zinapanda. Kwa nini Zitto asijishughulishe na mambo yanayomsuhu yeye moja kwa moja badala ya kuingiza pua kwenye ofisi za wengine? Zitto ana ujuzi gani wa ziada kwenye mambo ya umeme? kasomea umeme? Mnyika alialikwa kwenye huu mjadala akakataa?

Kweli Zitto apelekwe kwenye mdahalo utakaozungumzia Tanzania na Thamani ya Shillingi Tuitakayo au Tanzania na aina za Posho Tuzitakazo na wala siyo huko kwenye Nishati. Au Zitto ni kiraka?
 
Manufaa ya huu mdahalo ni nini? Au Star TV wanatafuta airtime tuu? Yale yale ya kukaa na kuliongelea tatizo bila kulitatatua.
 
Manufaa ya huu mdahalo ni nini? Au Star TV wanatafuta airtime tuu? Yale yale ya kukaa na kuliongelea tatizo bila kulitatatua.

Hii ni porojo ya wazi, washiriki wa huo mdahalo watakuwa kwa namna moja au nyingine wanufaika wa hili giza
kama wameamua kuja kwa jamii wasema wazi ni nani katufikisha hapa na hatua atakazo chukuliwa sio hadithi
 
mimi nashindwa hata kusema maana tukisema tutaambiwa tuna zitophobiasis ama tunamchukia zito kutokana na dini yake me thithemi bhana
 
mimi nashindwa hata kusema maana tukisema tutaambiwa tuna zitophobiasis ama tunamchukia zito kutokana na dini yake me thithemi bhana

Kaka mm nasema tu penye ukweli bila kujali mambo ya dini mm mwenyewe ni dini hyo hyo ya zitto lakini hiki kimbele mbele chake kinakera sana bana.
 
Kweli Zitto apelekwe kwenye mdahalo utakaozungumzia Tanzania na Thamani ya Shillingi Tuitakayo au Tanzania na aina za Posho Tuzitakazo na wala siyo huko kwenye Nishati. Au Zitto ni kiraka?

Hapo patamu kaka atakuwa kiraka japo kajitwika mwenyewe.
 
Zitto aje hapa jamvini aseme ni kwann aende yeye wakati waziri kivuli yupo? Hiki kitakuwa kimbele mbele na uroho wa madaraka. km kwenye midahalo tu anakuwa mroho hv je akipata huo urais si atakuwa anaenda hadi kwenye midahalo ya kata

Hivi huu uwaziri-kivuli ni hadi nje ya Bunge? Mie naona kama ni mdahalo juu ya Nishati, kipindi cha bunge kilichopita Zitto alikuwa kwenye Kamati ya Nishati na an ufahamu wa matatizo haya tangia yalipoanzia hadi hapa tulipo.
 
Hapo patamu kaka atakuwa kiraka japo kajitwika mwenyewe.

Kaka mm nasema tu penye ukweli bila kujali mambo ya dini mm mwenyewe ni dini hyo hyo ya zitto lakini hiki kimbele mbele chake kinakera sana bana.

mimi nashindwa hata kusema maana tukisema tutaambiwa tuna zitophobiasis ama tunamchukia zito kutokana na dini yake me thithemi bhana

Mkuu kwa kweli umeuliza swali la msingi sana. Hapa ilikuwa John Mnyika awepo kwenye huo mdahalo. Labda ana udhuru ndio maana anaenda Zitto. Na kama hana udhuru na Zitto akapendekezwa na kukubali basi hapo kuna kashida manake ni kuingiliana katika madaraka.

Zitto wa 2007 alikuwa bora kuliko Zitto wa 2010/11. Kuna kila dalili ya 'uswaiba' kati ya Zitto na January Makamba. Na kwa kiasi kikubwa huu uswaiba hauna manufaa kwa watanzania wa kawaida waliopigika kimaisha, ni wa 'ki-mtandao zaidi. Kwenye sherehe za Sudan ya Kusini Zitto alikuwa kwenye msafara na niliuliza kwa nini yeye na sio 'waziri kivuli'? Sasa kwenye mjadala wa nishati kwa nini yeye na sio waziri kivuli? Kamaliza kuchunguza UDA? Huu mng'aro wa Zitto CCM haujakaa vizuri hata kidogo!

Pili, Zitto ni waziri kivuli wa fedha, shilingi ya Tanzania inashuka thamani kila kukicha, uchumi unashuka bei za bidhaa zinapanda. Kwa nini Zitto asijishughulishe na mambo yanayomsuhu yeye moja kwa moja badala ya kuingiza pua kwenye ofisi za wengine? Zitto ana ujuzi gani wa ziada kwenye mambo ya umeme? kasomea umeme? Mnyika alialikwa kwenye huu mjadala akakataa?

Kweli hata mimi napendekeza waziri kivuli Mh John Mnyika akapambane na hao,maana ndo waziri kivuli wa wizara hiyo,any way kama kunamtu anajua vigezo vilivyotumika basi atuambie

Kweli Zitto apelekwe kwenye mdahalo utakaozungumzia Tanzania na Thamani ya Shillingi Tuitakayo au Tanzania na aina za Posho Tuzitakazo na wala siyo huko kwenye Nishati. Au Zitto ni kiraka?

Guys nyie ndio ambao huwa mnaharibu credibility zenu, post zenu zote hazina hoja, hazina ujazo wala haziwezi kumsaidia mtu yeyote zaidi ya majungua ambayo unajua yanapikwa na wajinga fulani fulani hivi

1. Nani kaitisha mdahalo?
2,. Je walimualika Zito au alijialika?
3. Je walialika chadema kuwa wachague mtu na chadema imemchagua zito?
4. Je mdahalo ni lazima awepo waziri kivuli? criteria hii ana iset nani? zito au waandaaji
5. why zito?

kwenye maswala ya energy huwezi ukamfananisha Mnyika na Zito mtu yeyote ambaye hajui uhusika wa zito kwenye nishati lazima aidha kilaza au hajui!

Mnyika ni waziri yes, lakini kwenye upe wa nishati hamfikii Zito..tuseme ukweli

sijawahi kuona article, speech, au swala lolote la kutatua matatizo ya nishati ambayo Mnyika ameishawahi kuweka mezani ..hakuna

in other words output ya Mnyika kwenye energy issues iz zero whether is shadow minister or shallow minister

semeni lingine!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom