Zitto: Mahakama Kuu imetoa hukumu kuwa Rais wa Tanzania anaweza kushtakiwa kwa makosa ya uvunjaji wa Katiba

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Ameandika Zitto Kabwe:

"Mahakama Kuu imetoa hukumu kuwa Rais wa Tanzania anaweza kushtakiwa kwa makosa ya uvunjaji wa Katiba. Jaji Lameck Mlacha ametoa hukumu hiyo katika hukumu ndogo kwenye shauri nililofungua kumshtaki Rais @MagufuliJP kwa kumvua uCAG Prof. Assad. Shauri la msingi linaendelea"-Zitto Kabwe.
====


Leo Machi 18, 2020, Mahakama Kuu Nchini imeeleza kuwa Rais wa Tanzania anaweza kushtakiwa kwa makosa ya uvunjaji wa Katiba

Jaji Lameck Mlacha wa Mahakama hiyo ametoa hukumu hiyo katika hukumu ndogo kwenye shauri lililofunguliwa na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe dhidi ya Rais Magufuli

Zitto alifungua shauri Mahakamani hapo akidai Rais Magufuli alivunja Katiba baada ya kumteua Charles Kichere kuwa CAG akichukua nafasi ya Prof. Mussa Assad

Katika shauri hilo ambapo Zitto anadai CAG haondolewi kwenye nafasi hiyo mpaka astaafu, Serikali ilipeleka mapingamizi sita ambapo leo Mahakama imeyakataa. Shauri la msingi linaendelea
 
Kwenye kesi ya Wakurugenzi kusimamia uchaguzi Mahakama kuu iliwazuia wasisimamie uchaguzi Mahakama ya rufaa ikaja ikatengua uamuz wa Mahakama kuu. Hukumu za hizi mahakama naonaga ka mchezo wa draft mtu anakupa kete moja unachekelea kumbe amekuset anajua wapi atakupiga kete zako tatu
 
Ameandika Zitto Kabwe.
"Mahakama Kuu imetoa hukumu kuwa Rais wa Tanzania anaweza kushtakiwa kwa makosa ya uvunjaji wa Katiba.Jaji Lameck Mlacha ametoa hukumu hiyo katika hukumu ndogo kwenye shauri nililofungua kumshtaki Rais @MagufuliJP kwa kumvua uCAG Prof. Assad. Shauri la msingi linaendelea"-Zitto Kabwe.
Naogopa hata kucomment...mtukufu aweza kushtakiwa?? :eek:

Everyday is Saturday.....................:cool:
 
Ameandika Zitto Kabwe:

"Mahakama Kuu imetoa hukumu kuwa Rais wa Tanzania anaweza kushtakiwa kwa makosa ya uvunjaji wa Katiba. Jaji Lameck Mlacha ametoa hukumu hiyo katika hukumu ndogo kwenye shauri nililofungua kumshtaki Rais @MagufuliJP kwa kumvua uCAG Prof. Assad. Shauri la msingi linaendelea"-Zitto Kabwe.
Ni kweli Rais anaweza kushtakiwa akivunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo akivunja katika na ikathibitika hashtakiwi mahakamani bali bunge linaanza mchakato wa kumfanyia impeachment

Sent using Jamii Forums mobile app
 
basi tuanze ........ lakini nahofika shauri likifikia pale kwenye Rufani yaani Jajaji watatu ndipo kwenye shinda, kwa mfano mgombea binafsi iliamuliwa YES lakini hadi leo hakuna utekelezaji wowote ule.

Bado mahakama zetu haziko huru ki hivyo!!
 
Mweke ndani sasa ili asigombee hiyo October!! Zitto anatafutaga kukiki kinguvu anajua kabisa anatuchuria ila ashaona tz kunawapambe vizabizabina wengi wataomsifu.
Yeye atueleze mke wa Deo vp??
 
Back
Top Bottom