Zitto, Lipumba na mkakati wa kuidhoofisha CHADEMA

Huu ni utabiri kama wa tabiri nyingine tu na wasomaji wachukulie kama utabiri. Sina mazungumzo yeyote na chama chochote kuhusu kugombea Urais. Ni kweli nina ambition. Ambition zangu zimo ndani ya CHADEMA, chama ambacho nimeshiriki kukijenga.
Kumekuwa na juhudi za makusudi za watu kutaka nitoke CHADEMA, narudia tena siwezi kutoka. Narudia, sijawahi kuwa mwanachama wa chama kingine choochote maishani mwangu tofauti na CHADEMA. Narudia, zaidi ya nusu ya umri wangu nimeutumia CHADEMA. Nimetumia nguvu zangu, akili zangu na rasilimaliu zangu kusaidiana na wenzangu kujenga CHADEMA.
Kwamba nazungumza na NCCR ni uwongo, ni uzushi na propaganda yenye nia mbaya kwangu.
Sizungumzi na mtu yeyote kuhusu kuhujumu chama changu. Nimeshasema yeyote mwenye ushahidi na jambo hili autoe. Gazeti la Mwanahalisi lilitoa muda na namba za simu za watu ninaozungumza nao. Nimewachallenge waseme nilikuwa nazungumza nini. Watoe content ya mazungumzo na kama itaonekana kwa namna yeyote ile nilihujumu chama changu nitawajibika.
Watanzania wamekuwa na tabia ya kuamini mambo kwa mkumbo.
Uzushi dhidi yangu umekuwa ukichukuliwa na watu kama ukweli tena ukweli mtupu. Watu kwa malengo yao wamekuwa wakitumia majina zaidi ya moja kwa mtu mmoja na kuingia JF kuandika uzushi (kama huu wa leo) ili kunichafua na kunigombanisha na wenzangu. Bahati mbaya sana baadhi ya viongozi wenzangu wa chama wanachukua chuki, fitna na uwongo unaoandikwa humu kama ukweli. Inasikitisha sana.
Ninapenda kuwafahamisha wasomaji wote wa JF kuwa sehemu ya habari iliyoandikwa hapa katika thread hii ni uwongo wa makusudi dhidi yangu. Ni imagination ya mtu ambaye anaumwa ugonjwa wa ZITTOPHOBIASIS! Ugonjwa ambao watu wengi wanaumwa na ninasikitika kuwa dawa ya ugonjwa huu hata kwa babu haupo maana ni ugonjwa unasambazwa na ugonjwa wa chuki, fitna, na WIVU!

hapo umenena kiongozi. Mkapa alipendelea kusema uvivu wa kufikiri ambao wa tz wengi tunao. Chapa mzigo
 
niliwahi kueleza kwenye post nyingine jinsi ccm na intelijensia yao wanavyofanya mkakati wa kuidhoofisha chadema. Mkatati huu unahusu kutoa rushwa kwa watu wenye ushawishi katika jamii kuishambulia chadema kila mara kwa kudai kuwa chama hiki kinataka kumwaga damu, kuvuruga amani na umoja wa taifa.

Kwenye taarifa ya tbc1 leo asubuhi, wameweka habari ndefu ya mwenyekiti wa cuf, prof. Ibrahim lipumba, akitoa shutuma kali kwa chadema. Habari hiyo ya lipumba imepewa muda mrefu sana na kupambwa. Eti wameoneshwa baadhi ya wananchi (ingawa ni wachache) wa tandahimba "wakishindwa kuzuia hisia zao na kusukuma gari la lipumba." katika hali isiyo kawaida kwa tbc1 kuripoti mikutano ya wapinzani, eti baadhi ya wananchi wakahojiwa na kusema wanampenda sana lipumba na wamekuwa wanamsubiri kwa hamu. Likaoneshwa kundi dogo la wanafunzi wa primary kama 20 wanashangilia msafara wa cuf na mwandishi akasema eti kwenye kila njia lipumba alilazimika kusimama kuongea na wananchi waliokuwa na hamasa kubwa ya kumuona.

Umati ulikuwa wa watu kama mia 2 tu, si maelfu ya wananchi ambao huendaga kwenye mikutano ya chadema kumuona dk. Willibrod slaa. Lakini tbc1 wakataka kuonesha eti lipumba na cuf ni maarufu sana.

Anyway, kikubwa ni hotuba ya lipumba ambayo aliishambulia vikali chadema. Bila kuitaja chadema, alisema eti "kuna baadhi ya chama cha kisiasa cha kaskazini ya tanzania kinadhani kitatawala nchi nzima." akaongeza kuwa eti wananchi wakatae vyama vya siasa vinavyotaka kuvuruga umoja na amani ya nchi.

Ni dhahiri kuwa lipumba kwa kutumwa na ccm na intelijensia yao, anaendelea kuishambulia chadema kwa propaganda za kutungwa kuwa eti ni chama cha wachagga tu na kinataka kumwaga damu na kuleta udini.

Ukiacha cuf na lipumba, ccm na intelijensia yao pia mara nyingi wamekuwa wanawatumia viongozi wengine wa vyama vya upinzani kuishambulia chadema. Hawa ni pamoja na john cheyo wa udp, james mbatia wa nccr mageuzi, augustino mrema wa tlp na viongozi wengine.

Pia hivi karibuni wamemtumia mufti simba wa bakwata kuishambulia chadema lakini sisi waislamu wengi tumempuuza mufti huyu aliyekosa msimamo kwa kutumiwa na ccm.

Ccm wanacheza mchezo hatari sana wa kutumia dini kujaribu kupambana na chadema kisiasa. Hii sumu ya udini itakuja kuwatafuna watawala wenyewe siku moja.

Pia, baadhi ya vyombo vya habari vinaendelea kutumiwa kuishambulia chadema, mfano tbc1, mtanzania/rai (magazeti ya rostam aziz), jambo leo (gazeti la ridhwani kikwete, malegesi wa epa), channel ten (tv ya tanil somaiya wa kashfa ya rada) na wengineo.

hata hivyo, mkakati mkubwa kuliko wote uliobaki wa kuidhoofisha chadema ni kuhakikisha kuwa mabadiliko ya katiba wanayosema yatafanywa 2014, yatahakikisha kuwa umri wa kugombea urais unashushwa kutoka miaka 40 mpaka 35 au 37.

Lengo ni kumruhusu zitto kabwe wa chadema agombee urais mwaka 2015. Ccm na intelijensia yao wanajua fika kuwa zitto ana ambitions kubwa sana za kutaka kuwa rais wa tanzania. Zitto pia anajua kuwa bora agombee 2015 kuliko kusubiri 2020 kwani ni mbali na hawezi kuwa na uhakika kama atakuwa bado ana ushawishi kwani umaarufu wake umekuwa unaporomoka kwa kasi.

Zitto, ccm na intelijensia yao wanajua fika kuwa chadema kamwe haiwezi kumteuwa zitto kuwa mgombea wake wa urais mwaka 2015 hata kama katiba ikibadilishwa kuruhusu yeye kugombea.

Hivyo basi, zitto tayari ana makubaliano ya kimsingi na nccr mageuzi kuwa mgombea wa urais wa chama hicho kwenye uchaguzi wa 2015. Jitihada zinafanywa ili zitto aweze kuondoka na baadhi ya wabunge wa chadema na viongozi wengine wakubwa wahamie nccr mwaka 2015 ili kujaribu kuidhoofisha nguvu chadema.

Mkakati ni to "neutralise" chadema na kuidhoofisha ionekane kuwa chama hiki kinameguka na viongozi wake wanahamia nccr mageuzi.

Zitto amekuwa na mazungumzo ya siri ya mara kwa mara na ccm na intelijensia yao. Tayari imeripotiwa kuwa zitto amekuwa akiwasiliana kwa karibu na jakaya kikwete, rostam aziz na baadhi ya viongozi wa intelijensia (usalama wa taifa) kutoka tanzania intelligence and security services (tiss) ambao eti wanadhani kuwa jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kuwa ccm inaendelea kutawala milele.

Ccm na intelijensia yao wamepanga kufanya wizi mkubwa wa kura kwenye uchaguzi wa 2015 kama walivyofanya 2010. Ila safari hii watachakachua zaidi kura za wagombea wote wa urais wa vyama vya upinzani ili matokeo ya kupikwa ya uchaguzi wa 2015 yawe kama ifuatavyo:

1. Ccm of course kushinda urais na kuongoza kwa idadi ya wabunge
2. Zitto kuwa mshindi wa pili na nccr iwe chama kikuu kipya cha upinzani
3. Cuf iwe chama cha tatu kwa kura
4. Chadema itupiliwe mbali na kudaiwa eti ni chama cha 4 kwa umaarufu

lengo ni kuhakikisha kuwa ccm na intelijensia yao wanaimaliza kabisa chadema na wanakuwa wanamcontrol "kiongozi" mpya wa upinzani, zitto kabwe, na chama chake, nccr mageuzi.

Asalaam aleykum.


haka ka-thread kana harufu ya kuchanganya wana cdm na kuleta mfakano kwa makusudi. Kwanza (1) si amini kuwa zitto ndiye zitto mwenyewe anayejibu humu kwa kuwa nahisi ni mtu kajibandika jina hilo. (2) mleta hoja na wachangiaji walio wemgi wameingia kichwa kichwa ili kuhamisha ya ya uvccm cdm ili kuwa pumuzisha ccm na mtafaruku wao. (3) nashauri viongozi cdm na wana cdm kusimamisha malumbano haya kwa kuwa hayana tija bali mtoa hoja na baadhi ya watu wana lengo lao-kusambaratisha cdm. Usiku mwema.
 
Mkuu mtoa mada inaonekana anasema ukweli, na umeanza kuthibitisha kwa kukiri kuwa una ambition kwenye urais, tunamuamini mtoa mada kuwa una nia ya kukivuruga chama kwa maslahi ya chama cha upinzani ccm, kwa ambition ulizonazo unasomeka kujituma kutumia njia yoyote ikibidi kukivuruga chama, futa fikra za kuwa rais wetu, isipokuwa tumekuambia sisi watanzania, kwa mwenendo tunaokuona babo huko sawa.

unataka asiwe na ambition, hata nyani wana ambitions. Let's be serious we should have dreams in our life. Then we plan and execute to achieve those vision.
 
haka ka-thread kana harufu ya kuchanganya wana cdm na kuleta mfakano kwa makusudi. Kwanza (1) si amini kuwa zitto ndiye zitto mwenyewe anayejibu humu kwa kuwa nahisi ni mtu kajibandika jina hilo. (2) mleta hoja na wachangiaji walio wemgi wameingia kichwa kichwa ili kuhamisha ya ya uvccm cdm ili kuwa pumuzisha ccm na mtafaruku wao. (3) nashauri viongozi cdm na wana cdm kusimamisha malumbano haya kwa kuwa hayana tija bali mtoa hoja na baadhi ya watu wana lengo lao-kusambaratisha cdm. Usiku mwema.

good and well done.
 
Tumuogope nani wakati Mungu yuko upandewetu??

Heko sana Mpambanaji kwa taarifa hizo muhimu. Nadhani, kwa kuwa hivi sasa vyombo vyote vimegawanjika katikati kwa kusimama ama na wananchi au MAFISADI nchini kote tangu ndani ya CCM yenyewe, Ikulu, TISS, mashambani; hao wanaopanga njama dhidi ya umma wa Tanzania wasije wakajikuta ndani ya hilo shimo wanalochimbia wengine kwa sasa.

Enyi think-tank wa CHADEMA na walahoi nchini; mbinu zote za ushindi ziko wazi na ziko mikononi mwananchi mwenye; hii chess-board game mbona ni ngumu zaidi kwa mafisadi na wanafiki kuliko wale waliosimama kwenye mwanga???

Fine, CHADEMA may well be pushed into striking the jackpot sooner than later with these rising levels of ineptitude within a section of the daily thining political landscape
 
Kama viongozi wenzake Zitto wanaamini yanayosemwa humu lazima na yeye ajiulize why....Unless anaamini kuwa na wao pia wana chuki binafsi dhidi yake...

At the same time, hata yeye Zitto kama ilivyo kwa viongozi wenzake, anajua kuwa si kila lisemwalo humu JF ni uongo ama uzushi...Just kama ilivyo kuwa si kila libandikwalo humu ni ukweli.Na kama anaona ni uzushi,basi ni jukumu lake ku waprove wrong na si kushabikia hatua ambazo zinashabikiwa na ccm.

Halafu pia ajiulize kwanini wengi wanaompa sapoti ni maadui wa chama chake....Kina Mr Mark,Majimshindo,waberoya,Kinja,Mji Mpya,Kadogoo na wengine wote wenye mwelekeo wa kifisadi fisadi humu,na wenye chuki za wazi na chama chako...Wakishabikia eti unaonewa kwasababu wewe ni musilam,nk.
Kiutaratibu,mtu ukiona mwezako anapewa sapoti na adui yako utafikiria vipi?Ni maswali simpo tu ya kutumia common sense kuliko kukurupuka na kusema kila kitu ni chuki binafsi...Kama ulifikia hapo ulipo bila matatizo,then lazima sasa utakuwa umebadilika,maana wao labda wanaona wewe si Zitto yule yule mpambanaji.

Halafu wengine sio wananchama wa chama chochote cha siasa,however tunaweza kuona yanayoendelea kama ni kinyume na msimamo wa chama chako,na fikra za wananchama na viongozi wenzako,halafu mambo hayo yanafurahiwa na maadui wenu/wao ie ccm,cuf nk,unategemea uchekewe tu?Sidhani kama watafanya hivyo.

Tumieni akili sometimes si kila mtu ni mjinga,na pia si kila mtu anachambua issue humu kiushabiki.
 
Huu ni utabiri kama wa tabiri nyingine tu na wasomaji wachukulie kama utabiri. Sina mazungumzo yeyote na chama chochote kuhusu kugombea Urais. Ni kweli nina ambition. Ambition zangu zimo ndani ya CHADEMA, chama ambacho nimeshiriki kukijenga.
Kumekuwa na juhudi za makusudi za watu kutaka nitoke CHADEMA, narudia tena siwezi kutoka. Narudia, sijawahi kuwa mwanachama wa chama kingine choochote maishani mwangu tofauti na CHADEMA. Narudia, zaidi ya nusu ya umri wangu nimeutumia CHADEMA. Nimetumia nguvu zangu, akili zangu na rasilimaliu zangu kusaidiana na wenzangu kujenga CHADEMA.
Kwamba nazungumza na NCCR ni uwongo, ni uzushi na propaganda yenye nia mbaya kwangu.
Sizungumzi na mtu yeyote kuhusu kuhujumu chama changu. Nimeshasema yeyote mwenye ushahidi na jambo hili autoe. Gazeti la Mwanahalisi lilitoa muda na namba za simu za watu ninaozungumza nao. Nimewachallenge waseme nilikuwa nazungumza nini. Watoe content ya mazungumzo na kama itaonekana kwa namna yeyote ile nilihujumu chama changu nitawajibika.
Watanzania wamekuwa na tabia ya kuamini mambo kwa mkumbo.
Uzushi dhidi yangu umekuwa ukichukuliwa na watu kama ukweli tena ukweli mtupu. Watu kwa malengo yao wamekuwa wakitumia majina zaidi ya moja kwa mtu mmoja na kuingia JF kuandika uzushi (kama huu wa leo) ili kunichafua na kunigombanisha na wenzangu. Bahati mbaya sana baadhi ya viongozi wenzangu wa chama wanachukua chuki, fitna na uwongo unaoandikwa humu kama ukweli. Inasikitisha sana.
Ninapenda kuwafahamisha wasomaji wote wa JF kuwa sehemu ya habari iliyoandikwa hapa katika thread hii ni uwongo wa makusudi dhidi yangu. Ni imagination ya mtu ambaye anaumwa ugonjwa wa ZITTOPHOBIASIS! Ugonjwa ambao watu wengi wanaumwa na ninasikitika kuwa dawa ya ugonjwa huu hata kwa babu haupo maana ni ugonjwa unasambazwa na ugonjwa wa chuki, fitna, na WIVU!

Kutokana na mwenendo wako, inakuwa ngumu kukuamini unapojitetea. Lakini hata hivyo siwezi kukuhukumu maana sina na sijauona ushahidi wowote dhidi yako. Nafuatilia nyendo zako kwa karibu kwakuwa upinzani imara ni kwa maslahi ya watz wote. Nakumbuka nilivyoumia NCCR ilivyosambaratika baada ya kuamusha ari ya mageuzi ndani ya moyo wangu, sitapenda kuona hilo likitokea tena..
 
Mimi nilikwisha sema I will always stand by Zitto kama kiongozi mahiri mwenye vision na nia njema kwa chama...
Challenges within the party ni kukua kwa demokrasia hasa ktk nchi ambayo haina tofauti za Itikadi..kwa maana nyingine ni sawa na kusema - Nchi yetu haina itikadi isipokuwa watu wake ndio wanazo. ..

Nitasema wazi hata mimi kuna vitu sikubaliani na Mbowe, Dr.Slaa, Zitto,Mnyika,viongozi woote kwa ujumla wao na hata baadhi ya sera za Chadema kulingana na mtazamo wangu..
Hii haina maana naisaliti Chadem au viongozi wa chama isipokuwa kutokubali kwangu kunakuza wigo la kifikra na demokrasia kwani haiwezekani sote tukafikiria sawa sawa..
Ingekuwa rahisi hivyo sote tungekuwa malaika hatuna vyama vya siasa wala dini za kuabudu..
Maadam Zitto bado ni kiongozi wa chama nitaendelea kumpa support kama viongozi wengine na pengine kukubali kutokubaliana naye.kwa lengo la kujenga chama na nchi yetu...
 
Huyu Lipumba atapendwaje leo ghafla hivi kwenye mikoa iliyokuwa ngome yake lakini wananchi wakambwaga kwenye kura 2010..?ama leo ndo kawa CUF pale(2010) alikuwa CDM? Lipumba kukusanya watoto wa primary si ileile ya Makamu wa Raisi huko mwanza..? huyu Zitto,kila siku Ztto..Ztto..

amejibu akihoji alikuwa akiongea nn na R Az..ila sijaona akikanusha mawasiliano hayo kati yao! waliongea nn? awe na subira na siku yaja atajulishwa,

watu wanaipenda CDM si kwa majina ya watu ama sura zao..NO.. NO ..NO! bali kwa kazi zinazofanywa na CDM..Watu watakuja.,watu watakwenda kazi za chama ndo jibu..
 
Mheshimiwa Zitto Kabwe habari. Ni ukweli ambao kuna siku itabidi uukubali ingawa sasa utaona uzushi kama uzushi mwingine. Hawa watu (JF na Viongozi wa Chadema) hawakuamini kabisaaa! Mfano baadhi ya viongozi wenzako wanatumia magazeti yao kukuchafua kila uchao. Bila kuuma uma maneno hawan kuamnini kwa sababu ni MUISLAMU! Sina uhakika na uislamu wako ila hilo lina watia hofu sana. Umekuja mara nyingi hapa kujitetea lakini bado hawakuamini so long you are still a MUSLIM.<br />
<br />
Ukitaka wakuamini, badili DINI uwe MKRISTO ikiwezekana MKATOLIKI kisha tafuta binti wa waasisi umuoe! Hapo utapewa uwenyekiti!
<br />


CRAP!!!
 
Mheshimiwa mbunge wa kigoma you are too ambitious and because of that una loose focus ni tabia ya kuwa too much ambitious. Wakati ni vizuri kuwa ambitious lakini pia ilibidi badala ya kutumia njia za uchochoroni, ujenge credibility yako kwenye public. Ukiwa na macho utaona hapa watu wametoa hisia zao na many opinion ziko negative towards you; ask yourself why! Ukiangalia members humu wamegiregister bila condition ya uanachama so this is a very big sample kwa elites wa nchi hii kupima opinion yao. Tunashindwa kuelewa sababu na nia za kuwa so ambitious kuutaka urais kwa nguvu zote badala ya kujenga ushawishi kwenye public ili ijikute inahamasika kukupendekeza wewe tu kuwa rais. Dr. Slaa has inspired many people you can read from this forum why cant you see kwamba ni kwakumjenga yeye ndiyo rahisi kwako ku inspire wengine wewe kuwa rais how can you be an opponent to the man who is well accepted by almost everybody?

Utaniuliza kuwa kwanini na sema una compete badala ya ku work as a team; kwanza umetamka kwa mdomo wako kuwa una ambitions za kugombea why wakati tayari mwenzako ameshaonyesha kukubalika usim support ili yeye akisema hagombei aku recommend wewe kwa supporters wake? Does it mean you believe you are more popular than him? If you say you are equally popular why then dont you capitalize on this ili muwe na supporters wengi if you work like a team?

Second you oppose Dr. wazi wazi since you did not support his concern pale alipoonyesha kuwa hakutendewa haki kwenye uchaguzi; you choosed not to kwa sababu ya friendship basis dont you see to you JK matters a lot than him even though you all belong to CHADEMA? Je Dr. akikuchukia atakuwa na kosa maana you psychologically tortured him kwani mtu kama wewe ambaye ni Naibu wake kutom support just get a minute and put your self into his position to think of how it feels. Hata kama kweli JK is a friend kwa ubinadamu tu ilitosha wewe kuonyesha ume support feelings za mwenzako kuwa hakutendewa haki hata kama nikinafiki tu ingesaidia.

So all these contribute much into the problem ya public kutokuwa na imani na wewe. Usiilaumu JF laumu nafsi yako and try to be yourself. Hakuna anayekuchukia ila matendo yako yanachukiza wengi I included. Humanbeings are rational beings so dont you cheat yourself hawawezi ku read your heart they can thats why wanakuonyesha something is wrong somewhere.

Kila laheri!
 
Unasema unataka ushahidi wa content ya mawasiliano yako na hao mafisadi ikiwa proved km unahujumu chama then utawajibika! The fact kwamba umekubali kua unawacliana nao inatosha kbs kwa cc kukudiscredit muheshimiwa. How come unawacliana na watu km kina Rostam according to mwanahalisi alaf still u want us to have faith in u? Jus look at ur trent of behaviour these days.. Ulipinga kugomea hotuba ya rais bungeni against ur fellows, u communicate wth fisadis, u dnt want to take party ktk maandamano ya chadema ya hivi karibun. Of all these things from u, wat do u think will be the speculations in the society? Unafikr watu watakuonaje katk jamii? Kama co msaliti? There are convincing evidences to conclude that u r snitching arround and we don't like that.. Better prove us wrong or otherwise leave 4 NCCR coz CHADEMA can be better of without u. Hakuna mtu mwenye wivu na wewe kama ni wivu angeanza kuonewa Slaa.. Goodevening
 
Binafsi nimejitahidi kadiri nilivyoweza kujiweka mbali na mijadala inayomhusisha Zitto kwa muda sasa lakini leo naona niseme machache tu. Kuna wakati Zitto alikuwa kipenzi cha wengi na ole wake aliyejaribu kumnyooshea kidole Zitto, alionja joto la jiwe humu JF na tulikuwa wengi tuko tayari kuyarusha mawe ambayo hayakuwa haba.

Kuna waliojaribu kumtupia lawama kwa kumhusisha na dereva aliyesababisha kifo cha Marehemu Wangwe, hao tuliwatolea nje. Kuna waliomlaumu kwa kukubali kuteuliwa na Raisi kwenye kamati ya madini na kudai kanunuliwa, hao nao hatukuwakawiza kwa kuwapa vidonge vyao. Watu husema mpenda chongo huita kengeza.

Ukweli ni kuwa Zitto wakati huo alikuwa ni shujaa wetu na kamwe wengine hatukubali kuliona jina lake linachafuliwa kwa sababu zozote zile. Tuliendelea kufanya hivyo hata wakati alipoanza kutoa matamshi tatanishi katika majibu yake kwa baadhi ya michango ya wana JF. Nakumbuka majibu kama ya kumwonea wivu, kumiliki hammer n.k.

Kwa mara ya kwanza kabisa wengine tuliguna kidogo alipoitetea Dowans tukajiuliza he, vipi tena ! Hatujakaa sawa akaanza kummwagia sifa aliyekuwa Mkurugenzi wa Tanesco, Dr. Rashidi, kwa ufanisi na uadilifu uliotukuka na usio mfano sehemu nyingi na hasa nchini Tanzania ! Kwa kusitasita tupo tuliothubutu kuuliza, kulikoni ? Hata hivyo hatukuwa wengi.

Ninachojaribu kukieleza hapa ni kuwa Zitto katika muda kifupi ameweza kufanikisha mambo mawili yanayokinzana. Amekuwa controversial sana na sasa anaangaliwa kwa tahadhari kubwa upande moja huku upande wa pili akiamsha hisia tofauti kabisa na hakuna ubishi kuwa misimamo yake imeweza kuzua maswali kuliko majibu. Si ajabu tena hoja kama hii kutokea JF.

Zitto, kama vile merikebu, anapitia dhoruba na nachelea kusema mwisho wa safari yake utategemea nguvu na kasi ya upepo. Wengi wa wenye wasiwasi naye hivi sasa ni wale waliokuwa naye sana bega kwa bega hapo mwanzo lakini wengi wanaomtetea hivi sasa ni wale waliokuwa wanamwangalia kwa jicho la husuda lakini hawakuwa naye.

Binafsi sina kinyongo na Zitto wala uamuzi wake kuhusu njia atakayopitia ila sina hakika kuwa kweli kakamata usukani kwenye hiyo safari yake. Angekuwa kwenye usukani na dira anayo nina hakika maamuzi mengi ambayo ameyafanya mpaka sasa hivi hayangezusha utata kama tunavyoshuhudia. Hivyo namwomba Zitto ajiepushe na ahadi elea, safari bado ndefu.
 
Jus tell us mnawacliana nn na Rostam ambae chama chako kinamtaja kua fisadi na1? Wat bussines do u have with this guy? We ni mpelelezi frm Takukuru? Hapana. what do u guys normally talk about? Kama co kukihujumu CDM? Nawapongeza Mwanahalisi ambao waliweza kuprove kwamb u had communications wth this Guy na wew leo umeadmitt only that unataka ushahidi wa kilichokua kinazungumzwa.. To me I really dnt care mlizungumza nini, the fact that mlikua na mawacliano na umeadmitt inatosha kabisa kuprove that u r turning against us. Anyways kumbuka pia sauti ya wengi sauti ya Mungu, ni maneno hata wew ulishawai kuyatumia, sauti ya wengi humu JF na kwengineko against u ni sauti ya Mungu. Tuckilize na Ujipange, u r not the Zitto we used to knw.
 
Huko kote ni kutapatapa tu, hata wakidhoofisha chadema bado kutakuwa na chama kingine mbadala cha kuleta mageuzi na wala si vyama hivyo anavyokimbilia Zitto na hao CCM B. Watanzania wanataka mageuzi kwa sasa, na mageuzi hayo yako kwenye chama makini (CHADEMA). Zitto kwa sasa hana lolote na wala asifikiri ana umaarufu wowote wa kuweza kukiyumbisha chama tena. Watu wengi na hususan wanachama wa CHADEMA hawawezi kufuata mkumbo wa fikira za Zitto na watu wake wa CCM.
 
mheshimiwa zito kaa utafakari kwa umakini haya yote yanayosemwa.angalia usije ukapotezwa kama mrema agustino.lwamwai.kaburou.nk.kumbuka kuwa watanzania tunamlilia zito wa zaman si huyu wa sasa hivi sihuyu
 
Umeeleweka kiasi flani but ningeuliza hivi....wewe kama kiogozi wa chama ili wananchi waongoze imani juu yako huoni inafaa kuhudhuria maandamano ya chadema?Ni sababu zipi zinakufanya usikwepo kwenye maandamano ya chadema?
 
Nitakuwa wa mwisho kuamini kama huyu kweli ni Zitto Kabwe mwenyewe anaejibu majibu haya, na kama ni kweli huyu ni Zitto kabwe sio mtu mwingine anatumia ID yake, basi ni bora nikajisalimishe kwa Yusuf Makamba angalau na mimi niambulie makombo kama Tambwe Hiza. narudia kusema siamini kama huyu ndio alitaka kuwa mwenyekiti wa CHADEMA. hapa hana tofauti na Khadija Kopa. some time kukaa kimya ni busara kwa kiongozi kuliko kufyatuka na kuongea huu utumbo, wewe hauwezi kujivunia chochote hapa kinachojivunia ni nguvu ya umma. Period. by the way unaweza kutukokotolea mwaka 2005 ulishinda ubunge kwa kura ngapi na asilimia ngapi? na mwaka 2010 ulishinda kwa kura ngapi na asilimia ngapi? je kistatistic umepanda au umeshuka?
ukiijuwa kweli, nayo kweli itakuweka huru.

Nimechoka niwengi wanaorewa sifa majibu yakihuni kiasihichi sijaajuwa kama ni zito tunayemfaham au ni wakichina
 
Back
Top Bottom