MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,975
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.
Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.
Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.
Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.
Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.
Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa, alibainisha Zitto.
Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.
Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu, alisema mbunge huyo.
Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.
Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kungoa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.
Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu, alisema.
Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.
Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa, alisisitiza Zitto.
Habari: JAMBO LEO.
Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.
Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.
Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.
Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.
Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa, alibainisha Zitto.
Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.
Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu, alisema mbunge huyo.
Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.
Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kungoa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.
Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu, alisema.
Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.
Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa, alisisitiza Zitto.
Habari: JAMBO LEO.