Zitto, Kafulila, Kitila Mkumbo, Hussein Bashe na akina Ben Saanane waweza Kuanzisha chama kingine?

Siafiki na wala sipendi tabia ya fukuza fukuza inayofanywa na CHADEMA. Lakini pia sipendi tabia ya vijana kutumiwa na CCM kuvihujumu vyama vichanga kwa kutumia nguvu ya fedha za walipakodi ili kujaribu kuzuia mabadiliko kwa kutaka cha wachache kiendelea kuongoza nchi kiujanja ujanja.
Sipendi fukuza fukuza kwa sababu ni tabia ya uoga wa kukabiliana na changa moto. Sio matakwa ya vijana kutumiwa na chama tawala, wanazidiwa na mbinu. Ni kama msichana mwanafunzi anayepewa mimba na mibaba yenye pesa au madaraka. Ni kwa sababu anashida ya hela ya kula, mavazi, malazi, simu nzuri na mahitaji mengine anayopaswa kuwa nayo msichana wa kisasa. Ni changa moto. Vijana wetu wanasiasa wana mahitaji yao pia. Hawana ajira, wanataka madaraka, pesa na mambo mengine. CCM na watu waliomo kwenye madaraka wanatumia fursa hii ili kuwadanganya wanasiasa vijana vipesa na nafasi ya madaraka madogo madogo. Ukimwadhibu msichana aliyepata mimba peke yake na kumwacha FATAKI utakuwa hujafanya kitu.
Pengine kwa mtazamo wangu ni busara kuwalea vijana wetu vizuri kwa kuwaasa dhidi FATAKI CCM, kuwajengea mazingira yenye matumaini ya matokeo ya kudumu kuliko wanayoweza kuyapata kwa FATAKI CCM. Kufukuza peke yake hakutoshi kwa sababu atatokea kijana mwingine mzuri kisiasa hawataacha kumlubuni kwa visenti vyao vya ufisadi. Watanzania hatutaonja matamu yote ya upinzani. Tulianza na NCCR-Mageuzi wakalubuniwa, CUF halikadhalika Maalim Seif kalambishwa leo CHADEMA. Tutabaki hapohapo miaka yote bila kuiondoa madarakani CCM.
CHADEMA kuwa na mbinu moja tu ya kukabiliana na CCM ya kufukuza, bila kuwepo na mbinu ya kulea, kuonya, kukalipia hata kusimamisha kwa muda ili kuwapa vijana nafasi ya kujirekebisha haitasaidia. Wataalam wa saikolojia wanasema kumsamehe mtu mwenye kosa ni ishara ya kuwa na nguvu zaidi na pia humfanya mtu aliyesamehewa kuwa rafiki zaidi kuliko kumpatiliza kunakojenga chuki zaidi.
CHADEMA kama kinajua kwa uhakika kuwa kinahujumiwa na CCM, ni lazima nacho kitafute mbinu ya kukihujumu CCM. Daudi alimkabili Goliat pamoja na udogo wake. Katika mchezo wowote huwezi kujikinga tu bila kushambulia.
Lakini la tatu ni lazima kuwasema hadharani CCM kuwa tunawajua mbinu wanazozifanya (WHISLE BLOWING) Mkikaa kimya mkabaki kufukuzana mnawasaidia CCM. Vita vya panzi furaha ya kunguru.
Nimenukuu hii Wanabidii na Nuclear,


"Haya ni maneno ya Zitto kabwe kwenye ukurasa wake wa Facebook, mchezo usomeni mapema. Kuna thread ililetwa hapa lakini ukiunganisha dots utapata ukweli wenyewe

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-wa-sasa-kama-wa-el-jk-ac-ra-1995-2005-a.html

Ni dhahiri kwamba kuvuliwa uanachama kwa David ni jaribio kubwa kwa mfumo wetu wa demokrasia kama ilivyokuwa huko nyuma wakati kina Erasto Tumbo walipovuliwa uanachama wa chama chao cha UDP. Ninaamini NCCR-M watamaliza matatizo yao kwa mujibu wa katiba ya chama chao na ndugu David Kafulila atazikabili changamoto hizi kama kiongozi kijana wa kisiasa na kuona hii kama fursa badala ya kukata tamaa. Ifahamike wazi kabisa kwamba David ni mtu huru mwenye mawazo yake na maamuzi yake. Kwamba sisi ni marafiki wa karibu na kwamba tunatoka mkoa mmoja haina maana kwamba lolote afanyalo ama nimemtuma au ninahusika. Ninaheshimu misimamo yake na siku zote huwa nipo upande wa anayeonewa, kudhulumiwa na mnyonge. Msimamo huu wa msingi usiwape watu nafasi ya kunihusisha na mambo ya chama dhaifu kisicho na dira kama NCCR-M.
Kafulila akumbuke kwamba hakufukuzwa CHADEMA, alijiondoa mwenyewe. Milango yetu ipo wazi kwa mujibu wa Katiba, Kanuni na taratibu za chama chetu


Kitila ambaye anajulikana kuwa kambi ya Zitto na akina kafulila alichangia hivi jana.Wamejidhihirisha wazi

i)Nidhamu bila UHURU ni UTUMWA. Kama tunaweza kuwaambia Rais, Waziri Mkuu, mawaziri, Spika wa Bunge, n.k. kwamba uongozi wao ni dhaifu, hadharani na mbele ya kadmnasi, viongozi wa vyama vya siasa wanapata wapi utukufu wa kujifanya kwamba hawawezi kusemwa nje ya vikao? Viongozi wa vyama vya siasa ni viongozi wa umma na hawawezi kuficha udhaifu wao katika mwamvuli wa nidhamu.

ii)Maamuzi ya chama cha siasa chochote makini lazima yazingatie maslahi mapana ya kisiasa na kijamii kwa sababu chama cha siasa sio kitengo cha mahakama. Mahakama ina haki na wajibu wa kuchukua maamuzi yeyote madamu yamezingatia sheria zilizopo kwa wakati huo hata kama maamuzi hayo ni ya ovyo.Jambo hili haliwezi kufanywa na chama cha siasa makini cha watu.
iii)Vyama vya siasa vipo kwa lengo la kukuza demokrasia. Msingi wa demokrasia ni UHURU WA KUTOA maoni. Kama vyama vya siasa vitatumika kuziba watu midomo kwa kisingizio cha kulinda nidhamu ya chama vitakuwa vinaua demokrasia.

iv) Siamini,na haitatokea niamni, kwamba kumkosoa kiongozi yeyote hadharani ni utomvu wa nidhamu.


Haya hapa ni maneno ya Ben Saanane kwenye ukurasa wake wa Facebook jana

“Nimeshawahi kusema hapa mara nyingi kwamba harakati za vijana katika siasa zinafungwa speed governor na wazee wasiopenda mabadiliko ndani ya vyama vya siasa.Fikra huru zinashambuliwa ndani ya vyama vya siasa.....nimefurahishwa pia na maneno ya Nape Nnauye bila kujali itikadi za kisiasa.Pia nitoe wito kwa vijana wa vyama vyote vya siasa kuungana katika harakati hizi na kulaani kwa nguvu zote juhudi za baadhi ya watu ndani ya vyama vya siasa kujaribu kufifisha harakati za kimageuzi au kiunamapinduzi.I dare them to make a constructive desicion and desist from personal attacks.They should Learn to tackle issues, not personalities. Attempting to intimidate is for empty headed thugs”

Pia hapa JF Alidhihirisha upinzani wa wazi wazi na hoja iliyotolewa na Lema anayeaminika kuwa karibu na mwenyekiti wa chama kwa kuandika hivi kuchangia hoja ya Lema


My take:
Naona kuna dalili ya vijana wa aina hi"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom