Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,805
- 11,965
Salaam Wakuu,
Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT WAZALENDO, Zitto Kabwe ameshangazwa na Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya Tanga.
Akiandika kwenye Mtandao wa Twitter amesema:
"Mwaka 2019 Mamlaka ya Bandari Tanzania iliingia Mkataba wa USD 172M na Kampuni ya China Harbour Eng Ltd wa upanuzi wa Bandari ya Tanga. Baada ya Mwezi Kampuni hiyo ikaipa kazi hiyo hiyo kampuni nyengine ya CCCC-Tianjin Dredging kwa Gharama ya USD 16M! CAG hukuona hili?"
" Gharama za Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya Tanga zimefikia zaidi ya TZS 500 Bilioni. Mzabuni alipewa kazi ‘ikiaminika’ kuwa Eneo ya kuchimba lina mwamba."
" Mkandarasi akakuta lina tope tupu. Meneja wa Bandari Tanga alipohoji makao makuu, akahamishiwa Kigoma kisha akafukuzwa Kazi!"
" Watu wameumizwa sana na ‘Wazalendo’ waliokuwa wanajificha kwenye kichaka hicho kufanya ubadhirifu. Nataraji CAG atafanya Ukaguzi Maalumu kwa Mradi huu wa Tanga na kuchukua hatua stahiki Pamoja na Miradi mingine yote ambayo ilikuwa inatumika kufanya ubadhirifu wa Fedha za Umma". Mwisho wa Kunukuu.
Je, nini maoni yako kutokana na hiki alichokisema Zitto Kabwe?
Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT WAZALENDO, Zitto Kabwe ameshangazwa na Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya Tanga.
Akiandika kwenye Mtandao wa Twitter amesema:
"Mwaka 2019 Mamlaka ya Bandari Tanzania iliingia Mkataba wa USD 172M na Kampuni ya China Harbour Eng Ltd wa upanuzi wa Bandari ya Tanga. Baada ya Mwezi Kampuni hiyo ikaipa kazi hiyo hiyo kampuni nyengine ya CCCC-Tianjin Dredging kwa Gharama ya USD 16M! CAG hukuona hili?"
" Gharama za Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya Tanga zimefikia zaidi ya TZS 500 Bilioni. Mzabuni alipewa kazi ‘ikiaminika’ kuwa Eneo ya kuchimba lina mwamba."
" Mkandarasi akakuta lina tope tupu. Meneja wa Bandari Tanga alipohoji makao makuu, akahamishiwa Kigoma kisha akafukuzwa Kazi!"
" Watu wameumizwa sana na ‘Wazalendo’ waliokuwa wanajificha kwenye kichaka hicho kufanya ubadhirifu. Nataraji CAG atafanya Ukaguzi Maalumu kwa Mradi huu wa Tanga na kuchukua hatua stahiki Pamoja na Miradi mingine yote ambayo ilikuwa inatumika kufanya ubadhirifu wa Fedha za Umma". Mwisho wa Kunukuu.
Je, nini maoni yako kutokana na hiki alichokisema Zitto Kabwe?