Mdanganywa
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 620
- 342
[B]Kifyatu[/B], niliamua nichukue muda nipitie japo michango yako mbalimbali ya awali kabla sijauendeleza huu mjadala na wewe na amini usiamini nimepitia asilimia kubwa tu ya michango yako yote.
Lengo langu la kupitia hiyo michango ni hamu ya kutaka kujua misimamo yako katika hoja mbalimbali zinazotolewa humu JF na baada ya kufanya hivyo nimechukua uamuzi kama ifuatavyo.
Toka sasa utakuwa kwenye orodha yangu ya ignore kwa sababu naamini watu aina yako ni hatari kwa ustawi wa jamii na mmechangia kwa kiasi kikubwa uzoroteshaji wa utawala wa sheria.
Kuliko kujadiliana na wewe ni heri kujadiliana na meza ya kulia chakula (kama kweli umeishi Marekani utanielewa) Uzuri wa hiyo meza ni kwamba haina habari na utamu/uchungu wa kilichowekwa juu yake.
Samahani sana kama hatua yangu itakukwaza, ila ninayo tabia hii ya kuchagua ni nani wa kujadiliana naye...kwaheri.
Terrible mistake kum-ignore huyu, mkabe hoja kwa hoja akimbie yeye mwenyewe. Kama huwezi nikuunfishe kukabiliana naye. Moja ya post zangu nimemjibu hivi:
List ya mafisadi ilipopelekwa bungeni nini kilitokea? Ilipita? Ilipopelekwa kwenye mkutano wa hadhara pale Mwembeyanga nini kilitokea? Au hukuwa umezaliwa?
Moja ya post zake anasema hivi:
Hii sikua nimeiona.
Ndio mkuu, umenikumbusha mbali sana. Ujana wetu tulipitia mengi.
1. Tulicheza twist na kuvaa suruwali za kubana kama zenu siku hizi mpaka mzee Kawawa (waziri mkuu) akaamua kuzitia mkasi. TUKAPONA
Najua kuna mahali ni mwongo sasa sijui ni uongo kwamba kasoma UDSM Engineering au kaongopa kwamba alivaa suruali za kubana zilizokatazwa na Kawawa.
Tuanze kuchambua ongo zote mbili. Kama kasoma Engineering basi kaongopa kwamba alivaa suruali zile akiwa kijana, pale UDSM ile Faculty of Engineering (FFOE) imeanzishwa 1974 ndipo vijana wa pale wakaingia na ku-graduate kwa mara ya kwanza 1977.
Huyu anasema ujana wake suruali zake zilibana wakatiujana ule ulikuwa wa mwaka 1962 Kawawa akiwa PM na Nyerere akiwa mbunge tu. Sasa kama hiyo 1962 tusema alikuwa na miaka 18, basi maana yake alizaliwa walau mwaka 1944.
Vijana wa mwaka huo (1944) wengi waliochelewa wali-graduate mwaka 1974 wakiwa na miaka 30 na waliowahi wali-graduate hata FOE haijaanzishwa.
Hana chochote. Huyu ni mtu ambaye yuko exposed na mambo mengi na hivyo anawez ku-argeu na ukadhani CV yake ni sahihi na ukizingatia kuwa ameficha jina lake.
Halafu hajui kudanganya. Pale FOE first class Honors zinajulikana kila mwaka kuanzia hiyo 1977 zikiwemo za akina Prof. Materu, Prof. Nzali (RIP), Mr. Ishengoma, Dr. Zaipuna Yonah na hakuna hata mmoja unayeweza kumweka katika arguments za huyu bwana.
Msubiri aje uone nitakavyomshusha.