Zitto Kabwe:Tamko la Polisi dhidi ya Mikutano ya Siasa ni la "Mwendokasi"

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,816
Jeshi la Polisi wametoa kauli kufafanua uzuiwaji wa mikutano ya hadhara ya vyama vya Siasa. Polisi wanasema kuwa ' WAMEZUIA' mikutano ya hadhara na sio mikutano ya KIKATIBA ya Vyama vya Siasa. Hata hivyo Kamishna wa Polisi Nsato Mssanzya hakunukuu kifungu chochote cha Katiba kinachompa yeye au jeshi la Polisi mamlaka ya kuruhusu au kutoruhusu mikutano ya vyama.

Polisi sio mamlaka ya kutafsiri Sheria ya Vyama vya Siasa na kujua Vikao vya kikatiba ni vipi.


Polisi wametoa ufafanuzi wao kwa sababu ya Mkutano Mkuu wa CCM. Wanasahau kuwa mkutano waliozuia wa Act Wazalendo Kongamano la Bajeti ni kwa mujibu taratibu za Chama chetu kupitia Mfumo wa kuendesha Chama kupitia Kamati za Kitaifa. Kongamano lilikuwa ni shughuli ya kitendaji ya Kamati ya Fedha na Miradi ya ACT Wazalendo.

Pia naamini kuwa mahafali ya CHASO ni sehemu ya kanuni za Chama chao. Ufafanuzi wa Polisi unaonyesha dhahiri kuwa Jeshi hilo linaipendelea CCM.

Tutaona maajabu zaidi baada ya Mkutano Mkuu wa CCM. Chama hicho kina utaratibu wa kuzungusha Viongozi wao wapya kwenye miji mikubwa. Magufuli anaenda kuwa anointed kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Chama ambacho yeye hajawahi kuwa hata Balozi wa Shina. CCM wataacha utaratibu wao wa miaka yote kutambulisha Viongozi wao? Polisi watakuja tena na ufafanuzi mwingine? Tusubiri tuone.


Somo? Viongozi wajifunze kufikiri kabla ya kutamka. Matamko ya MwendoKasi haya yataleta madhara makubwa kwa Nchi.
 
Inayoamini kuwa ni akili kubwa inapoamua kutia ujinga akili ndogo.

Zitto na kampeni ya kutia taharuki raia dhidi ya serikali yao ungetegemea uachwe tu uendelee kumwaga sumu chafu???

Ni bahati nzuri na mbaya kwamba kwa Zitto bila kufanya anachojaribu kukifanya sasa basi maisha yake ya kisiasa hayana afya, na huenda ikawa mwanzo wa mwisho japo anaendelea kuamini hakuna wa kumshinda au kumwondoa kwenye reli nchi hii. Kuja kutambua zama si zake huenda ikawa too late....watu makini are no longer on his side....
Kwahiyo wewe ni mtu makini?
 
Iko wazi.

Jeshi la Polisi linafanya yote kwa maslahi ya chama dola-CCM.

Siwalaumu Polisi. Wao kazi yao nikupokea amri tu na kutekeleza bila kuhoji.

Wanapenda kupanda vyeo pia. Nani anayetoa vyeo? Nani anayeteua? Ni huyo anayekwenda kukabidhiwa uenyekiti CCM-Taifa.

Binafsi ninalaumu mfumo. Ninalaumu "double standard" inayofanywa na aliyeapa kuisimamia na kuilinda Katiba.

Ninalaumu ukiukwaji wa Katiba wa waziwazi dhidi ya haki ya uendeshaji wa vyama vya kisiasa kwa mujibu wa sheria.(Sheria ya 2005 Na.1 ib. 7.), 20.-(1)
 
Inayoamini kuwa ni akili kubwa inapoamua kutia ujinga akili ndogo.

Zitto na kampeni ya kutia taharuki raia dhidi ya serikali yao ungetegemea uachwe tu uendelee kumwaga sumu chafu???

Ni bahati nzuri na mbaya kwamba kwa Zitto bila kufanya anachojaribu kukifanya sasa basi maisha yake ya kisiasa hayana afya, na huenda ikawa mwanzo wa mwisho japo anaendelea kuamini hakuna wa kumshinda au kumwondoa kwenye reli nchi hii. Kuja kutambua zama si zake huenda ikawa too late....watu makini are no longer on his side....

Jadili hoja aliyoitoa Zitto, mbona Zitto mwenyewe tu? ..au ndo kina 'simple minds!'
 
Motto wa hii Serikali: Ikulu mwendo kasi, kukurupuka kwanza masahihisho baadaye.

Si mmesikia katamka hadharani hataki mtu amcheleweshe? Taratibu zote za kuendesha nchi kapuni this is a one man show mbele kwa mbele.
 
Ma RPC wote wakistaafu wanaingia kugombea ubunge na wengine wanateuliwa bado kuwa ma DC na makada! Wanajikomba kwa watawala!! Hawana lolote! Ile damu ya wasio hatia!! Mwangosi itamuandama Kamuhanda hadi kaburini!!
 
Ma RPC wote wakistaafu wanaingia kugombea ubunge na wengine wanateuliwa bado kuwa ma DC na makada! Wanajikomba kwa watawala!! Hawana lolote! Ile damu ya wasio hatia!! Mwangosi itamuandama Kamuhanda hadi kaburini!!
Wanatafuta vibarua baada ya maisha ya kustaafu
 
Aisee, ZITO katukumbusha jambo mwenyekiti wao na katibu watatakiwa kutambulishwa mikoani baada ya kuchaguliwa na kuteuliwa yaani hapo ndo njia ya muongo ni fupi. Yaani dk MASHINJI asitambulishwe mtarajiwa wa ccm atambulishwe atukubali atukubali atukubali tukutane Dodoma mura
 
Jana mameya wa ukawa wamefanya mkutano bila shida.

Leo mameya wa UKAWA wamefanya uchaguzi wao bila shida.

Hamna uvccm yoyote aliyeenda kuzuia hiyo mikutano. Sasa 23/ 7 tuje tuone kibavichaa kimetanguliza tumbo kuja Dodoma eti kuzuia mkutano wa ccm!!!!
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom