Zitto Kabwe: Sinunuliki

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Zitto Kabwe: Sinunuliki

na Salehe Mohamed
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe amesema hanunuliki kwani hana bei, na kamwe hatofumba mdomo kukemea ufisadi unaofanywa na viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia rasilimali za wananchi.

Zitto alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki mjini Tanga alipokuwa kwenye mkutano wa hadhara baada ya mkazi mmoja wa mjini humo kumuuliza kama kuteuliwa kwake katika kamati ya kuchunguza masuala ya madini kulikuwa na nia ya kununuliwa na kuukacha upinzani.

Akijibu swali hilo, alisema hawezi kununuliwa kwa sababu yeye ni mwanamageuzi, na anataka kuona watendaji wa serikali wakiwajibika kwa wananchi waliowateua, badala ya kuwanyenyekea matajiri na wawekezaji wachache ambao wanazifanya rasimali za taifa kuwa mali zao.

Alisema kuteuliwa kwake katika kamati hiyo na Rais Jakaya Kikwete, ilitokana na kelele zake na za wananchi kuhusu unyonyaji unaofanywa na wawekezaji katika sekta ya madini, ambayo imekuwa ikiwanufaisha zaidi wageni.

“Jamani asiwadanganye mtu kuwa mimi ninaweza kununuliwa, kwani bei yangu haijulikani, na sitegemei kunyamaza kwa wote wanaoshiriki katika kutafuna rasilimali za nchi,” alisema Zitto.

Alisema kama utaratibu wa kuwanunua wapinzania utashamiri, basi taifa litapoteza mwelekeo zaidi, kwani upinzani ndio unaoleta chachu kubwa katika maendeleo ya taifa lolote hapa duniani.

Zitto alisema katika kipindi ambacho upinzani, hasa NCCR- Mageuzi iliyumba, ndipo watendaji wa serikali walipojitwalia jukumu la kutafuna rasilimali za nchi kwa kuwa hakuna watu waliokuwa wakiwapiga kelele.

Alisema miaka 10 ya kulegalega kwa chama hicho ni pigo kubwa kwa wapinzani ambao hivi sasa wanaelekea kufanya vizuri zaidi katika kusimamia serikali, licha ya kuwapo kwa watu wanaorudisha nyuma juhudi za wapinzani hao.

“Kuna juhudi kubwa za kuudhoofisha upinzani, hasa kwa watu wanaoshiriki vitendo vya ufisadi ili waweze kuendeleza ufisadi wao, na kama tusipokuwa makini tutaingia katika mkenge wa hao mafisadi,” alisema Zitto.

Aidha, Zitto alisema ni vema Watanzania wakawa wanapiga kura kimkakati ili wasije kuibiwa kura zao na watu wanaotaka kujitwalia madaraka kwa njia za mlango wa nyuma, ambazo mara kwa mara zimekuwa zikifanywa na CCM.
 
wapashe zito, waambie ukweli kuwa wanaonunulika si wengine bali ni akina chitaliko, serukamba, na wanafiki wengine, wewe huna bei watakununua je? shame on you chitaliko and your fellows cowards
 
Hili kidogo kwa kweli hata mimi lilinitatiza kidogo baada ya kusikia kijana wetu Zitto yupo kwenye hii kamati maana nilijua atalipwa ela nzuri then ataacha kupayuka humo bungeni.Ila hongera baba usiwafumbie macho wape vidonge vyao mpaka wa kukome ila usisahau kujizatiti Kiafrika maana akina Kingunge na Chenge hawachelewi kutuma makombora.
 
Watu waliopinga kuteuliwa kwa Zito walikuwa na sababu gani za msingi? Maana si kila mmoja wetu (yaani watanzania ni mwenye roho ya ufisadi).
Ni kweli may be hiyo ndiyo ilikuwa lengo lakini kila kitu kinategemea moyo wa mtu binafsi.
Mi ninajua kama mtu ana moyo wa kifisadi hata kama hakuteuliwa kwenye kamati yoyote bado wanaweza kumnasa katika mtego mwingine kama hakuwa makini.
Haya ndiyo yaliyowakuwa wakina Kabarou na wenziwe.
 
Watu waliopinga kuteuliwa kwa Zito walikuwa na sababu gani za msingi? Maana si kila mmoja wetu (yaani watanzania ni mwenye roho ya ufisadi).
Ni kweli may be hiyo ndiyo ilikuwa lengo lakini kila kitu kinategemea moyo wa mtu binafsi.
Mi ninajua kama mtu ana moyo wa kifisadi hata kama hakuteuliwa kwenye kamati yoyote bado wanaweza kumnasa katika mtego mwingine kama hakuwa makini.
Haya ndiyo yaliyowakuwa wakina Kabarou na wenziwe.

Waliuliza kwasababu RIPOTI YA MADINI IKO KWA SICLAIR NA WATU WANAOIFAHAMU NI YEYE,KIKWETE,CHEYO,IDDI SIMBA,MARK BOMANI NA WANAKAMATI WENGINE WA MADINI.
Hivyo basi swali hilo la HUKO TANGA NI LA MSINGI.
Kwamba Zitto amelijibu VIZURI?
Well...Inategemeana na msimamo wako.
Msimamo wangu ni ISOMWE MARA MOJA!
 
In the tradition of strict attention to detail

"Jamani asiwadanganye mtu kuwa mimi ninaweza kununuliwa, kwani bei yangu haijulikani, na sitegemei kunyamaza kwa wote wanaoshiriki katika kutafuna rasilimali za nchi,"

Zitto anasema bei yake haijulikani au hana bei? Hivi ni vitu viwili tofauti.
 
Kumnunua mtu ni kuinunua akili yake,msimamo wake,imani yake ,ama ni kununua kitu gani?

Kumnunuwa mtu kunamfanya apoteze hayo yote hapo juu...Hence KUUPOTEZA UHURU WA KUWA NA MISIMAMO YA TOFAUTI, IMANI YA TOFAUTI NA UHURU WA KUFIKIRI TOFAUTI!

Hivyo basi tafsiri maalum ya kununuliwa ni KUPOTEZA UHURU WAKO!

Binafsi sidhani kama UHAI una BEI!

Hayo ni mambo ya KIFISADI.
There is NOTHING WORTHY OF FIGHTING OTRHER THAN FREEDOM ITSELF!
 
Kumnunua mtu ni kuinunua akili yake,msimamo wake,imani yake ,ama ni kununua kitu gani?

Kumnunua mtu ni kumhonga na kumziba mdomo ashindwe kufanya au kusema kile alichoamini kutokana na mambo ya mlungula, rushwa, hongo ufisadi na uzandiki baradhuli mwingine kama huo.
 
NI SIMPLE...KUUPOTEZA UHURU WAKO!
Hiyo ndiyo BOTTOM LINE!
Kwani hata wachungaji wengine wame PROVE HILO!
 
Hongera sana Zitto
Haya maneno unayasema mara ya pili kwa msisitizo .Mimi sikuwa nataka kuwa msemaji wako lakini umesema yale ambayo nilitaka kuwaambia baadhi ya wana CCM hapa na nje ya hapa .Walidhani una bei mie nikasema huna bei wakabisha .Tuendelee kuwapa somo hawa .Kaza buti
 
Waliuliza kwasababu RIPOTI YA MADINI IKO KWA SICLAIR NA WATU WANAOIFAHAMU NI YEYE,KIKWETE,CHEYO,IDDI SIMBA,MARK BOMANI NA WANAKAMATI WENGINE WA MADINI.
Hivyo basi swali hilo la HUKO TANGA NI LA MSINGI.
Kwamba Zitto amelijibu VIZURI?
Well...Inategemeana na msimamo wako.
Msimamo wangu ni ISOMWE MARA MOJA!
Mushi tunafahamu Zito asingeweza kumpa huyo fisadi ripoti ile.
Aliyempatia ni muungwana. Maana ni marafiki wakubwa wale/
Zito kama angetaka kuitoa nina hakika basi angeliiweka hapa jf maana mara nyingi amefanya hivyo.Na kama yeye au mwanakamati mwingine yeyote angethubutu kuitoa basi ungesikia kelele za wakina nani yule waziri anayetetea siri za serikali? ni ajabu anashindwa kuuliza yule mzungu kapata wapi nyaraka ya siri ya serikali.
 
Mushi tunafahamu Zito asingeweza kumpa huyo fisadi ripoti ile.
Aliyempatia ni muungwana. Maana ni marafiki wakubwa wale/
Zito kama angetaka kuitoa nina hakika basi angeliiweka hapa jf maana mara nyingi amefanya hivyo.Na kama yeye au mwanakamati mwingine yeyote angethubutu kuitoa basi ungesikia kelele za wakina nani yule waziri anayetetea siri za serikali? ni ajabu anashindwa kuuliza yule mzungu kapata wapi nyaraka ya siri ya serikali.

Sipingani na hayo unayosema!
Hata hivyo swali la jamaa wa TANGA NI MUHIMU SANA!
Isipokuwa...Kama tukijuwa kuwa SINCLAIR ALIPEWA RIPOTI KABLA YA KIKWETE..THEN HAINA MAANA KUMLAUMU KIKWETE!
Lakini...Kama Sinclair alipewa ripoti hiyo baada ya JK kupewa...Then na yeye jk mwenyewe atawekwa kwenye MKUMBO!
Tunajuwa ni rafiki wa SINCLAIR..Lakini haina maana kuwa ni yeye tu!
Ama pia haina maana kuwa hakuna mwingine yeyote yule ambaye hana ama hakuwa na uwezo wa either kumpa ripoti hiyo kwa madhumuni flani flani...Ama kuiuza kwa madhumuni flani flani pia.
 
Hakuna mtu mwenye haja ya kumnunua Zitto, wa nini? Yeye ni mpiga makelele tu. Kuna anayeweza kutathmini objectively makelele yake tangu ayaanze yameweza vipi kubadilisha utendaji wa serikali?
 
Zitto this is all I can tell you my friend,let veritas,justitia, ministeruium lead your conscious, if my parochial-school latin is still any good, it means "Truth, justice and service" should be your guide!!!
 
Hakuna mtu mwenye haja ya kumnunua Zitto, wa nini? Yeye ni mpiga makelele tu. Kuna anayeweza kutathmini objectively makelele yake tangu ayaanze yameweza vipi kubadilisha utendaji wa serikali?

Zitto mwenyewe ni member hapa hivyo ameisikia hii kauli yako na kwa ninavyofahamu hata yeye anaweza akawa anajuwa kuwa wewe ni Ballile...So anaweza kukujibu vizuri zaidi kwani mimi na wengineo tunakusikia kwa mbali tu kuwa umenunuliwa na MAFISADI mara baada ya kusomeshwa.
 
Mkapa <-------> In his inaugural address to the new Bunge (Parliament), he renounced his right to be addressed as Mtukufu (His Excellency) the customary epithet preceding the title of President. "I am not his Excellency," he ruled. Five words, so casually spoken, flung a prized cloak of sham and hypocrisy into the fire. Sycophants lost one word from their dictionary, but the lala hoi (ordinary street people) simply loved it.

He followed this up almost immediately by making an unprecedented disclosure of his personal wealth. The President said he owned two houses - one of which he had taken a mortgage to build - four vehicles including a Mercedes Benz, a 10 acre farm, and an undeveloped three acre plot in Dar es Salaam. This gesture was also calculated to indicate an eagerness to clean up the corruption-ridden administration.

Press reaction was instant: "President Mkapa's decision to bare the details of his personal wealth deserves a round of applause. He has shown the way," commented an editorial in Majira, a mass circulation tabloid. "But while disclosure is fine, we need a commissioner of some kind to control, regulate and generally keep an eye on things to prevent leaders using their public office for personal gain and aggrandisement," the editorial continued.


From: African Business | Date: 2/1/1996 | Author: Yahya, Ahmed


Kuna anayeyakumbuka haya?? Ni vema asisifiwe mtu kwa kusema tu ila tusubiri tusifie aliyofanya baada ya kumaliza utumishi wake kwa umma.

We hear your promisses Zitto, but we will be waiting for the summation of your deeds after your service to the wananchi.
 
Zitto mwenyewe ni member hapa hivyo ameisikia hii kauli yako na kwa ninavyofahamu hata yeye anaweza akawa anajuwa kuwa wewe ni Ballile...So anaweza kukujibu vizuri zaidi kwani mimi na wengineo tunakusikia kwa mbali tu kuwa umenunuliwa na MAFISADI mara baada ya kusomeshwa.

Kumbe na wewe ni conspiracist!
 
Zitto mwenyewe ni member hapa hivyo ameisikia hii kauli yako na kwa ninavyofahamu hata yeye anaweza akawa anajuwa kuwa wewe ni Ballile...So anaweza kukujibu vizuri zaidi kwani mimi na wengineo tunakusikia kwa mbali tu kuwa umenunuliwa na MAFISADI mara baada ya kusomeshwa.
Watu kwa kuotea......yaani Zema kawa balille tena?
 
Kumnunua mtu ni kumrubuni mtu akubali kuyaficha maovu yote na kuyatakasa makosa yote na kumlinda mfujaji na kuonekana mtu au raia mwema katika jamii kumbe nyuma ya pazia ameoza.Hii tabia imekuwapo sana katika serikali ya CCM mtu tunamwona hafai lakini kuna watu wananunuliwa ili kuwasafisha na kuonekana weupe hawana uchafu wowote ule.
Tunampongeza Zitto kwa kukataa mamilioni ya mafisadi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom