Hatimaye Zitto Zuberi Kabwe amenena.Amesema kuna mbinu nyingi zinafanywa na maadui wa chadema kumgombanisha na mwenyekiti wake Freeman Mbowe.Katika hilo ametupia lawama baadhi ya vyombo vya habari vinavyomilikiwa na maadui wa Chadema vinavyojaribu kuandika uongo kwamba anampiga vita mwenyekiti wake.Zitto amesema kwa mdomo wake kwamba mbinu za maadui hao kamwe hazitafanikiwa na kufanikiwa kwao ni kama mbingu na Ardhi.Amesema maadui hao wamekosa pa kushika baada ya kuona chadema iko kileleni kuingia ikulu.
Zitto Kabwe amewaambia maelfu kwa maelfu ya wananchi wa Iringa kwamba aliyemkuza kisiasa na kufika hapo alipo ni Freeman Mbowe....Amedai Mbowe alianza kumkuza,kumjenga na kumsaidia tangu akiwa chuo kikuu cha Dar es salaam.Amesema sasa ni nani mwenye ubavu wa kumgombanisha na mlezi wake?
Amewataka maadui wake kisiasa kutafuta mbinu nyingine kwani hiyo imeshindwa na kuzikwa.......
Nawasilisha!!
Zitto Kabwe amewaambia maelfu kwa maelfu ya wananchi wa Iringa kwamba aliyemkuza kisiasa na kufika hapo alipo ni Freeman Mbowe....Amedai Mbowe alianza kumkuza,kumjenga na kumsaidia tangu akiwa chuo kikuu cha Dar es salaam.Amesema sasa ni nani mwenye ubavu wa kumgombanisha na mlezi wake?
Amewataka maadui wake kisiasa kutafuta mbinu nyingine kwani hiyo imeshindwa na kuzikwa.......
Nawasilisha!!