Zitto Kabwe kuunguruma bungeni kuhusu serikali kuuficha umma juu ya kesi ya Acacia

M-mbabe

JF-Expert Member
Oct 29, 2009
13,203
23,020
Muda mfupi uliopita nimewasilisha swali la maandishi Bungeni kuitaka Serikali iueleze umma Kuhusu kesi zote ambazo Jamhuri ya Muungano imefunguliwa kwenye mahakama za kimataifa za usuluhishi ya migogoro ya Biashara, uwekezaji na mikataba. Watanzania wanafichwa Mambo mengi muhimu

Nimechukua uamuzi huu baada ya kupitia nyaraka nyeti za kesi ya Acacia Mining dhidi ya Jamhuri ya Muungano ( LCIA Arbitration No. UN173686 no. 87 ) iliyopo London na kugundua kuwa Serikali yetu inaficha Taarifa Kwa umma wakati Watanzania Ndio watalipa matrilioni ya shilingi....

Kesi iliyoamuliwa juzi dhidi ya @tanescoyetu ilizungumzwa kwenye Taarifa ya CAG ya mwaka huu kwa Hesabu za 2016/17. Lakini pia kesi hii haikuwa yetu kwani Benki ya SCBHK haijawahi kuwa na mkataba na nchi yetu. Uzembe mkubwa umefanyika na hivyo kubambikwa kesi si yetu

Suala la kesi hizi za kibiashara lisipojadiliwa kwa kina wengine tutaachiwa nchi ya kulipa madeni ya kesi tu. Lazima tupewe Taarifa. Mf. Eco Energy Bagamoyo $500m, Symbion $600m, SCBHK $700m, Acacia $2bn! Sasa si kuuza nchi huku pengine kwa kujitakia tu? Bungeni mahala mwafaka.
DmPVlz_WwAAh55y.jpg
 
Hivi ni mikataba ipi bunge lilijulishwa na Waziri wa Sheria kuwa majadiliano hayatawekwa wazi kwa umma?
 
Zitto anahangaika na tunachokiita 'political masturbation' achievement. Acacia haiwezi kuwa na locus stand iwapo itafungua kesi dhidi ya Tanzania kuhusiana na suala la kuzuiwa makinikia. Serikali ina ushahidi (damn evidence) juu ya vitendo vya kugushi (fraud & forgery) vilivyokuwa vikifanywa na Acacia - jambo ambalo ni kinyume na mkataba (MDA). Waache wajaribu waone.
Aidha, kwamba Acacia imeamua kumpatia Zitto kazi maalum (analipwa kwa consultancy assignment hii) ya kutangaza jambo hili hadharani, ni Dhahiri kuwa Acacia wanatafuta kuona public opinion/reaction, na hii ni ishara kuwa Acacia wanaona foreseeable collapse of their case in the London Arbitration Court. Tusubiri!
 
Huna tofauti na waliozikwa , huna hisia zozote kuhusu nchi yako , ni kama maiti ndani ya kaburi .
wewe una hisia gani na Nchi hii iliyoibiwa miaka yote
kwa hiyo wachembe tu na kuondoka na dhahabu, almasi, Tanzanite, na madini yote
leo tunakamata makaikia,
leo wanajificha chooni kwenye migodi
jamani hebu tuwe tofauti na wanaopinga kila kitu
Kim jong Korea kaskazini aligoma Assad wa Syria aligoma muafrika mwenzetu Mugabe aligoma leo Zitto na tundu lissu wanatutisha kuwa kuna wanaume wanazo 2 wanataka madini tuwachekee tu HAYA CHUKUENI
SPIKA TUPILIA MBALI HIYO hoja
 
Zitto anahangaika na tunachokiita 'political masturbation' achievement. Acacia haiwezi kuwa na locus stand iwapo itafungua kesi dhidi ya Tanzania kuhusiana na suala la kuzuiwa makinikia. Serikali ina ushahidi (damn evidence) juu ya vitendo vya kugushi (fraud & forgery) vilivyokuwa vikifanywa na Acacia - jambo ambalo ni kinyume na mkataba (MDA). Waache wajaribu waone.
Aidha, kwamba Acacia imeamua kumpatia Zitto kazi maalum (analipwa kwa consultancy assignment hii) ya kutangaza jambo hili hadharani, ni Dhahiri kuwa Acacia wanatafuta kuona public opinion/reaction, na hii ni ishara kuwa Acacia wanaona foreseeable collapse of their case in the London Arbitration Court. Tusubiri!
Tunza hii comment

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom