Mheshimiwa Zitto huwa amechemka kwenye hili. Uhusiano na Israel ni muhimu sana. Israel wametubeba kwenye mengi sana kiuchumi. Irrigation, JKT (hata magwanda ni kama ya IDF), mafunzo ya kijeshi, kibbutzim etc ni kutoka Israel. Aidha, kwa suala la dini pia Israel ni muhimu kama Saudia ilivyo muhimu kwa imani ya jamaa zetu wengine. Mimi binafsi nimeshakwenda Israel na nitaendelea kwenda Israel kwa ajili ya imani yangu. Pia nilishakwenda Saudia kwa masuala mengine. Tatu, kwa siasa za dunia zinakoenda ni lazima tujiweke vizuri hasa ukizingatia suala la ugaidi na tishio la nchi zinazofadhili ugaidi kama Iran. Ubalozi na Israel ni lazima. Mheshimiwa Zitto atuache na Israel yetu, yeye aendelee na siasa zake whatever his reasoning may be (kama ni alleged udini or anything else). Hongera Rais Magufuli.