MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,974
Zitto Kabwe amewashutumu viongozi wa upinzani walioenda kwenye sherehe za uhuru, Mwanza na kupanda jukwaani kuomba maridhiano ya kisiasa kwa Rais Magufuli.

Ametoa shutuma hizo kupitia mitandao ya kijamii akidai walichofanya ni kujipendekeza kwa Rais ili waachiwe nafasi chache za ubunge mwaka 2020 huku wakiwaacha njia panda wanachama wa vyama vyao waliowaambia wajitoe kwenye chaguzi za serikali za mitaa.

Zitto ameenda mbali zaidi na kudai kinachohitajika kwa sasa Tanzania Bara ni siasa kali kama zilizofanywa na wapinzani huko Zanzibar mwaka 2001 ambako kulipelekea CCM kutaka maridhiano (ametumia neno kuomba poo).

Amemaliza kwa kusema, maridhiano hayaombwi bali yanadaiwa.


Screenshot (7).png

Screenshot (8).png

Screenshot (9).png



====
Hoja za wadau

Mimi namuunga mkono Zitto, haki haiombwi wala hailetwi kwenye kisahani cha chai, inadaiwa.

Kama upinzani nchini unacholilia ni kutendewa haki, hadi ukajitoa uchaguzi wa serikali za mitaa, tulitaraji huo upinzani uidai hiyo haki, lakini sijaona juhudi za upinzani wowote nchini Tanzania ukifanya juhudi zozote kudai haki.

Magufuli alipoingia tuu alipiga marufuku mikutano ya siasa kinyume cha katiba, kilichotokea kwenye ushawishi/ununuzi wa viongozi wa upinzani kuunga mkono juhudi, sote tunakijua. Kilichotokea uchaguzi wa serikali za mitaa, sote tunakijua.

Mbowe akaona inatosha, Chadema haina uwezo wa kudai haki, hivyo ameomba poo kwa Magufuli kumaanisha sasa uendeshaji wa siasa za Tanzania ni kwa hisani ya Magufuli. Badala ya mapambano ya kudai haki, Mbowe ame opt kutafuta suluhu kwa maridhiano ya kisiasa.
P

Mkuu mie kwa hili naona Mbowe yuko sahihi, ni miaka 4 imepita ambayo siasa za upinzani zimepitia shida kubwa na kwa uchaguzi ulivyokuwa ni proof kuwa mwakani hakuna hopes za mpinzani yeyote kurudi.

Sasa kwa muda uliobaki (miezi 10) suluhu ya kisiasa inatakiwa ili uchaguzi huru na haki uhakikishwe so maridhiano ni jambo jema kama upinzani watatala CCM isikilize maoni yao ila siasa za mapambano kwa mtu kama Rais wetu haziwezi saidia sababu ana ego so yuko tayari hata kuua waandamanaji wote kuprove nguvu yake na hyo itakuwa na faida gani kwa upinzani?

Hata wakiandamana wataundiwa kesi nyingine kama ya Akwilina na mwaka unao wote wataishia selo tu. So kama Violent option sio viable ni heri njia zote za kidiplomasia zitumike ili zikifeli basi watakuwa hawana la kupoteza wakianza siasa za kibabe kama ODM kenya.
 
Siasa za Tanzania zinakwenda kwa kasi kweli!

Zitto wa leo anawashutumu viongozi wa CHADEMA kuwa ni wanafiki na wanajipendekeza!

Zitto wa leo yuko tayari kwa mapambano ya ''jino kwa jino'' kuhakikisha serikali ya awamu ya tano inaondoka madarakani!

Rhetoric politics with empty actions!

Tembea Tanzania uone mengi katika siasa!
 
Zitto kapanic kwa lile walilofanya CHADEMA jana, kashtukizwa hakutegemea, anatamani ile nafasi ingekuwa yake kwa tabia zake za ki_opportunist, toka jana ni twitter, insta habanduki huko, eti leo Zitto anataka siasa za mapambano anawafundisha CHADEMA!, wonders shall never end, wakati ule anaenda kukutana na JK watu wanamuuliza kulikoni anasema JK ni sawa na babake, vipi leo Magufuli sio sawa na babake pia?!
 
Aisee umempa za uso Hadi nimefurahi.
Zitto kapanic kwa lile walilofanya CDM jana, toka jana ni twitter, insta habanduki huko, eti leo Zitto anataka siasa za mapambano anawafundisha CDM!, wonders shall never end, wakati ule anaenda kukutana na JK watu wanamuuliza kulikoni anasema JK ni sawa na babake, vipi leo Magufuli sio sawa na babake pia?!
 
Nikiwa jirani wa Zitto Kabwe hapa Mwandiga Kigoma mahali alipozaliwa sijashangaa kabisa kuona upuuzi anaouandika huyu bwana mdogo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo jana ambapo ameshinda siku nzima anaibeza siku ya Watanzania kuadhimisha miaka 58 ya yangu Uhuru.

Hili suala naona kama halitiliwi mkazo inavyopaswa lakini ukweli ni kuwa Zitto hana asili ya Tanzania. Baba yake aliyekuwa Dereva wa Taxi ni mzaliwa wa DRC na Mama yake ni Mzaliwa wa Burundi .

Kwa hiyo Zitto sio mtu anayeguswa na Tanzania na ndio maana kila kitu kizuri kwa nchi hii yeye hupinga na amekuwa akiendesha harakati za kuichua Tanzania ndani ya nchi na kimataifa.

Jana kashupalia kumshambulia Mbowe kwa kuhudhuria sherehe za Uhuru kule Mwanza, sasa mjiulize kuna ubaya gani kwa viongozi wa vyama vya upinzani kuhudhuria sherehe za uhuru? Kwa sababu zile sio sherehe za CCM ni sherehe za nchi.

Ndio maana viongozi wetu wote walikuwepo Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Zanzibar, Waziri Mkuu, Makamu wa Pili wa Zanzibar, Maspika wote hadi wastaafu, Majaji wakuu na Marais Wastaafu wote ispokuwa Rais Mstaafu Kikwete ambaye sote tunajua yupo Marekani kwa majukumu muhimu ya kimataifa.

Mawaziri na Wabunge wenzake walikuwepo, Mabalozi wa nchi mbalimbali, viongozi wa dini nakadhalika.

Kwa tunaomjua na ajenda zake haki hii haiwezi kumpendeza hata kidogo, na mimi nimeamua leo niuseme huu ukweli ili Watanzania mjue.

Mnamuona anavyopambana kupinga miradi mikubwa ya maendeleo, yaani Zitto anatamani Watanzania wakose umeme, kwa hiyo anauchukia kabisa mradi wa bwawa la Nyerere utakaozalisha megawati 2,115 za umeme, anasikia raha kuona watu wanavyohangaika kusafiri kwa treni na ndege na hivyo hapendi kabisa kuona reli inajengwa na ndege zinanunuliwa, hapendi kuona vituo vya afya na hospitali zinajengwa, anafurahishwa kuona Watanzania wanakosa dawa hospitali, wanakosa mahali pa kupata matibabu na hivyo wanakufa. Anachukia kabisa kusikia Tanzania inapata mikopo nafuu kwa ajili ya kuwajengea wananchi miradi ya barabara, maji nakadhalika, na ndio maana anawatisha wananchi kuwa deni la Taifa kubwa mno wakati Wataalamu wa uchumi wanasema ni deni stahimilivu na fedha zinakopwa kwa mambo ya msingi kwa wananchi.

Kwake yeye Zitto taarifa za kuwa uchumi wa Tanzania ni mzuri hazifai, anashupalia shingo na kusikia raha kuwaaminisha Watanzania kuwa hali ya uchumi ni mbaya sana na yupo tayari kupika takwimu za kuonesha uchumi umezorota ili kuwatisha wawekezaji wasije kujenga viwanda na watanzania wakapata ajira na nchi ikapata kodi.

Na mengine mengi, naifahamu vizuri familia ya Zitto. Nashangaa kwa nini mmoja wa viongozi wa Kigoma ambaye baada ya Mama yake kukosa maziwa alipelekwa kunyonya kwa Mama yake Zitto hasemi ukweli huu kuwa huyu dogo hawezi kuguswa na mazuri ya Tanzania.

Zitto Kabwe pengine anaweza kufurahia uhuru wa DRC alikotoka Baba yake au Burundi alikotoka Mama yake. Na kama Watanzania mmesahau alipokuwa Chuo Kikuu Zitto alishaitwa mara kadhaa na Idara ya Uhamiaji kuhojiwa kuhusu uraia wake, kwa tunaofahamu hapa ndio palikuwa pa kupata ukweli wote na kama idara yetu ya uhamiaji ingekuwa shapu ingeumwaga ukweli huu ili Watanzania wajue.

Ndio maana kwa sisi majirani zake hapa Mwandiga hatushangai kuona jinsi anavyotumiwa na wazungu kuivuruga Tanzania, wazungu wanafanya hivyo kwa Zitto kwa sababu wanajua michezo hiyo hiyo ndio wanayoifanya DRC na Burundi ambako hakujatulia miaka na miaka na kila uchao ni mauaji tu. Wanatamani waivuruge Tanzania ili waje kuvuna rasilimali zetu kama wanavyovuna madini kule DRC.

Nampongeza Rais Magufuli na serikali yake kwa jinsi alivyombana Zitto, endelea hivyo hivyo na mwakani iwe ndio mwisho wa huyu mtoto mpuuzi. Alizoea huko tulikotoka walikuwa wanamkweza na kumfanya aonekane wa maana wakati ni kibaraka mkubwa na mtu asiyetakia mema Tanzania. Ni mpinzani asiye na faida kwa nchi. Muda wote anawaza machafuko tu.

Mbowe kazungumza maridhiano yeye anaona Mbowe kakosea, anataka fujo? Anataka vita? Hapo sasa watanzania ndio mnaweza kupata picha ya aina ya mtu huyu. Anachukizwa sana na hali ya amani ya Tanzania kwa sababu anajua hiyo ndio silaha kubwa inayomkwamisha.

Nawasihi watanzania wenzangu mpuuzeni, tujenge nchi yetu, wakati ni huu na kwa bahati nzuri tumepata Serikali ambayo inamwelekeo wa kututoa katika lindi la umasikini, ufukara na uombaomba. Tushike hapo hapo.

Mwananchi wa Mwandiga
Kigoma
Disemba 10, 2019
 
Mimi mwenyewe moyo wangu umesononeka na kuumia Sana wakati naona Magufuli hayuko tayari kuona upinzani nchini.

Magufuli ameua,amefunga wapinzani,amepoteza watu na kujeruhi wapinzani kwa Risasi Leo CDM kirahisi wanasema wanataka maridhiano na CCM hapo wameingizwa chaka,umehalilisha utawala unaokandamiza haki za watanzania.
 
Nitakuwa wa mwisho kumwamini Zitto, huyu ni muongo kupitiliza, huyu hata CCM wanamjua hamaanishi lolote bali anawauza wenzake ilhsli yeye usiku anakula meza moja na ccm
Siasa za Tanzania zinakwenda kwa kasi kweli!

Zitto wa leo anawashutumu viongozi wa CHADEMA kuwa ni wanafiki na wanajipendekeza!

Zitto wa leo yuko tayari kwa mapambano ya ''jino kwa jino'' kuhakikisha serikali ya awamu ya tano inaondoka madarakani!

Tembea Tanzania uone mengi katika siasa!
 
Wakati flani wenzake walimsusia rais bungeni yeye alibaki amesahau?
Zitto kapanic kwa lile walilofanya CDM jana, kashtukizwa hakutegemea, anatamani ile nafasi ingekuwa yake kwa tabia zake za ki_opportunist, toka jana ni twitter, insta habanduki huko, eti leo Zitto anataka siasa za mapambano anawafundisha CDM!, wonders shall never end, wakati ule anaenda kukutana na JK watu wanamuuliza kulikoni anasema JK ni sawa na babake, vipi leo Magufuli sio sawa na babake pia?!
 
Mimi namuunga mkono Zitto, haki haiombwi wala hailetwi kwenye kisahani cha chai, inadaiwa.

Kama upinzani nchini unacholilia ni kutendewa haki, hadi ukajitoa uchaguzi wa serikali za mitaa, tulitaraji huo upinzani uidai hiyo haki, lakini sijaona juhudi za upinzani wowote nchini Tanzania ukifanya juhudi zozote kudai haki.

Magufuli alipoingia tuu alipiga marufuku mikutano ya siasa kinyume cha katiba, kilichotokea kwenye ushawishi/ununuzi wa viongozi wa upinzani kuunga mkono juhudi, sote tunakijua. Kilichotokea uchaguzi wa serikali za mitaa, sote tunakijua.

Mbowe akaona inatosha, Chadema haina uwezo wa kudai haki, hivyo ameomba poo kwa Magufuli kumaanisha sasa uendeshaji wa siasa za Tanzania ni kwa hisani ya Magufuli. Badala ya mapambano ya kudai haki, Mbowe ame opt kutafuta suluhu kwa maridhiano ya kisiasa.
P
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom