Zitto Kabwe, Hayo ndio maazimio ya Bunge ambayo Werema anakwepa kueleza utekelezaji wake

ZZK amewataja walioficha fedha nje, kasema mawaziri wakuu 2003 - 2010 hapa alikuwa Sumayi, Lowassa, Pinda. Mawaziri wa nishati na madini toka 2003 - 2010 , makatibu wakuu wa nishati na madini, makamishna wa nishati na madini itabidi nimuulize Kafumu yeye ana ngapi, wakuu wa majeshi, 2003 -2010 waziri wa ulinzi .

Tuwe wakweli hapa, ni wazi anachokisema ZZK kina maana kubwa sana ya kuzuia mianya ya utoroshwaji wa fedha nje ya nchi na upatikanaji wa fedha haramu na kuzificha. Ila its too political kuliko reality. Je kwanini alisema ana majina kumbe ana vyeo vya wezi. Je kwanini uchunguzi huu anataka ubakie kwa wale wenye vyeo tu wakati BAE ilishirikisha hata wafanyabiashara uchwara.

Je watanzania wanaoishi nje, kufanya kazi, biashara na wana account zilizonona nao wapo kundi gani la kuchunguzwa. Wapo wafanyabiashara wenye account nje ili kurahisha ubadilishaji fedha hasa za kigeni sio wizi wala kukwepa kodi, na wengine ni wizi na kukwepa kodi.

Mpaka sasa sheria za nchi zinasemaje kuhusu mtanzania kuwa na account nje ya nchi. Vita hii itakuwa ngumu sana, kwani wnaotakiwa kuchunguzwa ni wale Prof Kapuya alisema ndio serikali hakuna wa kuwagusa. Hatuwezi kuchunguzi kupitia mfumo wa serikali wa sasa tukapata majibu. Kama EPA ilitiwa kapuni au Meremeta imekuwa donda ndugu, kwa serikali hii hakuna jibu hapa.

ZZK ilimpasa ashirikiane na chama chake ambacho yeye ameamua kukisambaratisha ili kupata majibu ya haya ila kwa solo siioni mbali.
 
Kabla ya kumshambulia Zitto, jiulize je hiyo hoja yake ina manufaa kwako wewe, kwa watoto wako na wajukuu wako au haina maana yoyote?
 
Another funny eti takukuru wachukue hatua.....which takukuru?

Hizi ni sarakasi za kutafuta pa kutokea ajiulize alipojikwaa ajisahihishe ili tuanze kumwamini tena but it will take time.
mkuu unaandika as if wewe ndo umeshikilia ufunguo wa kuaminiwa kwa Zitto. kiukweli Zitto bado anawaTanzania wengi sana ukiacha nyinyi mnaomchafua kwa malengo yenu binafsi. Naona mnatumia nguvu nyingi sana. Pole
 
Zzk ni msomi wala hafanyi mamno kwa kukurupuka, anaelewa anachokifanya tatizo akili zenu ndogo kama Lema ndiomaana hazifikii kile anachokifanya ZZK.

Mwambie Lema ataje majina ya walio lipua bomu c ajidai dvd anayo. Sasa anataka tume ya nini!View attachment 127276

Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa Zitto kamuiga Lema! Kwa sababu Lema hajataja walipuaji wa bomu Arusha na yeye Zitto ndio asitutajie walioficha pesa zetu ulaya!?

Ficha ujinga wako mzee, sio lazma wote wauone!!
 
KWA HIYO BASI naliomba Bunge lako Tukufu liazimie:-

(i) Kwamba Bunge lako Tukufu liunde Kamati Teule kuchunguza raia wa Tanzania wenye kumiliki fedha za kigeni na mali nje ya Tanzania. Kamati Teule hiyo ifanye kazi zifuatazo:-
(a)Kuchunguza mfumo mzima wa utoroshaji wa fedha na kufichwa nje ya nchi;
(b)Kuchunguza na kupambanua mali na fedha haramu dhidi ya halali zinazomilikiwa na raia wa Tanzania katika taasisi za fedha nje Tanzania;
(c)Kuchunguza utaratibu mzima wa kugawa vitalu vya utafutaji mafuta na gesi kati ya mwaka 2003 – 2008;
(d)Kuchunguza mtiririko mzima wa utoroshaji wa fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania kupitia kampuni ya Meremeta na pia kampuni tanzu ya Triannex pty ya Afrika Kusini naDeep Green Finance Limited na kupendekeza hatua za kuchukua dhidi ya wahusika wote wautoroshaji wa fedha kwenda nje;
(e)Kuchunguza umiliki wa Watanzania kwenye kampuni zote zenye mikataba ya utafutaji wa mafuta na gesi hapa nchini na namna umiliki huo umekuwa ukibadilika yaani proceedszilizotokana na mabadiliko hayo ya umiliki na kama kodi stahili zimekuwa zikilipwakutokana na mabadiliko ya umiliki huo; na
(f)Kuchunguza kwa kina mali za Watanzania wote waliowahi kushika nafasi za UwaziriMkuu kati ya mwaka 2003 mpaka 2010, waliowahi kushika nafasi za Uwaziri wa Nishati na Madini, Uwaziri wa Ulinzi, Ukuu wa Majeshi, Ukatibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Ukatibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi, Uanesheria Mkuu wa Serikali, Ukamishna wa Nishati, Ukurugenzi Mkuu waTPDC, Uenyekiti na Ujumbe wa Bodi waTPDC katika ya mwaka 2003 mpaka 2010.

(ii)Kwamba, Serikali ilete Muswada wa Sheria Bungeni ifikapo Mkutano wa 11 wa Bunge kwamba itakuwa ni marufuku kwa Kiongozi yeyote wa Umma au mume au mke wake au
watoto wake kuwa na akaunti katika mabenki nje ya nchi isipokuwa kwa sababu maalumu na kwa kibali rasmi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

(iii)Kwamba, Serikali iwasiliane na Benki ya Dunia ili kupitia Kitengo cha Assets Recovery Unit ili mabilioni ya Fedha na mali zisizoondosheka zinazomilikiwa na Watanzania katika mabenki ya nchini Switzerland, Dubai, Mauritius na visiwa na maeneo mengine yote ambapo hufichwa fedha na mali ili kukwepa kodi na kwamba mali hizo na mabilioni hayo yaliyopatikana kiharamu yarudishwe nchini mara moja.

(iv)Kwamba, katika Muswada tajwa hapo juu, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania aimarishiwe mamlaka ya kutoa kibali kwa Mtanzania yeyote anayetaka kufungua akaunti ya Benki nje ya nchi na kwamba kila mwaka Gavana atatangaza kwenye Gazeti la Serikali na magazeti yanayosomwa na wananchi wengi orodha ya Watanzania walioomba na walioruhusiwa kuwa na akaunti ya benki nje ya Tanzania;

(v)Kwamba, Watanzania wote wenye akaunti za fedha nje waeleze wamezipataje na TAKUKURU wachukue hatua za kisheria dhidi ya watu wote wenye kumiliki fedha na mali kinyume na mapato yao halali;

(vi)Kwamba, Serikali, katika Mkutano wa Bunge wa Kumi na Moja (11) na baada ya Taarifa ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu raia wa Tanzania wenye kumiliki fedha za kigenikwenye mabenki na mali nje ya Tanzania ilete taarifa ya hatua ilizochukua ili kuziba mianya ya utoroshaji wa fedha nje ya Tanzania.

(vii)Kwamba, Serikali katika Bajeti ya mwaka 2013/2014 itaanzisha kodi maalum ‘financial transaction tax’ ya angalau asilimia 0.5 ya thamani ya ‘transaction’ ili kuweza kuwa narekodi zauhakika za fedha ndani na zinazotoka nje ya nchi.

Swali, ni kipi kimefanyika hadi sasa zaidi ya jitihada za kuligeuza suala hili kuwa naming and shaming politics?

My take huu ni mwanzo wa ZZK kujibu mapigo kwa werema na baada ya muda tutamjua nani ni mnafiki kwa watanzania kuhusu fedha haramu zilizofichwa Uswis

SOURCE kwenye fb and twitter wall yake ZZK
Nadhani wananchi, bunge na serikali kwa ujumla tungefarijika sana iwapo Zitto angekuja na majibu ya hoja (I) a-f kwa vile alitutangazia kuwa anafanya uchunguzi/upelelezi ambao kisheria hana mamlaka nao na hata ushahidi wake hauwezi kukubaliwa katika chombo chochote cha kisheria, vinginevyo awe ni agent of legally recognisable investigation authorities e.g police, PCCB, TISS etc. Lakini pia akitoa majibu ya hoja nilizozitaja hapo juu itakuwa rahisi kushawishi umma au serikali kwamba kuna mwelekeo wa kupata dondoo za credible evidence, ambazo zitapelekea kufanyiwakazi hoja zake zilizoko (ii-vii) km kupeleka mswaada wa kutunga sharia bungeni. Lakini pia nina wasiwasi na uzito wa hoja zake kwa ujumla ambazo naziona kama ni nyepesi, za papala na za kufikirika kuliko uhalisia, yaani kwamba ni ngumu sana kutekelezeka, kwa mfano hoja (ii) mimi mtoto wangu au mimi nikiwa masomoni au Napata kazi nje ya nchi sihitaji mpaka nipate kibali cha rais kufungua akaunti benki ; au hoja (iv) lazima nitangaze ktk gazeti la serikali; au hoja (v) kumfanya kila mtu ni mtuhumiwa eti ahojiwe na PCCB juu ya akaunti/mapato yake simply ana akaunti nje? Mbona watanzania wana akaunti za kigeni hata hapa nchini tu basi nao wazuiwe kuwa na hela za kigeni kwa vile sote watanzania tunalipwa kwa madafu na ndiyo hela halali inayotakiwa kutumika Tanzania kote; na mwisho hoja ya kutoza kodi mtanzania akiweka hela nje ni ndoto za alinacha - mtanzania anatozwa interests/kodi huko nje aliko hawezi kutozwa mara mbili, kitu ambacho ningemwelewa Zitto ni kupendekeza serikali ya Tanzania ifanya makubaliano ya kodi, badala ya raia wake kutozwa huko nje waliko basi watozwe nchini kwao km ilivyo kwa tajiri wa Chelsea Abramovich au Makampuni ya nje km Starbucks company wanalipia kodi zao nchini kwao Urusi na Marekani siyo Uingereza. Zitto pia amesahau kuwa yapo maswala ya human rights, freedom of movements, labour and capital ambayo alipaswa ayaone katika lenzi ya hoja zake.
 
Anazidi kunikera huyu zittomafesbuku, huku jf ni member mbona haji kujadili pamoja nasi, anadhani yeye ni wa level tofauti sio?
Unaonaje ukımfuata hukohuko facebook umueleze jınsı anavyokukera. Ila ıtabıdı utumıe ID ya kwelı ukıwa fb na ınabıdı uweke na pıcha ılı ajue anamkera nanı.
 
Mie nina Account niliyopewa huko German kwa kucheza Porn, yaani picha za wakubwa.

Sasa sijui TAKURURU watataka bado niendelee kutoa habari kamili ilikuwaje kwenye hiyo picha?

Kweli Wanasiasa wanajua kuchemka hadi wanafuka mvuke kama Boiler.
 
Zitto simamia msimamo wako pesa ya wa tz irudi. Achana nao hao umewatonesha na hayo makasiri na mapesa yao huko nje ndo maana wanatoa mapovu.
 
Last edited by a moderator:
Mwizi aliyekamatwa ajichunguze mwenyewe weka wazi kila mwenye fedha na jina lake harafu wapelekwe mahakamani au washitakiwe kwa wananchi zzk shusha vitu vinginevyo porojo ndy maana hufiki hata ofisini kwako
 
Haikuundwa Kamati Teule Kama ilivyopendekezwa. Mwekundu tuletee maazimio ya Bunge kwa mujibu wa Hansard ya Bunge. Kisha Mh Zitto na wengine wote wenye taarifa ya kuisaidia timu inayoongozwa na Mh Werema kuchunguza utoroshaji wa fedha (au fedha za Uswiss Kama inavyojulikana)wapeleke tarifa hizo. Majina na Acct za watanzania hao ni muhimu na msingi wa uchunguzi huu.
 
Kumbe wenye MAPESA na vijisenti Uswisi ni hawa basi tunawajua maana si hawa Watanzania wote waliowahi kushika nafasi za
UwaziriMkuu kati ya mwaka 2003 mpaka 2010 ni......
waliowahi kushika nafasi za Uwaziri wa Nishati na Madini ni.....
Uwaziri wa Ulinzi.......
Ukuu wa Majeshi.......,
Ukatibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini.......
Ukatibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi,......
Uanesheria Mkuu wa Serikali..........
, Ukamishna wa Nishati,......
Ukurugenzi Mkuu waTPDC,....
Uenyekiti na Ujumbe wa Bodi waTPDC katika ya mwaka 2003 mpaka 2010.

JAZA NAFASI Zilizoachwa wazi

Fumbo mfumbie mjinga...mwerevu amefumbua. BRAVO mkuu, nafikiri MM ameshayataja majina ya walioficha fedha kiaina. Hata hivyo staili aliyoitumia ni dhaifu iliyojaa woga, anajua kabisa kwa bunge hili hoja hiyo kamwe haiwezi kupitishwa, alitakiwa kumbatanisha vielelezo ili kuwaaminisha watu kuhusu ukweli na uwepo wa jambo hili vinginevyo.....
 
Anazidi kunikera huyu zittomafesbuku, huku jf ni member mbona haji kujadili pamoja nasi, anadhani yeye ni wa level tofauti sio?

Humu ndani watu wako so emotional aisee..... hata penye facts watu wanaweka hisia . Kijana mwenzetu Zitto apewe urais hapo 2015 kama vipi kwa ticket hata ya mgombea binafsi atuongoze kwenda huko tunakokutaka . Kijana ana uweledi wa hali ya juu na ndio maana kila kukicha anaundiwa zengwe .
 
Zitto simamia msimamo wako pesa ya wa tz irudi. Achana nao hao umewatonesha na hayo makasiri na mapesa yao huko nje ndo maana wanatoa mapovu.

Hii vita sio ndogo kama unavyoleta ushabiki.
Kinachomfanya ZZK apate shida ni kauli zake ku-flip flop kwamba alikuwa na majina kumbe alikuwa na vyeo. Hili swala ni nyeti na halihitaji siasa, na kwajinsi dogo anavyolipeleka yeye na mashabiki wake ni la kisiasa sana na sifa binafsi.

Swala la fedha za nje lazima kushirikisha TRA, Takukuru, Bunge, BOT, Ikulu na wananchi ili kulidhibiti na kupata ukweli wa fedha za nje. Kumbuka sio wote wezi wenye account, nyumba, viwanda, nk nje ya nchi. Wapo watanzania wengi sana wenye fedha na kuishi nje, hakuna bank duniani itakayotoa account ya mteja kama njugu kesi moja ya kukiuka haki za mteja bank inaweza kwenda kuzimu.

Hawa wateja kabla account zao kutolewa lazima mlalamikaji bila chenga adhibitishe mahakamani kuwa mteja fulani ni mwizi, fisadi, mkwepa kodi, muuza madawa ya kulevya, mhujumu nk na lazima nchini anapoishi mahakama zithibitishea na nchi alimoficha fedha sheria lazima ithibitishe.

Leo USA (serikali) minahangaika sana kupata kodi ya fedha zilizofichwa Uswiss, sema wenzetu wanatumia nguvu ya kifedha na uchumi kuwabana waswiss hata bado ngoma mbichi, na hii imechukua seriali miezi kama sio miaka.

Swala hili kama ni agenda ya kushinda uchaguzi tu au mtu kuwa maarafu na kupata sifa haiwezi fanikiwa kwani wezi nchi kama TZ ni wengi sana kuliko wenye vipato halali.(kwa wenye fedha). Tz ni nchi pekee duniani kwa kila mwenye zaidi ya milioni 50 TSH zaidi ya 95% ya wenye hizo fedha wamezipata kwa njia isiyohalali, ama wamekwepa kodi, au hawajalipa kabisa, au wameiba, au wameuza mali ya wizi, au wamenunua mali ya wizi, au wamezulumu masikini, nk nk.

Ni wangapi wanalipa kodi wanaponunua bidhaa madukani, au wanaomba risiti ambazo zimelipiwa kodi. Wangapi wanatengeneza magari kwenye garage bubu zisizo na leseni. Wezi ni wengi na wengi wanafaidika na fedha za wizi.

Wanasiasa wengi wamefanikiwa kwa kuchangiwa fedha za wizi nk. Kwa mfano kama unamshikaji yeyote kiongozi wa CCM kuanzia mkoa kwenda juu na amewahi kununulia kitu chochote kile-umekuala fedha ama ya EPA, Meremeta, Buzwagi, Minofu ya samaki kodi, Mkataba feki, Ukwepaji wa kodi, uhujumu uchumi, nk kwani fedha nyingi tunazozipigia kelele kurudishwa zinatokana na mikataba famba na backpay.

Mtandao wa fedha chafu na sawa na biashara ya mafia, kila mtu kwenye msururu kalambishwa kama yamini. Inahitaji ushirikishwaji wa wananchi na wana siasa safi wengi kupata vijisenti hivi. Swaga la fedha za Rada ni mfano ingawaje mpaka leo milioni zetu 5 dola za kimarikali visiwa vya jersey ni kimya sana. Achilia ile USD12 M kule uingereza kwa mhindi mtanzania aliyemgawia big B.

Uchumi wetu utalindwa siku wengi wakiacha unafiki, na kukubali kununuliwa kwa gari, nyumba, cheo na kuuza utu.
 
Back
Top Bottom