Zitto Kabwe apongeza juhudi za Mh.Rais katika ujenzi wa Reli ya kati

Kupongeza penye jambo jema ni mojawapo ya tabia za kistaarabu,kiwerevu na kibusara. Kukosoa penye makosa pia ni jambo jema na ni tabia ya kistaarabu,kiwerevu na kibusara.
Kupokea ushauri,pongezi,ukosoaji na changamoto nako ni jambo jema na la kistaarabu,kiwerevu na kibusara. Tatizo lipo kwako unayeangalia pongezi tu na bila kujali wala kuyaweka yale yaliyokosolewa. Wewe ulichofanya ni propaganda kama za wale aliosema mdau hapo juu kuhusu "hakuna Mungu".
Umenukuu "hakuna Mungu" badala ya kunukuu "Mpumbavu asema hakuna Mungu".
Hapo awali nilishasema kuwa "Mbwa Kumng'ata mtu sio habari kwani ndio kawaida yake ila Mtu akimng'ata Mbwa inakuwa ni habari " Tafsiri ni kwamba tumezoea kumsikia Zitto akikosoa kila uchao na kila jambo kinalofanywa na Serikali kiasi kwamba haiwezi kuwa ni jambo la kushangaza lakini leo hii tunasikia akiipongeza Serikali na haswa kiongozi mkuu..hii lazima iitwe habari na ina maana kubwa sana
 
Kupongeza penye jambo jema ni mojawapo ya tabia za kistaarabu,kiwerevu na kibusara. Kukosoa penye makosa pia ni jambo jema na ni tabia ya kistaarabu,kiwerevu na kibusara.
Kupokea ushauri,pongezi,ukosoaji na changamoto nako ni jambo jema na la kistaarabu,kiwerevu na kibusara. Tatizo lipo kwako unayeangalia pongezi tu na bila kujali wala kuyaweka yale yaliyokosolewa. Wewe ulichofanya ni propaganda kama za wale aliosema mdau hapo juu kuhusu "hakuna Mungu".
Umenukuu "hakuna Mungu" badala ya kunukuu "Mpumbavu asema hakuna Mungu".
Hapo awali nilishasema kuwa "Mbwa Kumng'ata mtu sio habari kwani ndio kawaida yake ila Mtu akimng'ata Mbwa inakuwa ni habari " Tafsiri ni kwamba tumezoea kumsikia Zitto akikosoa kila uchao na kila jambo kinalofanywa na Serikali kiasi kwamba haiwezi kuwa ni jambo la kushangaza lakini leo hii tunasikia akiipongeza Serikali na haswa kiongozi mkuu..hii lazima iitwe habari na ina maana kubwa sana
 
Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati". Zitto Kabwe.

Haya ni maoni ya ZZK.
Hujasoma post yake mpaka mwisho ; soma vzur halaf then rud uandike thread upya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
“ Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati. Hata hivyo, Serikali ni lazima ifungue masikio kusikiliza maoni mbadala katika utekelaji wa miradi mikubwa kama hii ambayo inatumia fedha nyingi, na tumeamua kutumia fedha za ndani.

Uamuzi wa kutumia fedha za ndani ni uamuzi mchungu kwani maana yake badala ya kuwekeza kwenye miradi ya Kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na bidhaa za kuuza nje, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuongeza vyuo vikuu na vyuo vya ufundi ili kuongeza maarifa na wataalamu katika nchi yetu, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuwekeza kwenye kumaliza kabisa tatizo la mtindio wa ubongo (stuntedness) ambalo ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa kwani Watanzania 34 katika 100 wametindiwa ubongo, tumeamua kujenga reli.

Kupanga ni kuchagua. (Serikali) mmeamua kwa niaba yetu kutumia rasilimali fedha zetu kidogo kujenga Reli (na kununua ndege) na haya mengine yasubiri kwanza. Uongozi ni uamuzi. Mmeamua, hatuna namna. Lakini tusikilizeni sisi wawakilishi wa wananchi, mawazo yetu ni kusaidia kupunguza maumivu ya maamuzi yenu bila kuathiri utekelezaji wa miradi husika. Mimi binafsi ninaunga mkono uwekezaji kwenye Reli, lakini siungi mkono namna uwekezaji huu unafanywa.”

Sehemu ya Hotuba yangu Bungeni April, 2017

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo awali nilishasema kuwa "Mbwa Kumng'ata mtu sio habari kwani ndio kawaida yake ila Mtu akimng'ata Mbwa inakuwa ni habari " Tafsiri ni kwamba tumezoea kumsikia Zitto akikosoa kila uchao na kila jambo kinalofanywa na Serikali kiasi kwamba haiwezi kuwa ni jambo la kushangaza lakini leo hii tunasikia akiipongeza Serikali na haswa kiongozi mkuu..hii lazima iitwe habari na ina maana kubwa sana
Anapokosoa anakosoa mambo yenye mantiki na ukosoaji wake huwa unafanyiwa kazi na kuheshimiwa kama anavyosifia? Au akikosoa apuuzwe akisifia ni binadamu kamuuma mbwa?
 
Hapo awali nilishasema kuwa "Mbwa Kumng'ata mtu sio habari kwani ndio kawaida yake ila Mtu akimng'ata Mbwa inakuwa ni habari " Tafsiri ni kwamba tumezoea kumsikia Zitto akikosoa kila uchao na kila jambo kinalofanywa na Serikali kiasi kwamba haiwezi kuwa ni jambo la kushangaza lakini leo hii tunasikia akiipongeza Serikali na haswa kiongozi mkuu..hii lazima iitwe habari na ina maana kubwa sana
Wala hata hajapongeza ; ni kukosa namna kama alivyosema:

“ Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati. Hata hivyo, Serikali ni lazima ifungue masikio kusikiliza maoni mbadala katika utekelaji wa miradi mikubwa kama hii ambayo inatumia fedha nyingi, na tumeamua kutumia fedha za ndani.

Uamuzi wa kutumia fedha za ndani ni uamuzi mchungu kwani maana yake badala ya kuwekeza kwenye miradi ya Kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na bidhaa za kuuza nje, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuongeza vyuo vikuu na vyuo vya ufundi ili kuongeza maarifa na wataalamu katika nchi yetu, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuwekeza kwenye kumaliza kabisa tatizo la mtindio wa ubongo (stuntedness) ambalo ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa kwani Watanzania 34 katika 100 wametindiwa ubongo, tumeamua kujenga reli.

Kupanga ni kuchagua. (Serikali) mmeamua kwa niaba yetu kutumia rasilimali fedha zetu kidogo kujenga Reli (na kununua ndege) na haya mengine yasubiri kwanza. Uongozi ni uamuzi. Mmeamua, hatuna namna. Lakini tusikilizeni sisi wawakilishi wa wananchi, mawazo yetu ni kusaidia kupunguza maumivu ya maamuzi yenu bila kuathiri utekelezaji wa miradi husika. Mimi binafsi ninaunga mkono uwekezaji kwenye Reli, lakini siungi mkono namna uwekezaji huu unafanywa.”

Sehemu ya Hotuba yangu Bungeni April, 2017

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wala hata hajapongeza ; ni kukosa namna kama alivyosema:

“ Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati. Hata hivyo, Serikali ni lazima ifungue masikio kusikiliza maoni mbadala katika utekelaji wa miradi mikubwa kama hii ambayo inatumia fedha nyingi, na tumeamua kutumia fedha za ndani.

Uamuzi wa kutumia fedha za ndani ni uamuzi mchungu kwani maana yake badala ya kuwekeza kwenye miradi ya Kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na bidhaa za kuuza nje, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuongeza vyuo vikuu na vyuo vya ufundi ili kuongeza maarifa na wataalamu katika nchi yetu, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuwekeza kwenye kumaliza kabisa tatizo la mtindio wa ubongo (stuntedness) ambalo ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa kwani Watanzania 34 katika 100 wametindiwa ubongo, tumeamua kujenga reli.

Kupanga ni kuchagua. (Serikali) mmeamua kwa niaba yetu kutumia rasilimali fedha zetu kidogo kujenga Reli (na kununua ndege) na haya mengine yasubiri kwanza. Uongozi ni uamuzi. Mmeamua, hatuna namna. Lakini tusikilizeni sisi wawakilishi wa wananchi, mawazo yetu ni kusaidia kupunguza maumivu ya maamuzi yenu bila kuathiri utekelezaji wa miradi husika. Mimi binafsi ninaunga mkono uwekezaji kwenye Reli, lakini siungi mkono namna uwekezaji huu unafanywa.”

Sehemu ya Hotuba yangu Bungeni April, 2017

Sent using Jamii Forums mobile app
anaunga mkono uwekezaji huu usimlishe maneno mengine
 
Hongereni sana MAJUHA WA CCM. Kuna mtu aliwahi kutamka kwamba: BIBLIA INASEMA "HAKUNA MUNGU"! Alinukuu Zaburi ya 14:1 na Zaburi ya 53:1. Tatizo ni kwamba jinsi alivyoichukua nukuu yake ni kama Zitto alivyonukuliwa na Gazeti hilo na mlivyobeba hiyo nukuu. Aya nzima inasema hivi: MPUMBAVU AMESEMA MOYONI MWAKE KWAMBA "HAKUNA MUNGU"
Kwa hiyo siyo kweli kwamba Biblia inasema hakuna Mungu, ila Biblia inachosema ni kwamba Mpumbavu husema moyoni mwake kwamba Hakuna Mungu. Sasa katika kuhangaika kuonesha kwamba hata Biblia inakiri kwamba Hakuna Mungu, ndiyo akajiingiza kwenye huo mchezo wa kupindisha maneno.

Zitto Kabwe alichosema ni kwamba kujenga Reli kwa ujumla wake ni jambo jema. sasa akaja kwenye kile kinachofanyika hapa kwetu chini ya Magufuli, Nukuu nzima ya Zitto katika para iliyonukuliwa ni hii:

Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati. Hata hivyo, Serikali ni lazima ifungue masikio kusikiliza maoni mbadala katika utekelaji wa miradi mikubwa kama hii ambayo inatumia fedha nyingi, na tumeamua kutumia fedha za ndani.

Zitto ameamua kuwa muungwana kwa kuanza kupongeza nia. lakini amekosoa sana utekelezaji.
Lakini kwa nini Gazeti limeamua kufanya hivyo? na kwa nini hawa MAJUHA wetu maarufu wa CCM wamekimbilia kuinukuu kwa kasi hivyo? THEY ARE DESPERATE FOR PRAISE FROM THE OPPOSITION. wana njaa ya kupata hongera kutoka upinzani. watapindisha maneno na kubadili usemi kila mara ili kuonesha kwamba Wapinzani wanaunga mkono vitendo vya serikali ya JPM. Hiyo desperation ndiyo harufu mbaya inayotuambia kwamba kuna mzoga mahali umefichwa.
Huyo Jpm mwenyewe huwa mnakata kakipande na kukajengea hoja,kwa Zito mnaleta ujuaji uchwara wa kucopy post nzima.Hata Usome vipi kuanzia akipoanza kupongeza ktk hiyo nukuu hadi kwenye nukta ni maelezo yaliyojitoshereza kabisa,Hiyo ya Hata hivyo haihusiani na pongez zake ktk swala la reli.Tuseme tu zito kapongeza ujenzi wa Reli ya kati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom