Zitto Kabwe aomba Bunge lisimamishe shughuli zote juu ya Jairo!

If Mizengo Pinda is man enough he should tenderer his resignation forthwith; he has lost his credibility in parliament and his integrity is in tatters!! As a primeminister hana hadhi tena afadhali afe njaa abaki na ubunge wake lakini awe na heshima; mkweree amemvunjia heshima kabisa na sasa hawezi kuwa effective!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Unajua ukiona baba mzazi anasimama na kusema mwanangu wa miaka 25 ni bikira na nina ushahidi jamani lazima
umwogope huyo mzee kama ukoma ...so sidhani beaty anahitaji kushindana zaidi na hawa waheshimiwa hali
mwanamke mwenyewe aakishirikiana na washenga wake cag na luhanjo wanajulikana sio bikira
 
Nasubilia huo mchakato kwa hamu. Lukuvi amejaribu kuizima kama kawaida yake Ndungai akagoma, ngoja tusikilizie. Af bungeni minong'ono ya chini inasikika sana nahisi hata wabunge wamekamia sana.
 
Maswali ambayo hata auditor hajayajibu ama kwa makusudi au kwa kusahau,
Wizara hiyo ina watumishi wangapi waliokwenda Dodoma ambao wanatafutiwa mabilioni hayo ya fedha?
Je, si kweli kwamba watumishi waliokwenda Dodoma wote walishaomba fedha zao za kujikimu?

Chukua ripoti nzima ya CAG uisome hayo yote yamo ! tafuta hiyo ripoti mie nimeisha isoma
 
Ombi maalumu kwa mama Beatrice Shelukindo (mbunge)

Tafadhali tunakuomba uombe radhi kwa wabunge na watanzania uliotudanganya kuwa David Jairo aliwahonga wabunge wakati ni mpango mahsusi unaofanyika wakati wote wa kipindi cha kuandaa bajeti ya wizara ya madini na nishati ya umeme
usiopatikana lakini malipo yanafanyika bila wasiwasi wowote.

Bila kutuomba radhi utajiweka kwenye orodha ya wapambanaji mfu kikundi cha CCJ, wakiongozwa na kamanda wao mfu SS.

Bila kutuomba radhi utawekwa kwenye kundi la mavuvuzela wa chama cha majangili wa rasilimali za watanzania kama kule Ngorongoro, wale wanyama wetu.

NATANIA TUU MAMA WALA USIHANGAIKE WATANZANIA NDIVYO TULIVYO.

Anayetakiwa kung'atuka ni Mhe. Pinda na Baraza lote la Mawaziri kwa kutojua kwamba ni KAWAIDA KWA IDARA HUSIKA KUCHANGIA FEDHA KUFANIKISHA JAMBO.
 
Mheshimiwa Zitto mbunge wa CHADEMA Hajaridhika kuhusu suala la kurudishwa kazini kwa Jairo kwa wanaofutalilia bunge leo ni siku ta ya kitimtim, tayari kamati ndogo ya bunge imeshaingia ndani kwa ajili ya kujadili jambo hilo ili waje na majibu kwa zitto

Zitto anataka shughuli zote za serikali bungeni zisimame na bunge iache kuzijadili kwa kuwa serikali imelidharau bunge, leo ni leo
 
zitto katoa hoja ya bungeni taarifa ya CAG ipelekwe bungeni mara moja..wabunge wengi wameunga mkono hoja ya zitto, ndugai kaenda kwenye faragha maana hali ni tete amemomba simbachawene avae joho kwa mda mfupi
Zitto we Magandwa ya Magamba unayatakia nini?

Utakutwa kwenye crossfire uwe collateral damage bure wakati tunakuhutaji kwenye vita vingine vya wananchi wa ukweli. We hujui vita vya panzi neema ya kunguru. Tena ukishupalia wewe, Magamba yataungana kama kawaida and then utakuwa umesaidia.

Sana sana tunachotaka kwako kama m/kiti wa kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma, UCHUNGUZE kama wizara zote zilikuwa zinafanya huu mchezo.
 
500millions zilizochangishwa zilitumikaje? Maofisa waliondaa bajeti na kwenda bungeni kuiwasilisha hawakuchukua imprest ktk idara zao?
Luhanjo alisema ni kawadi mamlaka zilizo chini ya wizara fulani kuchangia fedha kwa ajili ya kufacilitate bajeti yao. Naona hapa alitaka kutuaminisha kuwa Jairo hana kosa.
 
Tatizo sio kumwadabisha Jairo,aliwaona komedi kwa sababu kila kilichotokea hakikuwa sahihi kwake,sasa afanye nini? hana hatia.Pinda alizungumza bila ushahidi wowote,alitumia maneno ya wanasiasa kumhukumu jairo.

Kama hana kosa hakuna maamuzi magumu Ya nini? kwa manufaa ya Nani?...CCM inabaki chama bora chenye misingi imara na kinachosimamia tararibu na kanuni.

Ningekuwa karibu na wewe ningekupa mkono wa pongezi kwa kuthubutu kusimamia kile usichokiamini ili mradi mkono uende kinywani!!!!

Tiba
 
Kusingekuwa na ushabiki wa vyama serikali ya Kikwete ilikuwa inaanguka kwa ishu ya Jairo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
jamani mnashangaa nini? kama waliomtuhumu wameambiwa ni komedy na baadae wanafikiri kwa makalio,hakuna hatua zinazochukuliwa kwa kulinda serikali,ngoja na wengine watakuja na zito zaidi ya haya na bado bunge litafumbia macho tu!!!!!
 
Ghost Rider mm nakuaminia sana kwa kutoa live updates na za hapo kwa papo....nini kimetokea mbona mood imekwisha. Mkuu Invicible naomba mwongozo huyu jamaa ni muhimu sana..
 
Badala ya kupeleka PCCB wao walimwita CAG alafu wanasema hapakuwa na rushwa wala Jah hana hatia,kwani CAG anafanya kazi ya PCCB siku hizi?this country bwana!

Natamani iwe kama ya Richmond ambayo kwanza Joseah aliisafisha baadae bunge likaikomalia mpaka maDons wakachomolewa
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom