Zitto Kabwe alaumu Tanzania kutopiga kura kulaani vitendo vya unyama dhidi ya Rohingya huko Myanmar

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Mbunge wa Kigoma Mjini, (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe ameshangazwa na nchi ya Tanzania kutopiga kura kulaani vitendo vya unyama na ukatili unaofanywa na Serikali ya Myanmar.

"Juzi Umoja wa Mataifa kulikuwa na kura ya Azimio la kulaani vitendo vya unyama dhidi ya watu wa kabila la Rohingya huko Myanmar. Nchi yetu ya haikupiga kura (abstained).

Kitendo cha aibu sana Tanzania kushindwa kulaani vitendo vya namna hii. Sera yetu ya Mambo ya Nje imebadilika mno tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani.

Kule Rakhine State Myanmar watu wanauawa, watoto wa kike wanabakwa (sijui makamu wa rais Samia Suluhu Hassan anajisikiaje kuona wizara yake ya mambo ya nje inaona aibu kukemea ubakaji wa watoto wa kike).

Che Guevara alipata kusema kuwa rafiki yangu ni yule ambaye anatetemeka akisikia tu kuna mtu anaonewa popote pale duniani. Tanzania ya leo sio tu haitetemeki, inaona aibu kukemea uvunjifu wa haki za binadamu ". Amemaliza kwa kuandika hivyo kwenye ukurasa wake wa Twitter, Zitto Kabwe
 
huyo kibaraka kwelii hajui asemacho kwani abstain sio kura??hiyo ni kura ya kutofungamana na upande wowote,aache kuwarubuni watu labda wa huko kwao Kigoma. nchi 26 imepiga kura ya kutofungamana na jambo hilo 10 wamekataa,mwambieni aache kukurupuka na ajue hata kuabstain nayo ni kura.
kuna tofauti kubwa kati ya kutokupiga kura na abstention.
 
Nadhani hatua ya kulaani pekee bila kuchukua hatua ni unafiki pia
Inasaidia mkuu, kumbuka mauaji ya watu kutiwa katika viroba wengi wetu tunalaani hata kama hakuna uwezo wa kuchukua hatua. Unyama na ukatili lazima vilaaniwe, vikemewe na ikiwezekana vikomeshwe
 
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ameshangazwa na nchi ya Tanzania kutopiga kura kulaani vitendo vya unyama na ukatili unaofanywa na Serikali ya Myanmar.

"Juzi Umoja wa Mataifa kulikuwa na kura ya Azimio la kulaani vitendo vya unyama dhidi ya watu wa kabila la Rohingya huko Myanmar. Nchi yetu ya haikupiga kura (abstained).

Kitendo cha aibu sana Tanzania kushindwa kulaani vitendo vya namna hii. Sera yetu ya Mambo ya Nje imebadilika mno tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani.

Kule Rakhine State Myanmar watu wanauawa, watoto wa kike wanabakwa (sijui makamu wa rais samiah Suluh Hassan anajisikiaje kuona wizara yake ya mambo ya nje inaona aibu kukemea ubakaji wa watoto wa kike).

Che Guevara alipata kusema kuwa rafiki yangu ni yule ambaye anatetemeka akisikia tu kuna mtu anaonewa popote pale duniani. Tanzania ya leo sio tu haitetemeki, inaona aibu kukemea uvunjifu wa haki za binadamu ". Amemaliza kwa kuandika hivyo kwenye ukurasa wake wa Twitter, Zitto Kabwe
Mwambie yeye kama kiongozi mkuu wa chama chake alaani kwa niaba yetu! alishindwa kulaani ya kibiti hayo mengine yanamuwashia nini?
 
Hata tukilaani haitasaidia wasiendelee kuuwana ni unafiki tu ndiyo unasumbua hawa wanaojifanya kulaani bila hatua sitahiki hawa jamaa hawajaanza leo kuuwana ila hatujaona hatua stahiki zikichukuliwa na mataifa makubwa si wapeleke walinzi wa umoja wa mataifa
 
So ukipiga hiyo kura inasaidia nini kama hakuna hatua mahsusi zinazochukuliwa kumaliza hilo tatizo. Kama Ghadafi alipigwa kwa sababu za kutungwa tungwa tu kwa nini hayo mataifa makubwa yasiende kumaliza hilo tatizo Myanmar badala ya kusema eti ipigwe kula ya kulaani, hiyo laana inasaidia nini haswa.
 
Mbunge wa Kigoma Mjini, (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe ameshangazwa na nchi ya Tanzania kutopiga kura kulaani vitendo vya unyama na ukatili unaofanywa na Serikali ya Myanmar.

"Juzi Umoja wa Mataifa kulikuwa na kura ya Azimio la kulaani vitendo vya unyama dhidi ya watu wa kabila la Rohingya huko Myanmar. Nchi yetu ya haikupiga kura (abstained).

Kitendo cha aibu sana Tanzania kushindwa kulaani vitendo vya namna hii. Sera yetu ya Mambo ya Nje imebadilika mno tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani.

Kule Rakhine State Myanmar watu wanauawa, watoto wa kike wanabakwa (sijui makamu wa rais Samia Suluhu Hassan anajisikiaje kuona wizara yake ya mambo ya nje inaona aibu kukemea ubakaji wa watoto wa kike).

Che Guevara alipata kusema kuwa rafiki yangu ni yule ambaye anatetemeka akisikia tu kuna mtu anaonewa popote pale duniani. Tanzania ya leo sio tu haitetemeki, inaona aibu kukemea uvunjifu wa haki za binadamu ". Amemaliza kwa kuandika hivyo kwenye ukurasa wake wa Twitter, Zitto Kabwe
Ingekuwa wanao uwawa na kubakwa ni wakatoliki tungekuwa wa mwanzo kupiga kura ya ndio.
 
Back
Top Bottom