Cannabis
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 8,937
- 25,279
Kiongozi wa Chama, cha ACT Wazalendo ndugu Zitto Kabwe amekamatwa na kushikiliwa na Jeshi La Polisi baada ya kufika Kituo cha Polisi Oysterbay kuwaona Viongozi wa Vyama vya Upinzani waliokamatwa tangu Juzi kwa ajili ya kuandaa maandamano ya amani ya kudai Uchaguzi mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.
===
UJUMBE WA ZITTO KABWE KWA WATANZANIA KABLA HAJAKAMATWA NA POLISI
Mtanzania Mwenzangu
Kama Unasoma Ujumbe huu, fahamu kuwa nimeshikiliwa kituo cha Polisi Dar es salaam. Baada ya Viongozi wenzangu Kukamatwa kwa kudai Uchaguzi Mpya na Tume Huru za Uchaguzi Tanzania na Zanzibar, niliona leo ni vyema kwenda kuwaona, kuonyesha mshikamano nao na kuwafariji kuwa tulioko nje tunaendeleza mapambano.
Kuchagua Viongozi ni haki yetu ya Kikatiba, Haki hii imeporwa na watawala wakishirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama. Ni wajibu wetu wetu kama Wazalendo wa Taifa hili kuipigania haki hiyo iliyoporwa. Mimi naamini Maandamano ya Amani ni haki ya Kila raia
Mimi, Kiongozi wenu, SITACHOKA kuipigania haki hiyo mpaka pumzi ya mwisho ya uhai wangu. Nawasihi sana endelezeni mapambano hayo. Kukamatwa kwa Sisi Viongozi wenu kuwe chachu kwenu kuendeleza ya mapambano haya kwa njia za amani (Non Violence Means)
Sisi sio wa kwanza, na wala hatutakuwa wa mwisho kupitia mitihani hii. Mapambano ni ya kwenu na Kizazi chenu. Mapambano Haya ni yetu sote.
#TusiacheKupambana
#AlutaKontinyua
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Novemba 4, 2020
Dar es salaam
===
UJUMBE WA ZITTO KABWE KWA WATANZANIA KABLA HAJAKAMATWA NA POLISI
Mtanzania Mwenzangu
Kama Unasoma Ujumbe huu, fahamu kuwa nimeshikiliwa kituo cha Polisi Dar es salaam. Baada ya Viongozi wenzangu Kukamatwa kwa kudai Uchaguzi Mpya na Tume Huru za Uchaguzi Tanzania na Zanzibar, niliona leo ni vyema kwenda kuwaona, kuonyesha mshikamano nao na kuwafariji kuwa tulioko nje tunaendeleza mapambano.
Kuchagua Viongozi ni haki yetu ya Kikatiba, Haki hii imeporwa na watawala wakishirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama. Ni wajibu wetu wetu kama Wazalendo wa Taifa hili kuipigania haki hiyo iliyoporwa. Mimi naamini Maandamano ya Amani ni haki ya Kila raia
Mimi, Kiongozi wenu, SITACHOKA kuipigania haki hiyo mpaka pumzi ya mwisho ya uhai wangu. Nawasihi sana endelezeni mapambano hayo. Kukamatwa kwa Sisi Viongozi wenu kuwe chachu kwenu kuendeleza ya mapambano haya kwa njia za amani (Non Violence Means)
Sisi sio wa kwanza, na wala hatutakuwa wa mwisho kupitia mitihani hii. Mapambano ni ya kwenu na Kizazi chenu. Mapambano Haya ni yetu sote.
#TusiacheKupambana
#AlutaKontinyua
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Novemba 4, 2020
Dar es salaam