Zitto: Gharama ya Kitambulisho cha Taifa kupanda kutoka shilingi 17,000 mpaka kufikia shilingi 26,000 kuna giza nene

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371


Zitto amehoji kwa kirefu juu ya kupanda kwa gharama hizo katika ukurasa wake wa facebook na pia amegusia gharamaa za pasi za kusafiriia za kielekroniniki na kudai kuwa huko teundako kuna giza kuliko tutokako.

=========

Gharama za kitambulisho cha Taifa yapanda kutoka TZS 17,000 mpaka TZS 26,000

Mwaka 2016 Serikali ya awamu ya 5 iliwashitaki watendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ( NIDA ) kwa sababu gharama za kutengeneza kitambulisho zilikuwa kubwa mno.

Kamati ya PAC imekuta kwamba menejimenti mpya iliyopewa kazi ya baada kuwatumbua kina Dickson Maimu iliingia mkataba mpya na mkandarasi na kupandisha bei ya kitambulisho kwa shilingi 9,000 zaidi hadi kufikia TZS 26,000 kwa kitambulisho kimoja.

Mbunge wa Tarime vijijini ndg. John Heche ameibua jambo hilo Bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani hakuweza kutoa majibu ya kutosheleza.

Ni dhahiri juhudi za kuficha madudu ya Serikali ya awamu ya 5 hazitafanikiwa na kashfa za ufisadi za Serikali ya awamu ya 5 zitakuwa na madhara makubwa kwa Serikali kuliko inavyofikiriwa.

Jana Zimezinduliwa pasi mpya za kusafiria ambazo tunaambiwa zimeokolewa zaidi ya shilingi 250 bilioni zilizotaka kupigwa. Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya PAC inaonyesha kuwa e-passport ni eneo moja tu la mradi wote na hiyo gharama ya USD 57m ni ya eneo moja tu. Kwamba maeneo mengine kama ya e-visa, e-immigration services, e-border nk yana gharama zake. Nataraji CAG atafanya ukaguzi wa manunuzi ya mradi huu wa pasi za kusafiria.

Huko tuendako, kuna giza zaidi kuliko tutokako
 
Zimepanda tena.? mbona wamekipamba sana hivi? kumbe tunapigwa.! aisee hawa jamaa ni wabaya kwa mishiko!
 


Zitto amehoji kwa kirefu juu ya kupanda kwa gharama hizo katika ukurasa wake wa facebook na pia amegusia gharamaa za pasi za kusafiriia za kielekroniniki na kudai kuwa huko teundako kuna giza kuliko tutokako.

Fungua hiyo link ujisomee alichoandika.
Siku nzima unakaa kufukua mitandao upate habari za udaku udaku. Inakusaidia nini lakini?
 
hiyo ni gharama ya utengenezaji au ndo tunaanza kuuziwa??
 
Vitambulisho vya NIDA ni bure, kama gharama zinazobebwa na serikali zimepanda alete documents inayo halalisha ujumbe wake na si maneno tupu.
 
Vitambulisho vya NIDA ni bure, kama gharama zinazobebwa na serikali zimepanda alete documents inayo halalisha ujumbe wake na si maneno tupu.

Hakuna bure katika dunia labda oxygen tu nayo Vuta, usipolipa jua kuna njemba limeclear bill yako na docs toa wewe.
 


Zitto amehoji kwa kirefu juu ya kupanda kwa gharama hizo katika ukurasa wake wa facebook na pia amegusia gharamaa za pasi za kusafiriia za kielekroniniki na kudai kuwa huko teundako kuna giza kuliko tutokako.

Fungua hiyo link ujisomee alichoandika.

Zitto aliwahi kusema huko tuendako bada ya miezi mitatu nchi itapata baa la njaa la karne!
Sijui uchumi wake anasomea wapi,hata gharama za uchaguzi mwaka 2020,hazitakua sawa na 2015,atuambie basi na hili huko tuendako kuna nini?
 
Back
Top Bottom