Zitto: Dr Ulimboka kutekwa, kupigwa na kuumizwa; Serikali inawajibika kutueleza

Haiingii akilini kwa binaadam yeyote mwenye fikra japo kidogo, eti Serikali wakuchukuwe, wakupige, wakutupe Mabwepande halafu waje haki za binaadam kukuota.
Haikuingii akilini? Inakuingia wapi? Du! Mzee dhaifu kaleta mambo ya Cameroon naona yamekunogea
 
serikali ya ccm inatakiwa itafakari.. Je baada ya kumuua sokoine ufisadi/uhujumu uchumi uliwafikisha wapi, je ndo ulikuwa na manufaa au ndo laana inayoitafuna serikali hadi leo,je hali ya uhujumu uchumi imefikisha wapi taifa, je kama sokoine angebaki hai hali ingekuwa hivi????
Walipomuuwa kolimba, je kupoteza dira kwa ccm kumefikia wapi? Je kwa kuumua ndo walipata dira au ndo walipotea njia na kutokea hapa walipo? Je ccm iliimarika baada ya kumuuwa au ndo ilizidi kuyumba???
Walitarajia wamwmuua dr ulimboka, je wanafikiri kwa kufanya hivyo ndo wataimarisha huduma za afya? Je ndo migomo itaisha? Maslahi ya madaktari hayatadaiwa?

tunashughulika na kuilazimisha zanzibar ibaki kwenye muungano , hao madaktari na wanyamaze . Sio suala muhimu kwa wakati huu vyenginevyo tutawashughulikia ipasavyo hao wanatumiwa na waarabu kuleta usultani
 
pole sana dr. Ulimboka. Tunakuombea kwa mungu akupe nguvu ya uponyaji haraka.

Kwa wale wanaofikiria watazima vuguvugu la kujikomboa kwa mtanzania kwa kumteka na kumuumiza dr. Ulimboka wajue ya kwamba wameweka petroli kwenye moto. Ole wao, siku zao zimefikia mwisho.

Kwa wanaokumbuka historia ya ufaransa, binti mfalme marie-antoinette hakuelewa kwa nini watu walikuwa wanaandamana, akamuuliza mama yake malkia kwa nini wanaandamana. Alipojibiwa 'wanaandamana kwa kuwa hawana mikate', marie-antoinette alijibu 'si wale keki?'

hii inadhihirisha viongozi wa tanzania hawazijui shida za walalahoi wanaolala chini kwenye hospitali zetu, wanaokufa kila siku kwa kuwa hospitali hazina vifaa kama x ray, hakuna dawa, hakuna hata bandage za kufunga vidonda. Madaktari wanachodai ni mazingira bora ya huduma za afya na vitendea kazi. Kwa kifupi wanataka serikali iwakumbuke watanzania wanaoteseka bila huduma za afya ambazo ni haki yao ya msingi, wakati viongozi na familia zao wanakimbizwa afrika ya kusini, india na hata ulaya kupata matibabu. Badala ya kutafuta ufumbuzi wa madai haya, serikali inawajibu kwa vitisho na hata kufikia kumteka kiongozi wa madaktari.

Familia ya kifalme ufaransa iliondolewa madarakani na marie-antoinette pamoja na wenzake walielewa maana ya nguvu ya umma. Hatuhitaji keki, tunaomba haki yetu tupate huo mkate!

Mpaka kieleweke!

ulimboka anatumiwa na waarabu huyo anataka kuleta usultani tanganyika , serikali ya ccm itamshughulikia ipasavyo
 
Ulimboka ana hadhi kubwa kuliko hata Spika nadhani Serikali hawakujua .Ulimboka Mungu ampe afya njema apone kilicho jiri .Kuumizwa namna hii kunawafanya watu wa Mbeya kuwaza mara 2 sasa .Mwakyembe na sasa the guy kisa haki tu ambazo ziko wazi .Mimi naamini Rais na Amiri Jeshi mkuu Ndugu Jakaya Kikwete atasma tu hatangoja kwenda kumpa pole pekee au vinginevyo .Naamini Polisi IGP atasikika kwa kuwa swala hili litahamia sasa kwa wahisani .Tanzania si Russia .
 
kumbe mabwe pande imeachwa na serikali kuwa sirikali ya mauaji, basi msitu ule upigwe moto kwani hauna faida zaidi ya mauaji. Watu wanakosa viwanja wao wanaujaza damu za watu wasio na hatia.

yani bora serikari wajenge jiwe la msingi tu ktk msitu huu kuhitimisha eneo hili limetengwa kwa ajili ya kufanyia mauaji ya raia yanayofanywa na serikali. Get well Dr Ulimboka.
 
Jumatatu Asubuhi katika Kipindi cha Power Breakfast kinachoruswa na Radio Clouds...Mtangazaji mmoja (sina uhakika ilikua ni sauti ya PJ au Gerald Hando) aliongea maneno makali sana kuhusu Dr. Ulimboka.

Maneno ya kumdhalilisha, kumkashifu, kumfanya aonekane hana maana katika jamii, aonekane mbinafsi (naamini wengi tuliyasikia). Ni dhahiri hayakua maneno ya watangazaji bali wao walitumika tu!

Siku iliyofata (Jumanne Usiku) tunaskia Dr. katekwa na kupigwa. Kuna haja ya kuwachunguza watangazaji hawa..hakuna shaka aliyewaambia wayaongee maneno haya atakua amehusika au anajua waliohusika na mpango wa kumdhuru Dr. Ulimboka
 
Serikali inapokuwa inahusishwa na vitendo vya kinyama kama hivi ni hatari sana..ila kila lenye mwanzo halikosi mwisho
 
kwanza ndugu zangu watanzania tuungane mkono tuandamane kama ingekuwa ni arusha kusinge kaika sema dar masharobaro hawawezi
 
Haiingii akilini kwa binaadam yeyote mwenye fikra japo kidogo, eti Serikali wakuchukuwe, wakupige, wakutupe Mabwepande halafu waje haki za binaadam kukuota.

zomba nani mwingine anayeweza kufanya jambo kama hilo halafu akabaki salama? Serikali ina nguvu sana na ina resources za kufuatilia yale inayotaka kufuatilia.Kama ni mambo mema, basi nchi itajaa mema...kama ni ukauzu ndo hivyo tena...watu watakuwa wanaishi kama nchi siyo yao.
 
Last edited by a moderator:
fuatilia hii issue vizuri..... toka jana yule daktari aliyekuwa na komredi wakati akikamatwa aliwapigia simu watu mbalimbali waliwamo watu wa LHRC... ambao kwa uzoefu walizunguka vituo vyote vya polisi na kupata taarifa asubuhi kuwa mtu mmoja kaokotwa huko mabwepande ndipo walipoenda na kumkuta komredi ulimboka...... habari ndio hiyo
 
tume huru ya uchunguzi iundwe kufuatilia suala hili,iwe neutral,isiwe upande wa serikali au madaktari,hapo ndo tutaujua ukweli halisi,isije ikawa kuna watu wamecheza na alama za nyakati za hali halisi ya sasa ya nchi yetu kugain popularity kuhusu mgomo wa madaktari na kuichafua serikali
 
Kinachonistaajabisha humu ndani(JF) ni asilimia kubwa ya watu kuwa na mtazamo mmoja,eti Serikali imempiga Dk Ulimboka,hivi haya mawazo mgando ya kuamini kuhusika kwa serikali katika kutekwa na kupigwa kwa Dk yanatokea wapi?,kwanini inaonekana ni serikali ndo imefanya kitendo hicho na si Raia mwingine yeyote aliyepatwa na uchungu wa kumpoteza Mpendwa wake kwa kitendo cha kugoma kwa Madaktari chini ya uongozi wa Mhanga(Ulimboka) na ku'engeneer tukio hilo?
Mimi bwana siungi mkono kitendo cha kupigwa kwa Dk Ulimboka,lkn siungi mkono pia kitendo cha kugoma kwa Madaktari watu wengi sana jamani huwa wanaathirika kwa migomo ya aina hii,nyie mnaounga mkono hayajawahi kuwakuta tu,yakiwakuta siku moja mtakuja kukubaliana na wapinga migomo ya madaktari wote hapa Ulimwenguni
 
hivi nchi wahisani wakiona mambo yanayofanyika kama haya hivi wanatuonaje
kwa hiyo wewe unaishi na kufanya mambo ili wahisani wakuone? ishi kama utakavyo ili mradi usizuie wala kuingilia haki na mipaka ya wenzako........ usiwe mtumwa wa wahisani..
 
Back
Top Bottom