Zitto: Contracts review is a publicity stunt and creation of unnecessary uncertainty in the sector

Kimsingi sikubaliani na majumuisho ya jumla na dhanifu kuwa review hii ya mikataba inayotayarishwa na Prof Muhongo ni populist in nature.
Pamoja na mchango huu mzuri maudhui ya mchango wenyewe ni kwamba kwa vile pro active stance ya kurekebisha kasoro za mikatba hiyo inatoka kwenye serikali ya CCM, basi zoezi lenyewe ni naught.

Kuna watu waliojijengea mioyoni mwao kuwa na mtazamo hasi kwa kila kitu kinachofanywa na serikali ya CCM, hata kama ni kwa faida ya wananchi waliowengi.

Prof zmuhongo( na ndg Maswi) wamepigwa vita sana pale Wizara ya Nishati na Madini, vita ya wazi wazi na hata kisiasa kupitia Wabunge.

Siyo siri kuwa mikataba hii mibovu imetayarishwa na wanasiasa ambao baadhi wananufaika nayo hadi leo hii.

Ndiyo maana tulio wengi tunashangaa sana kuwa at last kapatikana mtu mwenye kuthubutu kuchambua the pandora box ya uchafu wa mikataba ya kifisadi, watu kama Zitto wanakuja juu.

Kwa msimamo huu, je CDM ni just an idler katika gurudumu la masahihisho ya mikataba hiyo?
Kulaumu tu from a safe distance?

Mimi nachelea kukubaliana na misimamo isiyo na misingi.
Tungependa vile vile Mzee Mwanakijiji kupata maoni yako ya kisera juu ya mikakati potofu na kifisadi kwa suala la Meya wa Moshi na safari ya masomo Kigali.

Zaidi ya maneno matupu sitegemei zaidi toka wenzetu wa CDM.

Kwani kanuni za mapitio, marejesho na mabadiliko ya mikataba, makubaliano ya hiyari na mikataba ya upendeleo inaruhusu waziri kufanya hizi decisions?
 
Zitto,
Mimi nashindwa kukuelewa wewe. Waziri amewataka wajumbe wa bodi wapitie hiyo mikataba mipya halafu wampe maoni yao kama inafaa au la. Wakati huo huo profesa mwenyewe atakuwa anafanya mapitio yake aone ni wapi atatofautiana au kukubaliana na wajumbe wa bodi. What is wrong with that? Wewe kumwita waziri ni irresponsible inaonyesha kuwa wewe ni irresponsible au uko mfukoni mwa "wawekezaji" ambao inaonekana unataka kuwapendeza zaidi ya maslahi ya nchi. Mwache waziri afanye kazi yake. Waache wajumbe wa bodi wapitie tusikie maoni yao. Kwenye madini kama nijuavyo, hakukuwa na mapitio. Mikataba ilisainiwa ikiwa ni siri kati ya yule aliyesaini kwa niaba ya serikali na mwekezaji. Hilo wengine tunalipinga. Waziri Muhongo hajasema kuwa hataiweka wazi mikataba baada ya kupitiwa na wajumbe wa bodi. Inaonekana wewe ndiye uliyeshoot from the hip.
Jasusi,I love you bro!coz msimamo wako ni dhabiti na haujawahi kuyumba!you're the man!bado hakuna aliyejibu bandiko langu!lakini nakuhakikishia kwamba tuko pamoja!Nasubiri atakaye jibu,maana watu wanakwepa hoja za watu flani flani!and I can't belive it!kwasababu watanzania wengi wetu ni wafuasi wa watu tu!Anyways I'm around,usishangae nikajibu posti iliyoelekezwa kwako kama yangu haijajibiwa!
FYI,he didn't shoot from the hoop!he shot before he aimed!niko around trust me!hoja kwa hoja!
Tuko pamojah!
 
Mkuu Kazi Ndio Kipimo cha Utu,
Mara baada ya Richmond kushindwa kazi na ku uhuisha huo mkataba kwa Dowans, tulipaswa tukatae, ili mkataba uvunjike kwa failure of performance, hivyo Richmond ange wind off na kunegotiate na sisi safe exist, akafungasha virago vyake na kusepa, kwa sababu mashine tulisharigharimia kwa kuzikodisha kwa bei kubwa kuliko hata kununua mpya!.

Trick ya kuuvunja mkata mbovu ni kumsokomeza kwenye kona, yule aliyeshindwa kutimiza wajibu wake na sio kumbeleza kama tulivyofanya!. Mkataba angevunja yeye na mitambo ingekuwa yetu!.
Hili ndiyo nililoliandika labda tungelifanya wakati bado ni richmond lkn baada ya kuwa Dowans na tukakubali kuolewa na dowans hii ilikuwa ni ndoa nyingine na kukubali unafuu wa kuvunja ndoa ilikuwa ni kukubali kuinunua yani ndoa ingevunjika kwa masharti nafuu kuliko kuipeleka kuvunjwa mahakamani kwani tumekubali kulipishswa spouse support,child support,mgawanyo wa mali , gharama za uendeshaji kesi na asilimia kadhaa ya faida ya vitega uchumi mama hata baada ya ndoa kuvunjwa rasmi.Na hili ndiyo lililotokea!
 
Na mkimchaguwa Zitto kuwa mgombea wa Chadema 2015, nawarudishieni kadi yenu na kuhamia chama kingine. Anawezaje kumuita waziri anayejaribu kusafisha uozo "irresponsible?" Si ni huyu huyu Zitto aliyemtetea Mhando asiondolewe TANESCO? Ana maslahi gani na mafisadi? Tumeona uoza alioufuga Mhando TANESCO. Wamejaribu kumsafisha kwa kumpaka tope Waziri na katibu wake, zoezi ambalo naona Zitto anaendelea kulikomalia.

Mkubwa Jasusi,
Kwa nini jambo lolote analofanya Zitto, hata kama lenye maslahi kwenye chama chenu au maslahi ya kitaifa lazima upingane naye.
 
Last edited by a moderator:
Kwi kwi kwi kwi we una akili sana Mkuu jmushi1 ...mie wala siongezi neno....Mkuu Jasusi hata mie namkubali sana.

Jasusi,I love you bro!coz msimamo wako ni dhabiti na haujawahi kuyumba!you're the man!bado hakuna aliyejibu bandiko langu!lakini nakuhakikishia kwamba tuko pamoja!Nasubiri atakaye jibu,maana watu wanakwepa hoja za watu flani flani!and I can't belive it! kwasababu watanzania wengi wetu ni wafuasi wa watu tu!Anyways I'm around,usishangae nikajibu posti iliyoelekezwa kwako kama yangu haijajibiwa!

Tuko pamojah!
 
Last edited by a moderator:
Hapana.. kuinunua na hata sasa kulipa ni kosa kubwa kwa sababu ni morally wrong. Dowans haikutakiwa kabisa kuwa na mkataba wa Tanesco na Richmond. It is as simple as that. Ubaya wa yote haya ni kuwa haikuwahi kuhojiwa hata mara moja na Bunge au na watu wengine ilikuwaje Dowans wachukue mkataba wa Richmond na Tanesco, at least not on the ground ambayo niliandikia huko nyuma. Kumbuka kuwa kesi hii haikuwa inahoji suala la Dowans kuchukua mkataba wa Richmond kitu ambacho mimi nilikisemea nyuma.
Kumbuka mimi sizungumzii ya kabla ya Dowans kwani hayo yote yalikuwa makosa nazungumzia baada ya kuwa ndani ya ndoa na dowans kwani hapa ndipo lilipozaliwa wazo la kununua au kutaifisha.Ukizingatia kwamba mkenge tulishauvaa kununua ndiyo ilikuwa nafuu.
Dowans haikurithi mkataba wa Richmond kihalali. Sasa kwenda kununua tena mashine zile kutoka kwa Dowans wakati tayari tulishalipia wakati zikiwa na Richmond ingekuwa ni ujinga wa hali ya juu. Hata hivi sasa wakilipia kama wanavyofanya tutakuwa tumelipa karibu shilingi bilioni 300 kwa majenereta ya bilioni 60! Kutaifisha siyo jambo geni na linafanyika mahali popote duniani kwa maslahi ya umma pale ambapo mashirika au taasisi zinakuwa zimefanya makosa dhidi ya umma - kitu ambacho naamini Dowans walikifanya. Wala lisingekuwa janga. Ikumbukwe tulikuwa hatutaifishi kitu kisicho chetu; tulikuwa tunataificha kitu ambacho kilichukuliwa pasi ya uhalali na kukirudisha mikononi mwa watu halali.
Mzee MKJ!
Kumbuka wazo la kuinunua au kuitaifisha lililetwa baada ya kuwa tupo tayari ndani ya ndoa mpya na DOWANS ,Yaliyopiya yote yalikuwa makosa na kati ya haya mawili tulipokuwa tumefikia lenye maslahi ilikuwa kuinunua kwani ingekuwa hasara inayokoma na haindelei na si kubwa ukilinganisha na kugoma kutimiza masharti ya mkataba na kuitaifisha kwani haya yote ndiyo yametufikisha na yangetufikisha hapa tulipo.
 
Kama majibu haya ya Zitto kusema ni siasa,basi naamini na yeye ameyasema kwa kutumia siasa.


na kauli zake dhidi ya Muhongo zina dalili ya chuki maybe kwasababu alisema kuwa kapokea rushwa na kupelekea uchunguzi ufanyike?

Kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu,karibia yote aliyoyasema Prof Muhongo yameonekana kuwa ya ukweli(mfano mpango wa Tanesco,ambapo mgawao sasa haupo),tunasubiri tu hizo tuhuma za rushwa uchunguzi wake ukamilike na kusiwe na hizo siasa dhidi ya Muhongo.

Halafu ndugu Zitto anasema anshangaa kwanini hiyo article yake haikuletwa humu,anasema hivyo na wakati yeye ni member,haya bwana mkubwa.


Kuiweka wazi binafsi naamini haitasadia kwasababu bunge wengi ni wa ccm,na ikiwekwa wazi kitakachofanyika sana sana ni kwa wabunge baadhi ya wapinzani kuhongwa kama vilivyokuwa zile issue za Barrick na mambo bado yakabarikiwa na bunge la ccm wakishirikiana na baadhi ya mamluki wa upinzani.




Endapo mjadala huu utaendelea kwa muda,basi na mimi nitakuja kuchangia baada ya kuwasoma wote Zitto na Muhongo,nashindwa kufanya hivyo sasahivi kwasababu Zitto amesema yale ya Muhongo ni siasa,wakati wengi wetu hatujaona hivyo.Hilo limenifanya niamini kuwa yeye ndo ameleta siasa,kama kuna watu watajadiliana hapa si kwa kuwajadili Zitto na Muhongo,wala kuwatukana wana JF kwa hasira na kuwaita vichwa maji as if Muhongo ndo mwana JF!Tusijadili kitu kingine bali hoja zao,hapo nitarudi na kuweka mchango wangu zaidi(hoja kwa hoja),na hilo ni baada ya kuwasoma wote vyema,na kuanalyze articles zao.

Mjadala mwema.

......haikambe.....Mangi....!
 
uko karibu kiasi; mkataba ulitakiwa kuvunjwa na Tanesco kwa sababu Richmond aliurithisha kwa Dowans bila kuitaarifu Tanesco kama mkataba ulivyotakiwa. It was as simple as that.
Tulipokumbuka shuka tulishafungwa goli la kisigino hivyo tulitakiwa tuzuie kutokufungwa mengi lakini tulianza rafu zilizosababisha penati nyingi na red cards kibao, ambapo matokeo yake tulicheza wachache na kuzidiwa zaidi na kupata kichapo kikubwa,ambapo yote mengine yaliyojiri mchezo ulipoanza imebaki kuwa simulizi zisizo na tija na hadithi za kale lakini ubao mwisho unasomeka goli kibao kwa bila!Hapo ndipo tulipoifikisha timu Tanzania chini ya Kocha Tanesco!
 
Zitto,
Mimi nashindwa kukuelewa wewe. Waziri amewataka wajumbe wa bodi wapitie hiyo mikataba mipya halafu wampe maoni yao kama inafaa au la. Wakati huo huo profesa mwenyewe atakuwa anafanya mapitio yake aone ni wapi atatofautiana au kukubaliana na wajumbe wa bodi. What is wrong with that? Wewe kumwita waziri ni irresponsible inaonyesha kuwa wewe ni irresponsible au uko mfukoni mwa "wawekezaji" ambao inaonekana unataka kuwapendeza zaidi ya maslahi ya nchi. Mwache waziri afanye kazi yake. Waache wajumbe wa bodi wapitie tusikie maoni yao. Kwenye madini kama nijuavyo, hakukuwa na mapitio. Mikataba ilisainiwa ikiwa ni siri kati ya yule aliyesaini kwa niaba ya serikali na mwekezaji. Hilo wengine tunalipinga. Waziri Muhongo hajasema kuwa hataiweka wazi mikataba baada ya kupitiwa na wajumbe wa bodi. Inaonekana wewe ndiye uliyeshoot from the hip.

.....hii ya Zitto na Dr. Mkumbo ndiyo inaitwa........ "shoot first...aim later"......lol
 
Mzee MKJ!
Kumbuka wazo la kuinunua au kuitaifisha lililetwa baada ya kuwa tupo tayari ndani ya ndoa mpya na DOWANS ,Yaliyopiya yote yalikuwa makosa na kati ya haya mawili tulipokuwa tumefikia lenye maslahi ilikuwa kuinunua kwani ingekuwa hasara inayokoma na haindelei na si kubwa ukilinganisha na kugoma kutimiza masharti ya mkataba na kuitaifisha kwani haya yote ndiyo yametufikisha na yangetufikisha hapa tulipo.

si kweli; sisi wengine tulitoa mawazo ya kuitaifisha mitambo hii tangu ikiwa wakati wa Richmond waliposhindwa! Wengine walikuja baadaye nakuona ukweli wa hili. Na mwisho wengine tukasema (na tulikuwa sahihi) kuwa Dowans ni LAZIMA watalipwa kabla hata ya kesi kujulikana hukumu yake kwa sababu hakukuwa na namna yoyote ambayo wasingelipwa. Dowans ni dudu ambalo halikuwa na namna ya kulikwepa. Huwezi kuwa na mmiliki mkubwa wa Dowans kama yule na usilipwe.
 
Tulipokumbuka shuka tulishafungwa goli la kisigino hivyo tulitakiwa tuzuie kutokufungwa mengi lakini tulianza rafu zilizosababisha penati nyingi na red cards kibao, ambapo matokeo yake tulicheza wachache na kuzidiwa zaidi na kupata kichapo kikubwa,ambapo yote mengine yaliyojiri mchezo ulipoanza imebaki kuwa simulizi zisizo na tija na hadithi za kale lakini ubao mwisho unasomeka goli kibao kwa bila!Hapo ndipo tulipoifikisha timu Tanzania chini ya Kocha Tanesco!

Angalia hiki ambacho tulikifanyia kazi Julai 2009.. kipengele D

Ziara ya Dowans HQ in Costa Rica na Meremeta
July 14, 2009 11:20 AM PDT

Hi everyone; I'm back, wounded and limping but still kicking LOL. With some of my "little ones" we were able to travel extensively through Europe, US and Costa Rica as well as making some contacts in Singapore, U.A.E (this was published in one of previous Cheche editions. What we have discovered is nothing less than shocking!

I visited the so called Headquarters of Dowans S.A in Costa Rica and had access to relevant organs that deal with businesses there. Some of the things we were able to raise with the Costa Rican gvt and the US gvt were addressed in the meeting in London when the major economic powers addressed the current economic crisis. If you can recall, Costa Rica was named as one of the countries that unless they change their legal framework concerning offshore accounts they will be blacklisted. We are glad as we left the Costa Rican gvt decided to change some of the laws and regulations. We are eternally grateful to those people who made the trip worthy taking and fruitful.

We learned a number of things about Dowans:
a. If It was registered in Costa Rica then simply as a briefcase company. Due to the legal and procedural laxity that existed then in Costa Rica it was very easy for some shady businessmen to appoint a "lawyer" who would act as their middleman and a point of contacts.

After our extensive investigations through different lawyers organisations we were unable to find the lawyer involved with Dowans nor his/her address or whereabout. One authority told us confidently that such a person does not exist except in papers.
b. We visited the offices of Dowans Costa Rica as indicated in their BRELA forms. In these forms Dowans (T) has listed two companies as one of the major shareholders, one is Dowans S.A of AVENIDA DE LA ROSAS 3J CALLE BLANCOS, 1150 sAN JOSE, COSTA RICA and the other company is a major Singaporean company and world world leader in Port Management.. Portek Internation of 20 HARBOUR DRIVE #02-01 PSA VISTA, SINGAPORE 117 612 (Portek International Limited).

The later (Portek) assured us with no qualifications that it has no share, none whatsoever in the Dowans (T). And it is not involved in energy products in Tanzania. The only project they had was the sale of some logistics equipments to TICTIS. This can be verified easily by contacting: Tel: (65) - 6873 1114 or Fax: (65) - 6873 2224. The former (Dowans S.A) has been a pain in some places better left unmentioned. The report of our investigation team under my able leadership came to this conclusion "there is no such a business in Costa Rica operating under that name".

Indeed my visit to the address mentioned in BRELA forms led me to a free trade zone. A check of the business located there revealed no such company. After combing public and private records such as the National Registry of Costa Rica, Telephone, electricity, automobiles and database searches all revealed nothing. Not about Bernal Zamora Alce (the "lawyer") nor the company itself.

Our conclusions then are as follows:

a. Dowans entered into Tanzania under false pretenses, providing misleading information and therefore has engaged in fraud. b. Due that fact in a, Dowans in Tanzania was wrongly registered and its activity as a company had no legal basis
c. Due to (a and b) Dowans lacks legal standing in our courts to ask compensation as an illegal entity operating illegally.
d. The government should seize all of Dowans assets and take everybody who was involved in enabling this company to enter into a contract with Tanesco to a court of law for abusing their offices and authority.
e. Its choice of Costa Rica as a country of incoporation (knowing fully the laxity and the nature of their tax laws and their business regime) was done with the full blessings of two longtime friends. One is the legal director of Dowans Tanzania Gen (rtd) Mohammed Al-Adawi and the other a prominent businessman and politician.
 
uko karibu kiasi; mkataba ulitakiwa kuvunjwa na Tanesco kwa sababu Richmond aliurithisha kwa Dowans bila kuitaarifu Tanesco kama mkataba ulivyotakiwa. It was as simple as that.
Mkuu Mzee Mwanakijiji,

  1. Kwenye sheria ya mikataba, kuna "void contracts" "batili" na "voidable" sikumbuki Kiswahili chake.
  2. "void" ambao ni batili, hapa ni sawa na hakuna mkataba, wanasheria wanaita "void ab initio" yaani hapajawahi kuwepo mkataba na haurekebishiki! kwa sababu hau exist kisheria!.
  3. "voidable" ni mkataba wenye makosa ambayo yakirekebishwa unakuwa sawia.
  4. Kitendo cha ku uhuisha mkataba wa Richmond kwenda Dowans bila ridhaa ya Tanesco, kunaufanya mkataba ule kuwa "voidable" na sio "void", baada ya Tanesco kuridhia, kuliuhalalisha ule mkataba!.
  5. Kitendo cha Richmond kuwa ni kampuni hewa, kungeweza kuufanya ule mkataba wa Richmond, kuwa "void" ila hakuna kesi yoyote, iliyofunguliwa kuuvunja, hivyo kitendo cha Richmond hewa kuiza mitambo yake Dowans, ambayo ni kampuni ya ukweli, kimeuhalalisha ule mkataba wa kampuni hewa kuwa ni kampuni ya ukweli!.
  6. Mitambo ya dowans ni mitambo ya ukweli, na kufua umeme, walifua umeme wa ukweli as a result kitendo cha Tanesco kuja kuuvunja baadae ni ukiukaji wa mkataba halali, hivyo ile tuzo ya IIC kuwa Dowans lazima walipwe ni tuzo halali na lazima tutailipa tutake tusitake!, huu ucheleweshaji ni just wastage of time!.
  7. Mfano rahisi kwa wasioelewa masuala ya kisheria, ili ndoa kuwa ni halali, lazima, hao wanandoa wote wawili waridhie ndoa ile.
  8. Ukimbaka msichana, nae ili kuepuka aibu, akaamua bora tuu atulie kwako, ukaamua kuandaa hati za ndoa na wewe ukazisaini, yule mwanamke akagoma kuzisaini kwa sababu hakukuridhia, lakini bado anaishi kwako na huduma za kindoa sasa anazitoa bila kubakwa, ndoa hiyo inakuwa ni ndoa halali kwa performance ya duty za kindoa, hata kama mwana ndoa mmoja amekataa kusaini hati za ndoa, na hawezi baadae kuja kudai eti ndoa ile sii halali kwa sababu mwana ndoa mmoja hakuridhia!'
  9. Kitendo cha Richmond kuuhuisha mkataba kwa Dowans ni sawa na Tanesco, ilipomuoa dada mdogo, baada ya dada mdogo kujiona "rigwaride rinamshinda" na huku anaye dada mkubwa bingwa na muda wa huyo mkubwa kuolewa umepita, usiku mmoja mume Tanesco kaingia chumbani badala ya kumkuta mkewe, kamkuta dada mtu, baada ya dada mtu kumueleza kwa nini yuko pale, meme Tanesco aliendelea kujipatia huduma stahiki, ndipo mdogo mtu akaaga rasmi na kumkabidhi nyumba dadaye na yeye kutokomea zake. Kitendo cha mume Tanesco kula mafao ya huduma za dada mtu, kunamhalalisha dada mtu kuwa sasa ndie mke halali wa bwana tanesco na kilichobaki ni kubadili tuu makaratasi!.
  10. Au kitendo cha kuu huisha ule mkataba ni kama kuibaka Tenesco, kitendo cha Tanesco kutoupinga ubakaji ule, na kukubali kutulia na huyo mbakaji na kumtimizia, kunamaanisha tanesco aliridhia na kumkabali mbakaji yule, hawezi kuja kulalama kuwa alibakwa!.
  11. The right forum ilikuwa ni kwa Tanesco kuuvunja ule mkataba wa Richmond mara baada ya kugundua Richmond ni kampuni hewa, na kikawaida kabla mkataba haujaingiwa, kuna kitu kinaitwa "due diuligence report" hufanyika kabla, ikidanyanya, yule aliyedanganya anakosa haki zake zote, mitambo inakuwa yetu!.
  12. Kitendo cha Tanesco kuendelea kuutumia umeme wa Dowans, na baadaye kuvunja mkatana na kugoma kuulipia umeme waliotumia, na kulipia capacity charge ya mitambao hiyo, kumeipa ushindo Dowans na sasa tunadaiwa!, dawa ya deni ni kulipa!, na walipaji sio Tanesco, ni sisi Watanzania, tutalipa, tutake tusitake!.

Pasco.
 
si kweli; sisi wengine tulitoa mawazo ya kuitaifisha mitambo hii tangu ikiwa wakati wa Richmond waliposhindwa! Wengine walikuja baadaye nakuona ukweli wa hili. Na mwisho wengine tukasema (na tulikuwa sahihi) kuwa Dowans ni LAZIMA watalipwa kabla hata ya kesi kujulikana hukumu yake kwa sababu hakukuwa na namna yoyote ambayo wasingelipwa. Dowans ni dudu ambalo halikuwa na namna ya kulikwepa. Huwezi kuwa na mmiliki mkubwa wa Dowans kama yule na usilipwe.
Unajua wote tulisema kwamba usahihi ni kuitaifisha richmond lkn kuna yeyote kwenye bunge au kamati za bunge au uongozi wa serikali walilifanyia kazi au hata kulisemea.wazo pekee ambalo lilitoka kwenye mtu ambaye yupo karibu na vyombo vya kushauri kisheria na hata mhimili wa bunge ni Zitto na hatua ya richmond ilishapita tulikuwa ndani ya Dowans na katka choice mbili alizozitoa kama mbadala kununua ndiyo ilikuwa choice Bora na hii ndiyo ilikuwa nafasi pekee ya mwisho ya kuzuia maafa makubwa yasitokee kutokana na handaki richmond lilobadilishwa jina na kuitwa dowans.
 
Pasco;

Hapa umeeleza vizuri na ndiyo nikasema fursa ya kujitoa kwenye matope tuliziacha kwa maksudi kwani baada ya kutafuta fursa ya kujitoa kwenye janga tulikuwa tunatafuta fursa ya kuhakikisha deal linatimia na ndiyo fursa za kujinasua zilifumbiwa macho lakini za kuhalalisha deal zilitafutwa kwa kila mbinu.
 
Last edited by a moderator:
Unajua wote tulisema kwamba usahihi ni kuitaifisha richmond lkn kuna yeyote kwenye bunge au kamati za bunge au uongozi wa serikali walilifanyia kazi au hata kulisemea.wazo pekee ambalo lilitoka kwenye mtu ambaye yupo karibu na vyombo vya kushauri kisheria na hata mhimili wa bunge ni Zitto na hatua ya richmond ilishapita tulikuwa ndani ya Dowans na katka choice mbili alizozitoa kama mbadala kununua ndiyo ilikuwa choice Bora na hii ndiyo ilikuwa nafasi pekee ya mwisho ya kuzuia maafa makubwa yasitokee kutokana na handaki richmond lilobadilishwa jina na kuitwa dowans.

Sidhani kama ni wote tulisema hivyo. Wapo ambao tulipotoa hili tulionekana tunataka kurudisha mambo ya Azimio la Arusha! hata kama tulijua kuwa ni haki lakini hakukuwa na viongozi waliokuwa tayari kulisimamia hili. Binafsi naamini ni CCM na serikali yake wanapaswa kubeba lawama za Dowans na si watu wengine. Siyo wale ambao walisema au ambao hawakusema. Mkataba wa Dowans/Tanesco uliiingiwa kwa sababu wabunge wa CCM na serikali yao walishindwa kuzuia kwa sababu walijua ni mkataba wenye wakubwa ndani yake.
 
Hapa umeeleza vizuri na ndiyo nikasema fursa ya kujitoa kwenye matope tuliziacha kwa maksudi kwani baada ya kutafuta fursa ya kujitoa kwenye janga tulikuwa tunatafuta fursa ya kuhakikisha deal linatimia na ndiyo fursa za kujinasua zilifumbiwa macho lakini za kuhalalisha deal zilitafutwa kwa kila mbinu.
Na hapa ndipo EL come along na kubeba zigo la watu!.
 
Huyu Muha ameshaanza kuwa mpuuzi tu sasa. Ndo maana kila saa mgongoni mwa JK:sleepy: Hatufaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
labda urudi nyuma uniambie ni lini Tanesco waliridhia mkataba wa Richmond kwenda Dowans.
Components za mkataba ni performance ya terms za mkataba, hata kama Tanesco hawakuridhia popote "expreslly kwa maandishi", kitendo cha kuendelea kuutumia umeme wa Dowans, na kuilipa Dowans ile capacity charge, kunahalalisha huo mkataba by performace!.

Nikakutolea na mfona wa mwanamke aliyebakwa mwanzo, alipoamua kuishi na mbakaji na kutoa huduma zote bila kubwa , anahesabika ameridhia, hivyo amehalalisha kitendo kile cha kubakwa ndio stahili ya kuto..za kwa mmewe. Hata kwa Wasukuma hiyo ipo, inaitwa "Chagulaga", mabinti waliofika umri, hujitokeza kucheza maziwa nje, huku wanaume waoaji wamewazunguka, ngoma ikizimwa tuu mijibaba hutoka mbio kuwakimbiza wale warembo kuwagombania na mtembo sana hukimbizwa na wanaume wengi na kumgombania, wanaume hao hutwangana na mwenye nguvu ndio hushinda humbeba mrembo juu juu mpaka mahali muafaka na kumbaka, kesho yake ngombe hupelekwa familia ya mwanamke na ndoa ndio tayari!.

Kama Tanesco haukuridhia, ilitakiwa isikubali performance ya ile contract kuendelea!.
P.
 
Sidhani kama ni wote tulisema hivyo. Wapo ambao tulipotoa hili tulionekana tunataka kurudisha mambo ya Azimio la Arusha! hata kama tulijua kuwa ni haki lakini hakukuwa na viongozi waliokuwa tayari kulisimamia hili. Binafsi naamini ni CCM na serikali yake wanapaswa kubeba lawama za Dowans na si watu wengine. Siyo wale ambao walisema au ambao hawakusema. Mkataba wa Dowans/Tanesco uliiingiwa kwa sababu wabunge wa CCM na serikali yao walishindwa kuzuia kwa sababu walijua ni mkataba wenye wakubwa ndani yake.
Mzee MKJ!
Unajua kuna mambo kama Leo hii unanipa Nchi na Unaniambia ni yafanye AZIMIO LA ARUSHA ni moja ya mambo ningeyafanyia mapitio na yale mazuri kuyaandikia mswada na kuyapeleka bungeni yapitiwe na ya ridhiwe kuwa sheria na zikiambatana na adhabu kali ili kuzui hawa mafisadi na wanaotamani kuwa mafisadi kupitia siasa au ofisi za umma.Contract Review ingekuwa kipau mbele na mikataba yote yenye mianya ya misamaha ningefuta watake wasitake na asilimia tatu ningetread kwa angalau asilimia 40.vinginevyo ningekuwa Nyerere 24 hrs out of the country.Na ningesubiri vikwazo kwani kuna faida gani kuwa na mali ambayo haikunufaishi na inaendelea kuwanufaisha wengine wakati hata bajeti ya kuwapa huduma bora wananchi wako inakushinda.Hatuwezi tukawa tunatembeza bakuli wakati tunauwezo wa kupitia upya mikataba na kuona njia mbadala ya kupata win - win deal na ikishindikana ni maamuzi magumu na niazime msemo wa Mh Waziri Mkuu Mizengo Kayanda mwana wa Pinda :
'"LIWALO NA LIWE",Nipo tayari kushirikiana na China kwenye migodi kama watakuwa tayari na win - win deal wao watujengee nchi kupitia viwanda,kilimo,mifugo ,miundombinu,na mchango kuendeleza elimu ya juu na kufungua wigo la ajira.
 
Back
Top Bottom