Kabwe Zitto amemaliza punde kuongea Bungeni akilia na suala la elimu ambapo amependekeza shule za VETA ziunganishwe na kambi za JKT ili vijana wanaomaliza huko watoke na elimu zitakazowasaidia moja kwa moja katika maisha kwa faida yao na nchi na akasisitiza walimu wathaminiwe! Wakati wa kumalizia hoja yake amemnukuu mwanasiasa na mpigania haki wa India hayati Indira Ghandi, ambapo Naibu Spika Ndugai amemsifu jinsi alivyomalizia hoja yake kwa nukuu hiyo! (sijainyaka vyema hiyo nukuu). Nimeshainyaka nukuu yenyewe: "First they ignore you, then they laugh at you, then they fight you, then you win" (Thanks Jabulani!).