Zitto awazindua Wasanii: 153 wameshasaini kuvunja mkataba

kwa hili zito apewe respect yake yeye ndo amewazindua hao wasanii wasiojua haki zao
 
Kwa akili hizi matope sitashangaa mkimwita Zitto freemason
 
siku hizi ukiandika zitto ujue habari yako itasomwa kama nini na vyombo vya habari wamesha jua na wanauza vibaya
 
Zitto thru "Leka Dutigite" ndie alie- emphasize hii kitu, na aliipigia debe sana.

Fikiria Tigo wanakusanya hela za "Caller tune" kiasi cha kupata faida na kulipa zawadi mbalimbali ikiwamo Tshs 10Mil, wasanii wanafaidikaje?

Mwakilishi gani wa wasanii anaehusishwa kukagua idadi ya wateja wanaotumia nyimbo ya msanii fulani??

I like this movement, makampuni yaache unyonyaji.

"LEKA DUTIGITE" wadau.
 
Kazi ya Zitto ni kutetea wananchi, na ndivyo alivyofanya. Alitoboa hiyo siri bungeni na sasa wasanii wamegundua kuwa wanaliwa. Sasa sijui wakati wanasaini hiyo mikataba walikuwa hawasomi kwanza, na repercussion na kutengua au kuvunja mikataba nayo lazima wazielewe na si kukurupuka tu. I hope watakuwa wamepata na kusoma vizuri ushauri wa kisheria kabla hawajavunja hiyo mikataba..
 
kwani wasanii wa nyimbo za dini nao wanataka haki gani wakati ring tone zinaeneza ujumbe wa neno la mungu? kwa maoni yangu muziki wa dini ni sadaka na si biashara ,kwahiyo kuwazuia makampuni ya simu ni sawa na kuweka makwazo kwa neno la mungu!

Mkuu uko wapi? these days they're less concerned na usambazaji wa neno la Mungu. Ni biashara paseee!
 
PRESS RELEASE:
YAH: KUFUTA MIKATABA NA KUSIMAMISHA KUUZA MUZIKI WA BONGO FLEVA,GOSPEL,DANSI NA TAARABU KWENYE MITANDAO YA SIMU.
Husika na kichwa cha habari hapo juu,
Kwa ujumla wetu sisi Wasanii toka Tanzania tunaofanya muziki wa Gospel, Rhumba , Taarabu pamoja na Bongo fleva tumeamua kutoa agzio kwenu la kusimamisha mauzo ya kazi zetu za muziki katika mtindo wa Ringtone na Callertunes katika mitandao ya simu ya Vodacom, Zantel,Tigo na Airtel na kufuta mkataba tuliosaini kati yetu sisi Wasanii na Kampuni yako mpaka hapo tutakapokaa sisi kama wasanii, nyinyi kama wasambazaji wa muziki wetu, pamoja na Mitandao ya simu ili kuzungumzia namna mpya ya sisi na nyinyi tutakavyofanya kazi.

Sababu ya sisi Wasanii kusimamisha na kufuta mikataba kati yetu na wanaofanya biashara ya kuuza maudhui yetu ni pamoja kampuni husika kushindwa kuweka wazi taarifa za mauzo ya nyimbo pamoja na kutolipa katika muda husika kama ilivyoanishwa katika mikataba husika.
Sababu ya pili ni mitandao ya simu kuchukua kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni asilimia themanini ya mauzo yote ya maudhui yetu, jambo hili linatuumiza na limetufanya tuendelee kuishi kwa kutegemea aina moja ya pato toka kwenye shoo.

Hivyo tumeziagiza kampuni zote zinazofanya kazi ya kuuza maudhui yetu kutoa maelekezo kwenye mtandao husika kuwaelekeza kusimamisha mauzo ya kazi zetu za sanaa ndani ya siku saba kuanzia leo tarehe 30/07/12 ikiwa pamoja na kusimamisha matangazo yote yanayotangaza mauzo ya kazi zetu kwa njia ya Television , Radio , blogs, website, Magazeti na Ujumbe Mfupi wa maneno mpaka hapo tutakapofikia muafaka.

Jumla ya wasanii 153 wameshasaini barua hizo na wengine wanaendelea kusaini.
Mwisho tunawashukuru kwa ushirikianao wenu, na tunaambatanisha sahihi zetu ili kuonyesha uthibitisho wa umoja wetu katika jambo hili.

Asante.

Nawapongeza wasanii wa Tanzania kwa kukataa kuibiwa na makampuni ya simu kupitia tungo zao na vipaji vyao.
Ni kweli kuwa zidi ya 75% yamapato yao yanachukuliwa na makampuni ya simu kupitia waunganishi wao kama Push Mobile na wengineo.

Mimi nimeona mkataba wa redio fulani ambayo kila caller hit( unapopiga simu redioni), mapato ya zaidi ya 75% yanaend Vodacom na Push Mobile.
Na mapato yenyewe redio hiyo ndogo ilitapeliwa na hayo makampuni.

Wizi mtupu!
 
Kwanza suala hili halihusiani na siasa umeamua kutaja jina la Zitto ili kuiingiza humu, humu sio mahala pake peleka kwingine

Linahusiana na zitto!km ulifuatilia bunge,zitto aliweka wazi jinsi wasanii wanavyoibiwa na makampuni ya sim hivyo kupelekea wasanii kufunguka na kufikia uamuzi huu
 
wasanii wa bongo ni wanafiki sana...na uhakika hizi harakati ni za kinafiki na watasalitiana tu! maana waasisi wake ni wanafiki!
 
Madaktari, walimu now wasanii! Mmh kweli tumethubutu, tumeweza na sasa tunasonga mbele.
 
Zitto amehusika sana kuwashtua wasanii kwa jinsi wanavyoibiwa mapato ya kazi zao, nafkiri wote tuliskia hotuba yake bungeni. Makampuni ya simu hayakaa kimya, tusubiri tuone kitakachofuata.
Hivi kumbe mtu ukimshtua mwenzio kuwa anaibiwa unaweza kuingia matatizoni ee...? Sijapata logic...
 
Zitto amehusika sana kuwashtua wasanii kwa jinsi wanavyoibiwa mapato ya kazi zao, nafkiri wote tuliskia hotuba yake bungeni. Makampuni ya simu hayakaa kimya, tusubiri tuone kitakachofuata.
Hivi kumbe mtu ukimshtua mwenzio kuwa anaibiwa unaweza kuingia matatizoni ee...? Sijaona logic...
 
kwani wasanii wa nyimbo za dini nao wanataka haki gani wakati ring tone zinaeneza ujumbe wa neno la mungu? kwa maoni yangu muziki wa dini ni sadaka na si biashara ,kwahiyo kuwazuia makampuni ya simu ni sawa na kuweka makwazo kwa neno la mungu!

Kama ni sadaka kwa nini hao makampuni ya simu wauze na kujipatia faida? Wewe unaona ni haki mtu kutumia sadaka ya mtu mwingine kujinufaisha? Basi na hayo makampuni nayo yatoe ringtones bure kama sadaka.
 
sio tu kawashtua wasanii bali hata sisi kila mara unaambiwa umekatwa sh 300 kwa siku kwa ajili ya music wa akupigiaye mara callertune sasa tumeshtuka kwa watumiaji 26,000,000 x 300/= ni hela nyingi wanapata. Hii kitu hata January Makamba hajaigundua kuwa na bahati nasibu zote ni utapeli mtupu kwa hiyo mpaka Zitto aitoe
 
alaaaaaaaaaah!!kumbe wasanii walikuwa hawajui kama wanaibiwa kwenye ringtones na zitto ndio amewafumbua macho!!??

kumbe ili la wizi wa kazi za wasanii ni jipya na ndio ameanza kulizungumzia zitto!!

big up zitto kwa hilo!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom