Zitto awasilisha Bungeni hoja kuhusu Zimbabwe

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163
Zitto Kabwe leo asubuhi amewasilisha hoja akitiliataka Bunge kuacha shughuli nyingine ili kujadili hali ya kisiasa na kidemokrasia inayotokea Zimbabwe kwa maelezo kuwa hiyo ni dharura.

Zitto amejenga hoja yake chini ya mambo yanayotokea nchini humo, an uamuzi wa Zimbabwe kumuondoa balozi wake nchini, siku chache baada ya membe kutoa msimamo wa nchi dhidi ya yanayofanywa na serikali ya Zimbabwe.

Amesema uamuzi wa Zimbabwe kumuondoa balozi wake ni sawa na kutangaza vita ya kidemokrasia na kuna uwezekano hata balozi wa Tanzania huko Zimbabwe akawa hatarini.

Amesema vitendo na Kauli ya Serikali ya Zimbabwe kwamba ZANU PF haiwez\i kuachia madaraka hata ikishindwa uchaguzi inaashiria shari na "viongozi kama akina Mugabe ambao walikuwa na heshima kubwa na mfano wa kuigwa kwa viongozi vijana wa Afrika, wanapofanya vitendo kama hivyo anavyofanya sasa wanatutia aibu na kulichafua bara la Afrika."

Kwa maana hiyo, Zitto alitoa hoja kuwa Bunge lijadili kwa ufupi hali hiyo ya Zimbabwe na kwamba balozi wa Tanzania aliyeko harare arudi nyumbani mara moja ili kuonyesha Zimbabwe, Afrika na Dunia kwa ujumla kwamba Tanzania ipo thabiti katika kulinda demokrasia na haki za binadamu.

Lakini, pamoja na kukiri kuwa hoja hiyo ni nzito, Spika alisema kuwa haitaweza kujadiliwa Bungeni moja kwa moja hivyo ameipeleka kqwenye Kamati ya Mambo ya Nje, ikajadiliwe huko kwanza kabla ya kuchukua hatua zaidi.
 
Wacha tungoje kusikia watasema nini .Kama kawaida hoja imetolewa na Mpinzani wana ogopa kama nini .Hali ya Zimb ni mbaya sana .
 
Tumemlea wenyewe Mugabe hasa wakati wa utawala wa Mkapa kama Marekani ilivyofanya kwa Osama kabla hajawageuka. Jeshi na vyombo vyote vya Usalama nchini Zimbabwe vinamtaka Mugabe, Mke wake naye anataka aendelee kuwa First Lady kwa kuwa umri unamruhusu na kuna watu ndani ya utawala wa Mugabe wanafaidika sana, wanataka mzee huyu afie madarakani.
 
umesahau kuwa huyu ni jongwe wazee? jogoo huyu anawika na kusikika kwa mbali. wanaomjua mugabe wanajua kuwa ni dikteta wa siku nyingi ndo maana hico chama kimepasuka toka zanu-pf toka zanu original ya yule marehemu nimemesahau, ambaye walichuma na mugabe baadaye akampeleka kizuizini mpaka akafia huko

mugabe anavyoonekana kwa nje utadhani ni bonge la shujaa, lakini anapelekwa puta na wamama ile mbaya. marehemu sally yule mke wa kwanza mghana ali-saidia sana ku-contain, lakini huyu secretary wake cum first lady ndo kwanza anasema mzee haondoki madarakani labda atolewe akiwa kwenye jeneza. sasa wewe kama morgan tsangarai uende kwenye uchaguzi kufanya nini?
 
umesahau kuwa huyu ni jongwe wazee? jogoo huyu anawika na kusikika kwa mbali. wanaomjua mugabe wanajua kuwa ni dikteta wa siku nyingi ndo maana hico chama kimepasuka toka zanu-pf toka zanu original ya yule marehemu nimemesahau, ambaye walichuma na mugabe baadaye akampeleka kizuizini mpaka akafia huko

mugabe anavyoonekana kwa nje utadhani ni bonge la shujaa, lakini anapelekwa puta na wamama ile mbaya. marehemu sally yule mke wa kwanza mghana ali-saidia sana ku-contain, lakini huyu secretary wake cum first lady ndo kwanza anasema mzee haondoki madarakani labda atolewe akiwa kwenye jeneza. sasa wewe kama morgan tsangarai uende kwenye uchaguzi kufanya nini?

Mkuu nakubaliana na hoja zako, lakini kwa jinsi ninavoijua Zimbabwe na interest za Uingereza na US kwa nchi hiyo, nalazimika kusema kwamba ni heri Mugabe akaendelea kuitawala nchi hiyo hata kwa miaka minne zaidi.

MUNGU IBARIKI ZIMBABWE.
 
Zitto nakuelewa lakn naona kama unachanganya bana...... mi naona danadana tu zinazidi kwenye ishu ya EPA, weka vitu hapo bungeni, wabaneni hao jamaa, uliruhusu ishu ya zim ije hapo una maana umewafurahisha maana ishu ya EPA ndo watakuwa wanaipatia muda wa kuiundia uongo, kuhusu balozi ... wote wezi tu hao, watajuana wenyewe aje au asije, lkn kwanza tunataka EPA na RICHMOND vieleweke kwanza.........
 
Tumemlea wenyewe Mugabe hasa wakati wa utawala wa Mkapa kama Marekani ilivyofanya kwa Osama kabla hajawageuka. Jeshi na vyombo vyote vya Usalama nchini Zimbabwe vinamtaka Mugabe, Mke wake naye anataka aendelee kuwa First Lady kwa kuwa umri unamruhusu na kuna watu ndani ya utawala wa Mugabe wanafaidika sana, wanataka mzee huyu afie madarakani.

Na istoshe Tabia za Mugabe ni kopi rait ya CCM....
 
Mkuu nakubaliana na hoja zako, lakini kwa jinsi ninavoijua Zimbabwe na interest za Uingereza na US kwa nchi hiyo, nalazimika kusema kwamba ni heri Mugabe akaendelea kuitawala nchi hiyo hata kwa miaka minne zaidi.

MUNGU IBARIKI ZIMBABWE.

Nadhani term ya uraisi zimbabwe ni miaka 7 unless wamebadili hivi karibuni
 
Haya tena! Bado tuna ya kwetu yanatuzibu bado tunataka kuingilia ya wengine. Huu si ulimbukeni jamani wa Kisiasa? wakati unafanya forecasting ya nchi yako unahitajika kukocentrate hilo kwanza mambo mengine baadaye.

Mimi nafikiri hiyo ni hoja muhimu sana lakini sio sasa, muda wake bado.
 
Natofautiana na wote ambao wanaona haina haja ya kujadili suala la zim.
Hamuoni viashiria vya vita kutokea zim. Au mnasubiri kuomboleza baada ya kuona majeneza ya watanzania wanaoishi/kufanya kazi zim?
Au mnasema tusubiri ili tujenge makambi ya wakimbizi wa Zim pale mbeya na kwingineko?
Zitto upo right, suala hili ni nyeti lijadiliwe haraka na serikali ifanye jitihada kurudisha wa-tz kabla vita haijaanza.Maana viashiria vinaonyesha.
Zitto nakupongeza kwa wazo lako bungeni
 
mugabe-01.gif


Viongozi wa nchi za Afrika saidieni kuleta maelewano nchini Zimbabwe, Kabla Babu Mugabe hajaipasua vipande vipande Zimbabwe kwa tamaa zake za madaraka.

zimb.600.jpg


Maelfu ya raia wa Zimbabwe wakivuka mpaka kukimbia vipigo kutoka kwa askari watiifu wa Mugabe na wapenzi wa chama chake kwa raia wanaotiliwa shaka kushabikia chama cha upinzani.
 
Zitto nakuelewa lakn naona kama unachanganya bana...... mi naona danadana tu zinazidi kwenye ishu ya EPA, weka vitu hapo bungeni, wabaneni hao jamaa, uliruhusu ishu ya zim ije hapo una maana umewafurahisha maana ishu ya EPA ndo watakuwa wanaipatia muda wa kuiundia uongo, kuhusu balozi ... wote wezi tu hao, watajuana wenyewe aje au asije, lkn kwanza tunataka EPA na RICHMOND vieleweke kwanza.........

Mkuu, kama utaweza kusikiliza Bunge leo jioni, tafadhali msikilize Dk Slaa atakavyomuumbua Mkulo kuhusu EPA. Anao ushahidi kuonyesha kuwa fedha za EPA ni za serikali na atautoa kupitia hotuba yake akijibu hotuba ya Pinda iliyowasilishwa leo asubuhi
 
Wacha tungoje kusikia watasema nini .Kama kawaida hoja imetolewa na Mpinzani wana ogopa kama nini .Hali ya Zimb ni mbaya sana .

Jamani kama sura hii ni ya wanasiasa basi naona wengine tutajitoa kabisa. Kila saa wapizani wapizani. Hivi nyie mmefunikwa macho kabisaaaaaaaaa.

Hamjui kabisa kwamba vyama vya siasa ni miradi ka miradi mengine like NGO, projects n.k. Kama hujui basi we shabikia tu mwishowe utajikuta unamkata shemejio shingo kwa kumtetea mtu anayekula na kulindwa kwake. Na kama mambo yakimzidi anaenda kufia Newyork na kuzikwa Huston Marekani shauri lenu.


I hate Politics !! I hate! I hate all of politics ideas MMMMMMRRRRRRRRRR!!!!!!
Kabwe naye hana nyimbo zaidi ya kutaka urasi tu. Akifika huko anakuwa more The Mugabe, the Mkapas and all culprits arround mm!
 
Mkuu nakubaliana na hoja zako, lakini kwa jinsi ninavoijua Zimbabwe na interest za Uingereza na US kwa nchi hiyo, nalazimika kusema kwamba ni heri Mugabe akaendelea kuitawala nchi hiyo hata kwa miaka minne zaidi.

MUNGU IBARIKI ZIMBABWE.


Uwiiiiii!, kumbe mpo wengi! Yaani huko Zimbabwe au ndani ya ZANU PF (kama kweli hao MDC ni wakoloni) hakuna mwingine zaidi ya Mugabe anayeua watu ili abaki madarakani? Nyie wenye mawazo haya mnatisha kuliko hofu yenyewe!

Hapa tueleze mwenzetu jinsi unavyoijua Zimbabwe ili nasi tuamke usingizini!
 
Mimi nikisema ukweli naambiwa eti najichukia mwenyewe....mmmhhhhh......haya bana.

Hawa wanaokulaumu wanatakiwa wasome Keith Richburg's Out of America: A Black Man Confronts Africa. Huyu jamaa mweusi, pamoja na mambo mengine, anaeleza kwa nini yeye anashukuru kwamba alizaliwa nje ya bara la Afrika.

Tatizo letu wengi wafrika tupo kwenye denial na ndio maana tunashindwa kutatua matatizo yetu. Ni vigumu kutatua tatizo hadi ukubali kwamba una tatizo. Sasa sisi kama hadi leo kuna watu wanamsifia Mugabe na wanakubaliana na utahira wake kwamba yeye ataondolewa na Mungu, na hawa wanaosema hivi ni vijana ambao wengine watajakuwa viongozi wa nchi za Afrika, wewe unafikiri kuna kupona hivi karibuni? Hawa akina Serukamba si ndiyo marais na wakuu wa AU huku mbele, sasa hapo unaona kuna mwanga kweli?
 
Zitto nakuelewa lakn naona kama unachanganya bana...... mi naona danadana tu zinazidi kwenye ishu ya EPA, weka vitu hapo bungeni, wabaneni hao jamaa, uliruhusu ishu ya zim ije hapo una maana umewafurahisha maana ishu ya EPA ndo watakuwa wanaipatia muda wa kuiundia uongo, kuhusu balozi ... wote wezi tu hao, watajuana wenyewe aje au asije, lkn kwanza tunataka EPA na RICHMOND vieleweke kwanza.........
Mkuu hapo tupo pamoja swala la zimbabwe linaweza kusubiri tumalize kwanza ya kwetu yanayotuumiza vichwa. kwa kutoa angalizo tu ni kwamba Serikali yetu ifunge ubalozi wetu kule kama wao na itoe tamko kwa watanzania wanaoishi zimbabwe warudi kwanza nyumbani mpaka hapo hali itakapotulia. KODI wanayosaga wabunge pale Dom kwa siku inatisha wakiongeza tena siku kwa swala la ZIMb mmhh!! itatuumiza. Kama wao wamemwondoa balozi wao kwenye nchi ya amani sisi tunachelea nini kumtoa wa kwetu kwenye nchi ya Vurugu???
 
Mkuu nakubaliana na hoja zako, lakini kwa jinsi ninavoijua Zimbabwe na interest za Uingereza na US kwa nchi hiyo, nalazimika kusema kwamba ni heri Mugabe akaendelea kuitawala nchi hiyo hata kwa miaka minne zaidi.

MUNGU IBARIKI ZIMBABWE.

Kunguru,

Nafikiri bado una zile politics za kizamani. Hivi hizo propaganda za akina Mugabe na wenzake ili waendelee kukaa madarakani bado unazikubali. Kwa mtindo wako wapinzani hawana chao. Hivi ni nchi gani ambayo imepiga hatua na hawa the so called "wapigania uhuru??" TZ inabidi tuamke, la sivyo maendeleo tutayasikia bombani na tutaishia kulalamikia na kuwatukana Mafisadi kwenye JF tu wakati wao ndiyo kwanza wanapeta. Kweli kelele za Mpangaji....... Hili game la Mugabe ndiyo wanatuchezea CCM ndiyo maana wakati wa uchaguzi Mbowe alipoleta Helicopta wakaanza kumlink na Conservative Part ya UK. Fumbua macho mzee!!!!!!
 
Zito bwana...hatima ya nchi ya Zimbabwe ipo mikononi mwa Wazimbabwe wenyewe.Kama tulivyo sisi hapa TZ hatima ya kuendelea kuyakumbatia mafisadi au kuyatosa ipo mikononi mwa wananchi wenyewe lasivyo tutakuwa tunampigia gitaa mbuzi.
Zitto komaa na mafisadi tu endelea kuwafichua huko Zimba waachie wenyewe TZ hatuwezi lolote kwani mzee Julius aliye kuwa anaweza kuzima maswala kama haya hatunae tena walio bakia ni wanafiki hawawezi chochote.
Kitu kingine kule Waingereza ndo wanachangia sana mgogoro huu.
 
Jamani kama sura hii ni ya wanasiasa basi naona wengine tutajitoa kabisa. Kila saa wapizani wapizani. Hivi nyie mmefunikwa macho kabisaaaaaaaaa.

Hamjui kabisa kwamba vyama vya siasa ni miradi ka miradi mengine like NGO, projects n.k. Kama hujui basi we shabikia tu mwishowe utajikuta unamkata shemejio shingo kwa kumtetea mtu anayekula na kulindwa kwake. Na kama mambo yakimzidi anaenda kufia Newyork na kuzikwa Huston Marekani shauri lenu.


I hate Politics !! I hate! I hate all of politics ideas MMMMMMRRRRRRRRRR!!!!!!
Kabwe naye hana nyimbo zaidi ya kutaka urasi tu. Akifika huko anakuwa more The Mugabe, the Mkapas and all culprits arround mm!


You hate politics yet yo do not know that what yon are doing here is politics ? Kuwa JF pekee na kuandika ni siasa na hili kumbe hulijui na huku unachukia siasa ?Pole wewe hata hivyo una mawazo giza sana kusema Siasa na Vyama ni NGO kwa kulinganisha .Unaonekana unakurupuka wewe ndiyo wale wale wa kuja kuangusha JF .
 
Back
Top Bottom