Zitto Kabwe aipongeza CCM Send to a friend
Wednesday, 21 April 2010 19:05
Salim Said
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe ameifagilia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanikiwa kufanya uwekezaji mkubwa wa miradi ya maendeleo kuliko nchi yoyote kusini mwa bara la Afrika.
Zitto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (Nac), aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma jana alipokuwa akiwasilisha ripoti ya kamati yake kwa 2008/09.
Akiwasilisha ripoti hiyo aliyoisoma kwa muda wa nusu saa, Zitto alianza kuusifia uwekezaji wa miaka mitatu wa mradi mkubwa uliomo ndani ya ilani ya CCM wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma.
Mheshimiwa Spika uwekezaji huu wa miaka mitatu wa Chuo Kikuu cha Dodoma unagharimu jumla ya Sh800 bilioni ni mkubwa sana kwa nchi yetu lazima tupongeze, alisema Zitto.
Uwekezaji huu ni mkubwa kuliko uwekezaji wowote uliofanywa katika nchi zilipo kusini mwa bara la Afrika na ni zaidi ya uwekezaji wa miaka 10 kutoka nje, aliendelea kusifu.
my note:
Lakini pamoja na kufagilia
Sijaona jinsi ajira milioni kadhaa kwa vijana zilivyotekelezeka. Na pia sijaona maisha bora kwa kila mtanzania.
Wednesday, 21 April 2010 19:05
Salim Said
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe ameifagilia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanikiwa kufanya uwekezaji mkubwa wa miradi ya maendeleo kuliko nchi yoyote kusini mwa bara la Afrika.
Zitto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (Nac), aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma jana alipokuwa akiwasilisha ripoti ya kamati yake kwa 2008/09.
Akiwasilisha ripoti hiyo aliyoisoma kwa muda wa nusu saa, Zitto alianza kuusifia uwekezaji wa miaka mitatu wa mradi mkubwa uliomo ndani ya ilani ya CCM wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma.
Mheshimiwa Spika uwekezaji huu wa miaka mitatu wa Chuo Kikuu cha Dodoma unagharimu jumla ya Sh800 bilioni ni mkubwa sana kwa nchi yetu lazima tupongeze, alisema Zitto.
Uwekezaji huu ni mkubwa kuliko uwekezaji wowote uliofanywa katika nchi zilipo kusini mwa bara la Afrika na ni zaidi ya uwekezaji wa miaka 10 kutoka nje, aliendelea kusifu.
my note:
Lakini pamoja na kufagilia
Sijaona jinsi ajira milioni kadhaa kwa vijana zilivyotekelezeka. Na pia sijaona maisha bora kwa kila mtanzania.