Zitto ataka Tanzania isitishe uhusiano na nchi za Magharibi: Kisa? Libya

haogwa

Member
Jun 18, 2010
20
11
Nampenda sana Mbunge kijana, machachari na mahiri, Zito Kabwe. Lakini katika wazo la kusema kuwa Tanzania ivunje uhusiano na mataifa yanayoishambulia Libya ambalo Kabwe amelitoa leo Bungeni, amekosea. Kwanza ni lazima afahamu kuwa Nato pamoja na marafiki zao ndio wanaowezesha bajeti ya tanzania kwa sehemu kubwa. Plili miradi mingi ya huduma na maendeleo inapata pesa kutoka kwa washirika hao. Kwa hiyo kufuta 'diplomatic relations' na watu hao ni sawa na kuiua serikali ya CCM. Jambo hilo haliwezekani hata kidogo. Wana jamii mnasemaje katika hilo.
 
Nampenda sana Mbunge kijana, machachari na mahiri, Zito Kabwe. Lakini katika wazo la kusema kuwa Tanzania ivunje uhusiano na mataifa yanayoishambulia Libya ambalo Kabwe amelitoa leo Bungeni, amekosea. Kwanza ni lazima afahamu kuwa Nato pamoja na marafiki zao ndio wanaowezesha bajeti ya tanzania kwa sehemu kubwa. Plili miradi mingi ya huduma na maendeleo inapata pesa kutoka kwa washirika hao. Kwa hiyo kufuta 'diplomatic relations' na watu hao ni sawa na kuiua serikali ya CCM. Jambo hilo haliwezekani hata kidogo. Wana jamii mnasemaje katika hilo.
Nikuulize mwenyewe unarafikiyako jambazi anakusaidia unapo kwama ukitambua huyo ni jambazi utafanyeje? utakubali uendele kujidhalilisha utu wako kwavile we hujitoshelezi? Namisada unayo sema selikali yetu simakini tunavyanzo vingi vya mapato hatusitahili kupewa misada sisi ndo wakutowa misada kunamkulima alitoka kijijini na mihogo mibichi kupeleka mjini kuuza alipoiuza akaendelea na mizunguko yake akakuta mihogo imelositiwa akanunua kipande aliomba atafutiwe mbegu asijuwe niyeye ameileta tanzania tunakira kitu wasimamizi hatuna vitu vinachukuliwa bule dhahabu tunabadilishana na gololi shanga nk nilijua babu zetu kwavile hawakusoma leo wasomi nyomi bado madini wanyama vinachukuliwa bure zito yupo sahihi ao hawana lafiki
 
Nampenda sana Mbunge kijana, machachari na mahiri, Zito Kabwe. Lakini katika wazo la kusema kuwa Tanzania ivunje uhusiano na mataifa yanayoishambulia Libya ambalo Kabwe amelitoa leo Bungeni, amekosea. Kwanza ni lazima afahamu kuwa Nato pamoja na marafiki zao ndio wanaowezesha bajeti ya tanzania kwa sehemu kubwa. Plili miradi mingi ya huduma na maendeleo inapata pesa kutoka kwa washirika hao. Kwa hiyo kufuta 'diplomatic relations' na watu hao ni sawa na kuiua serikali ya CCM. Jambo hilo haliwezekani hata kidogo. Wana jamii mnasemaje katika hilo.

Thread yako iko KINAFIKI ZAIDI.
 
Thread yako iko KINAFIKI ZAIDI.

mkuu kama unahoja za kumpinga mtoa hoja si uzitoe badala ya kujaza maneno yasiyo ya lazima? Kama kila mtu akiliita wazo asilokubaliana nalo kwa jina kebehi hapa patabaki kuwa home great thinkers?
 
Kuna makanisa yamekataa misaada ya nchi zinazounga mkono ushoga; kwanini serikali yetu iendelee kupokea misaada toka kwa watu wanaoua wananchi wasio na hatia?
 
Nikuulize mwenyewe unarafikiyako jambazi anakusaidia unapo kwama ukitambua huyo ni jambazi utafanyeje? utakubali uendele kujidhalilisha utu wako kwavile we hujitoshelezi? Namisada unayo sema selikali yetu simakini tunavyanzo vingi vya mapato hatusitahili kupewa misada sisi ndo wakutowa misada kunamkulima alitoka kijijini na mihogo mibichi kupeleka mjini kuuza alipoiuza akaendelea na mizunguko yake akakuta mihogo imelositiwa akanunua kipande aliomba atafutiwe mbegu asijuwe niyeye ameileta tanzania tunakira kitu wasimamizi hatuna vitu vinachukuliwa bule dhahabu tunabadilishana na gololi shanga nk nilijua babu zetu kwavile hawakusoma leo wasomi nyomi bado madini wanyama vinachukuliwa bure zito yupo sahihi ao hawana lafiki
Kwa nyngeza, huyu bwana inabidi atafute yale maandiko ya Nyerere kuhusu siasa za kutofungamana na upande wowote, asome na aelewe vema kabla hajatoa mchango mwingine kuhusu hili
 
nadhani yeye binafsi anaamini kuwa sisiemu ikifa tunaweza kutoka kwenye hali ya 'uombaomba' wa sasa
Nampenda sana Mbunge kijana, machachari na mahiri, Zito Kabwe. Lakini katika wazo la kusema kuwa Tanzania ivunje uhusiano na mataifa yanayoishambulia Libya ambalo Kabwe amelitoa leo Bungeni, amekosea. Kwanza ni lazima afahamu kuwa Nato pamoja na marafiki zao ndio wanaowezesha bajeti ya tanzania kwa sehemu kubwa. Plili miradi mingi ya huduma na maendeleo inapata pesa kutoka kwa washirika hao. Kwa hiyo kufuta 'diplomatic relations' na watu hao ni sawa na kuiua serikali ya CCM. Jambo hilo haliwezekani hata kidogo. Wana jamii mnasemaje katika hilo.
 
Waacheni wa Libya waamue mambo yao.
Wenyewe ndo walianza kumkataa Ghadafi, NATO inawasaidia kutimiza lengo
Nyie shida yenu nini?
Zitto ni kutaka tu aonekane kila siku anaongea. Nadhani kaanza kuishiwa hoja za maana.
Suala la Libya halipaswi kutupotezea muda tuna mambo yetu ya kushughulikia mengi.
 
Tuko utumwani kwa kila kitu, kifikra na kihalisia. Zito is right 100%.

mkuu huko sahihi kabisa yaani hawa wazungu sijui wanatuona vipi, kwanini wasiache Libya ifanye maamuzi yake yenyewe!!!!! ina maana wao wanavyoua raia wasio na hatia kwa kisingizio kwamba wanawa protect!!! that's pathetic ukweli ni kwamba wana interest zao tu (wizi wa mafuta, soko la silaha among other things!!) Fikiria gharama kubwa itakayo tumika ku-rebuild Libya ambayo imekua destructed na hiyo sijui NATO, resources za Libya ndo zitatumika yaani nina siwapendi hao NATO....ZITTO yuko right kabisa, Maskini Ghaddafi
 
Waacheni wa Libya waamue mambo yao.
Wenyewe ndo walianza kumkataa Ghadafi, NATO inawasaidia kutimiza lengo
Nyie shida yenu nini?
Zitto ni kutaka tu aonekane kila siku anaongea. Nadhani kaanza kuishiwa hoja za maana.
Suala la Libya halipaswi kutupotezea muda tuna mambo yetu ya kushughulikia mengi.

Ya jimboni kwake kamaliza?
 
Tuko utumwani kwa kila kitu, kifikra na kihalisia. Zito is right 100%.

Huo ni mtazamo wa zitto lakini sisi watanzania tukivunja uhusiano na USA, UK , FRANCE na RUSSIA na NATO kwa ujumla tutasalimika kweli?
hii sio issue ya kupewa misaada tu hata vituko vya hao jamaa tunaweza kuviimili? Tanzania tusijifanye na sisi tuna sauti bana ukweli unabaki pale pale hata kwenye familia kunakuwa na mkubwa, hata nchi ina mkuu na dunia ni hivyo hivyo hao ni wakubwa na lazima tuwafuate la watatufundisha adabu na uwezo wanao.
wakianza kuujumu mifumo yetu ya computer, bank na ulinzi tunauwezo wakujiposha, IRAQ iko wapi na nuklia zao? tuwe na heshima na wakubwa ili tupate mkate wetu BANA sio kupiga kelele tena za mambo ambayo hata hayatuhusu,
haya ndiyo alifanya NYERERE kuikombo AFRIKA ni nani anatukumbuka kwa vita tulivyowapigania?
LEO HII waafrika kusini wanatunyosha na makapuni yao badala ya kutusaidia kama tulivyofanya wakati wa uhuru, tuliwapa ardhi lakini hata leo hukienda hapo mahali (dakawa) hakuna ujenzi wote wote kutoka afrika kusini kama shukurani
Zimbabwe walijaribu nadhani hali hali hiko wazi, sasa cha kutufanya twende huko kwa manufaa ya LIBYA ni yepi?

mimi ninaishi na walibya wao wenyewe hawamtaki Gaddafi kutoka na ufisadi wake, ZItto kwanza aeleze kama Gadaffi ni fisadi au sio fisadi sio kukurupuka tu na hoja zisizo timilika au sadikiki , RUSSIA walikuwa wanapinga hivyo vita sasa wamekuwa msitari wa mbele kumtoa Gaddafi,

kuna wanawake walibakwa kwa kumpinga Gadaffi wanajeshi wake walipewa Viagra na kuwashugulikia hao hakina mama naposema kina mama nina maana wengi sio wawili watatu na hiyo ni moja ya mashitaka yanayomkabi Gadaffi,
tusiingii kupinga mambo kwa kuangalia AL JEZEERA sometime they wrong.
vita ilipo anza walikuwa ni walibya kwa walibya Gadaffi alionywa kutotumia siraha kali zidi ya waasi lakini hakusikia, sasa yanamrudi watu wanaleta misukumo ya dini kutetetea na kukwamtazamo huu ndio maana mimi huwa naona ZITTO hafai kuwa NATIONAL leader ni mkurupukaji na mtafuta nafsi kutwaa madaraka.

hawa wanasiasa wasitubuluze na kelele zao za makopo, sasa ni wakati wa kujenga inchi yetu mbona Amerika kusini kuna nchi kibao zinamatatizo na marekani jirani tu hapo ajishughulishi nazo.
INDIA ina ikandamiza NAPEL lakini mchina yuko kimya, zimbambwe imetendwa mbaya lakini afrika kusini anaendelea na biashara zao
 
Mimi nachokiona hapa ni kuwa viongozi wa kiafrika wanafuata prostitution legacy。 Ghadafi akishinda wote pamoja na JK wetu watafunga safari kumpongeza kwa kupambana na mabeberu na kuyashinda, na akishindwa wataenda Marekani kumpongeza Obama kwa kuleta demokrasia Libya. Yaani sawa na kahaba aliyekunywa bia za wanaumbe wawili, na kuwagombanisha, atakayeshinda ndiye atakayechukua.
Zitto yuko sahihi, ila ushauri wake utatekelezeka baada ya vita kumalizika. Serekali itaamua impongeze nani na imsusie nani.
 
unafikiri nini siku hao watoa misaada unaowasema waseme kwamba baadhi ya nchi wanazosisaidia watoe wanajeshi kwa ajili ya hiyo crisis na wanasema msipofanya hivyo hatutoi misaada sijui ungefanya nini? Inamaana na wewe unakwenda kushiriki kuua watu wasio na hatia, hapo ndipo utakapotambua kwamba utu wa mtu ni muhimu kuliko hiyo misaada unayoitaka, kwanza si misaada wanajaribu kurudisha vya kwetu walivyokwapua na wavyoendelea kukwapua. Zitto yupo sawa!!!!!!

weakness people always prove their power through force
 
Waacheni wa Libya waamue mambo yao. Wenyewe ndo walianza kumkataa Ghadafi, NATO inawasaidia kutimiza lengoNyie shida yenu nini? Zitto ni kutaka tu aonekane kila siku anaongea. Nadhani kaanza kuishiwa hoja za maana.Suala la Libya halipaswi kutupotezea muda tuna mambo yetu ya kushughulikia mengi.
kwahiyo tujitenge na watu wa nje? Kisa tunamatatzo,nawahurumia majirani zako.
 
Tanzania ni tone la wino katika bahari - itasaidia nini katika kuvunja uhusiano na nchi za magharibi na ufisadi huu ulioshamiri. kama nia ni kuing'oa CCM ni sawa maana hali ya maisha itakuwa sio duni lakini horrendous na siasa mbadala ndo itawini. Usiniambie mbona tulifaulu kushinda ukombozi wa africa - bila urusi, uchina na cuba - thubutu!!!
 
Back
Top Bottom