Zitto ataka kuandika kitabu kuhusu Chifupa!!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
haya jamani tuisomeni vyema hii habari na tuangalie jinsi gani mzee misifa anavyotaka kukwepa lawama na kutaka kujisafisha kwa madudu alioyafanya.


Zitto aandika kitabu kuhusu Amina

Mwandishi Wetu Novemba 21, 2007



MBUNGE machachari wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe yuko mbioni kuandika kitabu kuhusu maisha ya mtangazaji, shabiki wa taarab na aliyekuwa mbunge machachari wa Vijana kwa tiketi ya UVCCM, marehemu Amina Chifupa.



MAREHEMU Amina Chifupa

Katika mahojiano na Raia Mwema wiki hii, Zitto alisema kwamba kitabu kuhusu maisha ya Amina aliyefariki Juni 26, mwaka huu, pamoja na kingine kuhusu ni kwa nini na jinsi gani alishinda ubunge wa Kigoma Kaskazini, viko katika hatua za mwisho.

Marehemu Chifupa alikuwa shabiki mkubwa wa muziki wa taarab, aliyefanya juhudi kubwa kuupandisha chati muziki huo akiwa mtangazaji wa Redio Clouds na hata kuongoza vyema maonyesho ya muziki huo kiasi cha kujulikana kama Mama Shughuli.

Akizungumzia kifo chake na ukaribu wake naye, Zitto alikiri kwamba alikuwa ni rafiki yake wa karibu na kwamba kitabu anachotunga kitahusu kazi zake akiwa bungeni.

“Kwa hakika Amina alikuwa ni rafiki yangu wa karibu. Tulishirikiana kwa mambo mengi. Tulijifunza mambo mengi tukiwa pamoja.
“Amina alikuwa ni mwanamke jasiri sana na mtu ambaye alijifunza mambo kwa haraka sana. Kweli hakustahili kufa.

“Hivi sasa ninakusanya kazi alizozifanmya akiwa bungeni na kuzichapa kama kitabu. Ninataka watu pamoja na kizazi kijacho wafahamu kuwa tulikuwa na mbunge kijana mwanamke jasiri.

“Rafiki yangu mmoja alipata kunitania mara baada ya kuwasilisha hoja yangu binafsi bungeni mwezi Agosti. Mama huyo alinitumia ujumbe wa simu akisema: ‘Ujasiri wa Amina, kipaji cha uzungumzaji wa Mwalimu na kujiamini kwa Zitto.’

“Hii ilikuwa ni baada ya kuwasilisha hoja yangu kwa ustadi mkubwa. Hoja hiyo ndiyo iliyonifanya nisimamishwe ubunge,” anasema Zitto. Akiwa bungeni, Amina aliwashangaza wengi kutokana na ujasiri wake wa kuibua mambo mazito na hata kujitolea kuongoza mapambano dhidi ya biashara ya dawa za kulevya waziwazi.

Akichangia mjadala wa Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Biashara ya Fedha Haramu wa Mwaka 2006, Amina aliiomba Serikali kuwa makini na vita dhidi ya dawa za kulevya kwa kutomwonea haya yeyote. Alitaka vita hiyo iendeshwe kama zoezi la Bomoa bomoa ambalo halikuwa na huruma kwa yeyote.

“Mheshimiwa Naibu Spika, kama ni mimi Amina ninauza nikamatwe, hata kama ni Mbunge, kama ni mume wangu anauza hata kama ni mume wa Mbunge akamatwe, kama kuna Mbunge humu ndani anafanya biashara ya dawa za kulevya jamani akamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria na sheria ziwe kali.

“Kama kuna kiongozi mwingine yeyote wa nchi, sheria ni msumeno kama nilivyosema imkute kila mtu ikate kila mahali. Lakini siyo sheria ni msumeno kwenye bomoabomoa tu na mazoezi mengine, inapokuja kwenye issue ya dawa za kulevya sielewi kinachofanyika kwa kweli sielewi,” alisema.

Marehemu Amina ambaye alifariki kutokana na kuzidiwa na kisukari na malaria, alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Ushindi ya Dar es Salaam na baadaye akajiunga na Shule ya Sekondari ya Kisutu.

Alipomaliza kidato cha nne, Amina Chifupa alijiunga kidato cha tano katika Shule ya Sekondari Makongo.

Tangu akiwa shuleni, marehemu Amina alishaanza kazi ya utangazaji wa redio. Mwaka 2005, Amina alitwaa ubunge baada ya kufanya vyema katika uchaguzi mkuu kupitia tiketi ya viti maalum (Vijana-CCM). Hadi anafariki alikuwa na umri wa miaka 27.
 
i wonder how long he*ZITTO* has been with amina chifupa mpaka kuandika kurasa zoooote hizo kuhusu amina (alisema alikuwa nae katika kuhesabu kura, na walikuwa wabunge
-je amina huyo amekaa bungeni muda gani mpaka kuelewana na zitto hivyo ?
je zitto alikuwa "rafiki tu" au walikuwa zaidi ya marafiki ?
-je kuna uwezekano zitto akawa anajua nini kilichomsibu amina kama rafiki yake wa karibu sana
-mengine meeengi kuja baadae !
! kama sio hivyo basi ASITUMIE JINA LA AMINA KUPATA UMAARUFU !!
 
Bwana Zitto mambo kama haya ya kumwandikia Amina Chifupa kitabu wewe hayakufai, shika moja lenye maana. Kitabu cha Chifupa hakitakusaidia lolote, na kina hatari ya kukuporomosha. Waandishi wa udaku nao wameandika vyao, sasa na wewe unataka kudandia ya udaku? Kama unadhani Amina anahitaji kuelezewa tofauti, wapo watu wa kufanya kazi hiyo, na wewe unaweza kutoa mchango wako kwao. Kwanza unatuhumiwa kuhusika katika kuachika kwake, sasa unapoyafufua haya unajitafutia matatizo ya bure. Ni ushauri tu, jilindie heshima yako ndugu Zitto.
 
HII STORY YA JUMATANO ILIYOPITA, LEO JUMAPILI IMELETWA HAPA BAADA YA ZITTO KURUHUSIWA KUENDELEA NA KAMATI

TUJADILI KWA TAHADHARI KUBWA AMA TUKAE KIMYA NA KUTUMIA MUDA KUJADILI MADA NYINGINE?
 
haya jamani tuisomeni vyema hii habari na tuangalie jinsi gani mzee misifa anavyotaka kukwepa lawama na kutaka kujisafisha kwa madudu alioyafanya.


Zitto aandika kitabu kuhusu Amina

Mwandishi Wetu Novemba 21, 2007



MBUNGE machachari wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe yuko mbioni kuandika kitabu kuhusu maisha ya mtangazaji, shabiki wa taarab na aliyekuwa mbunge machachari wa Vijana kwa tiketi ya UVCCM, marehemu Amina Chifupa.



MAREHEMU Amina Chifupa

Katika mahojiano na Raia Mwema wiki hii, Zitto alisema kwamba kitabu kuhusu maisha ya Amina aliyefariki Juni 26, mwaka huu, pamoja na kingine kuhusu ni kwa nini na jinsi gani alishinda ubunge wa Kigoma Kaskazini, viko katika hatua za mwisho.

Marehemu Chifupa alikuwa shabiki mkubwa wa muziki wa taarab, aliyefanya juhudi kubwa kuupandisha chati muziki huo akiwa mtangazaji wa Redio Clouds na hata kuongoza vyema maonyesho ya muziki huo kiasi cha kujulikana kama Mama Shughuli.

Akizungumzia kifo chake na ukaribu wake naye, Zitto alikiri kwamba alikuwa ni rafiki yake wa karibu na kwamba kitabu anachotunga kitahusu kazi zake akiwa bungeni.

“Kwa hakika Amina alikuwa ni rafiki yangu wa karibu. Tulishirikiana kwa mambo mengi. Tulijifunza mambo mengi tukiwa pamoja.
“Amina alikuwa ni mwanamke jasiri sana na mtu ambaye alijifunza mambo kwa haraka sana. Kweli hakustahili kufa.

“Hivi sasa ninakusanya kazi alizozifanmya akiwa bungeni na kuzichapa kama kitabu. Ninataka watu pamoja na kizazi kijacho wafahamu kuwa tulikuwa na mbunge kijana mwanamke jasiri.

“Rafiki yangu mmoja alipata kunitania mara baada ya kuwasilisha hoja yangu binafsi bungeni mwezi Agosti. Mama huyo alinitumia ujumbe wa simu akisema: ‘Ujasiri wa Amina, kipaji cha uzungumzaji wa Mwalimu na kujiamini kwa Zitto.’

“Hii ilikuwa ni baada ya kuwasilisha hoja yangu kwa ustadi mkubwa. Hoja hiyo ndiyo iliyonifanya nisimamishwe ubunge,” anasema Zitto. Akiwa bungeni, Amina aliwashangaza wengi kutokana na ujasiri wake wa kuibua mambo mazito na hata kujitolea kuongoza mapambano dhidi ya biashara ya dawa za kulevya waziwazi.

Akichangia mjadala wa Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Biashara ya Fedha Haramu wa Mwaka 2006, Amina aliiomba Serikali kuwa makini na vita dhidi ya dawa za kulevya kwa kutomwonea haya yeyote. Alitaka vita hiyo iendeshwe kama zoezi la Bomoa bomoa ambalo halikuwa na huruma kwa yeyote.

“Mheshimiwa Naibu Spika, kama ni mimi Amina ninauza nikamatwe, hata kama ni Mbunge, kama ni mume wangu anauza hata kama ni mume wa Mbunge akamatwe, kama kuna Mbunge humu ndani anafanya biashara ya dawa za kulevya jamani akamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria na sheria ziwe kali.

“Kama kuna kiongozi mwingine yeyote wa nchi, sheria ni msumeno kama nilivyosema imkute kila mtu ikate kila mahali. Lakini siyo sheria ni msumeno kwenye bomoabomoa tu na mazoezi mengine, inapokuja kwenye issue ya dawa za kulevya sielewi kinachofanyika kwa kweli sielewi,” alisema.

Marehemu Amina ambaye alifariki kutokana na kuzidiwa na kisukari na malaria, alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Ushindi ya Dar es Salaam na baadaye akajiunga na Shule ya Sekondari ya Kisutu.

Alipomaliza kidato cha nne, Amina Chifupa alijiunga kidato cha tano katika Shule ya Sekondari Makongo.

Tangu akiwa shuleni, marehemu Amina alishaanza kazi ya utangazaji wa redio. Mwaka 2005, Amina alitwaa ubunge baada ya kufanya vyema katika uchaguzi mkuu kupitia tiketi ya viti maalum (Vijana-CCM). Hadi anafariki alikuwa na umri wa miaka 27.

Haya wacha a andike...
Lakini Zitto utafanikiwa! kama na ni kama tu!!!( if and only if) ni mkweli....Nime angaika sana ninitaka Uwanja wa Taifa Mpya uitwe Amina lakini hakuna alie ona ninacho ona


Na utanisaidia sana!! Kufahamu dhana...na kupima Ninacho fikiria kuhusu Amina...hebu tuleetee Kopi Wana JF kabla Hauja Kirusha Sokoni...
SAFI SANA ZITTO...nilikwambia tulia...
 
Ovyooooo, ananikumbusha usemi wa "mgema akisifiwa....................."
 
Kama ningekuwa mshauri wa Zitto ningemwambia hakuna umuhimu wowote wa kuandika kitabu hicho. Zitto ana mambo mengi ya muhimu ambayo yanahitaji muda wake mwingi kuliko kuandika kitabu hicho.
 
Tanzania ni nchi huru na kila mtu anafanya apendavyo hasa akiwa ni Mbunge. Hatukatai kwamba huyu Zitto anayaingia maji marefu ambayo atatakiwa kuogelea vizuri na pia kupiga “mbwiza” ingawaje anatoka Kigoma na kaogelea katika Ziwa Tanganyika. Mawimbi ya bahari ni tafauiti sana na yale ya ziwa!
Sasa kwanza anaujuzi wa kutunga kitabu? Tutakiitaje hiko kitabu chake, KUSADIKIWA! Kwani KUSADIKIKA tayari kipo cha hayati Shaban Robert!

Wanasiasa ndivyo wa livyo na wakisifiwa sana basi hukithiri mipaka yao na vipaji vyao.

KWELI MGEMA AKISIFIWA BOMBE HUITIA MAJI.

Ingawaje yeye si mjuzi wa madini yumo katika Tume ya Madini alioichagua rais J.Kikwete.

Basi kwa nini hatungi kitabu kuhusu UFUJAJI WA MADINI TANZANIA?

Huyu jamaa hana lolote na msimtukuze sana!
 
Kama ningekuwa mshauri wa Zitto ningemwambia hakuna umuhimu wowote wa kuandika kitabu hicho. Zitto ana mambo mengi ya muhimu ambayo yanahitaji muda wake mwingi kuliko kuandika kitabu hicho.

Kama Ungekua Mshauri wa Zitto Angekufukuza kazi..Ushauri wako Ni Hovyooo...!!
 
Kithuku-
Bwana Zitto mambo kama haya ya kumwandikia Amina Chifupa kitabu wewe hayakufai, shika moja lenye maana. Kitabu cha Chifupa hakitakusaidia lolote, na kina hatari ya kukuporomosha. Waandishi wa udaku nao wameandika vyao, sasa na wewe unataka kudandia ya udaku? Kama unadhani Amina anahitaji kuelezewa tofauti, wapo watu wa kufanya kazi hiyo, na wewe unaweza kutoa mchango wako kwao. Kwanza unatuhumiwa kuhusika katika kuachika kwake, sasa unapoyafufua haya unajitafutia matatizo ya bure. Ni ushauri tu, jilindie heshima yako ndugu Zitto.


UJINGA MTUPU.!!!
 
Ndugu zanguni, ZITTO ni binadamu mwenye feeling kama alivyo binadamu yeyote.

Mathalani leo hii ZITTO angesema aandike kitabu kuhusu Mwalimu Nyerere bila shaka hakuna ambaye angelitizama hili.

Amina(RIP) alikuwa kijana mfano wa kuigwa, kijana ambaye kizazi kilichopo na kizazi kijacho kinahitaji kuelewa kwa dhati kile alichokipigania hata kumkuta mauti.Leo hii Mheshimiwa ZITTO ameguswa na haya na kujaribu kumuandikia shujaa wetu Marehemu Amina kitabu,watu mnaanza kuleta vioja.

Watu katika dunia hii wameandikiwa vitabu nakala mamilioni, kina Muhammadi Ally, Bob Marley, Mandela, rosa park, Shaaban Robert, William Wilberforce, kwa nini isiwe kwa Marehemu dada yetu kipenzi chetu Amina?

Mimi naamini Sifa siyo karata ya kwanza ya mheshimiwa Zitto(yeye ndo anajijua zaidi),mimi naamini Utaifa, Taifa la Tanzania na watu wake, Watanzania na Mashujaa wake walio hai na walio tangulia mbele ya haki. hivi niwaulize wapendwa wana JF Amina Hastahili kuandikiwa kitabu?. Mimi na wewe hatustahili kumuandikia Amina kitabu kama Tunaweza?. Mheshimiwa ZITTO hastahili kumuandikia Amina kitabu?...Ni nani sasa anastahili kumuandikia Amina kitabu?.

Jamani Hebu msilimit mawazo yenu katika Politics tu, taifa linajengwa na mambo mengi mno, kuna social issues, kuna economy etc. msimlimit mheshimiwa katika mjukwaa ya kisiasa pekee, bado yeye ni mtu mwenye uwezo wa kutoa mchango wake kupitia mambo kadhaa ,ikiwemo uandishi n.k.

Tanzania tuna watu kibao ambao jamii yetu na vizazi vyetu vinatakiwa vijue habari zao,watu kama Ally Sykes, Mbaraka MWinshehe, Tuntemeke sanga, Hamis Thobias gaga, issa Matona, Amina Chifupa. woote hawa mchango wao katika jamii ulikuwa wa wazi.

Mheshimiwa ZITTO, keep on doing what you want to do sir provided that it is a right thing to do

not only if it is right to you but right to the nation and the World at Large.dont let prejudices stop you from marching forward. Your pen will Give honour to that Sister and for sure she really deserve it sir,may her soul rest in peace!
 
Mi nilishasema hapa, despite his valuable expose huyu bwana Zitto anasumbuliwa na Mremaism.Watu waliokuwa infatuated wakaniona kama natupa madongo, sasa Kikwete hahitaji hata kummaliza, anamuacha mwenyewe anajifunga kamba shingoni.
 
Hivi kwani kuna kosa gani akiandika hicho kitabu? Mbona hakuna hoja za maaana za kuonyesha kosa litakuawa wapi
 
Hivi kwani kuna kosa gani akiandika hicho kitabu? Mbona hakuna hoja za maaana za kuonyesha kosa litakuawa wapi
Hata mimi ninashangaa Ndugu yangu. Yaani wanataka kumgeuza ndugu ZITTO kama mtumwa wao, ambaye hana utashi wa kuwa huru kueleza maoni yake binafsi nje ya duru la Siasa za mafisadi.

Hebu tuelezeni ZITTO akiandika hiki kitabu kitamfunga kutetea wananchi bungeni?.

Hizo sifa mnazozisema ni zipi?. mbona hazina correlation na uandishi wa kitabu?. au waandika vitabu kuhusu wasifa za watu maarufu ni watafita sifa?
 
Ungeanzisha Campuni Yako Inayoitwa Wivu Tanzania LTD

Wivu gani na kwanini hasa? watu wengine bwana......kijiti hicho kinakuzingua!!!. Andika kitabu bwana Zitto tena kitakuwa best seller, lakini kaa ukijua kwamba ipo siku(hasa kama hautakuwa makini ktk kuchagua maneno) kitabu hicho kitatumika na mtu/watu against wewe ktk lingo za kisiasa.........kazi kwako!!!.
 
Back
Top Bottom