Zitto ana Turufu

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Kama nionavyo chaguo la Mh.Zitto katika kamati ya kuchunguza iliyoundwa na Mh.Jakaya Kikwete hivi karibuni ni jambo la hatari ikiwa tu Zito ataweza kuitumia nafasi hiyo na kumwezesha kupata umaarufu maradufu ya aliokwisha jipatia.
Zito anaweza kucheza kama Kocha na wanakamati wote akawaburuza vile anavyotaka yeye,anaweza akafanya maamuzi ya mwisho kuwa ni yake na hakuna wa kuyapinga.
Hii ni karata au turufu ya Upinzani ambayo kama itatumika vizuri inaweza kuiangusha serikali ya Kikwete au kuiporomosha hapo ilipo,kwa maoni yangu Zitto asikae mpaka muda ukaisha ajitoe pengine baada ya mwezi mmoja tu ,sasa kitu ambacho kinahitajiwe akifanye ili aibuke na ushindi mwengine kwanza ni kuwachambua washiriki wa kamati hiyo ambao wote wanaonekana wapo katika kundi la mafisadi na wengine inasemekana wamehusika hadi kwenye utiaji saini kwa mantiki hiyo hawataweza kuhakikisha uchunguzi ni wa wazi na hautopendelea au kuwalinda wengine ikiwemo serikali,baada ya mwezi Zitto atakuwa ameshakusanya data za kutosha kuweza kubuni mbinu ya kuzitumia data hizo na kuziuza kwa wananchi kirahisi kabisa data ambazo zitampa nguvu ya kijuiengua katika kamati hiyo,natumai nimeeleweka nini afanye Zitto ili kuibuka mshindi.Kama kuna wengine wana uwezo wa kuelezea zaidi kwa kina nafasi ipo wazi ili kuwasaidia upinzani kuitumia nafasi hii aliyopata wenzao.
Na huku ndiko kufanya siasa,tunasikia huko ulaya chama kidogo kilichoshirikishwa kinaweza kujitoa na kuhatarisha uongozi mzima uliokuwepo,ila hapa kidogo naona upo ufanano.
 
Mwiba,
Hii habari ya Umaarufu mnaipata wapi haswa wakati swala linalozungumziwa ni maslahi yetu sote. Haya haya ndiyo yalileta Ugonvi wa kijinga kati ya Mandela na Oliver Tambo yaani waafrika siku zote title ni kitu muhimu kuliko malengo ya mapambano.
Who cares, kama Zitto atapata Umaarufu na kwa nini asiende kucheza sinema ama mashindano ya Big brother Africa!... kuna sifa zaidi huko. Come on now, ebu acheni unazi wenu.
 
Mwiba,
Hii habari ya Umaarufu mnaipata wapi haswa wakati swala linalozungumziwa ni maslahi yetu sote. Haya haya ndiyo yalileta Ugonvi wa kijinga kati ya Mandela na Oliver Tambo yaani waafrika siku zote title ni kitu muhimu kuliko malengo ya mapambano.
Who cares, kama Zitto atapata Umaarufu na kwa nini asiende kucheza sinema ama mashindano ya Big brother Africa!... kuna sifa zaidi huko. Come on now, ebu acheni unazi wenu.
Tatizo ni uundaji wa hizi kamati,kwa kumbukumbu zako ni kamati ngapi zimeundwa kuhusiana na hili jambo la madini na nini hitimisho lake,so far the same tactics used again and the expected result will be the same kutokana na matokeo ya kamati zilizopita ,haya mambo ya kamati mbona watu wameshayachoka na hata mwanafunzi wa darasa la tano anaweza kukupa jawabu, hata wewe ukifuatilia mwisho wa kamati zilizopita utaona huishia ndani ya makabati.Nitajie kamati moja tu unayoiona iliundwa na ripoti yake kuwasilishwa kwa uwazi moja tu ,hizi ni tactics sa siasa hivyo wachezaji(wapinzani) wanapaswa kuzitambua mapema ili waunde formation ya kuikabili,kwa kumtumia Zitto wanaweza kuvuruga tactic hii.
 
Mwiba,
Nakubaliana na wewe ikiwa kichwa cha habari hii kinahusu KAMATI na sio ZITTO. Usije dhani nataka kukupinga tuu ili mradi napinga isipokuwa najaribu sana tuwe na mwelekeo ktk hoja zetu. I mean hili swala la Zitto nafikiri sisi ndio tunaemjengea Hekalu na sio JK ama CCM. Badala ya yeye Zitto kufanya kazi tukampa support zetu ili tupate tukafahamu uwezo wake.

Pili, Acha maswala ya kamati zilizopita, mimi nachotazama hapa ni kwamba JK alipoingia madarakani tu alisema kuwa - Mikataba yote ya madini itatazamwa upya na sheria ya madini kurekebishwa - Wananchi wote tuli support na pengine yaweza kuwa moja ya sababu kubwa ya kura zetu. Kwa hiyo hizi kamati zipo serikali zote duniani na haziwezi kwisha kwani mara nyingi huteuliwa kutokana na matatizo yanayojitokeza. Ikiwa Mkapa alifanya kosa na kamati zake hazikutoa matunda basi tulazimike kukubali matokeo...huu sidhani kama ni ushauri mzuri hata kidogo.
Kwa mara ya kwanza toka ahadi ile ya JK tumeona kamati ikiundwa kutimiza yale tuliyoahidiwa tena ktk sura inayoridhisha zaidi, leo sisi tena tunajivika vibwebwe kuanza kupinga kile tulichomuomba.

Hapa swala la kujiuliza ni je kweli hii kamati inaweza kuleta mabadiliko yoyote ktk mikataba ambayo tayari imekwisha sainiwa?... ikiwa haiwezekani bora tujadili yale yaliyomo ktk mikataba hiyo kisha tuelezee ni vitu gani vinaifanya hii kamati mpya kuwa bogus! hapa mtaweza tusaidia wengi tusiofahamu sheria ama kilichomo ktk mikataba hii.
 
nashauri zitto aitumikie kamati ..ila lazima auweke msimamo wake wazi mbele ya wajumbe ..kuwa hatakubali kuwa dictated..na ajue IMANI kubwa wananchi walio nayo juu ya role ya opposition ...nguvu ya upinzani ndio imemfanya rais kuwaambia wajumbe wa mkutano mkuu kuwa tayari kufanya nao kazi...

lakini hapo pia wapinzani waichukulie hii fursa kwa makini..inawezekana pia lengo la rais ni kuvunja nguvu ya upinzani kwani kama patatokea UFISADI kwenye hiyo kamati wapinzani watakosa la kusema kwa kuwa WAMESHIRIKISHWA..

ikiwa zitto ataona dalili ya kuzamishwa kwenye meli asichelee kujitosa baharini...ajitoe ..kama mzee ndesamburo alivyohisi kuburuzwa kwenye ile Kamati ya MENGI/MALIMA...lazima awe na uwezo wa kukusanya taarifa za kiinteligensia na kuamua haraka..mfano hadi sasa anatakiwa wawe wameshajua hasa SABABU KUU YA NDANI YA KUTEULIWA ZITTO na kama watahisi kuna namna bora ajitoe mapema....Muheshimiwa cheyo siyo wa kumuamini sana ..maana siku zote yeye ni mfanya biashara na rahisi sana kuwa PUDLE...HASA kikikumbuka alivyohongwa lile BMW X 5 ...Alivyokuwa mwenyekiti wa kamati ya hesabu za serikali bungeni..na wajanja pale alipokuwa akifuatilia ubadhirifu ubalozini london[enzi ya kebelloh]...sio mtu wa wapinzani kumuamini sana ..pamoja na kuwa makelele yake si haba...
 
Mwiba,
Hii habari ya Umaarufu mnaipata wapi haswa wakati swala linalozungumziwa ni maslahi yetu sote. Haya haya ndiyo yalileta Ugonvi wa kijinga kati ya Mandela na Oliver Tambo yaani waafrika siku zote title ni kitu muhimu kuliko malengo ya mapambano.
Who cares, kama Zitto atapata Umaarufu na kwa nini asiende kucheza sinema ama mashindano ya Big brother Africa!... kuna sifa zaidi huko. Come on now, ebu acheni unazi wenu.

Mkandara,

Sitashangaa wenye kadi uliyoomba ya chama wakaamua kuichukua maana unapingana na maslahi ya baadhi ya watu.

Vyama vya siasa na wanasiasa wengi ni mafia, wanachofikiria ni namna ya wao kupata umaarufu au chama chao kupata umaarufu badala ya maslahi ya taifa.

CCM walipomfungia Kabwe hawakuwa wanafikiri maslahi ya taifa, bali walitaka kumkomoa Kabwe, kuwakomoa upinzani, bahati nzuri matokeo yake yamekuwa kinyume. Walikuwa wanafikiria maslahi ya CCM.

Muhimu ni kuweka maslahi ya nchi mbele na kama kwa kufanya hivyo Zitto atapata umaarufu basi ni bahati yake.

I hope vichwa vya CHADEMA wataliona hili na kuamua kwamba maslahi ya taifa ni muhimu mno na hivyo kumwachia Kabwe aingie kwenye hiyo kamati. Kumruhusu pekee hakuna maana kama huku nyuma wataendelea kupigana vijembe, inatakiwa wakae na kuwa na msimamo mmoja, wamtume Kabwe kwenye kamati kwa mikono miwili na kumpa support zote.

Ni muhimu wasipuuze wanaolalamika na badala yake wakabiliane nao kwa hoja ili kupata msimamo mmoja ambao unakubaliwa na watu wengi. Kuitana majina kwa sababu tu mtu ana msimamo tofauti, naona haisaidii na pia ni mwanzo wa migogoro zaidi.
 
Hivi ratiba ya hiyo tume ikoje? Ni kwa muda gani wanatakiwa kufanya uchunguzi wao na kutupa majibu/ mapendekezo waliyonayo?
 
Nadhani tukubali kwamba hii si kamati ya Zitto, na wala si kamati ya mtu fulani kulazimisha maoni yake. Inapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia hadidu za rejea ilizopewa na kutoa matokeo yatakayojibu maswali yaliyosababisha kamati hiyo iundwe. Na uzuri au ubaya wa kazi itakayofanywa na kamati hiyo utachukuliwa ni wa kamati, na si wa Zitto. Sidhani hapa kazi ni kujenga au kubomoa umaarufu wa mtu yeyote, kwani Mh Rais angekuwa na mawazo hayo angepata kazi ngumu sana kuteua kamati hiyo. Ujumbe wangu kwa kamati hiyo ni kwamba watumikie maslahi ya taifa letu.
 
Na ikifika mezani ataifanyia nini? Atatusomea au ataiweka kwenye drowa na tutasahahu kama tulivyosahau zilizotangulia...
 
Mkandara,

Sitashangaa wenye kadi uliyoomba ya chama wakaamua kuichukua maana unapingana na maslahi ya baadhi ya watu.

Sio kwa CHADEMA hili; it is a free party that allows ideas made by members to flow freely. Ndiyo maana hata mhe Wangwe na wengine umeona wakitoa mawazo kama kawaida kama individual membets. Of course, kama mjumbe wa kikao akaenda kinyume na maamuzi ya kikao, hiyo ni tofauti.
 
Na mimi Nyani Ngabu nikiomba uanachama nitapewa? Au sina sifa za kuwa mwanachama wenu?
 
Na ikifika mezani ataifanyia nini? Atatusomea au ataiweka kwenye drowa na tutasahahu kama tulivyosahau zilizotangulia...
That is the point,na Zito kama atasubiri mpaka iwekwe kwenye draw basi upinzani utakuwa umepoteza nafasi ya kuikurupusha serikali kama serikali walikuwa wamejaribu kwa njia mbali mbali kuizima hoja ya ufisadi,bila ya shaka yeyote hapo watakuwa wamefanikiwa kwa kiasi fulani kama si chote,kumbukumbu zinaonyesha tactics za kamati zimefanikiwa kuzima hoja mbalimbali na kuishia ukimya unaoulizika lakini usiopata jibu zaidi ya hatujui imeishia wapi ,maana unaona kimya jiii ,wakorofi wanasonga mbele kwa kasi mpya na ari mpya,aidha Zitto kama hatajitoa kabla ya kufikia mwisho basi ni lazima afanye juu chini avujiche siri ya kamati hiyo ili apate nguvu ya kujiengua na kuiponda kamati nzima kwa nguvu zake zote bila ya kusaza kitu,hatari ikiwa atabakia mpaka mwisho halafu mambo yakawekwa kwenye madraw CCM wataibuka kidedea,au mnaonaje?
 
Tatizo ni uundaji wa hizi kamati,kwa kumbukumbu zako ni kamati ngapi zimeundwa kuhusiana na hili jambo la madini na nini hitimisho lake,so far the same tactics used again and the expected result will be the same kutokana na matokeo ya kamati zilizopita ,haya mambo ya kamati mbona watu wameshayachoka na hata mwanafunzi wa darasa la tano anaweza kukupa jawabu, hata wewe ukifuatilia mwisho wa kamati zilizopita utaona huishia ndani ya makabati.Nitajie kamati moja tu unayoiona iliundwa na ripoti yake kuwasilishwa kwa uwazi moja tu ,hizi ni tactics sa siasa hivyo wachezaji(wapinzani) wanapaswa kuzitambua mapema ili waunde formation ya kuikabili,kwa kumtumia Zitto wanaweza kuvuruga tactic hii.
Kamati zote ni usanii mtupu
 
Back
Top Bottom