Anaandika Zitto Zuberi Kabwe katika ukurasa wake wa facebook
Ndugu, Jamaa na Marafiki, mtakumbuka kuwa mnamo tarehe 7/11/2017 Jeshi la Polisi walichukua Simu yangu kwa ajili ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma dhidi yangu kwa mujibu wa sheria ya takwimu na sheria ya makosa ya mtandao. Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku 2 tu.
Nilikwenda polisi KAMATA siku 3 baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20/11/2017, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo.
1) Nawakumbusha kuwa msitumie simu ile 0767777797 kwani bado imeshikiliwa na Polisi
2) Katiba ya Nchi yetu kifungu cha 16(1) na (2) imeweka msingi wa nguvu sana haki ya FARAGHA kwa raia na kwamba hata sheria ikitaka haipaswi kuingilia mawasiliano binafsi ya Raia.
Nina mashaka kuwa Jeshi la Polisi linakaa na Simu yangu muda wote huu kwa sababu za zaidi ya uchunguzi wao wa makosa wanayonituhumu nayo. Nimeamua kuwaachia Simu mpaka hapo watakapotosheka lakini wajiandae na kesi ya kikatiba ambayo pia italinda haki za wananchi wengi wanaothirika na matumizi mabaya ya sheria ya Mtandao ( cybercrime act )
Ndugu, Jamaa na Marafiki, mtakumbuka kuwa mnamo tarehe 7/11/2017 Jeshi la Polisi walichukua Simu yangu kwa ajili ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma dhidi yangu kwa mujibu wa sheria ya takwimu na sheria ya makosa ya mtandao. Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku 2 tu.
Nilikwenda polisi KAMATA siku 3 baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20/11/2017, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo.
1) Nawakumbusha kuwa msitumie simu ile 0767777797 kwani bado imeshikiliwa na Polisi
2) Katiba ya Nchi yetu kifungu cha 16(1) na (2) imeweka msingi wa nguvu sana haki ya FARAGHA kwa raia na kwamba hata sheria ikitaka haipaswi kuingilia mawasiliano binafsi ya Raia.
Nina mashaka kuwa Jeshi la Polisi linakaa na Simu yangu muda wote huu kwa sababu za zaidi ya uchunguzi wao wa makosa wanayonituhumu nayo. Nimeamua kuwaachia Simu mpaka hapo watakapotosheka lakini wajiandae na kesi ya kikatiba ambayo pia italinda haki za wananchi wengi wanaothirika na matumizi mabaya ya sheria ya Mtandao ( cybercrime act )