Zitto aitaka Serikali ya Mama Samia kuhakikisha vyama vya siasa na vyombo vya habari vitakuwa huru kutekeleza majukumu yake

Politics of the United Arab Emirates take place in a framework of a federal presidential elective constitutional monarchy (a federation of absolute monarchies).

Tanzania

Republic, Unitary state, Socialist state, Presidential system, Constitutional republic Multy Party Democracy
sinza pazuri
Nachokwambia ndio ulichoandika hapo, umeenda kukopi vitu hata uvielewi.
Dubai hakuna vyama vya siasa, hakuna uhuru wa habari hakuna uchaguzi wa wananchi. Na ina maendeleo.
 
Nachokwambia ndio ulichoandika hapo, umeenda kukopi vitu hata uvielewi.
Dubai hakuna vyama vya siasa, hakuna uhuru wa habari hakuna uchaguzi wa wananchi. Na ina maendeleo.
Fuvu lako gumu sana kuelewa sasa mwambie Polepole tubasilishe Katiba ili tuhamie kwenye Constitutional Monarchy ili Taifa hili litawaliwe na Mfalme wa Kisukuma iwe kama Afrika ya Kati enzi za Bokasa
 
Fuvu lako gumu sana kuelewa sasa mwambie Polepole tubasilishe Katiba ili tuhamie kwenye Constitutional Monarchy ili Taifa hili litawaliwe na Mfalme wa Kisukuma iwe kama Afrika ya Kati enzi za Bokasa
Dubai hakuna vyama vingi na kuna maendeleo ya kutisha. Mama Samia vunja miguu awa wajinga waliooza meno watakusumbua hata Nyerere walimsaliti.
 
Sijaona kama ni jambo la msingi sana, tukiangalia nchi zilizoendelea haraka kiuchumi Uhuru wa siasa si jambo la msingi sana. Nchi kama Korea kaskazini wapo mbele Ila siasa sio cha msingi sana itatupotezea muda tyu, mfumo uliotumiwa na mtangulizi JPM uendelezwe au uboreshwe zaidi.
Korea kaskazini hii hii ambayo Kim Na mashoga zake wa vyeo vya juu jeshini ndio wenye uhakika wa kula!? Ondoa huu utopolo hapa.
 
Wengi wao wa hawa watu wanaodai uhuru huo hawajui maana yake. Wengine hawaelewi kwamba uhuru bila mipaka ni fujo. Wapo wanoshindwa kutofautisha kati ya kukosoa na kutukana. Ni shida sana.
Ondoa huu utopolo wa kurudi kule kule ambapo kila jamaa akikosolewa alikuwa anadai anatukanwa.
 
Hakuna nchi iliyopiga hatua ya kimaendeleo ikiwa inatumia mfumo wa democracy kutawala. Rudi darasani ujifunze.
Acha upotoshaji. Udikiteta ni mbaya.

Hizo United Arab Emirates unazozisema ni falme. Wafalme wa Dubai,Oman na hata Saudia siyo madikteta.
 
Sijaona kama ni jambo la msingi sana, tukiangalia nchi zilizoendelea haraka kiuchumi Uhuru wa siasa si jambo la msingi sana. Nchi kama Korea kaskazini wapo mbele Ila siasa sio cha msingi sana itatupotezea muda tyu, mfumo uliotumiwa na mtangulizi JPM uendelezwe au uboreshwe zaidi.
Hivi huu upuuzi manajifunziaga wapi?

Unawezaje kuwaambia watu Korea Kaskazini kuna maendeleo?

Wale watu wa ile nchi ni kama wamefungiwa kwenye gereza la halaiki vile. Wamechoka usipime!
 
Chama cha Zito ni sehemu ya serikali ya Zanzibar.Mama Samia asiwaruhusu awa wapuuzi kuandamana,kuhamasisha migomo na kutukana viongozi wa serikali wakisukumwa na ushawisi wa mabeberu.
 
Nyie pangeni tuu ila Uzuri wa mama Samia hana maneno mengi, hanaga muda wa malumbano wala mabishano. Hapangiwagi, kwa hiyo hayo mawazo yooote yanayowekwa huku ni kama kubet tuu

Ukipatia ni bahati yako, ukikosea jaribu tena baadae
 
Dubai hakuna vyama vingi na kuna maendeleo ya kutisha. Mama Samia vunja miguu awa wajinga waliooza meno watakusumbua hata Nyerere walimsaliti.
Robo za namna hii ndio zimesababisha Mungu aingilie kati ili kuzikomesha. Nyerere alituachia nchi ya amani ya watu wanaopendana.

Kuinuka kwa roho za kikatili kama yako ni matokeo ya siasa mbaya ambazo mwasisisi wake Mungu ameamua kukomesha utawala wake! Acha Mungu aitwe Mungu.
 
KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema, yuko tayari kumuunga mkono Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, endapo serikali yake itahakikisha vyama vya siasa na vyombo vya habari, vitakuwa huru kutekeleza majukumu yake.

Mwanasiasa huyo ametoa sharti hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter, jana Jumanne tarehe 23 Machi 2021, wakati anazungumzia picha rasmi ya Rais Samia, iliyotolewa na Serikali.

Rais Samia amechukua madaraka kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, kilichotokea tarehe 17 Machi 2021, kwenye Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam.

Akizungumzia utawala wa Rais Samia, Zitto amesema yuko tayari kumpa ushirikiano wake, endapo masharti yake hayo yatafanyiwa kazi.

Pia, amesema kiu yake katika serikali hiyo, ni kuona demokrasia inatamalaki kwa kuwa ndiyo suluhisho la changamoto za Tanzania.

“Ninachohitaji katika nchi yetu pendwa ni demokrasia, demokrasia ni suluhisho la changamoto zetu.”

“Nitatoa msaada wangu kwa Rais endapo vyama vya siasa vitakuwa huru pamoja na kuhakikishiwa uhuru wa vyombo vya habari,” ameandika Zitto

Wito huo wa Zitto umetolewa siku kadhaa tangu Katibu Mkuu wa chama chake, Ado Shaibu kusema kwamba ACT-Wazalendo kiko tayari kushirikiana na Rais Samia.

Akizungumza katika shughuli ya kuuaga mwili wa Hayati Rais Magufuli katika Uwanja wa Uhuru mkoani Dar es Salaam, tarehe 20 Machi 2021, Ado alisema kauli iliyotolewa na Rais Samia juu ya Watanzania kuzika tofauti zao na kusonga mbele, inaleta matumaini.

Na kwamba, anaamini mchango wa vyama vya siasa vya upinzani katika ujenzi wa nchi, utaheshimiwa kama ilivyokuwa zamani.

Rais Samia alitoa wito kwa Watanzania kushikamana na kuzika tofauti zao, tarehe 19 Machi 2021, wakati anahutubia taifa baada ya kuapishwa kushika mikoba ya Hayati Magufuli, Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Hayati Magufuli alifariki dunia akiwa madarakani, baada ya kupata matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo na mwili wake unatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Chato mkoani Geita, Ijumaa tarehe 26 Machi 2021.

Mwanasiasa huyo aliiongoza Tanzania katika kipindi cha miaka mitano na miezi mitano 5 Novemba 20215 hadi 17 Machi 2021.

Chanzo: Mwanahalisi Online
Wazo zuri kabisa
 
Back
Top Bottom