gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
Shark hivi kweli wafikiri kwamba ilikuwa ama ingekuwa ni busara kumwacha Mhando madarakani huku ukiendelea kumchunguza? kama ndivyo mbona katibu mkuu wa wizara hii alitolewa akaekwa pembeni kwanza ndipo uchunguzi ukaendelea. ukweli ni kwamba akiacha basi atafunika makosa yake kwa stail yeyete ile tofaut na akiekwa pembeni ili watu wamchunguze kwa undani.Nafikiri tumekua tunamfikiria vibaya sana Zitto kiasi cha kwamba baya lolote linalopita mbele yake au karibu yake basi ni la kwake.
Hakuna ushahidi wa wazi kua kala rushwa,bali ni kwa vile nae alitaka Mhando asifukuzwe kwanza.
Ukiishia hapo juu nilipoishia, utamuona anamtetea Mhando, but jiulize why Mhando asifukuzwe kwanza?? Jibu ni kua, mhando angeweza kusaidia taarifa muhimu nyingine nyingi tu za ufisadi kabla ya kufukuzwa kuliko alivyo sasa.
Ni rahisi kwa wale aliokula nao kumpoza ili asiwataje sasa, kuliko wakati yuko madarakani. Ndo kusema kua kwa sasa tutapata shida kujua taarifa nyingi muhimu kuliko kama angeachwa kwanza akachunguzwa. Kwakua jamii imeshamuona Mhando kama fisadi, basi hata wenzake ambao hatuwajui itakua rahisi kujificha nyuma ya mhando wakimpa chochote.
Kamati ya POAC ilitaka imhoji kwanza Mhando kwa namna ambayo yenyewe ingeona inafaa, ndipo aeunguliwe.
Zitto ana mapungufu yake, but Jf-Members kama Great Thinkers tusiwe tunajadili mambo kama wale wasiopo humu. Otherwise tutaonekana either "Tumevamiwa" au "Tunatumiwa", or even both.
Binafsi simpingi zitoo kuja na hoja hii ila ninachojiuliza amesema hayo halafu nini kitakachofuata? manake kusema tu haina mashiko yeyote manake kaisema tu tena wenye tv. kama kweli ameliona hili angeomba kuwasilisha hoja binafsi ambatyo kaifanyia utafiti kisha tuone tanesco ikiambiwa wakareview mkataba na pia mkaguzi mkuu wa serikali na takukuru waende wakachunguze.
Last edited by a moderator: