MJIMPYA
JF-Expert Member
- Mar 27, 2011
- 506
- 271
WAZIRI kivuli wa Wizara ya Fedha, Zitto Kabwe na wajumbe wa Kamati ya Mashirika ya Umma wamedaiwa kuhongwa sh milioni 60 ili walitetee shirika hodhi la mali za umma (CHC).
Tuhuma hizo zilitolewa jana na mbunge wa viti Maalum, Anastazia Wambura, ambaye alisema kuna baadhi ya wabunge ambao wanaitetea CHC ili lipewe muda zaidi.
Wambura alitaka serikali itoe kauli juu ya jambo hilo kwani linadhalilisha Bunge na serikali.
Katika majibu yake Mkulo alikiri kupokea tuhuma hizo na wamewaomba Mdhibiti na Makaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG azifanyie kazi.
"Nimesikia rushwa waliyopewa ni sh milioni 60, hili la rushwa lilitajwa hapa bungeni, tumemuomba CAG achunguze madai kuwa kuna rushwa ilitembea kushawishi CHC lipewe muda wa kudumu badala ya muda uliopendekezwa na serikali.
Awali Zitto, alisema yuko tayari kujiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu ya Mashirika ya Umma (POAC) na ubunge iwapo itathibitika kuwa yeye au mjumbe wa kamati yake amehongwa.
"Naomba uchunguzi wa tuhuma hizo ufanywe kwa uwazi na endapo zitathibitika kuwa na ukweli mimi niko tayari kujiuzulu ubunge na uenyekiti wa kamati," alisema.
Zitto alisema anazo hadidu za rejea kutoka bodi ya CHC kwenda kwa CHC na amemuomba Mkulo na Waziri wa Utawala Bora aiagize Takukuru ifanye uchunguzi.
"Uchunguzi huu utangazwe na uwekwe wazi, Waziri Mkulo aahidi kuwa ikigundulika amesema uzushi na uongo mara moja ajiuzulu," alisema Zitto.
Zitto pia alimtaka Mkulo kuhakikisha kuwa hadidu za rejea zinazopelekwa kwa CAG zinafanyiwa marekebisho ili aweze kuzichunguza na kuweka wazi matokeo ya uchunguzi huo.
"Namuomba Waziri Mkulo aweke ahadi mbele ya Bunge kuwa atajiuzulu kama nitakavyofanya mimi endapo matokeo ya uchunguzi huo yatagusa pande zetu kulingana na tuhuma zilivyotolewa," alisema.
Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo, alikana kuziona hadidu za rejea zilizoandikwa na bodi ya CHC kwenda kwa CAG.
"Mheshimiwa Zitto tuhuma hizi ni nzito ndiyo maana nikasema zitafanyiwa kazi kwani serikalini tuna utaratibu wa kuviagiza vyombo vya serikali kufanyia kazi mambo mazito," alisema.
"Utaratibu wa kujiuzulu unatokea kwa namna mbili kwanza tungesubiri uchunguzi ufanyike, taarifa ipatikane halafu lije suala la mtu kujiuzulu ama kutojiuzulu," alisema.
Mkulo alisema baada ya uchunguzi huo wa CAG taarifa itapelekwa bungeni mara moja.
Juni 23 wakati Bunge lilipokuwa likijadili Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2011, Zitto alipinga kauli ya serikali iliyowasilishwa na Mkulo na kudai Baraza la Mawaziri limerubuniwa ili kuliua CHC.
Katika maelezo yake, Zitto alisema kipengele cha kuhamisha kazi za CHC kilikataliwa na Kamati ya Fedha na Uchumi kwa kuwa kuhamishia kazi za CHC katika Ofisi ya Msajili wa Hazina kulilenga kuyaua mashirika ya umma nchini.
Najiuliza ni kwa nini TZ Daima wameamua kutumia title nzito kama hii "Zitto adaiwa kuhongwa kuitetea CHC" au ndo mwendelezo wa malalamiko ya Zitto juu ya gazeti la m/kiti wake?
Tusubiri uchunguzi tuone.
Tuhuma hizo zilitolewa jana na mbunge wa viti Maalum, Anastazia Wambura, ambaye alisema kuna baadhi ya wabunge ambao wanaitetea CHC ili lipewe muda zaidi.
Wambura alitaka serikali itoe kauli juu ya jambo hilo kwani linadhalilisha Bunge na serikali.
Katika majibu yake Mkulo alikiri kupokea tuhuma hizo na wamewaomba Mdhibiti na Makaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG azifanyie kazi.
"Nimesikia rushwa waliyopewa ni sh milioni 60, hili la rushwa lilitajwa hapa bungeni, tumemuomba CAG achunguze madai kuwa kuna rushwa ilitembea kushawishi CHC lipewe muda wa kudumu badala ya muda uliopendekezwa na serikali.
Awali Zitto, alisema yuko tayari kujiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu ya Mashirika ya Umma (POAC) na ubunge iwapo itathibitika kuwa yeye au mjumbe wa kamati yake amehongwa.
"Naomba uchunguzi wa tuhuma hizo ufanywe kwa uwazi na endapo zitathibitika kuwa na ukweli mimi niko tayari kujiuzulu ubunge na uenyekiti wa kamati," alisema.
Zitto alisema anazo hadidu za rejea kutoka bodi ya CHC kwenda kwa CHC na amemuomba Mkulo na Waziri wa Utawala Bora aiagize Takukuru ifanye uchunguzi.
"Uchunguzi huu utangazwe na uwekwe wazi, Waziri Mkulo aahidi kuwa ikigundulika amesema uzushi na uongo mara moja ajiuzulu," alisema Zitto.
Zitto pia alimtaka Mkulo kuhakikisha kuwa hadidu za rejea zinazopelekwa kwa CAG zinafanyiwa marekebisho ili aweze kuzichunguza na kuweka wazi matokeo ya uchunguzi huo.
"Namuomba Waziri Mkulo aweke ahadi mbele ya Bunge kuwa atajiuzulu kama nitakavyofanya mimi endapo matokeo ya uchunguzi huo yatagusa pande zetu kulingana na tuhuma zilivyotolewa," alisema.
Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo, alikana kuziona hadidu za rejea zilizoandikwa na bodi ya CHC kwenda kwa CAG.
"Mheshimiwa Zitto tuhuma hizi ni nzito ndiyo maana nikasema zitafanyiwa kazi kwani serikalini tuna utaratibu wa kuviagiza vyombo vya serikali kufanyia kazi mambo mazito," alisema.
"Utaratibu wa kujiuzulu unatokea kwa namna mbili kwanza tungesubiri uchunguzi ufanyike, taarifa ipatikane halafu lije suala la mtu kujiuzulu ama kutojiuzulu," alisema.
Mkulo alisema baada ya uchunguzi huo wa CAG taarifa itapelekwa bungeni mara moja.
Juni 23 wakati Bunge lilipokuwa likijadili Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2011, Zitto alipinga kauli ya serikali iliyowasilishwa na Mkulo na kudai Baraza la Mawaziri limerubuniwa ili kuliua CHC.
Katika maelezo yake, Zitto alisema kipengele cha kuhamisha kazi za CHC kilikataliwa na Kamati ya Fedha na Uchumi kwa kuwa kuhamishia kazi za CHC katika Ofisi ya Msajili wa Hazina kulilenga kuyaua mashirika ya umma nchini.
Najiuliza ni kwa nini TZ Daima wameamua kutumia title nzito kama hii "Zitto adaiwa kuhongwa kuitetea CHC" au ndo mwendelezo wa malalamiko ya Zitto juu ya gazeti la m/kiti wake?
Tusubiri uchunguzi tuone.