GuDume
JF-Expert Member
- Jan 18, 2015
- 6,652
- 14,247
Wakati tunakua ilikuwa ni jambo baya sana kusema kuwa Mtu mzima muongo, ni mbaya zaidi hata akitoa gesi kusema ni yeye ametoa gesi na kuchafua hali ya hewa. mpaka sasa naamini ni vivyo hivyo.
Zitto ndugu yangu una ubishi wa kijinga sana. Wewe humsikilizi kabisa Rais. Msikilize Rais anachosema kama Rais kasema ni gawio basi nawe anza kuamini kuwa hilo ni gawio. sasa wewe unakuja na ubishi wako kuwa si Gawio ni Maduhuli. why do you do that? acha ubishi bwana. Rais akisema amesema nawe inabidi usikilize anachosema.
kuna mama mmoja alikuwa na mumewe wanapendana sana. ikatokea siku moja mumewe alianguka toka kwenye mnazi akazimia. yule mama kwa haraka akaita usafiri na kumpeleka mumewe hospital. daktari alimwangalia yule bwana haraka haraka akiwa amelazwa kitandani. akasema "mama huyu mumeo ameshafariki nenda tu ukamzike"
yule bwana bahati nzuri akawa naye ndo ameshtuka akimsikia daktari anampa maelezo yule mama kuwa "kutokana na kudondoka kule huyu mumeo amesababisha utumbo mwembamba huko tumboni uvunjike na hivyo kuzuia damu kwenda kwenye ubongo na kusababisha mumeo afariki,mchukue tu akazikwe"
jamaa akasikia akashtuka na kusema kwa sauti ya chini kuwa
Mume :"daktari mimi sijafa nipo hai"
mkewe alimfuata mumewe kwa ukali kidogo na kumkemea huku akilia kwa kwikwi.
Mke: "mume wangu acha ubishi msikilize mtaalamu anachosema.kama kasema umeshakufa basi umekufa subiri tu tukakuzike.siyo unaanza kubishana na wataalam"
Zitto ndugu yangu una ubishi wa kijinga sana. Wewe humsikilizi kabisa Rais. Msikilize Rais anachosema kama Rais kasema ni gawio basi nawe anza kuamini kuwa hilo ni gawio. sasa wewe unakuja na ubishi wako kuwa si Gawio ni Maduhuli. why do you do that? acha ubishi bwana. Rais akisema amesema nawe inabidi usikilize anachosema.
kuna mama mmoja alikuwa na mumewe wanapendana sana. ikatokea siku moja mumewe alianguka toka kwenye mnazi akazimia. yule mama kwa haraka akaita usafiri na kumpeleka mumewe hospital. daktari alimwangalia yule bwana haraka haraka akiwa amelazwa kitandani. akasema "mama huyu mumeo ameshafariki nenda tu ukamzike"
yule bwana bahati nzuri akawa naye ndo ameshtuka akimsikia daktari anampa maelezo yule mama kuwa "kutokana na kudondoka kule huyu mumeo amesababisha utumbo mwembamba huko tumboni uvunjike na hivyo kuzuia damu kwenda kwenye ubongo na kusababisha mumeo afariki,mchukue tu akazikwe"
jamaa akasikia akashtuka na kusema kwa sauti ya chini kuwa
Mume :"daktari mimi sijafa nipo hai"
mkewe alimfuata mumewe kwa ukali kidogo na kumkemea huku akilia kwa kwikwi.
Mke: "mume wangu acha ubishi msikilize mtaalamu anachosema.kama kasema umeshakufa basi umekufa subiri tu tukakuzike.siyo unaanza kubishana na wataalam"