Zitambue wilaya za Tanzania na fursa zake ki biashara, ufugaji na kilimo kwa hiki kipindi...

kinundu

JF-Expert Member
Oct 12, 2016
2,029
2,128
Kwanza nianze na kusema kwamba fursa Ni nyingi sana ila tatizo mitaji tuu... Ma haswa watu wasio na mitaji kama mimi hizi fursa tunaziona sanaa..

1.KYELA, MBEYA TANZANIA NA FURSA ZAKE
=ufugaji
Hii wilaya ina uhaba wa wafugaji wa kuku wa mayai, kuku wanyama na ng'ombe wa maziwa

Kyela tunategemea mayai kutoka tukuyu haswa haya mayai ya kisasa, tunategemea maziwa kutoka tukuyu kuanzia mgando hadi fresh wenye mitaji wote hii ni fursa kuwekeza

Kuku wa nyama haswa watu wa huku wanapendelea sanaa kuku wa kienyeji hvyo ukiwa mfugaji wa kuku wa kienyeji utakula sana pesa kwa maana wanunuzi wanapata shida kwa kuzunguka na matenga kusaka kuku vijijini hivyo ukiwa na mifugo yako wanunuzi wote wanakuja kwako...

= biashara
Kuna ujenzi wa barabara ya rami kutoka kyela mjini hadi matema beach.. Hivyo basi ni FURSA kwa wafanya biashara kuleta daladala zenu hoi bara bara ikikamilika...

Mtakua na root kama hizi
-Boda to ipinda
-Kyela mjini to ipinda
-ipinda to ngyekye
-ngyekye to matema beach

Kwa sahivi tunatumia Noah ambazo wanatuchaji 1500 kama Paulo NA umbali kutoka mabibo hadi kariakoo hiyo root ha kyela to ipinda mkileta costa itapendeza kwa 500 itakua shangwe..

= kilimo
Mpunga kyela unalipa sanaa ila tumekosa kuliko cha kisasa ili tupate mazao mengi mnoo kilimo chetu ni cha kutegemea mvua japo tuna mito mitatu mikubwa moto mbaka, kiwila, lufilyo na mto songwe jumlisha na ziwa nyasa

Lakini kuna maeneo kama mabunga wanalima kilimo mara mbili maana mashamba yao yanatunza unyevunyevu.. Kumbuka mpunga wa kyela unasoko NC hi nzima na ni mtamu alafu unabei kubwa..

Kokoa Nazo zipo NA zinastawi vizuri..

Wenye kipato na mitaji karibuni kyela..

Hali ya hewa ni joto sip baridi...

twambie fursa za wilaya uliopo tuje tufanye kazi kumbuka uzalendo ni kupeana deal.. Karibuni
 
Mimi nipo shinyanga kwa sasa lakin bado sijaona fursa nilikua kahama kwa kahama naweza sema watu wa pale wanalima mpungunga wanalisha baadhi ya wilaya jiran pia kuna kilimo cha dengu maeneo ya msalala na kishapu hizo ni halmashauri jiran na kwa sababu magari mengi ya kwenda congo, rwanda kigali na burundi hivyo usafirishaji wa bidhaa kutoka nchi izo ni rahisi kupelekea mzunguko wa kibiashara kuwa mkubwa hapa kahama. Naomba kama kuna mtu wa shinyanga mjini au hata old shy anipe fursa plz
 
Mood naomba huu uzi uwe endelevu usiutoe wala kuunganisha na mwingine

Kwanza nianze na kusema kwamba fursa Ni nyingi sana ila tatizo mitaji tuu... Ma haswa watu wasio na mitaji kama mimi hizi fursa tunaziona sanaa..

1.KYELA, MBEYA TANZANIA NA FURSA ZAKE
=ufugaji
Hii wilaya ina uhaba wa wafugaji wa kuku wa mayai, kuku wanyama na ng'ombe wa maziwa

Kyela tunategemea mayai kutoka tukuyu haswa haya mayai ya kisasa, tunategemea maziwa kutoka tukuyu kuanzia mgando hadi fresh wenye mitaji wote hii ni fursa kuwekeza

Kuku wa nyama haswa watu wa huku wanapendelea sanaa kuku wa kienyeji hvyo ukiwa mfugaji wa kuku wa kienyeji utakula sana pesa kwa maana wanunuzi wanapata shida kwa kuzunguka na matenga kusaka kuku vijijini hivyo ukiwa na mifugo yako wanunuzi wote wanakuja kwako...

= biashara
Kuna ujenzi wa barabara ya rami kutoka kyela mjini hadi matema beach.. Hivyo basi ni FURSA kwa wafanya biashara kuleta daladala zenu hoi bara bara ikikamilika...

Mtakua na root kama hizi
-Boda to ipinda
-Kyela mjini to ipinda
-ipinda to ngyekye
-ngyekye to matema beach

Kwa sahivi tunatumia Noah ambazo wanatuchaji 1500 kama Paulo NA umbali kutoka mabibo hadi kariakoo hiyo root ha kyela to ipinda mkileta costa itapendeza kwa 500 itakua shangwe..

= kilimo
Mpunga kyela unalipa sanaa ila tumekosa kuliko cha kisasa ili tupate mazao mengi mnoo kilimo chetu ni cha kutegemea mvua japo tuna mito mitatu mikubwa moto mbaka, kiwila, lufilyo na mto songwe jumlisha na ziwa nyasa

Lakini kuna maeneo kama mabunga wanalima kilimo mara mbili maana mashamba yao yanatunza unyevunyevu.. Kumbuka mpunga wa kyela unasoko NC hi nzima na ni mtamu alafu unabei kubwa..

Kokoa Nazo zipo NA zinastawi vizuri..

Wenye kipato na mitaji karibuni kyela..

Hali ya hewa ni joto sip baridi...

twambie fursa za wilaya uliopo tuje tufanye kazi kumbuka uzalendo ni kupeana deal.. Karibuni
Kweli usemayo mimi nimekaa kiwira karibu na mto kiwira wanalima mananasi kwa wingi
 
Mimi nipo shinyanga kwa sasa lakin bado sijaona fursa nilikua kahama kwa kahama naweza sema watu wa pale wanalima mpungunga wanalisha baadhi ya wilaya jiran pia kuna kilimo cha dengu maeneo ya msalala na kishapu hizo ni halmashauri jiran na kwa sababu magari mengi ya kwenda congo, rwanda kigali na burundi hivyo usafirishaji wa bidhaa kutoka nchi izo ni rahisi kupelekea mzunguko wa kibiashara kuwa mkubwa hapa kahama. Naomba kama kuna mtu wa shinyanga mjini au hata old shy anipe fursa plz
Huo no uzalendo mkuu... Kumbuka uzalendo ni kupeana deal
 
Fursa nzuri mkuu, bt as long as una afya njema, mikono na miguu nadhani sio sahihi kusema mtaji ni tatizo.
 
Musoma mjini tumezungukwa na ziwa victoria hivo kupelekea watu wengi hasa kabila la wajita, wakwaya na jamii zake kuwa wavuvi wa samaki na dagaa, kwangu mimi naona fursa kubwa ni kuanzisha mradi wa ufugaji wa samaki hasa sato kwaajili ya kuuza viwandani na kupeleka masoko kama ya nyasho, kamnyonge na town mwigobero kwani bei ni nzuri hebu nambie samaki wa kilo mbili unauza mpaka 9000. Mungu anisaidie nimemalize chuo lazima niwekeze kwenye ufugaji wa samaki. karibuni msoja mjini
 
Kweli usemayo mimi nimekaa kiwira karibu na mto kiwira wanalima mananasi kwa wingi

Ikuti ndani ya wandali na wanyaki

Nyanya wameanza kulima nazo kama wawili hivi.

Tikitiki maji mmoja

Vitungu bamia nyanya nyungu hoho karoti mboga za majani tangawizi vyooooote hivi na vingine havina mlimaji

Wanalima kwa mazoea

NANASI imekuja Leo

Daàah tango haukuna

Au tatizo hali ya hewa?
 
Mkuu niliwahi kuskia shinyanga Pumba ya mahindi wanauza bei cheap sana means ukisafirisha kuja kuuza maeneo km arusha italipa sana,, nipitaman kufanya iyo tho cjupata taarifa sahihi kama ni kweli ni cheap au laa,,
Kwa livoskia gunia la kg50 wanauza 8000-10000 akat kwa arusha ni 24000-25000
Mimi nipo shinyanga kwa sasa lakin bado sijaona fursa nilikua kahama kwa kahama naweza sema watu wa pale wanalima mpungunga wanalisha baadhi ya wilaya jiran pia kuna kilimo cha dengu maeneo ya msalala na kishapu hizo ni halmashauri jiran na kwa sababu magari mengi ya kwenda congo, rwanda kigali na burundi hivyo usafirishaji wa bidhaa kutoka nchi izo ni rahisi kupelekea mzunguko wa kibiashara kuwa mkubwa hapa kahama. Naomba kama kuna mtu wa shinyanga mjini au hata old shy anipe fursa plz
 
MBARALI MBEYA.
1.Fursa ya kilimo cha mpunga, hapa utapata mashamba kwa bei rahisi kwa sehemu zisizo na skimu ya kutumainiwa sana kama vile vijiji vya kuanzia ilongo kushuka chini yaani igalako, ruiwa,mwela,mahango, mpaka nako. Pia utapata sehemu za kulima kwa kumwagilia kama vile mradi wa kilimo cha umwagiliaji Kapunga-chimala.

Pia kilimo cha vitunguu maji Igawa-Mbarali, kilimo cha mahindi yanakubali sana ingawa wadau wanalima sana mpunga na kilimo cha maharage haya hukubali hasa kwenye mashamba ambayo hayalimi mponga. Pia bila kusahau kilimo cha alizeti, matikiti maji, matango na nyanya, hoho nk.

2. Ufugaji, hapa utafaidika na ukubwa wa eneo la hii wilaya na ardhi huwa inauzwa sio kwa bei kubwa sana. Hapa ufugaji wa kuku na nguruwe itakulipa sana. Ila ufugaji wa ng'ombe huwa changamoto sana hasa kipindi cha kiangazi maana mvua hukata katikati ya april na kufanya eneo kuwa kavu sana hivyo kukosa sehemu sahihi ya malisho ingawa kuna sehemu za malisho ya serikali.

3. Biashara sio mahari sahihi sana kutokana na idadi ya watu na ukubwa wa eneo maana idadi ni ndogo hivyo uwezo wa manunuzi ni mdogo. Na pia miundombinu ya barabara na afya si mizuri ,ukitoa barabara ya lami iliyopita kutoka Igawa kwenda mbeya mjini na iliyotoka Igawa kwenda Ubaruku hakuna nyingine zaidi.

Kwa watafutaji wa kutumia nguvu zaidi , nyakati za hela ni kipindi cha kuanzia November mpaka March mwishoni ndio kunakua na kazi nyingi za kuandaa mashamba ya mpunga, kupanda mpunga na kupalilia. Pia nyakati za mavuno kuanzia May- july kwa wabeba mizigo kazi zipo na wale wakushona na kuanika vipeto vya mpunga.

Kwa wazee wa fursa za biashara kipindi cha Mavuno ni kizuri maana utapata mpunga kwa bei rahisi nawe ukakonoe uuze mchele au uweke stoo uuze baadae ( zingatia hiyo biashara siyo rahisi kama mtu anavosimulia maana kupigwa kupo ukienda kizembe).

Zingatia kipindi cha maandalizi ya shamba, kupanda mpunga mpaka kupalilia wanawake wanahelea ( vichenchi kuliko wanaume zao) hiyo ni kulingana na hali ya uchumi wa wanachi wakule. Na kama unaalergy na jua hakika si sehemu salama nadhani ukitoa jua la Wang'ing'ombe-Njombe pale jua ni kama moto wa jehanam hasa miezi ya february, na june,july, August(Hatari sana) mpaka October.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom