Zipo wapi hoja za kumkosoa Rais Magufuli? Kama tumeishiwa bora tuungane naye tu

Mbona tumeambiwa wiki ijayo kampeni za uchaguzi zinaanza? Hiyo sio demokrasia?
Kwa mambo mazuri ya serikali, miradi mikubwa hali mzuri ya uchumi na kila kitu ndio ilipaswa kuwa wakati mzuri wa demokrasia hapa tz Yan wapinzani wakose cha kuongea na sio kuwafanya wakose cha kuongea kwa mizengwe
 
Wapinzani hawana cha kupinga, kila kitu kiko mukide, rais kahamia Dodoma, gesi imeshuka bei, umeme ni wa uhakika, ajira za kumwaga reli mpya imekabidhiwa na mengine mengi.

Tuwazomee wapinzani, tuwasemee wananchi wanaoendelea kuteseka kwenye awamu hii

Umeongea point Mkuu,Wapinzani wangejinyamazia tu
 
Sasa kama Wapinzani wanatambua umuhimu wa Maendeleo kwa nini wanapinga maendeleo yanayoletwa na Magufuli?
Serikali kuleta maendeleo kwa wananchi wake sio hisani au matakwa ya MTU Bali ni wajibu wake kufanya hivyo haipaswi kusifiwa na isipofanya hivyo inapaswa kulaumiwa.
 
Tuache visingizio tupambane kwa hoja tushawishi wapiga kura

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni toka Rais Magufuli aingie madarakani Nchi inazidi kupaa kimaendeleo Echolima1,
 
kinole1984,

kwanini unakimbilia kuilalamikia serikali , sehem za kuajiriwa sio serikalini tu, kuna sekata binafsi, kuna nje ya nchi: sasa ukishindwa na sekta binafsi unalalamika serikali: hii ni akili kweli? ama hujiamini?
 
Dar ipi hiyo Mkuu

Inaweza kuwa unaishi mbali na nyumba yako ipo peke yako Mkuu

Sio rahisi Tanesco kupeleka umeme umbali wa KM kadhaa kwa nyumba moja
Kabisa unasema umeme kila kona ya nchi?? Hapa hapa DSM umeme tu hakuna mimi tangia mwaka 2016 tuliambiwa tunaletewa umeme mpaka sasa haujafika na ni DSM.
 
Maisha yamebadilika sana daah nakumbuka wakati wa JK, kila mtu humu alikua anaazisha uzi wa kumpiga JK na maneno kibao ya kejeli na dharau, wapi sasa hii hali wakuu kulikoni.
 
Maisha yamebadilika sana daah nakumbuka wakati wa JK, kila mtu humu alikua anaazisha uzi wa kumpiga JK na maneno kibao ya kejeli na dharau, wapi sasa hii hali wakuu kulikoni.

Utawala huu kuna ufisadi mkubwa kuliko awamu zote ingawa wanatumia mikwara mingi kutawala
 
Kiboko yake mzee Assad.
Mbombo kafu
IMG-20191106-WA0026.jpeg
 
Naunga mkono hoja.
P

Paskal mayala hupati ukuu wa wilaya wala katibu Tawala hata wilaya ya mbali kama Tunduma au mtukula, umejitoa fahamu zote hujui kuwa hakuna uhuru wa kufanya siasa? Ebu ongea kwa kisukuma wambie Naibu Rais Daud Bashite na mtukufu magufuli waruhusu mikutano ya siasa hata mwezi mmoja tu waone kivumbi chake , ubaya wao wizi wao na kila kasoro zao zote zitaanikwa live na ndipo utajua kuwa upinzani upo mioyoni mwa watu wengi Nchini.
 
Umeandika pumba hueleweki kabisa

Njoo na hoja sasa tujadili
Wewe mbweha acha uongo kwani nini kazi ya upinzani? Kazi ya upinzani ni kuikosoa Serikali kwa mapungufu yake yote kuanzia madogo kabsa mpaka makubwa matukio kila baya la serikali, wananchi wa wapi wanawapuuza wapinzani? Labda wananchi wako na ukoo wa panya, vya kupinga vipo vingi na hakuna aliyewaacha solemba acha kuvuta Bangi huko Ghetto kwa cyprian kisha kuja na propaganda za kishamba toka kolomije. Mmemkimbiza CAG kwa kuogopa kivuli chake juu ya ufisadi wa Ndege na uozo wa ACTL, ufisadii kila kona miradi yote mikubwa wana 10% zao na kampuni zao binafsi ndizo zina upendeleo kwenye supply vifaa, wamekamata madini pesa mipakani Bandarini Airport wanagawana kienyeji Mtukufu na Naibu Rais Daud Bashite na wenzao hata chato Airport imejengwa kienyeji pasipo idhini ya bunge, ufisadi upo mwingi utawala huu wa kidikiteta kuliko Tawala zote endelea kuvuta Bangi huko ghetto na Le mutuz lakini ujue watanzania siyo wajinga kama wewe,
 
Naisikitia Nchi yangu unaendelea kuzalisha wajinga wengi kama we
Watetezi wa CCM kwa 97% wapo ghetto kwa cyprian Musiba na Le mutuz ndiyo wanalipwa mabilioni na CCM kwa kazi ya kuwatetea mitandaoni, lakini Le mutuz pesa nyingi hutafuna na michepuko ni jitu lidhaifu sana matokeo yake wameenda kuwaajiri mbumbumbu vilaza kuwatetea CCM, chunguza utetezi wao unafanana sana kwa sababu hawatumii Akili zao binafsi kuitetea CCM bali wamekariri ujinga wote wa cyprian Musiba na Le mutuz.
 
Back
Top Bottom