Chemtrail
JF-Expert Member
- Aug 15, 2016
- 827
- 442
Nimepokea kwa masikitiko kutoka kwa ndugu zangu walioko Wilayani Lushoto kwamba hali ya usalama Wilayani humo, hasa Lushoto ya Kaskazini ni tete sana. Wote tutakumbuka matukio ya Tanga kule Amboni na Magamba. Inaelekea huu ni muendelezo wa matukio yale.
Taarifa nilizonazo kutoka Lushoto ni kwamba yapo mauaji ya watu wapatao kumi na sita yaliyofanywa maeneo ya Shume kwenye kijiji cha Gologolo baada ya miili ya watu hao kukatwa viungo na hatimaye kutelekezwa. Zipo pia taarifa za isolated incidences za wauaji hao kukata viungo vya miili ya wananchi maeneo mbalimbali na hatimaye kuitelekeza miili hiyo msituni.
Watu hao wanaoaminika kuwa makao yao makuu yapo maeneo ya Kata ya Rangwi. Wilayani humo katika "msikiti fulani mpya" pia wanahusika na wizi kwenye majumba ya watu ya vitu mbalimbali. Tunadhani hii ni katika haarakati za kupata fedha kwa ajili ya kuendeleza harakati zao hizo. Mama yangu mzazi ambaye ni mzee amekubwa na zahma ya kuvunjiwa nyumba na kuibiwa!
Tunaomba serikali na jeshi la polisi wafanye uchunguzi. Kwa vile maeneo yanayokumbwa na balaa hili yapo Kaskazini mwa Wilaya ya Lushoto na mpakani na nchi ya Kenya, tunaoiomba serikali na Jeshi la Polisi wawe makini katika uchunguzi wao kwa vile inawezekana matukio haya ni maandalizi ya harakati pana zaidi za ugaidi.
Taarifa nilizonazo kutoka Lushoto ni kwamba yapo mauaji ya watu wapatao kumi na sita yaliyofanywa maeneo ya Shume kwenye kijiji cha Gologolo baada ya miili ya watu hao kukatwa viungo na hatimaye kutelekezwa. Zipo pia taarifa za isolated incidences za wauaji hao kukata viungo vya miili ya wananchi maeneo mbalimbali na hatimaye kuitelekeza miili hiyo msituni.
Watu hao wanaoaminika kuwa makao yao makuu yapo maeneo ya Kata ya Rangwi. Wilayani humo katika "msikiti fulani mpya" pia wanahusika na wizi kwenye majumba ya watu ya vitu mbalimbali. Tunadhani hii ni katika haarakati za kupata fedha kwa ajili ya kuendeleza harakati zao hizo. Mama yangu mzazi ambaye ni mzee amekubwa na zahma ya kuvunjiwa nyumba na kuibiwa!
Tunaomba serikali na jeshi la polisi wafanye uchunguzi. Kwa vile maeneo yanayokumbwa na balaa hili yapo Kaskazini mwa Wilaya ya Lushoto na mpakani na nchi ya Kenya, tunaoiomba serikali na Jeshi la Polisi wawe makini katika uchunguzi wao kwa vile inawezekana matukio haya ni maandalizi ya harakati pana zaidi za ugaidi.