King Sae
JF-Expert Member
- Mar 22, 2018
- 2,835
- 5,346
Baadhi ya wengi...Sio wengi hawana hatia ,sema baadhi hawana hatia
Baadhi ya wengi...Sio wengi hawana hatia ,sema baadhi hawana hatia
Hapana mkuubilashaka gereza la keko hilo
Gerezan huwez kugeuzwa mwanamke labda tu wewe mwenyewe uwe shoga ukifika utoe kwa hiyari kutokana na ushoga wako au upende maisha ya kitonga kwa kujitoa utu wako ila hakuna wa kukulazimisha na ni bonge la msala askari magereza wakigundua ww pamoja na mwezako mnaokulana patachimbika hapo ndan mtailewa vizuri Nini maana ya show showOngeza nyama kwa wale wafungwa wanaogeuzwa wanawake hii ni kweli
Kama unadhani jela ni shule mpeleke mwanao, sio kuzuri hata kidogo
Hakuna kitu muhimu kwa binadamu kama uhuru, ndugu zangu tuishi na watu vizuri tuepukeni migongano na ugomvi usio na maana hasa wale wenzangu na mimi wenye hasira za karibu na kupanic fasta.. wizi, udokozi na makosa madogo madogo ya kisheria tujiepushe nayo
Sidhan kama Sabaya ataweza kuyafuata haya
Hiii ni ngumu sana magereza wameidhibiti sana ukijulikana utapgwa rungu za mguu hadi ulemavuOngeza nyama kwa wale wafungwa wanaogeuzwa wanawake hii ni kweli
Nitaelezea vitu viwili ambavyo vinapeleka watu wengi jelaDuuh hii biashara haramu ni vile pesa tamu tuu. Kufungwa bahati mbaya.
Story za humu unaweza tamani kuacha ata michongo yako
EeNimewahi mtembelea mshkaji alipigwa miaka 5,aisee vile nilimkuta nililia sn sn.Ni mwezi tu alikuwa amekaa lakini hali niliyomkuta nayo inasikitisha.
Wanaume tumeumbwa mateso
Kwa maelezo haya ni dhahiri Magufuli yupo motoni, maana pamoja na dhahama zote hizi yeye alikuwa anaona hazitoshi aliwasema Askari magereza wawatese kwelikweli wafungwa.Maweni naona ndio gereza gumu sana kutokana na location yake ilipo utapiga sana kokoto kwenye jua pale wafugwa wengi pale wametoka magereza ya karanga(kilimanjaro) na kisongo(arusha) hawa ni wa vifungo virefu na wale wa pale tanga kule shuruba ni nzito sana wafungwa wa kunyongwa wapo pia pale wengii tyu (condemn) maweni hata askari magereza ni wakali sana upekuzi ni kila muda na vipigo ukienda kule mwezi utapauka na kua mweusi tiii kutokana na joto,kazi,mrundikano wakuu gereza la maweni ndio gereza naloliogopa kuliko yote tanzania likifuatiwa na gereza la songwe na gereza lililopo ruvuma!
Chief hapa duniani kabla haujafa hauna assurance yoyote. Kitu pekee ambacho kipo certain ni kifo tu. Haya mengine yanakuja na kupita so mtu asidhani kuwa haya yaliyoandikwa hapa hayamhusu. Ni njia yetu wote.Linapokuja sawa lolote baya akili ya mwanadamu imekuwa ikilisusa bila kutegemea, ni rahisi sana kususia habari za kifo mtandaoni na kutafuta vichekesho au habari za kufurahisha, Sio bahati mbaya ila ni maumbile asili ya mwanadamu.
Lakini hoja uliyoleta mkuu ni nzuri kwa mwanadamu yeyote ambaye bado hajafikwa na umauti. Sikuwahi hata siku moja kuwaza kwamba mimi mwenyewe ipo siku ntakanyaga rumande achana na gerezani, lakini nilipelekwa rumande. Hii ilinifanya niamini kitendo cha mimi kuwa mwanaume na harakati zangu za utafutaji basi lolote linawezekana.
Binafsi nikushukru, kwa kutoa hizi "basics" ntajitahidi kuwa raia mwema, lakini wakati wa upotofu basi zitumike aidha kwangu au ndugu nitakayemshauri pia.
Naomba unitag mkuu kama hutojaljNitaeleza kwa uzi nitakaoshare kuhusu mambo yanayopeleka wengi jela
Umeongea point sana dawa ni kuwaavoid watu wanaoweza kukupeleka ukoNilitumwa kikazi gereza fulani, aiseeee kumbe kule pasikie tu, jamani nyie lile limlango lione tu ila ukiingia kutoka ni ngumu.
Basi nilivyofika nikajitambulisha nimetumwa na mamlaka fulani kumuona mfungwa fulani nikaonyesha docs anazotakiwa kusaini.
Sikupata usumbufu wowote askari walinipokea vizuri.nilikalishwa sehemu baada ya muda wakamleta nikaongea nae ila mbele ya askari.
Niliongea nae akaomba hizo documents nimpelekee mtu fulani baada ya yeyekusaini na wakagonga mhuri wa magereza kuwa kapokea.
Nafasi aloipata ni kupitia hiyo document nilopeleka ataweza pata hata wakili waongee tho nafasi ya kumsaidia ilikuwa ni ndogo.
Machache niliyoyaona ndani ni kusafi sana maua kila kitu mazingira kwa nje ni safi.
Wafungwa ambao walikuwa hawajavaa sale niliona wakiwa katika vazi zao na wasafi tu.
Nilichogundua kule kuna nidhamu ya hali ya juu.kila kitu ni utaratibu.
Wakati nikiwa pale mlangoni kwa ndani maafande walinzi walinambia mtu anapoingizwa pale kwa mara ya kwanza uamini kuwa atatoka soon ila sio kweli, kuingia ni rahisi ila kutoka sio unavyodhani.
Kwa ulinzi ule inabidi kuwa mpole ukiwaza kutoroka lazima uumie. Kwanza unaanzaje kutoroka kwa fensi ile? Fensi ndefu vile kama barabara?
Nilijifunza tuishi kwa kuwa makini ukiona mtu anataka kukuletea msala jiweke pembeni.mambo ya ugonvi, kuzurumu watu na mambo mengine mabaya tuepukane nayo.