Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
BADILI TABIA
Ni matumaini yangu kwamba kwa wale ndugu zangu waislamu wameanza mfungo wa mwezi mtukufu salama kabisa.
Baada ya kupata nafuu naamini inshaallah wiki ijayo Jumamosi ya tarehe 28, Julai 2012 kipindi hili cha Zinduna talk show kitarejea kama kawaida na nimeona nianze na mtu muhimu sana hapa JF, Mama yangu wa hiyari BADILI TABIA.
Naomba kwa hisani yako mama uthibitishe uwepo wako katika kipindi hicho muhimu hapo juma lijalo naamini itakuwa ni fursa nzuri kwa wana JF kukufahamu vizuri na labda watapata pia fursa ya kujifunza mengi kupitia uzoefu wako katika mapenzi na mahusiano ya kijamii.
Pia ningependa kuwashukuru Smile na Erickb52 kwa kujitolea kuendesha kipindi hiki wakati nilipokuwa mgonjwa, naamini humu kuna vipaji vingi sana na sasa najua kuwa, kumbe hata nitakapokuwa na udhuru wapo wadau wa kusongesha Zinduna talk show kama kawa.
Nawatakia siku njema na ninaomba wiki ijayo tuwe pamoja katika kumkaribisha mama yetu BADILI TABIA
ONYO: Kipindi hakipo leo kwa hiyo msianze kumsakama mualikwa na maswali, subirini wiki ijayo ndio mje hapa na maswali yenu.
Last edited by a moderator: