Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Ciello
Samahani sana wapenzi wa JF chit chat, kwa ukimya wa muda mrefu. Leo mjengoni nipo na Ciello, mshindi wetu wa Miss Chit Chat wa mwezi Novemba 2012 ,ambaye kutokana na ushindi wake huo mnono nitafanya naye Exclusive Interview ili kujua siri ya ushindi wake huo.
Ciello ameshinda kwa ushindi wa kishindo alioupata baada ya mchuano mkali ambapo alishinda kwa kura nyingi sana zipatazo 51 dhidi ya charminglady aliyepata kura 07, lara 1 aliyepata kura kura 13 na Arabela aliyepata kura 16.
Niko hapa na Kidadavuzi Mpakato changu (Lap Top) na nitapokea maswali yenu na maoni yenu kwa njia ya simu, ujumbe wa simu ya kiganjani, barua pepe (Email) na tarakishi (Fax). Line za ku-post Comments ziko wazi, Mwana JF yeyote anaweza kutumia fursa hii kumuuliza Ciello swali lolote na yeye bila shaka atayajibu maswali yenu kwa kadiri atakavyopata muda.
Kwa kuanza ninayo maswali kumi na tano ambayo ningependa kumuuliza Ciello:
1. Je umezaliwa msimu gani?
2. Hebu nipe historia yako ya hapa JF kwa kifupi, yaani ulifahamuje kuhusu JF, ulijiunga lini na ni nini kilikusukuma hadi ukajiunga na JF?
3. Je Ni kitu gani kilikusukuma hadi ukaingia katika mashindano ya Miss Chit Chat ya Novemba?
4. Je ni nini siri ya ushindi wako?
5. Unazungumzia nini kuhusu rufaa iliyokatwa na C6 akipinga ushindi wako?
6. Una ushauri gani kuhusu Miss Chit Chat?
7. Je ulishawahi kucheza mchezo wa baba na mama na kupika pika utotoni?
8. Je umeolewa? Kama umeolewa, Je una watoto wangapi, na kama hujaolewa, Je unaye wa mpenzi wa kuchombeza, na kama huna unamalizaje matamanio yako ya kujamiiana?
9. Je ni tukio gani liliwahi kukuhuzunisha sana?
10. Je ni tukio gani liliwahi kukufurahisha sana?
11. Je unapenda kuvaa nguo za aina gani?
12. Je unapenda chakula cha aina gani?
13. Je ni jambo gani umewahi kulifanya kwa faida ya nchi yako na ambalo hata ukifa litabaki kama kumbukumbu kwa vizazi vijavyo?
14. Je ukipata fursa ya kupata staftahi na Mungi, ni jambo gani ungependa kuzungumza naye?
15. Una ushauri gani kuhusu hiki kipindi cha Zinduna Talk Show…….?
Haya nakaribisha maswali yenu wadau na hivi punde Ciello atakuja kuyajibu maswali yenu.
Karibuni sana
Wiki ijayo Jumamosi ya tarehe 10/11/2012 Zinduna Talk Show, mjengoni atakuwepo Aunt BADILI TABIA
Stay tune.
Last edited by a moderator: