Neiwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 728
- 633
Kumekuwa na hamasa hamasa ya maandamano kwa kupitia Mitandao ya Kijamii, haswa kupitia Instagram na Telegram. Hamasa hii imeamsha hisia za kila aina kwa wale ambao wanafuatilia kwa karibu.
Hamasa hii imezaa makundi matatu:
Kwa wale wasiojua, taarifa za awali za kutaka kufanywa maandamano ni Bi. Mange Kimambi ambaye baada ya kumshambulia kwa posts kadhaa Rais Magufuli kupitia mtandao wa Instagram, aliamua kuwa sasa inatakiwa kuandamana akidai kuwa Upinzani nchini Tanzania hauna nguvu wala mipango thabiti inayoeleweka kuweza kuutoa au kuushinda uongozi uliopo aidha kwa haki (uchaguzi) au kwa kupindua.
Bado ni mapema sana kuzungumzia nini kinatarajiwa kutokea hapa karibuni, ikiwa bado ni Mwezi na nusu toka sasa hadi tarehe iliyopangwa maandamano hayo.
La msingi kuliko yote ni kwamba ni wazi Serikali imeyasikia na tumesikia viongozi mbali mbali wakitoa matamko au kuzungumzia juu ya hamasa hizo za maandamano. Mrejesho huo wa viongozo mbali mbali ikiwemo na rais wa nchi, inafanya kuibuka kwa mijala kwa upana zaidi kama vile, kukuzwa kwa maandamano haya, kukuzwa kwa jina la Mange Kimbambi na kumfanya awe relevant zaidi, kutopokelewa na kutenda sahihi tokana na hamasa hizo, na masuala mengine kede kede.
Kwa wale ambao hawajabahatika kusikia baadhi ya kauli za viongozi unaweza soma hapa chini:-
CP Nsato Marijani (Mkuu wa Operation na mafunzo):
Kuna kikundi ambacho kimetumia mtandao wa Telegram kuhamasisha maandamano nchi nzima kinyume cha sheria na kutaka kwenda ikulu na kufanya hayo wanayotaka kufanya. Naomba nirudie kusema kwamba lolote linalotaka kufanyika katika nchi hii, sisi kama jesi la Polisi tunawaasa wananchi walifanye kwa mjibu wa sheria. Swala la kufanya maandamano ukiwa na nia ya kuiondoa serikali ni uhaini. Hatua kali zitachukuliwadhidi ya watu watakaovunja sheria na tusije kulaumiwa kwa lolote
Rais John Pombe Magufuli:
"Wapo watu wameshindwa kufanya siasa za kweli wangependa kila siku tuwe barabarani tunaandamana, watu wao wanahamia huku wao wanataka wabaki wanaandamana kule nimeshasema ngoja waandamane wataniona, kama kuna baba zao wanawatuma basi watakwenda kuwasilimulia vizuri, niliapa kwa Katiba kwamba nchi hii lazima iwe ya amani na tunataka tujenge uchumi wa kweli ili Watanzania watajirike na hali ya Watanzania imeanza kwenda vizuri mwanzo ni mgumu lakini nataka niwaambie watanzania tupo kwenye wakati mzuri tuvumiliane ili tufike sehemu Tanzania iwe nchi ya asali"
Msome Rais Magufuli: Rais Magufuli: Ole wake atakayeandamana, kama kuna baba zao wanawatuma, watakwenda kuwasimulia vizuri
Paul Makonda (Mkuu wa Mkoa wa Dar):
"Kuna kakundi hapa kanahangaika kweli usiku na mchana wengine wanahangaika kutumia mitandao ya kijamii kutukana viongozi, kuhamasisha sijui wanaita nini sijui maandamano nawapa pole sana, watafanya labda mimi nikiondoka nikiwa siyo Mkuu wa Mkoa kwenye huu Mkoa hiyo mipango mipango yao watafanya labda mimi nikiwa sipo lakini amani ya mkoa wa Dar es Salaam ni muhimu sana"
IGP Simon Sirro (Mkuu wa Jeshi la Polisi):
"Wote tunajua kwamba maandamano Katiba imetamka na sheria za vyama vya siasa imetamka kwamba maandamano ni haki kwa raia lakini kuna utaratibu wa maandamano, sasa kuna maandamano ambayo ni halali na ambayo si halali. Maandamano ambayo si halali maanake yanaashilia uvunjifu wa amani ni maandamano ambayo yanaelekea kutenda uhalifu sasa kama ni maandamano yanakuja kwa njia ya uhalifu na jeshi la polisi lipo kwa ajili ya kuzuia uhalifu maanake ni lazima tuhakikishe maandamano hayo hayafanyiki hivyo ni lazima juhudi ifanyike kabla ya hayo maandamano kufanyika"
Zaidi IGP anasema....
"Maandamano yakifanyika ambayo si halali uwezo wa kuudhibiti tunao sasa natoa tu salamu kwa wale ambao wanafikiri wataweza kufanya maandamano ambayo si halali ya kutaka kuleta vurugu ndani ya nchi ambao ni watu wachache wenye maanake ni lazima watapamba na jeshi la polisi ambalo linasimamia usalama wa nchi hii, lakini niwambie na wale vijana wadogo na wazazi, wazazi wajitahidi sana kulea watoto zao wajaribu kuwaambia watoto zao wasiingie kwenye kuvunja sheria kwani unaweza kuvunja sheria kirahisi ila madhara yake ni makubwa. Unaweza kuingia kwenye maandamano ambayo si ya halali halafu ukileta shida kubwa kwako na familia yako. Wanacheza na hiyo mitandao sijui tumefika mia moja, mia mbili siju elfu moja wajaze wanachosema lakini nasema nafasi hiyo hawataipata"
Msome zaidi IGP Sirro: IGP Sirro: Ole wake atakayeandamana bila kufuata sheria
Kamanda Lazaro Mambosasa:
"Kuna watu ambao wanaendelea kuhamasisha wananchi kuvunja sheria. Wanataka wajiandae kwa maandamano, tarehe wanazoendelea kutaja. lakini wanafanya hivyo wao wakiwa wamekaa sehemu salama. Wanataka kuwaingiza watanzania wengine kwenye shida,"
Msome Mambosasa: Polisi yawakamata wawili kwa mauaji ya Kiongozi wa CHADEMA. Kamanda Mambosasa akataza maandamano ya mitandaoni
Mkuu wa Majeshi (CDF), Jenerali Venance Mabeyo naye akasema: Jenerali Mabeyo(JWTZ): Kuna Viashiria vinavyotishia Usalama wa Nchi. Hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo
Uhalisia wa Hamasa hizi za Maandamano:
Kila mmoja ana lake la kusema, lile analoliamini na wengi wanakuwa wanasimamia mawazo yao hayo kwa vigezo mbalimbali....
Naomba kufahamu toka kwenu wana JamiiForums, ni nini uhalisia (tokana na mtazamo wenu) juu ya hamasa hii ya maandamano na namna inavyochukuliwa na viongozi wa juu pamoja na wananchi huko mitaani?
Maoni ya wananchi (Kwa hisani ya Kwanza TV)
Nawasilisha!
Hamasa hii imezaa makundi matatu:
Kundi la kwanza: Wale wanaoamini haya maandamano yana tija na yatafanikiwa.
Kundi la pili: Wale wanaoamini maandamano haya yana tija ila hayatafanikiwa.
Kundi la tatu: Wale ambao wanaamini haya maandamano hayana tija na wala hayatafanikiwa.
Kundi la pili: Wale wanaoamini maandamano haya yana tija ila hayatafanikiwa.
Kundi la tatu: Wale ambao wanaamini haya maandamano hayana tija na wala hayatafanikiwa.
Kwa wale wasiojua, taarifa za awali za kutaka kufanywa maandamano ni Bi. Mange Kimambi ambaye baada ya kumshambulia kwa posts kadhaa Rais Magufuli kupitia mtandao wa Instagram, aliamua kuwa sasa inatakiwa kuandamana akidai kuwa Upinzani nchini Tanzania hauna nguvu wala mipango thabiti inayoeleweka kuweza kuutoa au kuushinda uongozi uliopo aidha kwa haki (uchaguzi) au kwa kupindua.
Bado ni mapema sana kuzungumzia nini kinatarajiwa kutokea hapa karibuni, ikiwa bado ni Mwezi na nusu toka sasa hadi tarehe iliyopangwa maandamano hayo.
La msingi kuliko yote ni kwamba ni wazi Serikali imeyasikia na tumesikia viongozi mbali mbali wakitoa matamko au kuzungumzia juu ya hamasa hizo za maandamano. Mrejesho huo wa viongozo mbali mbali ikiwemo na rais wa nchi, inafanya kuibuka kwa mijala kwa upana zaidi kama vile, kukuzwa kwa maandamano haya, kukuzwa kwa jina la Mange Kimbambi na kumfanya awe relevant zaidi, kutopokelewa na kutenda sahihi tokana na hamasa hizo, na masuala mengine kede kede.
Kwa wale ambao hawajabahatika kusikia baadhi ya kauli za viongozi unaweza soma hapa chini:-
CP Nsato Marijani (Mkuu wa Operation na mafunzo):
Kuna kikundi ambacho kimetumia mtandao wa Telegram kuhamasisha maandamano nchi nzima kinyume cha sheria na kutaka kwenda ikulu na kufanya hayo wanayotaka kufanya. Naomba nirudie kusema kwamba lolote linalotaka kufanyika katika nchi hii, sisi kama jesi la Polisi tunawaasa wananchi walifanye kwa mjibu wa sheria. Swala la kufanya maandamano ukiwa na nia ya kuiondoa serikali ni uhaini. Hatua kali zitachukuliwadhidi ya watu watakaovunja sheria na tusije kulaumiwa kwa lolote
Rais John Pombe Magufuli:
"Wapo watu wameshindwa kufanya siasa za kweli wangependa kila siku tuwe barabarani tunaandamana, watu wao wanahamia huku wao wanataka wabaki wanaandamana kule nimeshasema ngoja waandamane wataniona, kama kuna baba zao wanawatuma basi watakwenda kuwasilimulia vizuri, niliapa kwa Katiba kwamba nchi hii lazima iwe ya amani na tunataka tujenge uchumi wa kweli ili Watanzania watajirike na hali ya Watanzania imeanza kwenda vizuri mwanzo ni mgumu lakini nataka niwaambie watanzania tupo kwenye wakati mzuri tuvumiliane ili tufike sehemu Tanzania iwe nchi ya asali"
Msome Rais Magufuli: Rais Magufuli: Ole wake atakayeandamana, kama kuna baba zao wanawatuma, watakwenda kuwasimulia vizuri
Paul Makonda (Mkuu wa Mkoa wa Dar):
"Kuna kakundi hapa kanahangaika kweli usiku na mchana wengine wanahangaika kutumia mitandao ya kijamii kutukana viongozi, kuhamasisha sijui wanaita nini sijui maandamano nawapa pole sana, watafanya labda mimi nikiondoka nikiwa siyo Mkuu wa Mkoa kwenye huu Mkoa hiyo mipango mipango yao watafanya labda mimi nikiwa sipo lakini amani ya mkoa wa Dar es Salaam ni muhimu sana"
IGP Simon Sirro (Mkuu wa Jeshi la Polisi):
"Wote tunajua kwamba maandamano Katiba imetamka na sheria za vyama vya siasa imetamka kwamba maandamano ni haki kwa raia lakini kuna utaratibu wa maandamano, sasa kuna maandamano ambayo ni halali na ambayo si halali. Maandamano ambayo si halali maanake yanaashilia uvunjifu wa amani ni maandamano ambayo yanaelekea kutenda uhalifu sasa kama ni maandamano yanakuja kwa njia ya uhalifu na jeshi la polisi lipo kwa ajili ya kuzuia uhalifu maanake ni lazima tuhakikishe maandamano hayo hayafanyiki hivyo ni lazima juhudi ifanyike kabla ya hayo maandamano kufanyika"
Zaidi IGP anasema....
"Maandamano yakifanyika ambayo si halali uwezo wa kuudhibiti tunao sasa natoa tu salamu kwa wale ambao wanafikiri wataweza kufanya maandamano ambayo si halali ya kutaka kuleta vurugu ndani ya nchi ambao ni watu wachache wenye maanake ni lazima watapamba na jeshi la polisi ambalo linasimamia usalama wa nchi hii, lakini niwambie na wale vijana wadogo na wazazi, wazazi wajitahidi sana kulea watoto zao wajaribu kuwaambia watoto zao wasiingie kwenye kuvunja sheria kwani unaweza kuvunja sheria kirahisi ila madhara yake ni makubwa. Unaweza kuingia kwenye maandamano ambayo si ya halali halafu ukileta shida kubwa kwako na familia yako. Wanacheza na hiyo mitandao sijui tumefika mia moja, mia mbili siju elfu moja wajaze wanachosema lakini nasema nafasi hiyo hawataipata"
Msome zaidi IGP Sirro: IGP Sirro: Ole wake atakayeandamana bila kufuata sheria
Kamanda Lazaro Mambosasa:
"Kuna watu ambao wanaendelea kuhamasisha wananchi kuvunja sheria. Wanataka wajiandae kwa maandamano, tarehe wanazoendelea kutaja. lakini wanafanya hivyo wao wakiwa wamekaa sehemu salama. Wanataka kuwaingiza watanzania wengine kwenye shida,"
Msome Mambosasa: Polisi yawakamata wawili kwa mauaji ya Kiongozi wa CHADEMA. Kamanda Mambosasa akataza maandamano ya mitandaoni
Mkuu wa Majeshi (CDF), Jenerali Venance Mabeyo naye akasema: Jenerali Mabeyo(JWTZ): Kuna Viashiria vinavyotishia Usalama wa Nchi. Hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo
Uhalisia wa Hamasa hizi za Maandamano:
Kila mmoja ana lake la kusema, lile analoliamini na wengi wanakuwa wanasimamia mawazo yao hayo kwa vigezo mbalimbali....
Naomba kufahamu toka kwenu wana JamiiForums, ni nini uhalisia (tokana na mtazamo wenu) juu ya hamasa hii ya maandamano na namna inavyochukuliwa na viongozi wa juu pamoja na wananchi huko mitaani?
Maoni ya wananchi (Kwa hisani ya Kwanza TV)
Nawasilisha!