ZIMBABWE: Watu wanne watupwa mbaroni kwa kumzomea mke wa Rais

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Watu wanne wamekamatwa nchini Zimbabwe wakituhumiwa kumzomea mke wa rais wa nchi hiyo Grace Mugabe wakati akihutubia mkutano wa hadhara siku ya jumamosi iliyopita.

Gazeti linalomilikiwa na Serikali la The Herald limeripoti kwamba watuhumiwa hao wanakabiliwa na mashitaka ya kupuuza mamlaka ya rais.

Kuzomea huko kuliibuka kati ya makundi mawili ndani ya chama tawala cha Zanu-PF yanayopambana juu na nani atakuwa mrithi wa rais Robert Mugabe ambapo kuna kundi linalimuunga mkono mke wa rais Grace Mugabe na lile linalomuunga mkono Makamu wa rais aliyefukuzwa Emmerson Mnangagwa.

Imedaiwa kwamba watu hao waliokamatwa ni wafuasi wa aliyekuwa Makamu wa Rais

Watu hao walikamatwa mara baada ya mkutano huo uliofanyika mjini Bulawayo,watuhumiwa hao inasemekana ni aliyefukuzwa Emmerson Mnangagwa .

Watuhumiwa hao waliokatwa ni wanaume watatu na mwanamke mmoja wako nje kwa dhamana.

Chanzo: EATV
 
Nchi wanaifanya kama familia Yao..Mugabe family.


Ewe Mugabe usiye na haya,usiye na roho ya huruma,uliye na kiburi..unayelitia aibu na umasikini Taifa la Zimbabwe..NINANI ALIYEKUROGA.????

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom