ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Sawa bana sisi huko mikoani zetu kuwaonea gele tu. mara utasikia
club raha leo show! ooooooooo!
asubuhi njema, mchana mwema, mara ombi lako, yaaani shambani juma hili, full michosho! hatukuzijua bendi hizo.japo tulipenda nyimbo hizo
 
Sawa bana sisi huko mikoani zetu kuwaonea gele tu. mara utasikia
club raha leo show! ooooooooo!
asubuhi njema, mchana mwema, mara ombi lako, yaaani shambani juma hili, full michosho! hatukuzijua bendi hizo.japo tulipenda nyimbo hizo
 
Habari zenu wapendwa mm ni mpenzi sn wa muziki wa dansi kuanzia mwaka 2000 na kuendelea nilikua naomba nyimbo zifuatazo , chuchu sound leila, ukweli, kusema sema rmx, na nyingine ni za mchinga sound inaitwa kidomo domo, nyingine ni juma kakere inaitwa ndoa ya lazima iko katika album yake ya betty, nyingine ni neema rmx hii nyimbo ilitungwa na mchawi wa solo tanzania adolph mbinga akiimba na ramadhani masanja.R.I.P, joniko flower maua, na nyimbo ya sikinde inaitwa adha ya chumba kimoja hz nyimbo nakumbuka zilikua zinapigwa na kituo cha radio one naombeni sn mwenye nazo anisaidie tafadhali
 
Napenda sana nyimbo za the Mushrooms. Zinanikumbusha sana marehemu babu yangu mjoli.
 
Salama wakuu?,ni jumapili nyingine tulivu....

Leo naomba tujikumbushe bendi zetu zilizotamba sana miaka ya 80 na 90,bendi ambazo ama zimekufa ama zinaendelea kusuasua na ambazo ukisikiliza muziki wake leo hii unatamani ungerudisha wakati nyuma.......

Kwa kuanzia tuanze na hawa Orchestra Vijana Jazz,bendi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Umoja wa vijana wa CCM,bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo ya Sindimba,Hekaheka,Heka koka,Watoto wa nyumbani,Air Pambamoto(awamu ya kwanza na ya pili) na baadae mtindo wa Saga Rhumba.....

Kwangu mimi bendi hii ndiyo ilikuwa chaguo langu hasa......Ukitaka kuujua ukali wa bendi hii sikiliza nyimbo kama Chiku,Mary Maria,Penzi lamea penye penzi,Shemeji,Bujumbura,Ilikuwa lifti,Tambiko la Pambamoto,Adza(Aza),Ngapulila,Ogopa Tapeli,Mwisho wa Mwezi,Penzi haligawanyiki,Wivu,Malaine,Nyongise,Shoga,Theresa,V.I.P,Mama Chichi na nyingine nyingi tu tamu....

Bendi hii imewahi kuundwa na wanamuziki kama Hemed Maneti 'Chiriku',Hamza Kalala 'Komando',Manitu Mussa,Issa Chikupele,Hassan Dalali,Hassan Shaw,Ally Jamwaka,Abuu Semhando,Bakari 'Baker' Semhando,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya zege',Eddy Sheggy,Shaban Yohana 'Wanted',Rashid Pembe 'Profesa',Kida Waziri,Beno Villa Anthony,Rahma Shally,Jerry Nashon 'Dudumizi',Suleiman Mbwembwe,Shaban Dogodogo,Aggrey Ndumbalo,John Kitime,Abdallah Mgonahazelu,Freddy Benjamin,Mohammed Gotagota,Said Hamis 'Misukosuko',Athumani Momba na wengine kibao...

Habari zaidi, soma=>Mashairi ya Kiswahili ya Nyimbo zote za Maquis du Zaire

Mkuu umenikuna sana katika uzi wako huu. Binafsi kuna wanamuziki wawili ambao huwa naona nyimbo zao na uimbaji wao ulikuwa wa kutukuka. Hawa si wengine bali ni Hemed Maneti (Chiriku) wa Vijana Jazz na Marijani Rajabu (Jabali la Muziki). Bahati mbaya hawa wote wakuwahi kuwaona live wala picha zao. Naomba angalau mwenye picha zao au hata video zao japo niwajue kwa sura maana wote ni marehemu. Wanamuziki hawa ni mfano wa vipaji vikubwa kuapata kutokea Tanzania ambavyo kusema kweli naona kama mapengo yao hayajazibika
 
Wakuu kwema?
Ebana kuna wimbo wa Sikinde kiitikio chake wanasema “kwa kauli yangu ya ukiwa siwalaumu enyi wakwe”
Mwenye kuujua jina lake au mwenye nao please yamenikuta mkongwe mwenzenu nauomba tafadhali

DDC Mlimani park - Kiu ya JiBu
 
Samahani kuna wimbo wenye maneno...ni penzi gani alilokupa huyoo na kuchanganyikiwa na kuisahau sura yangu siku ya harusiii...unaitwaje na ninaweza kuupata?
 
Samahani kuna wimbo wenye maneno...ni penzi gani alilokupa huyoo na kuchanganyikiwa na kuisahau sura yangu siku ya harusiii...unaitwaje na ninaweza kuupata?
Wimbo unaitwa THERESA ulipigwa na kuimbwa na Vijana Jazz Band wana Air Pambamoto Awamu ya Pili..
 
Jamani mimi binafsi naombeni mwenye wimbo wa Edina by Magereza Jazz afanye kuutuma kwa njia yoyote anayoona itafaa, kama link tuma, kama utaweza kuattach hapa sawa kama utanitumia kwa email basi tuma hapa mwalusasi@gmail.com Mpaka nafikia kuuomba kwenu huu wimbo ni kwa sababu ninaupenda mno pili nimeutafuta mara zote kwa Internet lakini bado nimeukosa! Inaniuma tafadhari nisaidieni!!
 
41 Reactions
Reply
Back
Top Bottom