ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Napenda kuuliza huyu mama Lady Isa (isabelle) alikuwa anatokea nchi gani kati ya DR Congo au Kenya?
Nyimbo zake
1. Kutereza si kuanguka,
2. Dunia ina mambo (lukumba lukumba)

 
Wakati UDA Jazz wanatamba Ally Choki alikuwa mtoto mdogo sana mkuu,sema UDA Jazz imepitiwa na mwalimu(baba wa muziki) wa Ally Choki Komando Hamza Kalala...

Bantu Group Band ndiyo imemtoa Ally Choki japo kuna taarifa kwamba aliwahi pia kupitia bendi ya Lola Afrika ya Profesa Vulata...

Sikiliza kibao cha Baba Jane na 1 cha Bantu Group utamsikia Ally Choki kwenye kiitikio 'Mimi ooooo(mimi oooooh) Baba Jane bye bye, bado nakupenda mume wangu,baba Jane bye bye, narudi nyumbani baba Jane,baba Jane bye bye, narudi kwa baba na mama,baba Jane bye bye"......Hapo Choki ndio kwanza alikuwa anaanza kusikika katika anga za muziki wa kibongo
Huu wimbo nimeusaka kila mahali nimeukosa. Kuna mahali mdau aliniwekea wimbo wa Vijana Jazz uitwao -Kapu la Mjanja- Hizi nyimbo kuna mambo fulani nikizisikia huwa kuna kumbukumbu fulan ambazo hunipa hisia kali sana. Kama mkuu Balantanda au mdau yeyote ataweza kuniwekea nitashukuru sana.
 
Nico Zengekala(R.I.P) pamoja na kilema chake cha upofu alikuwa habari nyingine mkuu,angalia mashairi ya nyimbo hizi utaona maana ya ninachokisema ama ulichokisema wewe hapo juu...

Jackie...


Mtoto Jackiee,mtoto wa Nirobi
Ingawa ni mara ya kwanza mimi nawe Jackiee
Tulipokutana palee Kampala kwenda Nairobi
Tulifurahiana sana kama tuliishi mwaka
Tabia yako njema kweli sitoisahau.

Mtotoo Jackie,mtoto wa mama Jackie wa mapendo
Japokuwa tuliachana stendi ukielekea Nairobi nyumbani eeh
Lakini tutakutana,nitakuja kutembelea,nawe karibu nyumbani eeh
Ooh Jackie yeyeeeh

Mtoto wa mama Jackie wa mapendo
Japokuwa tuliachana stendi,ukielekea Nairobi nyumbani eeh
LAkini tutakutana,nitakuja kutembelea,nawe karibu nyumbani eeh
Ooh Jackie yeyeeeh

Kiitikio:

Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau lakini nashindwa
Hasa ni ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU

Nimejaribu kukusahau lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua eeh

Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau lakini nashindwa
Hasa ni ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU

Nimejaribu kukusahau lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua eeh

Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau,lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU

Sauti yako nyororo inaniua sana na mwendo wako wa maringo unanikondesha mamaaah,ayoleli mwanamama nakuwinda sana Jackie yeyeyeeeh mwanamamaah aeaeeh

Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau,lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU

Mvumilivu hula mbivu,Jacki yeyeeeh,mvumilivu hula mbivu Jackie yeyeeeh
Jaribu kuvumilia yeeh tutaonana mamaah kama sio Kampala ni Tanzania mamaa
Jackie yeyeyeeh mwanamama aeaeeh

Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau,lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU



Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
Nitakuja Nairobi eeh nikuone mamaah
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
Tutafurahi pamoja mi na wewe mama yeeh
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
Jackie yeyeyeeh Maneno sema na yeye
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi

ama kitu Solemba

Solemba solemba solemba aaaaaaaaaah

Sitakuwa nikifika nyumbani kwako,aibu nilopata ni kubwa sana,
Ahadi nilopewa ilivunjwa oooh ooooh hata bila kosa,
Ulinipa ahadi tukutane kwenu,nikitumaini nimewahi,
Nilichopata kwako ni matusi oooh ooh na dharau tele,

Ungenieleza ukweli Solemba,kuliko kunidanganya ooh,
Najuta kuitimiza ahadi oooh ambayo si ya kweli,
Ungenieleza ukweli Solemba,kuliko kunidanganya ooh,
Najuta kuitimiza ahadi oooh ambayo si ya kweli,

Bridge

Ulinipa ahadi tukutane kwenu,nikitumaini nimewahi,
Nilichopata kwako ni matusi oooh ooh na dharau tele,
Ungenieleza ukweli Solemba,kuliko kunidanganya ooh,
Najuta kuitimiza ahadi oooh ambayo si ya kweli,

(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba

Zengekala: Ulinikana mbele za watu ati hunifahamu,
Ndugu zako na marafiki walianza kutoka nje,
Waliponiona ni mimi,walishangaa sana mama,
Mbona hivyo solemba mama eee

(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba

Zengekala: Nilikuuliza mbona ulinitendea hivyo Solemba,
Ulisema mimi hujipendekeza kwako tena sana,
Na kuwa hunipendi,nakusumbua bure mamaa,
Mola yupo Solemba,Eloi yupo mamaa.

(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba

Zengekala: Nilichomwa na jua toka asubuhi,
mpaka saa nane Solemba,Sababu ya kukungoja wewe
Kumbe ulikuwa ndani,unachungulia dirishani,
Huna huruma Solemba,I shall never forget you mamaa,

(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba

Zengekala: Sikutaki tena,sina haja nawe,
Nimeshapata mwingine anayenipenda kwa roho moja,
Tafuta bwana mwingine utakayembabaisha kama mimi,
Nimeshituka Solemba,nimeshituka solemba.

(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba

Zengekala: Lalala lalala lalala lalalalala
Nimeshapata mwingine anayenipenda kwa roho moja,
Tafuta bwana mwingine utakayembabaisha kama mimi,
Nimeshituka Solemba,lololo lolololo mama lo

(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba
Daaaaa,ni shida. Siku hizi jaman vipaji viko wapi?
 
FM ACADEMIA 2018 Dar es Salaam, Tanzania timu ni ile ile lakini kocha mpya full dozee wazee wa Ngwasuma chini ya Patcho Mwamba live HD


Source: saluti5.com
 
nyie wazee wa zamani mlishindwa hata kurekodi video za nyimbo zenu au hata performance
 
March 17, 2018
Dar-es-Salaam, Tanzania

Rashid Pembe aelezea siri ya anguko la muziki wa dansi Tanzania lilianzia mwaka 1994 na kufikia kilele mwaka 2004.

Ambapo wadau wakubwa kama studio, media n.k waliofadhili kutoa, kutangaza na kuuza album za muziki wa dansi kuelekeza nguvu zao ktk muziki wa bongo -flava ili hata watoto wadogo wa miaka hiyo ya 90 waikubali.

Anakubali media zina nguvu za kumnyanyua msanii au bendi na kutoa mfano Saida Karoli alivyobaniwa na media alipotea na kurudi kwao. Lakini media walipoamua kumpa airtime Saida Karoli amerudi upya na kuendelea na muziki wake.

Endelea kumsikiliza mpiga saxophone nguli wa Vijana Jazz Rashid Pembe akifunguka wanavyokabiliana na mabadiliko hayo kwa kwenda Facebook, youtube na WhatsApp ili kufikia umma wenye kufuatilia muziki wa dansi :

Source: saluti5.com
 
Nimeguswa na hisia za Mzee Pembe,Vijana Jazz ikiwa iko moto kweli kweli,ndo hivyo zimebaki stori!
Ila sikumpata vizuri,mbona miaka ya 1996/97,Vijana Jazz walitoa Album iliyo hit(Tafrija la Kuuaga Umaskini-Umaskini bye bye) ambapo ilifanya vizuri tu. Naona anguko la Dansi lilianza miaka ya 1999 kuja hadi 2000. Baada ya hapo ilikuja Dansi mpya ya Twanga Pepeta miaka hiyo ya 1999-2006!Twanga,Muungano,TOT,Tam Tam na FM Academia,Beta Musica,Extra Bongo na Dar Musica. Hata hivyo nazo zinaelekea kufutika.
 
Back
Top Bottom