Zilikuwa nyakati za Chico, Nat King Cole, Dean Martin, Sammy Davis Jr, Sidney Poitier..Ukipenda Sal

Alama, Mohamed Said, uliowataja karibia wote ni kaka zangu wa Kariakoo. Nnalia.

Dah! Ulipomtaja Salum Hiriz, nikamkumbuka na Ali Bobo.

Henin ananikumbusha enzi za Lumumba ilivyokuwa Lumumba haswa.

Mrisho Wanted unanikumbuka siku zake za mwisho akija nyumbani kuchukuwa kanzu zake za KUSWALIA, special kwa ajili yake zilizotoka Dubai kwa Jamil, Dennis Law.

Mohamed Saiwad (Chico) Allah amrehemu aturehemu nasi tulio hai. Amiiiin.
 
Pohamba,
Usitokwe na machozi bali shukuru kuwa Allah katoweka kiasi hiki
kwani wenzetu wengi wameshatangulia.

Tamim ni rafiki yangu wa miaka mingi sana.
Nikipata picha za zamani nitakuwekea hapa.

Ma sha Allah, juzi juzi Anko Tamim alikuwa akinipa kisa chenu na Henin na Black American mmoja aliyekuja 70s na kuponda ponda watu.

Nadhani utakikumbuka.
 
Taazia pelekeni nyumbani mkawadanganye ndugu zake. Tulio ishi na Chico hamuwezi kutuletea bandiko hili tukaacha kusema ukweli.
Jigsaw,
Huenda kuna baadhi ya ada zetu huzielewi na ndiyo maana umekuja na
maneno haya.

Mtu anapofariki inapendeza watu wakazungumza yale mema yake kwani
wapo nduguze walio hai hawatafurahi kusikia maiti yao inakashfiwa na hili
si jambo linalohitaji fikra sana.

Pili marehemu hayupo kujitetea ukiwa unamsema vibaya inakuwa kama vile
unamuonea.

Hakuna binadamu aliyekamilika kila mtu anazo kasoro na huu ndiyo hakika
ubinadamu wenyewe.

Ikiwa Chico alikuwa na ubaya wake basi na tumsamehe na tumuombe Allah
pia amsamehe kwani mwenzetu keshatangulia mbele ya haki.
 
Alama, Mohamed Said, uliowataja karibia wote ni kaka zangu wa Kariakoo. Nnalia.

Dah! Ulipomtaja Salum Hiriz, nikamkumbuka na Ali Bobo.

Henin ananikumbusha enzi za Lumumba ilivyokuwa Lumumba haswa.

Mrisho Wanted unanikumbuka siku zake za mwisho akija nyumbani kuchukuwa kanzu zake za KUSWALIA, special kwa ajili yake zilizotoka Dubai kwa Jamil, Dennis Law.

Mohamed Saiwad (Chico) Allah amrehemu aturehemu nasi tulio hai. Amiiiin.
Maalim Faiza,
Moja katika dua nizipendazo kuomba ni Allah kuniweka mbali na huzuni.

Nami nakuombea kwa Allah asitie moya wako huzuni kiasi ukabubujikwa
na machozi.

Hakika haya mie moyo huingia simanzi nikizikumbuka siku zile.
Haziwezi kuondoka katika fikra zetu maana zinatukumbusha mengi.

Ali Bobo na Abdallah Awadh nani asiyewajua Dar es Salaam.

Watu waungwana waliojishusha kuwa katika kila shughuli wao hujitolea
kuwaandalia watu chakula kwa ustadi mkubwa sana.

Salum Hiriz aka Sammy Davis Jr. ''gifted singer,'' akiimba kati ya nyimbo
nizipendazo, ''Summer Time.''

Jamil Hizam aka Denis Law, ''brilliant striker with Cosmopolitan.''

Sahib yangu tukifanyakazi pamoja East African Cargo Handling Serices
(EACHS).

ad29c72b-b60b-41ba-97eb-7fdacecc69fa
220px-Wanted_(1967_Film).jpg

Mrisho aka Wanted...
Mtu mkakamavu na mpirani ni mlinzi asiyechoka na mpiganaji wa kutumainiwa.

Mrisho alichukua, ''nickname,'' yake kutoka hiyo movie hapo juu 1966.

Wote hawa ni jamaa zetu na kwa pamoja tumeandika historia ya vijana wa
Kariakoo.
 
Ma sha Allah, juzi juzi Anko Tamim
alikuwa akinipa kisa chenu na Henin na Black American mmoja aliyekuja 70s na kuponda ponda watu.

Nadhani utakikumbuka.
Maalim Faiza,
Tamim
ni, ''super intelligent,'' asikuambie mtu.

Hebu soma haya maneno niliyoandika kuhusu Tamim kama, ''dedication,''
katika kitabu cha Sykes:
''Lastly I wish to pay special tribute to my friend Faraj Abdallah Tamim
whose thoughts and ideas are entangled with mine in this work.

I can only distinguish his thoughts from mine in Tamim’s gift of eloquence
and flow of words which appear in the work as well as in those references
attributed to me verbatim.''
 
Maalim Faiza,
Tamim
ni, ''super intelligent,'' asikuambie mtu.

Hebu soma haya maneno niliyoandika kuhusu Tamim kama, ''dedication,''
katika kitabu cha Sykes:
''Lastly I wish to pay special tribute to my friend Faraj Abdallah Tamim
whose thoughts and ideas are entangled with mine in this work.

I can only distinguish his thoughts from mine in Tamim’s gift of eloquence
and flow of words which appear in the work as well as in those references
attributed to me verbatim.''

Hahahaha, ipo hiyo katika ukoo, labda mimi ndiye niliyemrithi ammi yangu.
 
Hahahaha, ipo hiyo katika ukoo, labda mimi ndiye niliyemrithi ammi yangu.
Maalim Faiza,
Hilo nalikubali kabisa.

Tumekaa mimi, Tamim, Hamza Njozi na Prof. Mazrui Kampala Nile Hilton.
Tulikuwa kwenye mkutano na wenyeji wetu wametuweka hapo.

Tamim akawa anavipitia vitabu vya Prof. Mazrui moja baada ya kingine taratibu.
Prof. ''all ears,'' anamsikiza kwa makini.

Tamim akaingia katika kitabu cha Prof. ''The Trial of Christopher Okigbo.''
Prof. akamuuliza, ''Umependa nini katika kitabui kile?''

Bila kupepesa jicho Tamim akamwambia Ali Mazrui, ''They come at midnight...''
Prof. Mazrui alicheka.

51u2Qcw78UoY6TF-qNaIsj3OyYWrKI6UB-pdqHnna4IiqVYhYWXAsjWrna4US62_c4UPHuxp5T71Ah8cZYruxqe68M6n973RyjffXfnSai2IRJrdTswMxmg0gIckAtmwgHGPXbPFE107AcO1gc0mF8w_ezyCHMyxhB48lnT8v00MedACXj1-Tq5puPada9ZwH8-8MtD3B7dkva3wEdjgNMkdkarMoQVxwMnHN4KvbaD9EBM4SRFd0xlonWZ3bp6hIrCewAJ9Ri0_xXFupPLGKi8jvfJbSD62TflGwaHwwsYGE8p3pmBZdrnyfsHikg3OyHOBIwGn2sL1MEa4A0EeUYZyH5Y_hjladSORFxEj3X-nXmNSTL0etY-9joKhWLdrL1zUCm1f-u581IGNsfmWzlgiKjOZxXKcl_cXEyXd5YHTxbBuSjLqnqksbfHQvvo5DtaIRCRmgw9SjMcliG4po6-yNPrWuty36DKsjhPkoM6-PoSX5q3K_cmy5aA-sUf2olH1vjXGkRZwUwbTbvWSNZvK7rXDFsCw_NqGh6aCESCafeu7jn4aBNA39XWxS4Grx0KWdOW5mhtkTRxaYlbxd0XDyUNs85wrN9SUysBpH6ewpNNNCENN=w953-h692-no

Kushoto: Tamim Faraj, Prof. Ali Mazrui na Mwandishi Kampala 2003
 
Maalim Faiza,
Hilo nalikubali kabisa.

Tumekaa mimi, Tamim, Hamza Njozi na Prof. Mazrui Kampala Nile Hilton.
Tulikuwa kwenye mkutano na wenyeji wetu wametuweka hapo.

Tamim akawa anavipitia vitabu vya Prof. Mazrui moja baada ya kingine taratibu.
Prof. ''all ears,'' anamsikiza kwa makini.

Tamim akaingia katika kitabu cha Prof. ''The Trial of Christopher Okigbo.''
Prof. akamuuliza, ''Umependa nini katika kitabui kile?''

Bila kupepesa jicho Tamim akamwambia Ali Mazrui, ''They come at midnight...''
Prof. Mazrui alicheka.

51u2Qcw78UoY6TF-qNaIsj3OyYWrKI6UB-pdqHnna4IiqVYhYWXAsjWrna4US62_c4UPHuxp5T71Ah8cZYruxqe68M6n973RyjffXfnSai2IRJrdTswMxmg0gIckAtmwgHGPXbPFE107AcO1gc0mF8w_ezyCHMyxhB48lnT8v00MedACXj1-Tq5puPada9ZwH8-8MtD3B7dkva3wEdjgNMkdkarMoQVxwMnHN4KvbaD9EBM4SRFd0xlonWZ3bp6hIrCewAJ9Ri0_xXFupPLGKi8jvfJbSD62TflGwaHwwsYGE8p3pmBZdrnyfsHikg3OyHOBIwGn2sL1MEa4A0EeUYZyH5Y_hjladSORFxEj3X-nXmNSTL0etY-9joKhWLdrL1zUCm1f-u581IGNsfmWzlgiKjOZxXKcl_cXEyXd5YHTxbBuSjLqnqksbfHQvvo5DtaIRCRmgw9SjMcliG4po6-yNPrWuty36DKsjhPkoM6-PoSX5q3K_cmy5aA-sUf2olH1vjXGkRZwUwbTbvWSNZvK7rXDFsCw_NqGh6aCESCafeu7jn4aBNA39XWxS4Grx0KWdOW5mhtkTRxaYlbxd0XDyUNs85wrN9SUysBpH6ewpNNNCENN=w953-h692-no

Kushoto: Tamim Faraj, Prof. Ali Mazrui na Mwandishi Kampala 2003

Hahahaha, ipo hiyo katika ukoo, labda mimi ndiye niliyemrithi ammi yangu.

Maalim Faiza,
Tamim
ni, ''super intelligent,'' asikuambie mtu.

Hebu soma haya maneno niliyoandika kuhusu Tamim kama, ''dedication,''
katika kitabu cha Sykes:
''Lastly I wish to pay special tribute to my friend Faraj Abdallah Tamim
whose thoughts and ideas are entangled with mine in this work.

I can only distinguish his thoughts from mine in Tamim’s gift of eloquence
and flow of words which appear in the work as well as in those references
attributed to me verbatim.''
 
Nilipoona umeandika nikaenda mbio kusoma, pamoja na urefu wa ile taanzia nimeimaliza kuisoma,kaka hongera kwa kuifanyia kazi elimu yako kisawasawa,Mungu akufanyie wepesi uandike zaidi kwani ni wazi unayoyajua si haba. R .I. P Kamanda Chiko
 
Ma sha Allah, juzi juzi Anko Tamim alikuwa akinipa kisa chenu na Henin na Black American mmoja aliyekuja 70s na kuponda ponda watu.

Nadhani utakikumbuka.

Ohhh 1970's Itabidi nimuulize Tamim hiyo
 
Maalim Faiza,
Tamim
ni, ''super intelligent,'' asikuambie mtu.

Hebu soma haya maneno niliyoandika kuhusu Tamim kama, ''dedication,''
katika kitabu cha Sykes:
''Lastly I wish to pay special tribute to my friend Faraj Abdallah Tamim
whose thoughts and ideas are entangled with mine in this work.

I can only distinguish his thoughts from mine in Tamim’s gift of eloquence
and flow of words which appear in the work as well as in those references
attributed to me verbatim.''

Tamim machine nyingine kabisaaa mkuu

Kwanza tazama his prodigious volume of scholarship. Najua haha publish vitabu vine kama akina Njozi et al. Lakini I know he has published hundreds of essay and commentaries kwa bahai mbaya sina hakika kama alifanya film documentaries but he could be a valuable contributor na naamini ana so much secondary and primary resources. Miaka hiyo nilikuwa naenda naye maeneo mbali mbali alipokuwa anaenda kufanya public lectures na and its very difficult not to see the the range, probity as well as impact of his intellectual analyses, interventions, and debates ambazo in my humble opinion were short of nothing but extraordinary. Kwa bahai mbaya hakuna vijana ambao wamefuata nyayo zake kama yeye ninaowafaham zama hizi. Mimi hunikumbusha RK Dau by the way Dr anavyoweza ku move seamlessly between the kwa Klabuni hapo Pan na akina Captain Malik to classroom then to conference circuit, kwenye sports, and corporate boardroom, to the corridors of political power. As for Tamim ni mtu ambaye he often relishes intellectual debate and combat because he believed in the power of ideas na hasa ideas beyond haya mambo yetu ya kawaida. Nakumbuka articles zake Benzi za Africa events alivyokuwa akiwavuruga akina Ahmed Rajab and Co. Binafsi nakumbuka alinipa moja ya first copies za mwanzo za kitabu cha Partnership na vitabu vinginevyo na linguine nilikuwa naazima na soirudishi of course na ninavyo mpaka leo. In my opinion ni mtu aliyeamua ku dedicate his life kuendeleza watu na kwa bahati mbaya sana imekuwa kama case ya Mfalme asiyetambulika kwao. Muhim Allah SW anatambua mchango wake.


The man has a beautiful mind he could have been in the ranks za akina sheikh anta drop, Ivan Van sertima, Molefi Kente Asante, Horace Campbell na wengineo. Itabidi Maalim Mohammed Said tumfungulie Uzi wake
 
20170202_212905.jpg



Baada ya kusoma taazia ya Abdallah Tambaza sina nguvu ya kuandika chochote kuhusu rafiki yangu Mohamed Awadh maarufu kwa jina la Chico. Taazia ya Abdallah mimi imenitia simanzi kiasi ya machozi kunilengalenga kila ninapopita sentensi moja kwenda nyingine sababu ni kuwa Abdallah alikuwa ananitajia mambo na watu niliokuwa nawafahamu na wengine tayari wameshatangulia mbele ya haki. Nikawa kama vile watu hawa nawaona tena. Miezi kama miwili hivi nilikutana na Chico Masaki akiwa amekaa na wajukuu zake ndani ya gari. Tulisalimiana kwa bashasha sana na wala haukunipikitikia kuwa ile ndiyo itakuwa mara yetu ya mwisho kuonana. Mazikoni Kisutu nimekutana na Abdallah kisha nikamuona na ndugu yake Mwinyikhamisi yeye ni mkubwa kwangu kwa umri na aliponiona tu Mwinyikhamisi anahangaika kusimama maana alikuwa kakaa chini miguu inampa tabu. Kila nikimzuia kunisimamia yeye ndiyo anashikilia kushika mkono wangu asimame tusalimiane. Namwambia, ‘’Ka Mwinyi starehe, starehe…’’ Wapi hanisikii anailazimisha miguu yake isimame anisalimie mimi mdogo wake. Mapenzi na heshima iliyoje mkubwa kumsimamia mdogo. Hivi ndivyo wazee wetu walivyotufunza. Allah awarehemu.

8aobHTr34I-5Dcd0FRj6259scyuS8-r4Ev7p5lHr0PKU2WeNcEsbU4zrmsu44PgSJ6tlViMWa85m_Ikdc7lT7DTZ8cBbXBAxQhj09hTYV54JwuW-7LoGQre1I16OWtbxDISeF47Xo0sK1B8Bt8tm0_tpyvvrg3AXqNgShhzMkyTWII1NpXlIq1racegG2nH5qz2XkGNfHZ_ztNyY2wJt2hivI8bG2r4Qa9wZ6AZIK7matSK23WB4rWEiGILRV1HGrfLVZVMQlwHFzz2JyRWndPZF555l9adxjGqf2z9Sg5fPr0rgKTrW6mz71wS7Iqa7IzOa_7afhv3S9EQceXvNBY4kFjEvH1Vef9LpZIW16ls1XQmvUC0w0qdmwf7a1dn_DcAxXn68dt246pXE6Uorm4or73d_3C8kdsS1p61rsGyDiAiMCs5LkazhkC4dPRBPjLvS3iX_E8KhQuhLXNyPcwoeCfVUKCHWDnbVBsm47mvj1tkmeCI8PwHub8lyeMZ03UzPtxa35RfufdCj6-wzuGrG3OlZDA3vRVwDE1GAPJT8U8Nz5n0YjwtblTYMFw5MGqMIq4vFLE-TSy_r0mWN1IOgmLE3uLGFq03UyGZX7WJYh6vPYg=w923-h692-no

Kulia ni Mwinyikhamis, Abdallah Tanbaza na Ibrahim wote hawa ni ndugu
wakiwa katika khitma ya Dar es Salaam Saigon Club


Niko katika, ''keyboard,'' sasa naandika. Msiba wa Chico umetugusa wengi khawa vijana wa Dar es Salaam. Mwinyikhamis alikuwa mchezaji mpira wa sifa katika New Port Club wakati wa ujana wake. Leo Mwinyi hawezi kusimama. Inanijia mechi moja ambayo naamini iko katika kumbukumbu ya wenzangu wengi wa wakti ule. New Port imepangiwa kucheza na Brazil, timu ya wababe watu wakorofi wa sifa mji mzima unawafahamu kwa shari yao ingawa walikuwa na mpira mzuri wa wachezaji wa kusifika. New Port, club ya vijana waungwana, wastaarabu wanaocheza soka la kupendeza. Mashabiki wanajiuliza itakuwaje mpira huu leo na wahuni wale?

Saa kumi jangwani pamefurika. Hii ni mechi ya kikombe mfano wa ''league,'' kwa sasa. Wakati ule vilabu vya mtaani villikuwa na nguvu na uongozi thabiti wa kuweza kuchezesha mechi nzuri zilizojaza watazamaji na kuibua gumzo mji mzima. Brazili kuna Kitwana (Victor Mature) mbabe wa sifa, Mrisho (Wanted) mbabe wa sifa, Abdallah Mkwanda (Inger Johannsson), mbabe pia, Suleiman Jongo (Rory Calhoun) mchezaji mpole na muungwana sana lakini anacheza timu ya wababe, Mohamed Ndava. Shamte Kobe (Bingwa wa Mieleka na ngumi), Hamisi (Marlon Brando), Sadiki Ngwira (Kitonsa), Salum Hussein (Livingstone Madegwa) mtoto wa Sheikh Hussein Juma ana boli safi sana. Wengi katika hawa wametangulia mbele ya haki Allah awarehemu. New Port wanajua kuwa leo wanacheza meshi muhimu na watu washari na wababe wa mji.

New Port, akina Mwinyikhamis na wenzake wametandaza boli staili ya TPC mpira unatembea kwenye majani na wanakwepa hila zote za ubabe hakuna kukunjana mashati. Brazil imefedheheka kwa sababu mechi imeishia sare na wababe hawakuweza kutamba. Hata hivyo New Port wametoka kwenye mechi ile hoi kama wamepigana round 15 na Muhammad Ali. Brazil usiku ule ule wamewafata New Port club kwao kudai wapewe siku ya mechi ya marudiano. Wamefika New Port wamepanda baiskeli zao na kuziegesha kwa vishindo. Wanatafuta shari ile waliyoikosa uwanjani.

Uongozi wa New Port walifanya kikao cha haraka na uamuzi ukawa hawataki kurudiana na Brazil, wahuni wale na wapewe ushindi. Asubuhi taarifa zimeenea Kariakoo nzima na pembezoni kuwa ile mechi ya marudiano haitakuwapo New Port wamekataa kucheza na wametoa ushindi. Brazil wakautangazia mji kuwa New Port wamejisalimisha. Hii ilikuwa 1965 au 1966 maana nakumbuka mimi nilikuwa niko shule ya msingi.

Msomaji nimekuletea kisa hiki kirefu upate kujua Dar es Salaam aliyokulia Chico na sisi sote wa uzao ule ilikuwaje.

Chico alikuwa mmoja wa wacheazaji wa Everton Club iliyokuwa Mtaa wa Narung’ombe si mbali sana na nyumbani kwao Mtaa wa Tandamti mtaa aliokuwa akiishi Mzee Mshume Kiyate rafiki mkubwa wa Mwalimu Nyerere na mmoja katika wazee wa Baraza la Wazee wa TANU lililoongoza harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika. Mtaa huu umebadilishwa jina na kuitwa Mshume Kiyate lakini sasa takriban mwaka wa ishirini kibao cha jina la Mshume Kiyate hakijawekwa kwa sababu ambazi si tabu kuzifahamu. Sasa hii Everton baada ya mtafaruku ndiyo ilikuja kuundwa Saigon na baada ya muda na uhasama wa muda mfupi Everton ilikufa na wote wakajiunga na Dar es Salaam Saigon hii tuijuayo hivi sasa. Turudi kwa Chico.

Chico alikuwa akicheza kama mlinzi na namkumbuka Chico kwa uchezaji wake wa ukakamavu, staili ikiitwa ''kikiri,'' Chico akicheza, ''halfback,'' na alikuwa, ‘’hard tackler’’ mchezaji aliyekuwa akiingia kufata, ''loose ball,'' anakumba mpira na mguu wako. Navikumbuka viatu vyake vya mpira alivyokuwa akivaa – ''Adidas Admire.'' Kulikuwa siku zile na aina mbili za viatu vya Adidas, ''Adidas Admire,'' na ''Adidas La Plata.'' Maarufu ambavyo wengi tukivaa ilikuwa ni ''La Plata.'' Hivi vilikuwa na njumu yaani, ‘’studs,’’ unyayo mzima wakati, ''Admire,'' njumu zilikuwa chache na zilikuwa za kufunga na ‘’spanner.’’ Chico alikuwa kijana, ‘’special.’’ Simkumbuki kijana yoyote katika timu zetu za mitaani aliyekuwa akivaa, ''Admire.''

Ndani ya uwanja Chico alikuwa nahodha mzuri. Yuko nyuma na mbele marehemu Jumanne Masimenti, Jalala, Oshaka (Mazola), Mashaka (Alfredo Di Stefano), Juma Abeid, Ali Kodo, Maufi wanashambulia sauti ya Chico itasikika akihamasisha kwa Kiingereza kisafi kilichonyooka mpira upelekwe goli la adui. Utasikia akipiga kelele, ‘’Push the ball forward,’’ ‘’Score,’’ au ‘’On him,’’ yaani asiachiwe mpira adui. Inawezekana hapo anamuhimiza Ahmada Digila (Danny Blachflour) au Khalid Fadhil (George Young) wapeleke mpira mbele. Chico uongozi na ukamanda alianza toka utoto hakuanzia katika Jeshi la Polisi. Kwa kweli tulikuwa tukisikia sauti hii mori ulikuwa unapanda na hakika tukiongeza juhudi katika kushambulia au kulinda goli. Huyu Ahmada alikuwa umri wangu. Yeye ni mtoto wa Sheikh Digila wa Mtaa wa Nyamwezi nyumba yake ilikuwa karibu na msikiti wa Makonde. Ahmada alipata elimu kubwa sana ya dini. Ahmada alikuwa na kasi ya ajabu katika kusoma Qur’an. Kwenye khitma yeye anawea kukumalizia juzuu hata tatu wewe moja hujakamilisha. Alikuwa ''midfielder,'' hodari katika vijana wa Saigon pamoja na Hassan (Gilbert Mahinya). Hassan Gilbert baadae alikuwa kuwa mtaalamu wa, ''Systems,'' katika moja ya mashirika ya umma na siku tulipokutana Mlimani City akiwa na mabinti zake wakubwa waliojipamba kwa hijab alinifahamisha kuwa amestaafu kazi baada ya kufikisha miaka 60. Nilpomfahamisha kuwa nami nami pia nishapumzika akanambia taarifa zangu anazo kwani alikuwa akinifuatilia huko Tanga nilipokuwa nafanyakazi. Nilifarajika kusikia hayo kuwa hata baada ya miaka ya kutengana wana Saigon walikuwa wakitaka kujua nani yuko wapi na anafanya nini.

Hivi ninavyoandika ni kama vile najiona niko Mnazi Mmoja tunafanya mazoezi na wakati mwingine tukijifunza kuachiana pasi za haraka za kuwazuga maadui. Namuona Ghalib Hamza, maarufu kwa jina la Guy. Chico juu ya ushujaa wake wa kuwakumba washambuliaji hathubutu kumfata Guy akiwa na mpira. Guy alikuwa hana kimo, mfupi lakini ana maungo kiasi. Kilichokuwa kikitutisha kwa Guy ni ile, ‘’ball control,’’ yake na ‘’dribbling skills,’’ angeweza kumzunguka Chico na hata kumtia harusi, yaani kupitisha mpira katikati ya miguu yake. Kulikuwa na Mohamed Ramadhani Kondo (Garincha), Rashid Vava mchezaji rafu club nzima tukimuogopa. Wote wenzetu hawa wametangulia mbele ya haki. Naamini wasomaji vijana watapata tabu sana kuelewa haya majina niliyoyataja, hizi ''nicknames za akina Mazola, Di Stefano, Blanchflour. Hawa walikuwa katika wakati wetu wa miaka ya 1960 ndiyo wachezaji mpira maarufu wa vilabu tofauti vya Ulaya.

Chico alikuwa na baiskeli yake, ‘’sports’’ nyuma aliiandika, ‘’Thunderbird’’ na mwenyewe akiita baiskeli yake kwa jina hilo. Alikuwa anaipanda kwenda shule kavaa vizuri sana na kichwani kavaa, ‘’baseball cap.’’ Amechomekea shati lake jeupe alilolivalia T Shirt nyeupe ndani ndani na kiunoni amevaa, ‘’army belt.’’ Hii ilikuwa mikanda myeupe ya ‘’canvass,’’ yenye, ''buckle,'' ya fedha au ''gold,'' inayong’aa. Mmarekani amekwishakazi. Vijana wote tuliokuwa tukijiona, ‘’fashionable,’’ tukivaa hivyo lakini Chico mwenzetu alitushinda kwa kuwa ilikuwa kama vile mambo yale yako katika damu yake.

Nakikumbuka vyema chumba chake pale kwao. Kilikuwa nadhifu na alikuwa na ‘’record player,’’ yake na sahani za santuri nyingi za nyimbo mbalimbali za wanamuziki wa zama zile. Sasa hapo ndipo utakapotambua kuwa Chico alikuwa, ‘’special.’’ Mimi nilikuwa na ‘’record player,’’ yangu, ‘’Dansette,’’ imetengenezwa Uingereza, Sussex, nakumbuka ile label. Chico santuri zake zilikuwa ni Nat King Cole, Ray Charles, Dean Martin na wanamuziki mfano wa hao kama Sammy Davis na wengine. Muziki mgeni kwa wengi kwa wakati ule. Nyimbo alizokuwa akizipenda na akaniambukiza na mimi kuzipenda ni, ‘’Ramblin Rose,’’ na ‘’The Good Times,’’ zote za Nat King Cole. Hadi leo kila nikizisikia nyimbo hizi huwa nakumbuka utoto wetu katika mitaa ya Kariakoo.

sHTFOQNsLM1ftNy7aNpDDY6CfSN-YVm-7S_0d663cmLzyYRRfwHQJNbHx8Fl6FhNScbc_caBd9OBQH2hY9c56cwvQtr98JnH0TUV3wXiObetweotHpTUE3obU9Jpy2R5QR3ivzfc957Lnr56HmF7njG85Z_HAeARULLbUkWYabUS9lb1JzqEalMzpzPCWKnn70pShix4KosC6KOznIOPGMDTzzT7TkEAJZxqLrQO6QQIT1-SbqyJzqe1ofKqdYD7sUwC18-0QDOjmmTTKBov5ImT_Ivr5h7W4aoqruKRGTm4Yl_T1__PJQ854BwC3veLOrjMCgCd6Vsu-Mxym4lyoYx8R3V0AIR0lQJbr_Nwgrze6Tk9WIScs54zStx3oD3PSSvwHS7dWkHrHt9uOF3bqtSlEYIMSFd2ls0PggUR4jh95-5zLxQX7p0X92m6fZHaw1Z8NsWBHSUmyixdCbWTcPC8NAan6vTM0Dwye8dJsMLGbVj8pufVYseDmAvNdRFzDUupBJsMFPjWoC__r2BExB56f37y8dko1HqCfBiqFgeFPZLvEmWgbu__lP7gbym9W0L_oyApXpwXlQGASddeNDuLiQz2tTqDoCR9Bvg1oRSqmaKTJA=w480-h317-no


Kushoto mstari wa mbele Hussein Shebe, Henin Seif, kulia wa pili ni Raymond Chihota, Hussein,
(pass) Mbaraka ''Bata'' picha ilipigwa mapema 1960


Miaka ya 1960 ilikuwa miaka ya patashika si Dar es Salaam tu bali dunia nzima na ndiyo maana Waingereza wakaipa jina miaka hiyo kuwa ni, ‘’Roaring 60s.’’ Dar es Salaam ilikuwa na mastaa wake wakivuma kama Hussein Shebe, Raymond Chihota na Henin Seif kuwataja wachache katika Chipukizi Club, timu ya waimbaji vijana wakipigiwa muziki na The Blue Diamonds, ''band,'' ya vikana wa Kigoa. Kulikuwa na Sammy Davis Jr Salim Hirizi akiimba nyimbo maarufu, ''Summer Time,'' kwa umahiri mkubwa. Katika hawa waimbaji kubwa lao alikuwa Sal Davis. Siku Sal Davis alipokuja na Hussein Shebe Mtaa wa Tandamti kuwaamkia wazee wake Hussein nyumbani kwa kina Mohamed Jaggan ilikuwa gumzo la mtaa mzima na sisi ambao hatukuwapo kumuona Sal Davis tulisikitika sana. Uhuru wa Tanganyika uliingiza katika nchi mambo mengi kutoka Ulaya yaliyotuvutia sisi vijana. Huu ulikuwa wakati wa wazimu wa mambo mengi sana kutoka Marekani na Ulaya. Sote tukisukumwa na ujana tulikumbwa na wimbi hili. Haya ndiyo yalikuwa maisha ya sisi vijana katika Dar es Salaam ya miaka ile ya 1960 na Chico hakuweza kuliepuka wimbi hili kama vijana wengi walivyoshindwa.


5sZPOFll4GRIAJQlc13eyK4L3RzXOTxon-N42VImzBxus4z1BtUDthAzl_28uaWEKH-IgYe8k3F7ru4QddNyFQXEhtVWQ8f-lMJNAxFfbmzUPXW_3q3h-t7vmE2Z6B5G-bExO4PgXgtQhFoXhFGxZd5ExOgPt6frZbPnXG3Pypmk4mf7AQFDa6iiyga2tSbtT4_BMZT8c0GrwSx7GeuUDCf6NEK_zbyszX8Kq5Ebj4JMSJ4dHiVVUyHCzDNL8Dmb22GnkTiiXBPTD2KLGNj_Y2-NeIF6zlANJ8aW2QcwkQnbqc0ljwZb8C5j67MNqcYX8Rsk44yOJqxSVy6eEs8pR2VQML1PV_X_H1J_b0dhhpwzTDdClZLV1uwkciUlqCrsLHua26VXcX-mKe3aUY4Ujc6r9o2kpryTFXXczqaCK3P8I34-Xj7aoKyH1TudQyliHusZcElIW3_WjujZVNPLKqkVy3jjDYK0k_IQuL9ObRxXpiGAACefLuRvSw870p5oNRD1voq0rJwK-gUfk5trhp6OkkIy5G4XCH9Qp36o2utQdMQuB-t3XX2mRZOx005Z-WHEXGOJHieoHIbD3TuzTOiOq_LsVTUb5GsJ6F1Sj0Bgl558UMb5cw=w480-h360-no

Salum ''Sammy Davis Jr'' Hirizi kama alivyo hivi sasa

xQfAqWcEVCtCleTuI7SVqXH07ms6T7HCleDITMMrHvLZnq35gBYz2Sz-KoDn_GlyxQfn9KFkNZJlu_BpI8S5DQ5_yhdh4ksOX5oEIiHIPH_JwhoAHfoYhRzxfxSuLCVZ4z4EgPSVKP38_d8gemEP6ygJo5kPhXTturzHP8TLMjMGMIugjPd_39fN5yLSCZEeIXYHMVxdiioMpISkIx9Db9YQseuEoe-JoztznYTYQVncpuOy0zGat6Uf1NJY8gwdwb-6-l1ZishMyTXEoFAmG1OJvhQl4C0CCubzFWnNPkMLXpdor_SVQaZhLrWLevCvOxZms9IFV74LC-l4rl2C1cXDDPH95PhYkvNmEdjGnRjNr-LOPfr3Ub4ypkVhk8_h0ebW7gpTDXuWkpbXfRY9_x9aZfPR75qMzPBraTu6EFrNqeX3LLU5c7Xv-qSpeDuIS2GwxHa0pknDWLTW0genQsaSsqp3lKlrY2HWPHtkUBQ9SqyyiVhpkHVGh3ZmsPUrSyTmSVcZb5S5bHeESz0LrApryupHDJMuqbbGjeTSh5V46e-XFpXixEnVOOI4iKBGMRKSZLHtJVcqGYjv_t8vEpcl-Xiwrc_1O35317vD5YLBkS2a2Jyb=w392-h692-no

Sal Davis Katika Onyesho Ujerumani 1960s

Ilikuwa Chico ndiyo, ‘’alinijulisha,’’ mimi kwa Sidney Poitier na nikaanza kuingia kila senema yake ilipokuja mjini. Sidney Poitier katika miaka ile hakuwa maarufu kwa vijana wengi wa Dar es Salaam. Wengi wetu tulikuwa na John Wayne, Richard Widmark, Alan Ladd, Victor Mature, Marlon Brando na mfano wa hao na wala haikutupitikia kuwa tunaweza kwenda senema Empire, Avalon, Empress au Chox kuangalia senema, ‘’actor,’’ Mnegro kama Sidney Poitier au Jim Brown. Chico alikuwa, ‘’special,’’ yeye akimjua Sidney Poitier, Eartha Kitt na wengineo siku nyingi sana. Kuanzia hapo na mimi nikabadilika. Nakumbuka senema za Sidney Poitier alizokuwa akipenda kunihadithia kama ni kama ''Lilies of the Fied,’’ ‘’A Patch of Blue,’’ na nyingine nyingi.

p3173_p_v8_ac.jpg


Ujana haukawii kukimbia. Haukupita muda tukakua na ikawa lazima tukubali kuwa wakati wa mchezo umepita tunaingia ukubwani. Chico alitushangaza wengi alipojiunga na Jeshi la Polisi kwani si katika kazi ambazo, ‘’watoto wa mjini,’’ tulizipenda na kubwa ni kuwa kazi ya jeshi ilikuwa inahitaji kufanyakazi nje ya Dar es Salaam na wengi wakiona dhiki kuondoka mjini. Sasa hapa ndipo ninapotaka kuhitimisha kuwa Chico alikuwa, kwa kweli na kwa hakika kabisa alikuwa ‘’special.’’

Chico alijiunga na Jeshi la Polisi na aliitumikia nchi yake kwa uadilifu mkubwa. Alifanyakazi takriban kila mahali na kuacha jina lililotukuka. MIaka mingi baada ya sisi kutoweka hapa duniani, itakapokujaandikwa historia ya watoto wa Dar es Salaam na nini wamefanya katika taifa hili nina hakika Kamanda Chico jina lake litakuwa juu.

Allah amlaze pema ndugu yetu Mohamed Awadh Saiwaad maarufu kwa jina la Chico aliloishi nalo utotoni hadi ukubwani.

1SoH8DK4E3Rp_beqWUyYroAl-85hb9m-PN4bznGLJnUNTJ1wOrOPPizdFyw0WRQb4WwsF_y_c05aJ0Gpzw9FLkPTKYnmFxuDV2FCPT-IzVcux6cmW_FAK61H5TaBLc8UHpyhvAnAaMWONyVsBqcl9M8LNNUbsW6pb7ccfcpLpXJ49Yeuxmh7qHWC0JVJGuvvoJYOgaBPKQwvb_1HTQsz_1OAC6iNohPCGbWvUVMaKGhPe8J0r46TP6PUU9jxtRbYCwHZg2KAP9b2JTvqT2vygbWBBV1JylEp0X2kOLdhMP7kYM0CWmhiOgNg4-9vbhkWy7VloajuTqcvVPZ7KL5Rh7A5IETn6OXibuj86BEKZD6qct17MCwkzStB4eGGvtpKTiy80E0cH4ScWnCBwds6C05ft0A32XnFBhC-P2AqWaB6JbetvAN5WUc65LvAoY341l8tGAolg5XO70LVK2q221VfYr7WZ6C6VGKgLJOrYHp4SXP549dmX9dIYZw-lZ9JM_tCGziJx2au8B56vfz5RQRe38MNG3l9dkoXsxpftcUQc1RvAeMOs1qVeDM2Ul2ycDCsJwRY9s98Wz5XdSYTUElvdTvfWYjdq8WkmNZfSosaSte2AtCb_Q=w670-h526-no

Mwandishi akiwa Viwanja Vya Mnazi Mmoja ambako Everton na kisha Saigon
walikokuwa wakicheza mpira. Nyuma ni barabara iliykuja kupewa jina la Bi. Titi
Mohamed na ukivuka barabara hiyo ni Soko la Kisutu maarufu kwa jina la Soko
Mjinga. Picha ilipigwa 1966
Amazing story well narrated.....
 
Sal Davis nilibahatika kumsikia miaka ya 90s hap0 Euro Pub,nafkiri akiwa karejea toka Ulaya,kwakweli alikua na kipaji cha pekee,alifanya ninze kufatilia jazz kwa karibu.kwa akili yangu nikijua ni mmarekani Mweusi anayeishi TZ.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom