Zile hoja za ufisadi ziko wapi?

IsayaMwita

JF-Expert Member
Mar 9, 2008
1,127
140
Nakushukuru Mola kwa kunipa pumzi yako baba, bado ninaendelea kuishi, japo sitakiwi kuishi hapa duniani(Tanzania), najua ni mpango wako kuwa hapa duniani katika nchi njema ya Tanzania, nchi tajiri huku mimi nikiwa maskini wa kutupwa.

Ndugu zangu wana JF, kuna kipindi nilidhani mtalisaidia Taifa kwa kukemea maovu ya viongozi wetu na kuwaasa ya kufanya lakini mambo yamegeuka, MAFISADI wametuzidi nguvu tumesahau yote, yale ya BOT, EPA, RICHMOND na mengineyo mengi,.

Naomba sasa tujiulize kweli nini hatima ya watoto wetu kwa siku za usoni?

Hebu kweli tuna mikakati ya dhati ya kuleta mabadiliko 2010?,

Niliwahi kusema kuwa mbona huko kwenu mijini hakuna mageuzi ya kweli, na hapo ndipo kwenye vyombo vya habari vya kutosha? kwenye wasomi wa kutosha? waandishi wa kumwaga?
 
Ni jambo la kujiuliza hebu hizi kelele tunazopiga tutasikika? ni kwa nini sasa huko mijini msiamke kama sisi huku shamba tulivyoamua, kwamba CCM sasa basi?
 
Ni jambo la kujiuliza hebu hizi kelele tunazopiga tutasikika? ni kwa nini sasa huko mijini msiamke kama sisi huku shamba tulivyoamua, kwamba CCM sasa basi?

Kuwatoa ama kusema Basi kwa ccm tu si tiba kabisa Labda useme Basi kwa ccm na ndiyo kwa wepi na wenye sera zipi?

Juzi nilibaki mdomo wazi baada ya kusikia chama mbadala kinauza sera zake kule kwetu eti sera yake ni MSICHAGUE CHAMA CHA MAFISADI.

Yani ni vichekesho tu .Homeboy kazi ipo yawezekana leo usiniilewe lakini mwalimu mzuri ni Mda.
 
Nakushukuru Mola kwa kunipa pumzi yako baba, bado ninaendelea kuishi, japo sitakiwi kuishi hapa duniani(Tanzania), najua ni mpango wako kuwa hapa duniani katika nchi njema ya Tanzania, nchi tajiri huku mimi nikiwa maskini wa kutupwa.

Ndugu zangu wana JF, kuna kipindi nilidhani mtalisaidia Taifa kwa kukemea maovu ya viongozi wetu na kuwaasa ya kufanya lakini mambo yamegeuka, MAFISADI wametuzidi nguvu tumesahau yote, yale ya BOT, EPA, RICHMOND na mengineyo mengi,.

Naomba sasa tujiulize kweli nini hatima ya watoto wetu kwa siku za usoni?

Hebu kweli tuna mikakati ya dhati ya kuleta mabadiliko 2010?,

Niliwahi kusema kuwa mbona huko kwenu mijini hakuna mageuzi ya kweli, na hapo ndipo kwenye vyombo vya habari vya kutosha? kwenye wasomi wa kutosha? waandishi wa kumwaga?

Mstahiki Meya Leo bado utaweza Ongea haya?
 
Back
Top Bottom